Skip to main content

MUATHIRIKA ASIMULIA JINSI "ALIVYONYONYWA DAMU" NCHINI MALAWI.




Hadithi za mashambulizi ya usiku wa manane na 'Wanyonya damu' (Vampires) za kunyonya damu zinaendelea kusababisha matatizo nchini Malawi, kusini mashariki mwa Afrika.

Madai 'ya waathirika' wanashambuliwa usiku na 'wanyonya damu' yamesababisha vurugu za wananchi kuchukua sheria mkononi na vifo katika sehemu za kusini za nchi hiyo.

Watu takribani saba wameuawa katika wilaya moja, na mapema mwaka huu, wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa na wafanyakazi wa kujitolea kutoka Marekani waliondolewa katika eneo hilo.

Wakati wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa waliporudi sasa, hadithi za mashambulizi ya kunyonya damu zinaendelea.



Jamiya Bauleni, mama mwenye umri wa miaka 40, alisema kuwa mshambulizi aliingia nyumbani kwake na kunyonya damu yake nyumbani kwake katika wilaya ya Thyolo.

'Hii sio kusikia,' aliuambia umati wa watu  katika kijiji cha Ngolongoliwa kusini mwa nchi hiyo ambayo imekuwa katika hali ya hofu hivi karibuni juu ya uvumi wa shughuli za 'wanyonya damu'.

"Najua damu yangu ilinyonywa. Niliona mwanga kwenye kona ya paa langu. Nilishindwa kusimama kutoka kitandani kwangu na nikasikia kitu cha kimetoboa mkono wangu wa kushoto, "alisema, akionesha karibu na kifua chake.


Hadithi yake ni sehemu ya mlolongo mrefu wa ushuhuda sawa nchini Malawi, ambapo imani katika uchawi na shughuli za vampire zinaenea na kusababisha watu kulipa kisasi kwa kujichukulia sheria mkononi na kuwaua watuhumiwa wa uchawi.


Bauleni, ambaye hufanya uuzaji wa chakula cha mchana, alisema kuwa kabla ya kuanguka na kupoteza fahamu alisikia mtu anayekimbia eneo hilo.

Alipelekwa kwenye kliniki na baadaye aliachiliwa baada ya kupewa virutubisho vya vitamini, lakini aliamua kutokuripoti shambulio hilo.

Uvumi wa kuwepo kwa 'wanyonya damu' unasemekana kutokea nchi jirani ya Msumbiji na kuvuka mpaka kuenea mpaka kwenye wilaya za Malawi za Mulanje na Phalombe, kwa mujibu wa ripoti ya Umoja wa Mataifa.

Watu takribani saba wameuawa katika wilaya ya Mulanje baada ya kuwindwa, polisi wanasema.




Muathirika mmoja, Florence Kalunga, mwenye umri wa miaka 27, anasema alikuwa amelala pamoja na mumewe nyumbani kwake alipoona mwanga kama moto.


"Nilisikia mlango unafunguliwa... Nilihisi kitu kama sindano katika kidole changu, "alisema.

Watu wanaolengwa katika vurugu kulipa kisasi mara nyingi ni watu wenye utajiri katika sehemu za vijijini za nchi hiyo ya kusini mwa Afrika ambapo umasikini umezoeleka na kiwango cha elimu ni duni sana.

Mjasiriamali Orlendo Chaponda alifanikiwa  kukimbia mashambulizi wakati wanakijiji 2,000, baadhi yao waliokuwa wamebeba mapanga na mawe walipovamia nyumba yake huko Thyolo mnamo Septemba 30.

"Wao walisema nilikuwa nikiwahifadhi wanyonya damu,",
alisema Chaponda, ambaye alikuwa nje wakati huo.
"Wangeweza kuniua ikiwa wangenipata."

Aliwaita polisi ambao walitumia mabomu ya machozi ili kutawanya umati uliokua umezunguka nyumba yake kwa masaa matano.

"Hakuna ukweli juu ya wanyonya damu, ila watu wenye wivu na majambazi wanataka kuchukua nafasi hiyo kushambulia matajiri,"
Chaponda alisema.

"Ikiwa una gari nzuri, wewe ni mnyonya damu."

