Skip to main content

MADAI YA CUBA KWAMBA WAZIRI MKUU WA CANADA NI MTOTO WA FIDEL CASTRO.

Pichani ni waziri mkuu wa Canada, Justin Trudeau (kushoto), na Rais wa zamani wa Cuba, Hayati Fidel Castro (kulia).


Maelezo yaliyoandikwa na mtoto wa kwanza wa rais wa zamani wa Cuba , Fidel Castro, kabla ya kujiua yamelishtua taifa la Cuba wiki hii.

Maelezo hayo yaliyoandikwa na mtoto huyo mkubwa wa mwanamapinduzi na rais wa zamani wa nchi hiyo yalikuwa ya kushangaza baada ya  kuwa na madai ya kuwa Waziri Mkuu wa Canada Justin Trudeau ni mtoto wa nje wa baba yake marehemu Fidel Castro.


Maelezo hayo yaliyoandikwa kwa mkono na mtoto huyo wa Fidel Castro aliyejiua siku chache zilizopita kwa msongo wa mawazo, Fidel Castro Diaz-Balart, aliyekuwa na umri wa miaka 68, yalionekana kuthibitisha uvumi wa muda mrefu nchini Cuba kwamba Fidel Castro ni baba wa damu wa waziri mkuu wa sasa wa Canada, Justin Trudeau ikiwa ni matokeo ya uhusiano wa siri wa kimapenzi na mke wa mwanasiasa maarufu wa Canada, Pierre Trudeau, Margaret Trudeau mwaka 1970.


Kifo cha mwanasayansi wa nyuklia wa taifa hilo maarufu kama "Fidelito", au Little Fidel(Fidel mdogo) kwa sababu ya kufanana sana na baba yake kimuonekano, kililishangaza taifa hilo kwa maamuzi hayo ya kujiua na maneno aliyoyaacha yamezidi kuwaduwaza wananchi wa Cuba kwa madai hayo kuhusu waziri mkuu wa moja kati ya mataifa makubwa zaidi duniani, Canada.


Katikati ya malalamiko makubwa, maandishi yanasema Fidelito alikasishwa na baba yake marehemu Fidel Castro.
Fidelito aliandika kwamba baba yake, Fidel Castro,
 "alikuwa akinilinganisha mimi na Justin kimafanikio" na "kupuuza mafanikio yangu kwa kuyalinganisha na mafanikio yake(Justin Trudeau) huko Canada. "

"Lakini nilipaswa kufanya nini? Mimi  ni raia wa Cuba. Ndugu yangu ni raia wa Canada. Ikiwa alizaliwa na kukulia Cuba, angekuwa ameishi katika kivuli cha baba yetu milele kama mimi. "


Wakati Justin Trudeau anajulikana sana kama mtoto wa Waziri Mkuu wa zamani wa Canada, Pierre Trudeau, picha za kulinganisha za Pierre, Justin na Fidel zinaonyesha kunaweza kuwa na kitu kwenye madai ya watu wa Cuba.


KWENYE PICHA HIZI, KUSHOTO NI PIERRE TRUDEAU, 
KATIKATI NI JUSTIN TRUDEAU
NA KULIA NI MAREHEMU FIDEL CASTRO:






Mbali na kufanana kimwili madai hayo yanekuwa yakiungwa mkono na ukweli wa kihistoria.

Wakati mahali alipozaliwa Justin Trudeau, Ottawa, nchini Canada kunaweza kuwa mbali kutoka Havana, Cuba, mama yake Margaret Trudeau alitembelea Cuba miezi tisa kabla Justin kuzaliwa, na kuna picha za kujihusisha na Fidel Castro.


Margaret Trudeau na Fidel Castro jijini Havana, Cuba, miezi tisa kabla Justin kuzaliwa.


Kulingana na gazeti la Canada la Globe And Mail, Pierre Trudeau na mkewe Margaret walisafiri kwenda Havana na wakawa marafiki wa karibu na rais wa Cuba.

