Skip to main content

SABABU YA SOKO LA NYAMA YA MBWA KUONGEZEKA NCHINI CHINA.



Kila mwaka wakati wa msimu wa majira ya joto, tamasha la kula mbwa linafanyika Yulin, jiji lililo katika jimbo la kusini mwa China la Guangxi. 
Tukio la mwaka jana lilimalizika na utata usio wa kawaida. Picha za mbwa wakichinjwa kikatili na kukaangwa zilisababisha gumzo kubwa ulimwenguni kote.

Tamasha la Nyama ya Mbwa la Jinhua Hutou, kama linavyoitwa, lilifungwa ghafla wiki chache zilizopita.


Wanaharakati wa haki za wanyama na wabunge wa Marekani walitaka Uchina kupiga marufuku kula na mbwa na paka, kama vile Taiwan alivyofanya mwaka 2017. 

Serikali za mitaa za Yulin zilichukua hatua za kuzuia na kuficha baadhi ya shughuli za baadhi ya shughuli hizo kama vile kuuza mbwa katika masoko ya chakula. 
Hata hivyo, tamasha hilo lilifanyika na kufana zaidi ya miaka mingine. 

Kwa nini tabia hii isiyo ya kawaida kwa nchi nyingine imekuwa maarufu sana nchini China?




Nyama ya mbwa haijawahi kuwa kitu cha kawaida katika chakula cha Kichina.

Tofauti na sehemu nyingine ulimwenguni, kula nyama ya mbwa hakujawahi kuwa haramu, lakini tabia hiyo inaoneka kuwa sio maarufu katika siku za nyuma ukilinganisha na sasa.


Kwa mujibu wa Guo Peng kutoka Chuo Kikuu cha Shandong, mmoja kati ya watu wachache ambao walifanya utafiti kuhusu soko la nyama ya mbwa, ni Wachina wachache wenye asili ya Kikorea hula mbwa karibu kila siku kama chakula cha kawaida.
Anasema idadi kubwa ya watu wa kabila kubwa la Han, wanaiona kama chakula cha dawa, ambacho kinaaminika kuupa mwili joto kwa wakati wa majira ya baridi na kuupa mwili baridi wakati wa majira ya joto.

Bio Guo anasema, watu wengi wamekula mbwa agalau mara moja kwa mwaka, ikiwa ni sawa.

Kulingana na utafiti uliofanywa mwaka 2016 na Dataway Horizon, kampuni ya kupigia kura, na Shirika la Ustawi wa Wanyama wa Mifugo, Shirika lisilo la kiserikali la China, karibu asilimia 70 ya watu wa China wanasema hawajawahi kula mbwa. Kati yao, wengi wanasema walifanya hivyo kwa ajali wakati walipo alikwa kwenye chakula cha jioni au kwenye mikusanyiko mingine ya kijamii kama sherehe na kadharika.


Kwa nini tamasha la Yulin limejaa? Na kwa nini migahawa katika miji mingi hujaribu kuweka mbwa kwenye orodha? Jibu ni neno moja ni: uhalifu.
Nyama ya mbwa, kama vile madawa ya kulevya, imekuwa chanzo kikubwa cha mapato kwa wahalifu.
Kwa kipindi cha miaka kumi iliyopita Bio Guo amekuwa akienda kutoka kijiji hadi kijiji katika jimbo la Shandong, pwani ya mashariki, akiwauliza wenyeji kile kilichokuwa kinachotokea kwa wanyama wao. Katika kijiji kimoja wanakijiji walimwambia kuwa theluthi moja ya mbwa wao waliibiwa kati ya 2007 na 2011.

Pia aligundua kuwa wawindaji wamekuwa wakipita vijijini na magari wakiua mbwa na mishale yenye sumu na kuwauza kwa watu wa kati(madalali).
Wawindaji wanapata Yuan 10 ($ 1.30) kwa kilo ya nyama, hivyo mbwa wa ukubwa wa kati anaweza kuwa na thamani ya Yuan 70-80 sawa na takribani dola 7 mpaka 8 za kimarekani.
Kijana mmoja wa kiume ambaye alihojiwa naye alikuwa akiwinda ili aweze kupata mapato aweze kuoa.


CHANZO:
Economist Asia.

Comments

Habari Nyingine Kutoka Kioo17 Swahili;

ORODHA YA NCHI 80 AMBAZO MTANZANIA ANARUHUSIWA KUINGIA BILA VIZA.

         Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni amesema kuna zaidi ya nchi 80 ambazo watanzania wanaweza kusafiri bila ya kuwa na viza . Mhandisi Hamad Masauni amesema kuna zaidi ya nchi 80 ambazo watanzania wanaweza kusafiri bila ya kuwa na viza za kusafiria kama ilivyokuwa nchi za afrika Mashariki. Mhandisi Massauni amebainisha hayo leo bungeni wakati akijibu swali la Mbunge wa Mlalo kupitia tiketi ya CCM Rashid Shangazi aliyetaka kujua ni nchi ngapi ambazo watanzania wanaweza kusafiri bila ya kuwa na viza (viza on arrival). "Zipo nchi 16 kwa Afrika ambazo watanzania wanaweza kuzitembelea bila ya kuwa na viza na duniani zipo 67" alisema Masauni. Aidha Massauni amezitaja nchi hizo kuwa ni Benin, Burkina Faso, Cape Verde, Ivory Coast, Djibouti, Gabon, Gambia, Guinea, Guinea­Bissau, Liberia, Mali, Mauritania, Niger, Sierra Leone pamoja na Togo. Pamoja na hayo Masauni amesema...

MCHEZAJI WA ZAMANI WA UINGEREZA AMESEMA ALICHEZA NA WACHEZAJI WATATU MASHOGA KWENYE TIMU.

Carl Hoefkens (jezi no.2) alichezea West Bromwich Albion na Stoke City wakati wa enzi zake ligi kuu ya England. Beki wa zamani wa Ligi Kuu ya Uingereza amesema alicheza pamoja na wachezaji wenzake wawili wa mashoga ndani ya timu, na mmoja alikua na jina kubwa. Carl Hoefkens, West Bromwich Albion na Stoke City siku za nyuma, anasema wachezaji hao walikua wazi na hawakujificha kwenye vyumba vya kubadilishia nguo ingawa bado hawajulikani kwasababu ya maombi yao wenyewe ya kuomba kutotangazwa. Justin Fashanu, ambaye alijiua mwaka 1998, alikuwa mchezaji wa mwisho wa kazi nchini England kuja nje kama mashoga - mwaka 1990. Hoefkens alipokua (kushoto), alipokua anachezea Stock  City. Hoefkens aliyecheza Uingereza kwa miaka minne, akiondoka mwaka 2009, alidai kuwa mchezaji mwenzake mmoja wa timu alikua anaweza kuja kwenye uwanja wa mafunzo ya klabu na mpenzi wake wa kiume  lakini aliwaomba wenzake kutokuwaambia watu wangine wa nje ya timu. 'Nilicheza pamoja n...

ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2017, TANZANIA

MH.GEORGE SIMBACHAWENE .               Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Tamisemi) George Simbachawene ametoa idadi ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na masomo ya kidato cha tano na vyuo vya ufundi kwa mwaka 2017 huku jumla ya wanafunzi 2,999 wakiachwa.             Simbachawene ametoa kauli hiyo leo mjini Dodoma wakati akizungumza na waandishi ws habari na kusema kuwa ufaulu kwa mwaka huu umeongezeka kwa asilimia 3.75 ukilinganisha na matokeo ya mwaka 2015. Waziri amedai kati ya wanafunzi 96,018 waliofaulu kwa daraja la kwanza hadi la tatu ni wanafunzi 93,019 tu ndiyo waliochaguliwa kujiunga na kidato cha tano na vyuo vya ufundi.              Waziri Simbachawene amesema kuwa jumla ya watahiniwa wote waliofanya mtihani wa kidato cha nne kwa shule kwa mwaka 2016 ni 349,524 huku waliofanya mtihani wa kujitegemea ni 47,751 ambapo watahiniwa waliofanya mtihani wa shule...

TUPAC SHAKUR ALIBAKWA JELA !!!

             Ulimwengu wa filamu za Hollywood na muziki wa Hip Hop juzi ulipatwa na mshangao baada ya mtayarishaji wa filamu inayohusu maisha ya hayati Tupac Shakur ,L.T Hutton kuelezea sababu zilizomfanya kumbadilisha muongozaji wa filamu hiyo kutoka John Singleton na kumuweka muongozaji Benny "Boom" Douglas.  Filamu hiyo inayoitwa "all eyez on me" tayari imekwisha andaliwa na inatarajiwa kuzinduliwa leo tarehe 16 Juni 2017.       Akizungumza kwenye mahojiano redioni L.T Hutton amewashtusha watu wengi baada ya kudai kwamba walishindwana na muongozaji wa mwanzo bwana John Singleton sababu muongozaji huyo aling'ang'ania kuwepo kwa matukio (scene) ambazo kwa maoni yake zisingependeza.        Matukio ambayo John Singleton alipenda yawepo katika filamu hiyo ni pamoja na kutaka filamu hiyo ianze na scene ya Tupac akilazimisha kumlawiti msichana wa kizungu.!!!          Singleton pia ali...