Shirika la huduma ya damu ya kitaifa ya Malawi - taasisi pekee iliyoruhusiwa na serikali kukusanya damu kwa ajiri ya hospitali kutoka kwa watu wanaojitolea - limesema kwamba uvumi wa matukio ya 'wanyonya damu' pia umeanza kurudisha nyuma shughuli za taasisi hiyo.

"Suala hili limeleta athari sana...limtuzuia kwenda kukusanya damu katika maeneo yaliyoathirika, "alisema Bridon M'baya, mkurugenzi wa huduma za matibabu.

Watu takribani 250 wamekamatwa nchini Malawi juu ya unyanyasaji wa watu, na wengine 40 walikamatwa juu ya makosa sawa na hayo katika nchi jirani ya Msumbiji.

Rais wa Malawi Peter Mutharika alilazimika kukubali kuwa kumekuwepo na tatizo hilo na kusisitiza kwamba serikali tayari imelidhibiti.

"Hakuna ushahidi wa wanyonya damu. Ni uwongo wenye nia ya kudhoofisha kanda, "alisema hivi karibuni.

"Wale wanaoeneza uvumi huu watapambana na sheria."




Anthony Mtuta, mwalimu msaidizi wa anthropolojia katika Chuo Kikuu cha Katoliki cha Malawi, alisema mizizi ya vitisho vya 'Wanyonya damu' imeanzia katika shida za uchumi na madara katika jamii'

"Ni matajiri dhidi ya masikini. Maskini wanaamini kuwa tajiri ni wenye tamaa na wananyonya damu za watu masikini,", alisema.

Malawi kwa kiasi kikubwa inategemea misaada ya kigeni, lakini baadhi ya wenyeji wanapokea misaada kwa mashaka.

"Kwa wanakijiji, hufikiri kwamba hakuna zawadi utaipata bure ... utailipa kupitia damu," alisema Mtuta.




McDonald Kolokombe, karani katika hifadhi ya misitu ya Likhubula ya serikali, alibainisha kuwa idadi ya watalii waliotembelea eneo la Mulanje imeshuka tangu katikati ya Septemba.

"Jamii hutegemea wageni kulisha familia zao kwa kufanya kazi kama kuongoza watalii na kuwauzia bidhaa", alisema.



"Tuna njaa kwa sababu ya uvumi mbaya juu ya 'wanyonya damu,' ", aliongeza muongoza watalii(tour guide), Eric John.
"Ni uongo mkubwa."




CHANZO:
hinnews.com

Comments

Habari Nyingine Kutoka Kioo17 Swahili;

WASTANI WA ADA ZA VYUO VIKUU BORA ZAIDI DUNIANI.

            Elimu ya juu ya kupokea nje ya nchi (Nchi zilzo endelea) daima imekuwa kiwango cha kutambuliwa sana, na wanafunzi kutoka duniani kote siku zote wana ndoto kuhusu hilo.             Tovuti ya Bright Side imeamua kujua gharama za sasa za kujifunza * kwa wanafunzi wa kimataifa katika vyuo vikuu vya juu vya dunia, na tungependa kushiriki habari hii na wewe. * Wastani wa kila mwaka ada ya mafunzo ya shahada ya kwanza ; MAREKANI; Kwa maelezo zaidi kuhusiana na chuo hiki bonyeza hapa: http://www.harvard.edu/ Kwa maelezo zaidi kuhusiana na chuo hiki bonyeza hapa:  http://web.mit.edu/ UINGEREZA;     Kwa maelezo zaidi kuhusiana na chuo hiki bonyeza hapa; http://www.cam.ac.uk/     Kwa maelezo zaidi kuhusiana na chuo hiki bonyeza hapa: http://www.ox.ac.uk/ USWISI (SWITZERLAND ):     Kwa maelezo zaidi kuhusiana na chuo hiki bonyeza hapa:...

ORODHA YA NCHI ZA KWANZA NA ZA MWISHO KWA AMANI DUNIANI.