"Njia za Pierre Trudeau na Fidel Castro zilivuka kwa mara ya kwanza mwaka 1970," inasema ripoti ya Globe, kabla ya kuelezea kuwa wanafamilia hao walikuwa na wakati mzuri sana kwenye kisiwa hicho cha Caribbean kuwa "urafiki wa kudumu kati ya arch-liberal Pierre Trudeau na Marxist-revolutionary Fidel Castro.



Margaret Trudeau pia alirejea Cuba mara tu baada ya Justin kuzaliwa.


Kabla ya kuishagaza Canada kwa kuolewa na Waziri Mkuu wa Canada, mama ya waziri mkuu huyo wa sasa wa Canada ,Margaret alikuwa maarufu katika miaka ya 1970 kwa kashfa za mahusiano ya kimapenzi na watu mbalimbali.


Akiwa kama mtumiaji wa madawa ya kulevya aliyewahi kukiri mwenyewe hadharani, Margaret aliwahi kukamatwa na madawa ya kulevya aliyoweka katika begi la mumewe wakati wakiwa safarini.

Margaret pia na aliwahi kuonekana akiwa amevaa nusu utupu katika ukumbi maarufu wa usiku unaojulikana kama Studio 54, na bado picha hizo zinachapishwa sana kwenye mtandao wa intaneti.


Margaret Trudeau anafahamika sana linapokuja katika kashfa za ngono na wanaume matajiri na wenye madaraka.

Akielezea mahusiano yake ya mwaka 1974 na Ted Kennedy, Margaret Trudeau aliandika katika kumbukumbu yake kuhusu wakati alipokutana na Seneta huyo wa Marekani katika chakula cha jioni nchini New York:

"Hiyo jioni hiyo nilijisikia kuvutiwa nae na sikuweza kukaa karibu na mume wangu kwa mita kadhaa. Pierre(mumewe) hakupendezwa. "


Margaret kisha alihamia kwa mpiga gitaa wa bendi maarufu ya Uingereza ya Rolling Stones 'Ronnie Wood na kisha kuhamia kwa muimbaji wake, Mick Jagger mwaka 1977.


Magazeti ya udaku ya Uingereza yakiwa yamechapisha habari kuhusu kashfa za Margaret Trudeau na wanamuziki wa bendi ya Rolling Stones, mwishoni mwa miaka ya sabini.



Kashfa hiyo ilipelekea ugomvi na mwisho wa ndoa yake na Pierre Trudeau.

Mwanasiasa huyo wa siasa za kiliberali alishinda katika vita ya mahakama kubaki na watoto peke yake, na akakataa kulipa msaada wowote kwa mke.



CHANZO:
yournewswire.

Comments

Habari Nyingine Kutoka Kioo17 Swahili;

ORODHA YA NCHI 80 AMBAZO MTANZANIA ANARUHUSIWA KUINGIA BILA VIZA.

         Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni amesema kuna zaidi ya nchi 80 ambazo watanzania wanaweza kusafiri bila ya kuwa na viza . Mhandisi Hamad Masauni amesema kuna zaidi ya nchi 80 ambazo watanzania wanaweza kusafiri bila ya kuwa na viza za kusafiria kama ilivyokuwa nchi za afrika Mashariki. Mhandisi Massauni amebainisha hayo leo bungeni wakati akijibu swali la Mbunge wa Mlalo kupitia tiketi ya CCM Rashid Shangazi aliyetaka kujua ni nchi ngapi ambazo watanzania wanaweza kusafiri bila ya kuwa na viza (viza on arrival). "Zipo nchi 16 kwa Afrika ambazo watanzania wanaweza kuzitembelea bila ya kuwa na viza na duniani zipo 67" alisema Masauni. Aidha Massauni amezitaja nchi hizo kuwa ni Benin, Burkina Faso, Cape Verde, Ivory Coast, Djibouti, Gabon, Gambia, Guinea, Guinea­Bissau, Liberia, Mali, Mauritania, Niger, Sierra Leone pamoja na Togo. Pamoja na hayo Masauni amesema...

ODINGA NA HASSAN JOHO WALIMTUMIA ALI KIBA NDEGE BINAFSI..

