Skip to main content

MADAI YA CUBA KWAMBA WAZIRI MKUU WA CANADA NI MTOTO WA FIDEL CASTRO.

Pichani ni waziri mkuu wa Canada, Justin Trudeau (kushoto), na Rais wa zamani wa Cuba, Hayati Fidel Castro (kulia).


Maelezo yaliyoandikwa na mtoto wa kwanza wa rais wa zamani wa Cuba , Fidel Castro, kabla ya kujiua yamelishtua taifa la Cuba wiki hii.

Maelezo hayo yaliyoandikwa na mtoto huyo mkubwa wa mwanamapinduzi na rais wa zamani wa nchi hiyo yalikuwa ya kushangaza baada ya  kuwa na madai ya kuwa Waziri Mkuu wa Canada Justin Trudeau ni mtoto wa nje wa baba yake marehemu Fidel Castro.


Maelezo hayo yaliyoandikwa kwa mkono na mtoto huyo wa Fidel Castro aliyejiua siku chache zilizopita kwa msongo wa mawazo, Fidel Castro Diaz-Balart, aliyekuwa na umri wa miaka 68, yalionekana kuthibitisha uvumi wa muda mrefu nchini Cuba kwamba Fidel Castro ni baba wa damu wa waziri mkuu wa sasa wa Canada, Justin Trudeau ikiwa ni matokeo ya uhusiano wa siri wa kimapenzi na mke wa mwanasiasa maarufu wa Canada, Pierre Trudeau, Margaret Trudeau mwaka 1970.


Kifo cha mwanasayansi wa nyuklia wa taifa hilo maarufu kama "Fidelito", au Little Fidel(Fidel mdogo) kwa sababu ya kufanana sana na baba yake kimuonekano, kililishangaza taifa hilo kwa maamuzi hayo ya kujiua na maneno aliyoyaacha yamezidi kuwaduwaza wananchi wa Cuba kwa madai hayo kuhusu waziri mkuu wa moja kati ya mataifa makubwa zaidi duniani, Canada.


Katikati ya malalamiko makubwa, maandishi yanasema Fidelito alikasishwa na baba yake marehemu Fidel Castro.
Fidelito aliandika kwamba baba yake, Fidel Castro,
 "alikuwa akinilinganisha mimi na Justin kimafanikio" na "kupuuza mafanikio yangu kwa kuyalinganisha na mafanikio yake(Justin Trudeau) huko Canada. "

"Lakini nilipaswa kufanya nini? Mimi  ni raia wa Cuba. Ndugu yangu ni raia wa Canada. Ikiwa alizaliwa na kukulia Cuba, angekuwa ameishi katika kivuli cha baba yetu milele kama mimi. "


Wakati Justin Trudeau anajulikana sana kama mtoto wa Waziri Mkuu wa zamani wa Canada, Pierre Trudeau, picha za kulinganisha za Pierre, Justin na Fidel zinaonyesha kunaweza kuwa na kitu kwenye madai ya watu wa Cuba.


KWENYE PICHA HIZI, KUSHOTO NI PIERRE TRUDEAU, 
KATIKATI NI JUSTIN TRUDEAU
NA KULIA NI MAREHEMU FIDEL CASTRO:






Mbali na kufanana kimwili madai hayo yanekuwa yakiungwa mkono na ukweli wa kihistoria.

Wakati mahali alipozaliwa Justin Trudeau, Ottawa, nchini Canada kunaweza kuwa mbali kutoka Havana, Cuba, mama yake Margaret Trudeau alitembelea Cuba miezi tisa kabla Justin kuzaliwa, na kuna picha za kujihusisha na Fidel Castro.


Margaret Trudeau na Fidel Castro jijini Havana, Cuba, miezi tisa kabla Justin kuzaliwa.


Kulingana na gazeti la Canada la Globe And Mail, Pierre Trudeau na mkewe Margaret walisafiri kwenda Havana na wakawa marafiki wa karibu na rais wa Cuba.