Marekani:  Ripoti ya Taasisi ya Uchumi na Amani imepata mataifa kumi tu ulimwenguni ambayo hayapo katika vita na migogoro kabisa. Kwa mujibu wa Ripoti ya Kimataifa ya Amani 2016, Botswana, Chile, Costa Rica, Japan, Mauritius, Panama, Qatar, Uswisi, Uruguay na Vietnam ndio nchi pekee ambazo hazipo kwenye vita wala migogoro yeyote ile ya kuhatarisha amani.. Iceland inaongoza orodha ya nchi zinazoongoza kwa amani ulimwenguni, ikifuatiwa na Denmark, Austria, New Zealand, Ureno, Jamhuri ya Czech, Uswisi, Canada, Japan na Slovenia - wakati Marekani ikiwa kwenye nafasi ya 103. Palestina imepanda kutoka nafasi ya 163 mpaka nafasi ya 148. Syria iliyoharibiwa na vita imewekwa chini ya orodha, chini kuliko Sudan Kusini, Iraq, Afghanistan, Somalia, Yemen, Jamhuri ya Afrika ya Kati, Ukraine, Sudan na Libya. "Ripoti inalinganisha amani duniani kwa kutumia mandhari tatu pana: hali ya utulivu na usalama katika jamii; kiwango cha mgogoro wa ndani au wa kimataifa; na kiwango cha kije...

WAZIRI WA MAMBO YA NJE WA GAMBIA AMTAKA RAIS WA TOGO KUACHIA MADARAKA KWA HIARI.

RAIS WA TOGO, FAURE GNASSINGBE. BANJUL, Oktoba 23 (Reuters) "Rais wa Togo Faure Gnassingbe anapaswa kujiuzulu mara moja na Umoja wa Afrika na kanda ya kikanda ya Afrika Magharibi ECOWAS inapaswa kumshawishi kushuka ikiwa hawaja fanya hivyo",  Waziri wa Mambo ya Nje wa Gambia Ousainou Darboe amesema. Maoni ya Darboe ni ishara ya mwanzo kwamba yuko dhidi ya Gnassingbe ambaye alinyakua madaraka kwa nguvu mwaka 2005 baada ya kifo cha baba yake ambaye alikuwa ametawala tangu mwaka 1967. Togo ni inakabiliwa na mgogoro wa kisiasa ambao takribani watu 10 wameuawa katika maandamano tangu Agosti. "Nadhani Umoja wa Afrika na ECOWAS inapaswa kushiriki na kumshawishi rais wa Togo kung'ooka ," Darboe aliiambia Shirika la habari la Uingereza (Reuters) mwishoni mwa wiki hii, akiongezea kuwa nchi nyingine zinahitaji kushiriki. "Wakati serikali ya Togo inakiuka kanuni zinazokubalika sidhani kama suala hili linapaswa kuchukuliwa kama ni mambo ya ndani ya nd...

SABABU YA ZIPU NYINGI KUWA NA HERUFI "YKK".

Ikiwa umewahi kuchunguza kwa ukaribu zipu kwenye nguo zako nyingi, utakua tayari umeona herufi zinazosomeka "YKK," katika herufi kubwa, kwa mengi yao.Herufi hizi zipo kwenye kila kitu kutoka kwenye nguo za jeans, makoti hata kwenye mabegi. Herufi hizo zinasimama kwa niaba ya "Yoshida Kogyo Kabushikikaisha" ambayo, kutoka kwenye lugha ya Kijapani, inaelezea  "Yoshida Company Limited" yaani "Kampuni ya Yoshida"  Kampuni hii ni ya mtengenezaji wa zipu aitwaye Tadao Yoshida, ambaye aliianzisha mwaka wa 1934. Kwa wastani, kampuni hiyo inatengeneza nusu ya zipu duniani, ambayo ni zaidi ya zipu bilioni 7 kila mwaka. Kwa uhalisia Yoshida hakua mvumbuzi wa zipu duniani, zipu zilivumbuliwa na Mmarekani, Whitcomb L. Judson, miaka ya 1890.  Kampuni yake sasa ipo,  na inabuni na kutengeneza zipu za kisasa ikijulikana kama Talon, Inc. Bidhaa za kampuni hiyo hutumiwa makampuni kama Brooks Brothers na Uniqlo. Lakini YKK ina sifa isiyofananishik...

UGANDA IMEWAFUKUZA WATAALAM WA KIJESHI KUTOKA KOREA YA KASKAZINI.