Imebainika kwamba mgombea wa uraisi wa Kenya kupitia muungano wa NASA pamoja na gavana wa Mombasa Hassan Joho walituma ndege binafsi kumchukua muimbaji wa Tanzania Ali Kiba ili kusherekea kutenguliwa kwa matokeo ya uchaguzi wa uraisi nchini humo juma lililopita. Meneja wa Ali Kiba , Aidan Seif, alithibitisha kwamba Odinga alituma ndege hiyo siku ya ijumaa ili Ali Kiba ajumuike nao katika kusherekea. Chanzo kililiambia gazeti la Tanzania kwamba"upinzani wa Kenya unakubali msaada wa Kiba .Muungano wa NASA unaamini Kiba alisaidia sana katika kampeni zao kabla ya uchaguzi mkuu wa Agosti 8. Walituma ndege ya kibinafsi, ambayo ilimchukua mwishoni mwa Ijumaa. " Odinga, Joho na Kiba wanauhusiano wa karibu sana na mara kwa mara Ali Kiba alionekana akiwapigia kampeni wanasiasa hao wa Kenya majukwaani CHANZO: edaily.co.ke

TRUMP NA KIM JONG-UN FEKI WAHUBIRI AMANI KATIKA SHEREHE ZA UZINDUZI WA OLIMPIKI.

Waigaji wa Rais wa Marekani Donald Trump na kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong-un walikua wakihubiri amani katika sherehe za uzinduzi wa michezo ya Olympiki kwa majira ya baridi(Winter Olympic) jijini Pyeong Chang, Korea ya Kaskazini kabla ya kutolewa nje na wanausalama. Watu hao walionekana kwa muda mfupi katika jukwaa la uwanja huo mkuu wa Pyeongchang, Korea Kusini ili kuwasalimu watu. Waigaji hao ambao wote walikataa kutoa majina yao halisi - walikuja kwenye sherehe ya ufunguzi -   "kuonyesha dunia, hii ndio amani inaweza kuonekana kama viongozi hao wawili watakapokutana,"  alisema Kim bandia. Trump bandia alimwiga Rais Trump kwa kuvaa kofia nyekundu ya mpira wa magongo (baseball), lakini ikiwa imeandikwa "USA" sio "Make America Great again"(Unda Amerika Kuu tena) kauli mbiu ambayo mara nyingi huandikwa kwenye mavazi na matangazo ya Trump. Pia alivaa tai ndefu ya rangi nyekundu kama ambavyo rais Trump mwenyewe hupendele...

WAZIRI GEORGE SIMBACHAWENE AJIUZULU.

Waziri wa TAMISEMI George Simbachawene ametangaza kujiuzulu nafasi yake kutokana na kutajwa kwenye ripoti za uchunguzi wa tanzanite na almasi. Akiwasilisha ripoti yake kwa Waziri Mkuu Bungeni Dodoma, Mwenyekiti wa Kamati Maalumu ya Bunge iliyoundwa kuchunguza biashara ya madini ya tanzanite, Dotto Biteko, alisema Simbachawene aulizwe ni kwa nini alitoa uhamisho wa hisa za Sky Associate bila kuhusisha wataalamu kwa sababu kamati ilishindwa kuelewa ni kwa nini alifanya hivyo. “Kwa muktadha huo, ridhaa iliyotolewa Januari 30, mwaka 2015 na aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini wa wakati huo, George Simbachawene, ina dosari za kisheria na ukiukwaji wa kiutendaji na utoaji wa ridhaa hii, unainyima Stamico kipaumbele cha kununua Kampuni ya TML. “Kwa msingi huo, kamati imebaini dosari zilizofanywa za kubadilisha watoa maamuzi wa Kampuni ya TLM, zilifanyiwa kazi katika ngazi ya Wizara ya Nishati na Madini chini ya Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Kamishna wa Nishati na Madini na idara za sher...

ORODHA YA NCHI ZA KWANZA NA ZA MWISHO KWA AMANI DUNIANI.