"Njia za Pierre Trudeau na Fidel Castro zilivuka kwa mara ya kwanza mwaka 1970," inasema ripoti ya Globe, kabla ya kuelezea kuwa wanafamilia hao walikuwa na wakati mzuri sana kwenye kisiwa hicho cha Caribbean kuwa "urafiki wa kudumu kati ya arch-liberal Pierre Trudeau na Marxist-revolutionary Fidel Castro.



Margaret Trudeau pia alirejea Cuba mara tu baada ya Justin kuzaliwa.


Kabla ya kuishagaza Canada kwa kuolewa na Waziri Mkuu wa Canada, mama ya waziri mkuu huyo wa sasa wa Canada ,Margaret alikuwa maarufu katika miaka ya 1970 kwa kashfa za mahusiano ya kimapenzi na watu mbalimbali.


Akiwa kama mtumiaji wa madawa ya kulevya aliyewahi kukiri mwenyewe hadharani, Margaret aliwahi kukamatwa na madawa ya kulevya aliyoweka katika begi la mumewe wakati wakiwa safarini.

Margaret pia na aliwahi kuonekana akiwa amevaa nusu utupu katika ukumbi maarufu wa usiku unaojulikana kama Studio 54, na bado picha hizo zinachapishwa sana kwenye mtandao wa intaneti.


Margaret Trudeau anafahamika sana linapokuja katika kashfa za ngono na wanaume matajiri na wenye madaraka.

Akielezea mahusiano yake ya mwaka 1974 na Ted Kennedy, Margaret Trudeau aliandika katika kumbukumbu yake kuhusu wakati alipokutana na Seneta huyo wa Marekani katika chakula cha jioni nchini New York:

"Hiyo jioni hiyo nilijisikia kuvutiwa nae na sikuweza kukaa karibu na mume wangu kwa mita kadhaa. Pierre(mumewe) hakupendezwa. "


Margaret kisha alihamia kwa mpiga gitaa wa bendi maarufu ya Uingereza ya Rolling Stones 'Ronnie Wood na kisha kuhamia kwa muimbaji wake, Mick Jagger mwaka 1977.


Magazeti ya udaku ya Uingereza yakiwa yamechapisha habari kuhusu kashfa za Margaret Trudeau na wanamuziki wa bendi ya Rolling Stones, mwishoni mwa miaka ya sabini.



Kashfa hiyo ilipelekea ugomvi na mwisho wa ndoa yake na Pierre Trudeau.

Mwanasiasa huyo wa siasa za kiliberali alishinda katika vita ya mahakama kubaki na watoto peke yake, na akakataa kulipa msaada wowote kwa mke.



CHANZO:
yournewswire.

Comments

Habari Nyingine Kutoka Kioo17 Swahili;

JAGUAR KUACHIA WIMBO BAADA YA KUAPISHWA MBUNGE.

Mbunge wa Starehe, Kenya, "Jaguar" anajipanga kutoa wimbo mpya mara tu baada ya kuapishwa kua mbunge. Katika chapisho lake la kwenye akaunti yake ya mtandao wa kijamii, Jaguar aliupendekeza wimbo wake wa "Ndoto" kama salamu kwa Wakenya na watu walio nje ya Kenya. Charles Njagua, ambae ni maarufu kwa jina la Jaguar, ana Aliahidi mashabiki wimbo mpya baada ya kuapa rasmi kama mbunge.  Mimbaji huyo ambaye ametoa hits kadhaa lakini sasa anazingatia siasa baada ya kushinda kiti, aliwaambia mashabiki kwenye vyombo vya habari vya kijamii kwamba wimbo mpya, unaitwa "Ndoto", uko tayari na utaachiliwa haraka baada ya kuapa. "Sasa ni karibu miongo miwili tangu mimi kuweka mguu katika studio ya kurekodi,   alisema Jaguar katika chapisho lake. CHANZO: www.tuko.news

KASHFA YA MAPENZI KATI MH.MBOWE NA WEMA SEPETU.

