Skip to main content

MAREKANI INATAKA RAILA ODINGA ASTAAFU KISHA APANDISHWE HADHI.


Kutoka Gazeti TAIFA LEO | Nairobi, Kenya:

Katika juhudi zake za kukomesha mzozo wa kisiasa ambao umekumba Kenya tangu uchaguzi mkuu wa Agosti 8, 2017, imefichuliwa kwamba nchi hiyo yenye ushawishi mkubwa ulimwenguni inapendekeza Bw Odinga apandishwe hadhi kuwa kiongozi wa taifa na apewe mamlaka makubwa katika taifa.

Katika pendekezo hilo, Bw Odinga atapewa ofisi, wafanyakazi, msafara wa magari sawa na wa kiongozi wa nchi na marupurupu ambayo yatamwezesha kuzuru kote ulimwenguni kuwakilisha Kenya na kuhutubu kuhusu demokrasia.


Kiongozi huyo wa Chama cha ODM pia atalipwa marupurupu ya kustaafu kwa msingi wa miaka mingi ambayo ametumikia umma na ameahidiwa juhudi zake za kupigania mageuzi hasa haki katika uchaguzi zitaungwa mkono.

Duru zilisema mapendekezo hayo yaliwasilishwa kwa Bw Odinga na Balozi wa Marekani nchini Kenya, Robert Godec, ambaye amekuwa akikutana na wanasiasa wa NASA na Jubilee.

Haikuwezekana kuthibitisha haya kutoka kwa ubalozi wa Marekani nchini kufikia wakati wa gazeti hili kuchapishwa.

Hata hivyo, inasemekana Bw Odinga alikataa mapendekezo hayo kwa vile hayatatui maslahi ya Wakenya ambao wanataka kuona haki katika uchaguzi baada ya Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) kuvuruga uchaguzi wa urais wa Agosti 8, 2017.

“Hawajaeleza kwa kina kuhusu itakavyokuwa bali wanazungumza tu kuhusu kujumuisha wadau zaidi. Lakini nimewahi kusema wanaingilia masuala ya Kenya.
Hawana haki kuja kutuambia nani anafaa kuwa hiki wala kile. Tunazungumza kuhusu wizi wa kura na nia yetu ni kuleta mabadiliko yatakayotenda haki uchaguzini,” 
Bw Odinga akasema kwa simu Jumapili.


Mwanasiasa mmoja wa NASA aliambia ‘Taifa Leo’ kwamba Bw Odinga pia alisema mapendekezo hayo hayazingatii maslahi ya vinara wengine wa muungano huo.

Kinara huyo alinukuliwa kumwambia Bw Godec: 
“Tuseme nimekubali, nitawafanyia nini vinara wenzangu katika NASA?” 

Kiranja wa Wachache katika Bunge, Bw Junet Mohammed, alisema hana habari kuhusu mapendekezo hayo na kusisitiza kuwa kulingana na NASA Bw Odinga anafaa kuwa rais.
“Uongozi wa taadhima haupeanwi kwa mtu. Bw Odinga ameupata kupitia mchango wake na vitendo vyake kwa nchi hii na mataifa mengine ya Afrika na hakuna anayeweza kumkabidhi wadhifa huo,” 
akasema Bw Junet.

Lakini mwanasiasa mwingine wa NASA alisisitiza kuwa Bw Odinga amekabidhiwa mapendekezo hayo ingawa changamoto iliyopo ni kwamba inashukiwa yalibuniwa na Jubilee ambayo imekuwa ikimshinikiza astaafu katika siasa.

“Tuna kila sababu ya kuamini kwamba haya ni mapendekezo ya kibinafsi ya Godec au mbinu ya Jubilee ambayo balozi huyo amekubali kuhusika,” akasema mwanasiasa huyo ambaye aliomba asitajwe jina kwani hana idhini rasmi kuzungumzia suala hilo.


CHANZO:
public class HelloWorld {
 public static void main(String[] args) {
  System.out.println("Hello World");
 }
}
<script type="text/javascript">
  ( function() {
    if (window.CHITIKA === undefined) { window.CHITIKA = { 'units' : [] }; };
    var unit = {"calltype":"async[2]","publisher":"Kioo17swahili","width":550,"height":250,"sid":"Chitika Default"};
    var placement_id = window.CHITIKA.units.length;
    window.CHITIKA.units.push(unit);
    document.write('<div id="chitikaAdBlock-' + placement_id + '"></div>');
}());
</script>
<script type="text/javascript" src="//cdn.chitika.net/getads.js" async></script>

Comments

Habari Nyingine Kutoka Kioo17 Swahili;

ORODHA YA NCHI 80 AMBAZO MTANZANIA ANARUHUSIWA KUINGIA BILA VIZA.

         Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni amesema kuna zaidi ya nchi 80 ambazo watanzania wanaweza kusafiri bila ya kuwa na viza . Mhandisi Hamad Masauni amesema kuna zaidi ya nchi 80 ambazo watanzania wanaweza kusafiri bila ya kuwa na viza za kusafiria kama ilivyokuwa nchi za afrika Mashariki. Mhandisi Massauni amebainisha hayo leo bungeni wakati akijibu swali la Mbunge wa Mlalo kupitia tiketi ya CCM Rashid Shangazi aliyetaka kujua ni nchi ngapi ambazo watanzania wanaweza kusafiri bila ya kuwa na viza (viza on arrival). "Zipo nchi 16 kwa Afrika ambazo watanzania wanaweza kuzitembelea bila ya kuwa na viza na duniani zipo 67" alisema Masauni. Aidha Massauni amezitaja nchi hizo kuwa ni Benin, Burkina Faso, Cape Verde, Ivory Coast, Djibouti, Gabon, Gambia, Guinea, Guinea­Bissau, Liberia, Mali, Mauritania, Niger, Sierra Leone pamoja na Togo. Pamoja na hayo Masauni amesema...

MCHEZAJI WA ZAMANI WA UINGEREZA AMESEMA ALICHEZA NA WACHEZAJI WATATU MASHOGA KWENYE TIMU.

Carl Hoefkens (jezi no.2) alichezea West Bromwich Albion na Stoke City wakati wa enzi zake ligi kuu ya England. Beki wa zamani wa Ligi Kuu ya Uingereza amesema alicheza pamoja na wachezaji wenzake wawili wa mashoga ndani ya timu, na mmoja alikua na jina kubwa. Carl Hoefkens, West Bromwich Albion na Stoke City siku za nyuma, anasema wachezaji hao walikua wazi na hawakujificha kwenye vyumba vya kubadilishia nguo ingawa bado hawajulikani kwasababu ya maombi yao wenyewe ya kuomba kutotangazwa. Justin Fashanu, ambaye alijiua mwaka 1998, alikuwa mchezaji wa mwisho wa kazi nchini England kuja nje kama mashoga - mwaka 1990. Hoefkens alipokua (kushoto), alipokua anachezea Stock  City. Hoefkens aliyecheza Uingereza kwa miaka minne, akiondoka mwaka 2009, alidai kuwa mchezaji mwenzake mmoja wa timu alikua anaweza kuja kwenye uwanja wa mafunzo ya klabu na mpenzi wake wa kiume  lakini aliwaomba wenzake kutokuwaambia watu wangine wa nje ya timu. 'Nilicheza pamoja n...

ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2017, TANZANIA

MH.GEORGE SIMBACHAWENE .               Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Tamisemi) George Simbachawene ametoa idadi ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na masomo ya kidato cha tano na vyuo vya ufundi kwa mwaka 2017 huku jumla ya wanafunzi 2,999 wakiachwa.             Simbachawene ametoa kauli hiyo leo mjini Dodoma wakati akizungumza na waandishi ws habari na kusema kuwa ufaulu kwa mwaka huu umeongezeka kwa asilimia 3.75 ukilinganisha na matokeo ya mwaka 2015. Waziri amedai kati ya wanafunzi 96,018 waliofaulu kwa daraja la kwanza hadi la tatu ni wanafunzi 93,019 tu ndiyo waliochaguliwa kujiunga na kidato cha tano na vyuo vya ufundi.              Waziri Simbachawene amesema kuwa jumla ya watahiniwa wote waliofanya mtihani wa kidato cha nne kwa shule kwa mwaka 2016 ni 349,524 huku waliofanya mtihani wa kujitegemea ni 47,751 ambapo watahiniwa waliofanya mtihani wa shule...

TUPAC SHAKUR ALIBAKWA JELA !!!

             Ulimwengu wa filamu za Hollywood na muziki wa Hip Hop juzi ulipatwa na mshangao baada ya mtayarishaji wa filamu inayohusu maisha ya hayati Tupac Shakur ,L.T Hutton kuelezea sababu zilizomfanya kumbadilisha muongozaji wa filamu hiyo kutoka John Singleton na kumuweka muongozaji Benny "Boom" Douglas.  Filamu hiyo inayoitwa "all eyez on me" tayari imekwisha andaliwa na inatarajiwa kuzinduliwa leo tarehe 16 Juni 2017.       Akizungumza kwenye mahojiano redioni L.T Hutton amewashtusha watu wengi baada ya kudai kwamba walishindwana na muongozaji wa mwanzo bwana John Singleton sababu muongozaji huyo aling'ang'ania kuwepo kwa matukio (scene) ambazo kwa maoni yake zisingependeza.        Matukio ambayo John Singleton alipenda yawepo katika filamu hiyo ni pamoja na kutaka filamu hiyo ianze na scene ya Tupac akilazimisha kumlawiti msichana wa kizungu.!!!          Singleton pia ali...