Marekani:  Ripoti ya Taasisi ya Uchumi na Amani imepata mataifa kumi tu ulimwenguni ambayo hayapo katika vita na migogoro kabisa. Kwa mujibu wa Ripoti ya Kimataifa ya Amani 2016, Botswana, Chile, Costa Rica, Japan, Mauritius, Panama, Qatar, Uswisi, Uruguay na Vietnam ndio nchi pekee ambazo hazipo kwenye vita wala migogoro yeyote ile ya kuhatarisha amani.. Iceland inaongoza orodha ya nchi zinazoongoza kwa amani ulimwenguni, ikifuatiwa na Denmark, Austria, New Zealand, Ureno, Jamhuri ya Czech, Uswisi, Canada, Japan na Slovenia - wakati Marekani ikiwa kwenye nafasi ya 103. Palestina imepanda kutoka nafasi ya 163 mpaka nafasi ya 148. Syria iliyoharibiwa na vita imewekwa chini ya orodha, chini kuliko Sudan Kusini, Iraq, Afghanistan, Somalia, Yemen, Jamhuri ya Afrika ya Kati, Ukraine, Sudan na Libya. "Ripoti inalinganisha amani duniani kwa kutumia mandhari tatu pana: hali ya utulivu na usalama katika jamii; kiwango cha mgogoro wa ndani au wa kimataifa; na kiwango cha kije...

"GIGGS HAFAI KUWA KOCHA WA TIMU YA TAIFA", BABA YAKE ANASEMA...!!!

Ryan Giggs. Chama cha Soka cha Wales (FAW) siku ya jumatatu kilitangaza kumchagua winga wa zamani wa Manchester United Ryan Giggs kama kocha wa timu yao ya taifa kwa mkataba wa miaka minne. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 44 anachukua kazi iyoachwa na Chris Coleman, ambaye aliiongoza Wales kwenye nusu fainali za Euro 2016 lakini aliacha kazi mwezi Novemba ili kuchukua nafasi ya kuifundisha timu ya Sunderland ya ligi kuu ya Uingereza. Giggs alisema kuwa anajivunia kwa kupewa kazi hiyo na pamoja na changamoto iliyo mbele yake baada ya Wales kushindwa kufuzu kucheza fainali za Kombe la Dunia mwaka huu nchini Urusi na sasa wanazingatia michuano ya Ulaya ya 2020. "Siwezi kusubiri kuanza kufanya kazi na wachezaji tunapojiandaa kwa ajili ya michezo muhimu baadaye mwaka huu," alisema. Lakini baba mzazi wa Giggs, Danny Wilson ana maoni  tofauti sana...!!! Anakiri kwamba mwanae anamtia aibu na anasema hastahili kuchukua kazi hiyo ya ukocha wa timu ya t...

MCHEZAJI WA ZAMANI WA UINGEREZA AMESEMA ALICHEZA NA WACHEZAJI WATATU MASHOGA KWENYE TIMU.

Carl Hoefkens (jezi no.2) alichezea West Bromwich Albion na Stoke City wakati wa enzi zake ligi kuu ya England. Beki wa zamani wa Ligi Kuu ya Uingereza amesema alicheza pamoja na wachezaji wenzake wawili wa mashoga ndani ya timu, na mmoja alikua na jina kubwa. Carl Hoefkens, West Bromwich Albion na Stoke City siku za nyuma, anasema wachezaji hao walikua wazi na hawakujificha kwenye vyumba vya kubadilishia nguo ingawa bado hawajulikani kwasababu ya maombi yao wenyewe ya kuomba kutotangazwa. Justin Fashanu, ambaye alijiua mwaka 1998, alikuwa mchezaji wa mwisho wa kazi nchini England kuja nje kama mashoga - mwaka 1990. Hoefkens alipokua (kushoto), alipokua anachezea Stock  City. Hoefkens aliyecheza Uingereza kwa miaka minne, akiondoka mwaka 2009, alidai kuwa mchezaji mwenzake mmoja wa timu alikua anaweza kuja kwenye uwanja wa mafunzo ya klabu na mpenzi wake wa kiume  lakini aliwaomba wenzake kutokuwaambia watu wangine wa nje ya timu. 'Nilicheza pamoja n...