MH.FREEMAN MBOWE AKIWA NA WEMA SEPETU. Siku chache baada ya ile skendo ya ngono iliyosababisha wakili na mshauri wa Chama cha ACT -Wazalendo , Bwana Albert Msando kujiuzulu kwenye nyadhifa yake ya chama ,yameibuka mangine kwenye chama kikuu cha upinzani Tanzania ,CHADEMA ,baada ya kusambaa kwa kipande cha sauti kinachodaiwa kua ni mazungumzo kati ya mwenyekiti wa chama hicho na mbunge wa Hai Mh.Freeman Mbowe na Miss Tanzania 2006 ,mrembo Wema Isack Sepetu. SIKILIZA HIVI VIPANDE VYA SAUTI: Bonyeza hapa chini kusikiliza maongezi hayo yanayodaiwa kuwa ni kati ya Wema Sepetu na Mh.Freeman Mbowe; Bonyeza hapa chini kusikiliza majibu ya Wema Sepetu; Bonyeza hapa chini kusikiliza majibu ya Mh.Freeman Mbowe; VYANZO: Jamii Forums,                   YouTube.com,                   Perfect255.com.                   

ORODHA YA NCHI ZA KWANZA NA ZA MWISHO KWA AMANI DUNIANI.

Marekani:  Ripoti ya Taasisi ya Uchumi na Amani imepata mataifa kumi tu ulimwenguni ambayo hayapo katika vita na migogoro kabisa. Kwa mujibu wa Ripoti ya Kimataifa ya Amani 2016, Botswana, Chile, Costa Rica, Japan, Mauritius, Panama, Qatar, Uswisi, Uruguay na Vietnam ndio nchi pekee ambazo hazipo kwenye vita wala migogoro yeyote ile ya kuhatarisha amani.. Iceland inaongoza orodha ya nchi zinazoongoza kwa amani ulimwenguni, ikifuatiwa na Denmark, Austria, New Zealand, Ureno, Jamhuri ya Czech, Uswisi, Canada, Japan na Slovenia - wakati Marekani ikiwa kwenye nafasi ya 103. Palestina imepanda kutoka nafasi ya 163 mpaka nafasi ya 148. Syria iliyoharibiwa na vita imewekwa chini ya orodha, chini kuliko Sudan Kusini, Iraq, Afghanistan, Somalia, Yemen, Jamhuri ya Afrika ya Kati, Ukraine, Sudan na Libya. "Ripoti inalinganisha amani duniani kwa kutumia mandhari tatu pana: hali ya utulivu na usalama katika jamii; kiwango cha mgogoro wa ndani au wa kimataifa; na kiwango cha kije...

"GIGGS HAFAI KUWA KOCHA WA TIMU YA TAIFA", BABA YAKE ANASEMA...!!!

Ryan Giggs. Chama cha Soka cha Wales (FAW) siku ya jumatatu kilitangaza kumchagua winga wa zamani wa Manchester United Ryan Giggs kama kocha wa timu yao ya taifa kwa mkataba wa miaka minne. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 44 anachukua kazi iyoachwa na Chris Coleman, ambaye aliiongoza Wales kwenye nusu fainali za Euro 2016 lakini aliacha kazi mwezi Novemba ili kuchukua nafasi ya kuifundisha timu ya Sunderland ya ligi kuu ya Uingereza. Giggs alisema kuwa anajivunia kwa kupewa kazi hiyo na pamoja na changamoto iliyo mbele yake baada ya Wales kushindwa kufuzu kucheza fainali za Kombe la Dunia mwaka huu nchini Urusi na sasa wanazingatia michuano ya Ulaya ya 2020. "Siwezi kusubiri kuanza kufanya kazi na wachezaji tunapojiandaa kwa ajili ya michezo muhimu baadaye mwaka huu," alisema. Lakini baba mzazi wa Giggs, Danny Wilson ana maoni  tofauti sana...!!! Anakiri kwamba mwanae anamtia aibu na anasema hastahili kuchukua kazi hiyo ya ukocha wa timu ya t...