MFALME WA GHANA ASABABISHA AFISA MKUU WA BENKI KUFUKUZWA KAZI.

Afisa mtendaji mkuu wa benki alifukuzwa kazi na kuchunguzwa na Shirika la Uhalifu wa Taifa baada ya kuweka pauni za Uingereza 350,000 ( £ 350,000 ) pesa taslimu aliyopewa na Mfalme wa Ghana. Mark Arthur wa benki ya Kimataifa ya Ghana Bigwig aliitwa kwenye nyumba ya Osei Tutu II huko Henley-on-Thames na kupewa £ 200,000 pamoja na $ 200,000 na kuagizwa aiweke kwenye akaunti ya benki ya Mfalme huyo. Licha ya noti hizo kuwa na namba za mfululizo zinazofuatana (consecutive serial numbers) Bwana Arthur alisema aliona kuwa haifai kumhoji mfalme na kwenda kuiweka benki kwa kutumia usafiri wa teksi ya uber. Punde baada ya Bwana Arthur kuweka pesa hiyo benki, taarifa ya utakatishaji wa fedha ilifika katika jiji la London, Uingereza na kugharimu ajira yake. Bwana Arthur alielezea kwenye taarifa yake ya ushahidi kuwa Mfalme alimwambia kwamba pesa hizo zimekusanywa kutoka kwenye akaunti za benki za nchini Ghana na kupelekwa Uingereza. Pia alidai kwamba Mfale alimpa $ 200,000 ili ...

SABABU ZA KUVUNJIKA KWA KUNDI LA P-SQUARE.

WANAMUZIKI MAPACHA WA KUNDI LA PSQUARE, PETER (KUSHOTO) NA PAUL (KULIA) WAKIWA NA KAKA YAO AMBAE PIA NI MENEJA WAO, JUDES OKOYE. Mwanamuziki wa kundi la PSquare kutoka Nigeria, Peter Okoye ametangaza kujitoa kwenye kundi hilo la muziki wa Pop maarufu zaidi Afrika. Msanii huyo alidai kwamba amewasilisha maombi ya kuvunja kundi hilo katika barua aliyoandika kwa wakili wao Festus Keyamo. Kulingana na nakala ya barua iliyotolewa kwenye vyombo vya habari Jumatatu,Tarehe 25 Septemba, Peter alisema kuwa pacha wake na, Paul, na kaka yao, Judes waliahirisha ziara yao ya muziki ya Marekani bila kushauriana naye.Na hiyo ni moja kati ya sababu za msingi. Peter pia aliwalaumu Paul na kaka yao mkubwa mkubwa ambae ni meneja wao pia kwa udanganyifu walioufanya ili kutatua shida waliyokuwa nayo juu ya biashara ya muziki. Wasanii hao ndugu wamekua kwenye vita vya maneno kwenye mitandao ya kijamii tangu mwisho wa mwaka jana pamoja na juhudi za watu wao wa karibu kujaribu kuwapatanisha kifami...

ORODHA YA NCHI ZA KWANZA NA ZA MWISHO KWA AMANI DUNIANI.

Marekani:  Ripoti ya Taasisi ya Uchumi na Amani imepata mataifa kumi tu ulimwenguni ambayo hayapo katika vita na migogoro kabisa. Kwa mujibu wa Ripoti ya Kimataifa ya Amani 2016, Botswana, Chile, Costa Rica, Japan, Mauritius, Panama, Qatar, Uswisi, Uruguay na Vietnam ndio nchi pekee ambazo hazipo kwenye vita wala migogoro yeyote ile ya kuhatarisha amani.. Iceland inaongoza orodha ya nchi zinazoongoza kwa amani ulimwenguni, ikifuatiwa na Denmark, Austria, New Zealand, Ureno, Jamhuri ya Czech, Uswisi, Canada, Japan na Slovenia - wakati Marekani ikiwa kwenye nafasi ya 103. Palestina imepanda kutoka nafasi ya 163 mpaka nafasi ya 148. Syria iliyoharibiwa na vita imewekwa chini ya orodha, chini kuliko Sudan Kusini, Iraq, Afghanistan, Somalia, Yemen, Jamhuri ya Afrika ya Kati, Ukraine, Sudan na Libya. "Ripoti inalinganisha amani duniani kwa kutumia mandhari tatu pana: hali ya utulivu na usalama katika jamii; kiwango cha mgogoro wa ndani au wa kimataifa; na kiwango cha kije...