Uganda imefukuza wataalamu wa kijeshi wa Korea Kaskazini na wawakilishi wa makampuni ya Kaskazini ya Korea, ikiwa ni pamoja na mfanyabiashara wake mkubwa wa silaha za juu kutokana na mataifa ya Kiafrika kukabiliwa na shinikizo la kuzingatia vikwazo vya Umoja wa Mataifa(UN) juu ya mpango wa silaha za nyuklia wa Pyongyang. "Raia wa Korea ya Kaskazini waliobaki katika taifa hilo la Afrika Mashariki ni wanadiplomasia na watu binafsi tu ", Okello Oryem, naibu waziri wa mambo ya kigeni, aliiambia The Associated Press. "Tunafuatana kabisa," alisema Oryem, akiongezea kwamba Uganda ina uhusiano wa kawaida wa kidiplomasia na Korea Kaskazini. Uganda hasa ilidai kuondoka kwa watu wanaowakilisha Shirika la Biashara la Maendeleo ya Madini ya Korea. Ni mkataba wa msingi wa Korea Kaskazini na chini ya vikwazo vya U.N. na U.S. Uhamisho huo unaashiria mabadiliko ya sera kwa serikali ya Uganda, ambayo hapo awali ilikuwa na mahusiano ya mazuri na Pyongyang. Korea ya Kaska...

PAPA FRANCIS ASHINDANISHWA NA PABLO ESCOBAR KWA KUHESHIMIWA NCHINI COLOMBIA.

MedellĂ­n (Colombia) (AFP):  Katika saluni yake ya nywele, Yamile Zapata anatumia faida ya ziara ya Papa Francis ili kuuza pete za funguo zenye picha ya kiongozi huyo wa kanisa katoliki duniani. Lakini anadai sio ambapo pesa halisi iko kwenye mji wa Medellin nchini Colombia. Zawadi nyingi anazouza katika mji huu wa Colombia hubeba uso wa "mtakatifu" na shujaa wake mwenyewe: Pablo Escobar. Wakati Francis alikuwa akihudumia na kufundisha kama kuhani wa Yesuit katika miaka ya 1980, Escobar alikuwa akiua mamia ya watu na kufanya biashara ya madawa ya kulevya ya mabilioni ya dola za kimarekani. "Kila mtu anataka picha za papa sasa, lakini picha za Pablo zinauzika vizuri zaidi," , alisema Zapata, mwenye umri wa miaka 34, wakati ambao jiji hilo limeandaliwa kwa ajili ya mkutano wa Papa Francis wa wazi siku ya Jumamosi. PETE ZA FUNGUO ZENYE PICHA ZA PAPA FRANCIS NA PABLO ESCOBAR ZIKIWA ZINAUZWA KWENYE MITAA YA JIJI LA MEDELIN, COLOMBIA. Francis alitoa mane...

MCHEZAJI WA ZAMANI WA UINGEREZA AMESEMA ALICHEZA NA WACHEZAJI WATATU MASHOGA KWENYE TIMU.

Carl Hoefkens (jezi no.2) alichezea West Bromwich Albion na Stoke City wakati wa enzi zake ligi kuu ya England. Beki wa zamani wa Ligi Kuu ya Uingereza amesema alicheza pamoja na wachezaji wenzake wawili wa mashoga ndani ya timu, na mmoja alikua na jina kubwa. Carl Hoefkens, West Bromwich Albion na Stoke City siku za nyuma, anasema wachezaji hao walikua wazi na hawakujificha kwenye vyumba vya kubadilishia nguo ingawa bado hawajulikani kwasababu ya maombi yao wenyewe ya kuomba kutotangazwa. Justin Fashanu, ambaye alijiua mwaka 1998, alikuwa mchezaji wa mwisho wa kazi nchini England kuja nje kama mashoga - mwaka 1990. Hoefkens alipokua (kushoto), alipokua anachezea Stock  City. Hoefkens aliyecheza Uingereza kwa miaka minne, akiondoka mwaka 2009, alidai kuwa mchezaji mwenzake mmoja wa timu alikua anaweza kuja kwenye uwanja wa mafunzo ya klabu na mpenzi wake wa kiume  lakini aliwaomba wenzake kutokuwaambia watu wangine wa nje ya timu. 'Nilicheza pamoja n...