Skip to main content

MADAI YA CUBA KWAMBA WAZIRI MKUU WA CANADA NI MTOTO WA FIDEL CASTRO.

Pichani ni waziri mkuu wa Canada, Justin Trudeau (kushoto), na Rais wa zamani wa Cuba, Hayati Fidel Castro (kulia).


Maelezo yaliyoandikwa na mtoto wa kwanza wa rais wa zamani wa Cuba , Fidel Castro, kabla ya kujiua yamelishtua taifa la Cuba wiki hii.

Maelezo hayo yaliyoandikwa na mtoto huyo mkubwa wa mwanamapinduzi na rais wa zamani wa nchi hiyo yalikuwa ya kushangaza baada ya  kuwa na madai ya kuwa Waziri Mkuu wa Canada Justin Trudeau ni mtoto wa nje wa baba yake marehemu Fidel Castro.


Maelezo hayo yaliyoandikwa kwa mkono na mtoto huyo wa Fidel Castro aliyejiua siku chache zilizopita kwa msongo wa mawazo, Fidel Castro Diaz-Balart, aliyekuwa na umri wa miaka 68, yalionekana kuthibitisha uvumi wa muda mrefu nchini Cuba kwamba Fidel Castro ni baba wa damu wa waziri mkuu wa sasa wa Canada, Justin Trudeau ikiwa ni matokeo ya uhusiano wa siri wa kimapenzi na mke wa mwanasiasa maarufu wa Canada, Pierre Trudeau, Margaret Trudeau mwaka 1970.


Kifo cha mwanasayansi wa nyuklia wa taifa hilo maarufu kama "Fidelito", au Little Fidel(Fidel mdogo) kwa sababu ya kufanana sana na baba yake kimuonekano, kililishangaza taifa hilo kwa maamuzi hayo ya kujiua na maneno aliyoyaacha yamezidi kuwaduwaza wananchi wa Cuba kwa madai hayo kuhusu waziri mkuu wa moja kati ya mataifa makubwa zaidi duniani, Canada.


Katikati ya malalamiko makubwa, maandishi yanasema Fidelito alikasishwa na baba yake marehemu Fidel Castro.
Fidelito aliandika kwamba baba yake, Fidel Castro,
 "alikuwa akinilinganisha mimi na Justin kimafanikio" na "kupuuza mafanikio yangu kwa kuyalinganisha na mafanikio yake(Justin Trudeau) huko Canada. "

"Lakini nilipaswa kufanya nini? Mimi  ni raia wa Cuba. Ndugu yangu ni raia wa Canada. Ikiwa alizaliwa na kukulia Cuba, angekuwa ameishi katika kivuli cha baba yetu milele kama mimi. "


Wakati Justin Trudeau anajulikana sana kama mtoto wa Waziri Mkuu wa zamani wa Canada, Pierre Trudeau, picha za kulinganisha za Pierre, Justin na Fidel zinaonyesha kunaweza kuwa na kitu kwenye madai ya watu wa Cuba.


KWENYE PICHA HIZI, KUSHOTO NI PIERRE TRUDEAU, 
KATIKATI NI JUSTIN TRUDEAU
NA KULIA NI MAREHEMU FIDEL CASTRO:






Mbali na kufanana kimwili madai hayo yanekuwa yakiungwa mkono na ukweli wa kihistoria.

Wakati mahali alipozaliwa Justin Trudeau, Ottawa, nchini Canada kunaweza kuwa mbali kutoka Havana, Cuba, mama yake Margaret Trudeau alitembelea Cuba miezi tisa kabla Justin kuzaliwa, na kuna picha za kujihusisha na Fidel Castro.


Margaret Trudeau na Fidel Castro jijini Havana, Cuba, miezi tisa kabla Justin kuzaliwa.


Kulingana na gazeti la Canada la Globe And Mail, Pierre Trudeau na mkewe Margaret walisafiri kwenda Havana na wakawa marafiki wa karibu na rais wa Cuba.