MCHEZAJI WA ZAMANI WA UINGEREZA AMESEMA ALICHEZA NA WACHEZAJI WATATU MASHOGA KWENYE TIMU.

Carl Hoefkens (jezi no.2) alichezea West Bromwich Albion na Stoke City wakati wa enzi zake ligi kuu ya England. Beki wa zamani wa Ligi Kuu ya Uingereza amesema alicheza pamoja na wachezaji wenzake wawili wa mashoga ndani ya timu, na mmoja alikua na jina kubwa. Carl Hoefkens, West Bromwich Albion na Stoke City siku za nyuma, anasema wachezaji hao walikua wazi na hawakujificha kwenye vyumba vya kubadilishia nguo ingawa bado hawajulikani kwasababu ya maombi yao wenyewe ya kuomba kutotangazwa. Justin Fashanu, ambaye alijiua mwaka 1998, alikuwa mchezaji wa mwisho wa kazi nchini England kuja nje kama mashoga - mwaka 1990. Hoefkens alipokua (kushoto), alipokua anachezea Stock  City. Hoefkens aliyecheza Uingereza kwa miaka minne, akiondoka mwaka 2009, alidai kuwa mchezaji mwenzake mmoja wa timu alikua anaweza kuja kwenye uwanja wa mafunzo ya klabu na mpenzi wake wa kiume  lakini aliwaomba wenzake kutokuwaambia watu wangine wa nje ya timu. 'Nilicheza pamoja n...

TUPAC SHAKUR ALIBAKWA JELA !!!

             Ulimwengu wa filamu za Hollywood na muziki wa Hip Hop juzi ulipatwa na mshangao baada ya mtayarishaji wa filamu inayohusu maisha ya hayati Tupac Shakur ,L.T Hutton kuelezea sababu zilizomfanya kumbadilisha muongozaji wa filamu hiyo kutoka John Singleton na kumuweka muongozaji Benny "Boom" Douglas.  Filamu hiyo inayoitwa "all eyez on me" tayari imekwisha andaliwa na inatarajiwa kuzinduliwa leo tarehe 16 Juni 2017.       Akizungumza kwenye mahojiano redioni L.T Hutton amewashtusha watu wengi baada ya kudai kwamba walishindwana na muongozaji wa mwanzo bwana John Singleton sababu muongozaji huyo aling'ang'ania kuwepo kwa matukio (scene) ambazo kwa maoni yake zisingependeza.        Matukio ambayo John Singleton alipenda yawepo katika filamu hiyo ni pamoja na kutaka filamu hiyo ianze na scene ya Tupac akilazimisha kumlawiti msichana wa kizungu.!!!          Singleton pia ali...

MOHAMMED DEWJI NA BILL GATES KUTOA NUSU YA UTAJIRI WAO...!!!

MOHAMMED DEWJI AKIWA NA BILL GATES. Mfanyabiashara tajiri namba moja Tanzania (kwa mujibu wa jarida la Forbes) na mmiliki wa makampuni ya METL , Mohammed "Mo" Dewji ,wiki chache zilizopita amekua mmoja wa mabilionea 14 wapya kujiunga katika mpango wa kuchangia misaada kwa jamii uitwao "Giving Pledge".                 Mpango huo ulioanzishwa na familia ya mfanyabiashara tajiri namba moja duniani (kwa mujibu wa jarida la Forbes) na mmiliki wa kampuni ya Microsoft Bill Gates pamoja na rafiki yake bilionea Warren Buffet mwaka 2010, ulikua na tayari umeshaungwa mkono na mabilionea 154 mpaka mwanzo wa mwaka huu (2017). WAASISI WA "GIVIN PLEDGE",WARREN BUFFET, MELINDA GATES NA BILL GATES.         Mohammed Dewji anakua mmoja kati ya matajiri wachache sana kutoka Afrika kama Patrice Motsepe (Afrika Kusini) na Mo Ibrahim (Sudan) kujiunga na kampeni hiyo ambayo nia yake kubwa ni kushawishi watu matajiri kutoa angalau nu...