"Njia za Pierre Trudeau na Fidel Castro zilivuka kwa mara ya kwanza mwaka 1970," inasema ripoti ya Globe, kabla ya kuelezea kuwa wanafamilia hao walikuwa na wakati mzuri sana kwenye kisiwa hicho cha Caribbean kuwa "urafiki wa kudumu kati ya arch-liberal Pierre Trudeau na Marxist-revolutionary Fidel Castro.



Margaret Trudeau pia alirejea Cuba mara tu baada ya Justin kuzaliwa.


Kabla ya kuishagaza Canada kwa kuolewa na Waziri Mkuu wa Canada, mama ya waziri mkuu huyo wa sasa wa Canada ,Margaret alikuwa maarufu katika miaka ya 1970 kwa kashfa za mahusiano ya kimapenzi na watu mbalimbali.


Akiwa kama mtumiaji wa madawa ya kulevya aliyewahi kukiri mwenyewe hadharani, Margaret aliwahi kukamatwa na madawa ya kulevya aliyoweka katika begi la mumewe wakati wakiwa safarini.

Margaret pia na aliwahi kuonekana akiwa amevaa nusu utupu katika ukumbi maarufu wa usiku unaojulikana kama Studio 54, na bado picha hizo zinachapishwa sana kwenye mtandao wa intaneti.


Margaret Trudeau anafahamika sana linapokuja katika kashfa za ngono na wanaume matajiri na wenye madaraka.

Akielezea mahusiano yake ya mwaka 1974 na Ted Kennedy, Margaret Trudeau aliandika katika kumbukumbu yake kuhusu wakati alipokutana na Seneta huyo wa Marekani katika chakula cha jioni nchini New York:

"Hiyo jioni hiyo nilijisikia kuvutiwa nae na sikuweza kukaa karibu na mume wangu kwa mita kadhaa. Pierre(mumewe) hakupendezwa. "


Margaret kisha alihamia kwa mpiga gitaa wa bendi maarufu ya Uingereza ya Rolling Stones 'Ronnie Wood na kisha kuhamia kwa muimbaji wake, Mick Jagger mwaka 1977.


Magazeti ya udaku ya Uingereza yakiwa yamechapisha habari kuhusu kashfa za Margaret Trudeau na wanamuziki wa bendi ya Rolling Stones, mwishoni mwa miaka ya sabini.



Kashfa hiyo ilipelekea ugomvi na mwisho wa ndoa yake na Pierre Trudeau.

Mwanasiasa huyo wa siasa za kiliberali alishinda katika vita ya mahakama kubaki na watoto peke yake, na akakataa kulipa msaada wowote kwa mke.



CHANZO:
yournewswire.

Comments

Habari Nyingine Kutoka Kioo17 Swahili;

ORODHA YA NCHI 80 AMBAZO MTANZANIA ANARUHUSIWA KUINGIA BILA VIZA.

         Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni amesema kuna zaidi ya nchi 80 ambazo watanzania wanaweza kusafiri bila ya kuwa na viza . Mhandisi Hamad Masauni amesema kuna zaidi ya nchi 80 ambazo watanzania wanaweza kusafiri bila ya kuwa na viza za kusafiria kama ilivyokuwa nchi za afrika Mashariki. Mhandisi Massauni amebainisha hayo leo bungeni wakati akijibu swali la Mbunge wa Mlalo kupitia tiketi ya CCM Rashid Shangazi aliyetaka kujua ni nchi ngapi ambazo watanzania wanaweza kusafiri bila ya kuwa na viza (viza on arrival). "Zipo nchi 16 kwa Afrika ambazo watanzania wanaweza kuzitembelea bila ya kuwa na viza na duniani zipo 67" alisema Masauni. Aidha Massauni amezitaja nchi hizo kuwa ni Benin, Burkina Faso, Cape Verde, Ivory Coast, Djibouti, Gabon, Gambia, Guinea, Guinea­Bissau, Liberia, Mali, Mauritania, Niger, Sierra Leone pamoja na Togo. Pamoja na hayo Masauni amesema...

USWISI KURUDISHA DOLA MILIONI 321($321M) ZA WIZI KWA NIGERIA.

Serikali ya Nigeria imechukua zaidi ya dola bilioni 1 zilizoaminiwa kuibwa na Rais wa zamani Sani Abacha. CNN: Serikali ya Uswisi kurudisha dola za kimarekani milioni 321 nchini Nigeria ambazo zilikuwa zimechukuliwa kutoka kwenye familia ya Rais wa zamani wa nchi hiyo, Sani Abacha. Mali hizo zilifanywa kama sehemu ya kesi za jinai dhidi ya Abba Abacha, mwana wa Sani, ambaye alitawala Nigeria kwa miaka mitano mpaka kufa kwake mwaka 1998. Wachunguzi wa Nigeria wanaamini rais huyo wa zamani aliiba zaidi ya dola bilioni 4 ($4 Billion) muda wake katika ofisi. Serikali ya Uswisi ilitoa tamko Jumatatu kutangaza makubaliano hayo yaliyofikiwa na viongozi kutoka serikali ya Nigeria na Benki ya Dunia kwa marekebisho. "Marejesho ya fedha yatatokea katika mfumo wa mradi unaoungwa mkono na kusimamiwa na Benki ya Dunia," ,  ilisema taarifa hiyo. "Mradi utaimarisha usalama wa kijamii kwa sehemu maskini zaidi ya idadi ya watu wa Nigeria." Serikali ya Nigeria ilit...

SABABU ZA KUVUNJIKA KWA KUNDI LA P-SQUARE.

WANAMUZIKI MAPACHA WA KUNDI LA PSQUARE, PETER (KUSHOTO) NA PAUL (KULIA) WAKIWA NA KAKA YAO AMBAE PIA NI MENEJA WAO, JUDES OKOYE. Mwanamuziki wa kundi la PSquare kutoka Nigeria, Peter Okoye ametangaza kujitoa kwenye kundi hilo la muziki wa Pop maarufu zaidi Afrika. Msanii huyo alidai kwamba amewasilisha maombi ya kuvunja kundi hilo katika barua aliyoandika kwa wakili wao Festus Keyamo. Kulingana na nakala ya barua iliyotolewa kwenye vyombo vya habari Jumatatu,Tarehe 25 Septemba, Peter alisema kuwa pacha wake na, Paul, na kaka yao, Judes waliahirisha ziara yao ya muziki ya Marekani bila kushauriana naye.Na hiyo ni moja kati ya sababu za msingi. Peter pia aliwalaumu Paul na kaka yao mkubwa mkubwa ambae ni meneja wao pia kwa udanganyifu walioufanya ili kutatua shida waliyokuwa nayo juu ya biashara ya muziki. Wasanii hao ndugu wamekua kwenye vita vya maneno kwenye mitandao ya kijamii tangu mwisho wa mwaka jana pamoja na juhudi za watu wao wa karibu kujaribu kuwapatanisha kifami...

TUPAC SHAKUR ALIBAKWA JELA !!!

             Ulimwengu wa filamu za Hollywood na muziki wa Hip Hop juzi ulipatwa na mshangao baada ya mtayarishaji wa filamu inayohusu maisha ya hayati Tupac Shakur ,L.T Hutton kuelezea sababu zilizomfanya kumbadilisha muongozaji wa filamu hiyo kutoka John Singleton na kumuweka muongozaji Benny "Boom" Douglas.  Filamu hiyo inayoitwa "all eyez on me" tayari imekwisha andaliwa na inatarajiwa kuzinduliwa leo tarehe 16 Juni 2017.       Akizungumza kwenye mahojiano redioni L.T Hutton amewashtusha watu wengi baada ya kudai kwamba walishindwana na muongozaji wa mwanzo bwana John Singleton sababu muongozaji huyo aling'ang'ania kuwepo kwa matukio (scene) ambazo kwa maoni yake zisingependeza.        Matukio ambayo John Singleton alipenda yawepo katika filamu hiyo ni pamoja na kutaka filamu hiyo ianze na scene ya Tupac akilazimisha kumlawiti msichana wa kizungu.!!!          Singleton pia ali...

ALICHOANDIKA MH.NGELEJA BAADA YA KURUDISHA FEDHA ZA ESCROW.

MH.WILLIAM NGELEJA .            Waziri wa zamani wa Nishati na Madini na Mbunge wa Jimbo la Sengerema, William Ngeleja amerejesha rasmi Serikalini fedha alizozipata katika mgao wa Escrow ambazo ni kiasi cha Shilingi Milioni 40.4 ili kukwepa kuendelea kuandamwa na kashfa.        Ngeleja amesema ingawa alipewa fedha hizo kama sehemu ya msaada , ameamua kurudisha fedha hizo ili kukwepa kashfa hiyo ya ESCROW.     SOMA HAPA BARUA ALIYOITOA KWA WAANDISHI WA HABARI ;

MCHEZAJI WA ZAMANI WA UINGEREZA AMESEMA ALICHEZA NA WACHEZAJI WATATU MASHOGA KWENYE TIMU.

Carl Hoefkens (jezi no.2) alichezea West Bromwich Albion na Stoke City wakati wa enzi zake ligi kuu ya England. Beki wa zamani wa Ligi Kuu ya Uingereza amesema alicheza pamoja na wachezaji wenzake wawili wa mashoga ndani ya timu, na mmoja alikua na jina kubwa. Carl Hoefkens, West Bromwich Albion na Stoke City siku za nyuma, anasema wachezaji hao walikua wazi na hawakujificha kwenye vyumba vya kubadilishia nguo ingawa bado hawajulikani kwasababu ya maombi yao wenyewe ya kuomba kutotangazwa. Justin Fashanu, ambaye alijiua mwaka 1998, alikuwa mchezaji wa mwisho wa kazi nchini England kuja nje kama mashoga - mwaka 1990. Hoefkens alipokua (kushoto), alipokua anachezea Stock  City. Hoefkens aliyecheza Uingereza kwa miaka minne, akiondoka mwaka 2009, alidai kuwa mchezaji mwenzake mmoja wa timu alikua anaweza kuja kwenye uwanja wa mafunzo ya klabu na mpenzi wake wa kiume  lakini aliwaomba wenzake kutokuwaambia watu wangine wa nje ya timu. 'Nilicheza pamoja n...

ALICHOSEMA SHEIKH PONDA KUHUSU MIILI INAYOOKOTWA BAHARINI.

SHEIKH PONDA. KUTOKA GAZETI LA NIPASHE ,22 Agosti 2017; Akizungumza na Nipashe kwa simu jana, Sheikh Ponda ambaye pia ni Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Taasisi za Kiislamu Tanzania, alisema kwa muda mrefu wamekuwa wakipaza sauti kuhusu uwapo wa mauaji ya raia kwenye mikoa ya kusini mwa Tanzania, lakini haijasikilizwa. "Tunapongeza Nipashe kwa habari hii," alisema Sheikh Ponda kwa sababu "imefichua mambo mengi.", "Haya tumeshayasema lakini hakuna aliyetusikiliza. "Ni wakati mwafaka serikali ikatoa tamko kwa vile vyombo vya dola vimeonyesha kushindwa kueleza miili hiyo ni ya watu gani na inatoka wapi, (na kibaya) zaidi wanasema wanatambua miili mitatu iliyookotwa ambayo kwa sasa iko Muhimbili." Kaimu Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Lucas Mkondya, aliiambia Nipashe kwa njia ya simu juzi kuwa miili iliyookotwa ni mitatu na haikuwa kwenye viroba. Sheikh Ponda alisema mauaji hayo ni makubwa na hayajawahi kutokea kwa serikali z...