MFALME WA GHANA ASABABISHA AFISA MKUU WA BENKI KUFUKUZWA KAZI.

Afisa mtendaji mkuu wa benki alifukuzwa kazi na kuchunguzwa na Shirika la Uhalifu wa Taifa baada ya kuweka pauni za Uingereza 350,000 ( £ 350,000 ) pesa taslimu aliyopewa na Mfalme wa Ghana. Mark Arthur wa benki ya Kimataifa ya Ghana Bigwig aliitwa kwenye nyumba ya Osei Tutu II huko Henley-on-Thames na kupewa £ 200,000 pamoja na $ 200,000 na kuagizwa aiweke kwenye akaunti ya benki ya Mfalme huyo. Licha ya noti hizo kuwa na namba za mfululizo zinazofuatana (consecutive serial numbers) Bwana Arthur alisema aliona kuwa haifai kumhoji mfalme na kwenda kuiweka benki kwa kutumia usafiri wa teksi ya uber. Punde baada ya Bwana Arthur kuweka pesa hiyo benki, taarifa ya utakatishaji wa fedha ilifika katika jiji la London, Uingereza na kugharimu ajira yake. Bwana Arthur alielezea kwenye taarifa yake ya ushahidi kuwa Mfalme alimwambia kwamba pesa hizo zimekusanywa kutoka kwenye akaunti za benki za nchini Ghana na kupelekwa Uingereza. Pia alidai kwamba Mfale alimpa $ 200,000 ili ...

SABABU ZA KUVUNJIKA KWA KUNDI LA P-SQUARE.

WANAMUZIKI MAPACHA WA KUNDI LA PSQUARE, PETER (KUSHOTO) NA PAUL (KULIA) WAKIWA NA KAKA YAO AMBAE PIA NI MENEJA WAO, JUDES OKOYE. Mwanamuziki wa kundi la PSquare kutoka Nigeria, Peter Okoye ametangaza kujitoa kwenye kundi hilo la muziki wa Pop maarufu zaidi Afrika. Msanii huyo alidai kwamba amewasilisha maombi ya kuvunja kundi hilo katika barua aliyoandika kwa wakili wao Festus Keyamo. Kulingana na nakala ya barua iliyotolewa kwenye vyombo vya habari Jumatatu,Tarehe 25 Septemba, Peter alisema kuwa pacha wake na, Paul, na kaka yao, Judes waliahirisha ziara yao ya muziki ya Marekani bila kushauriana naye.Na hiyo ni moja kati ya sababu za msingi. Peter pia aliwalaumu Paul na kaka yao mkubwa mkubwa ambae ni meneja wao pia kwa udanganyifu walioufanya ili kutatua shida waliyokuwa nayo juu ya biashara ya muziki. Wasanii hao ndugu wamekua kwenye vita vya maneno kwenye mitandao ya kijamii tangu mwisho wa mwaka jana pamoja na juhudi za watu wao wa karibu kujaribu kuwapatanisha kifami...

ORODHA YA NCHI ZA KWANZA NA ZA MWISHO KWA AMANI DUNIANI.

Marekani:  Ripoti ya Taasisi ya Uchumi na Amani imepata mataifa kumi tu ulimwenguni ambayo hayapo katika vita na migogoro kabisa. Kwa mujibu wa Ripoti ya Kimataifa ya Amani 2016, Botswana, Chile, Costa Rica, Japan, Mauritius, Panama, Qatar, Uswisi, Uruguay na Vietnam ndio nchi pekee ambazo hazipo kwenye vita wala migogoro yeyote ile ya kuhatarisha amani.. Iceland inaongoza orodha ya nchi zinazoongoza kwa amani ulimwenguni, ikifuatiwa na Denmark, Austria, New Zealand, Ureno, Jamhuri ya Czech, Uswisi, Canada, Japan na Slovenia - wakati Marekani ikiwa kwenye nafasi ya 103. Palestina imepanda kutoka nafasi ya 163 mpaka nafasi ya 148. Syria iliyoharibiwa na vita imewekwa chini ya orodha, chini kuliko Sudan Kusini, Iraq, Afghanistan, Somalia, Yemen, Jamhuri ya Afrika ya Kati, Ukraine, Sudan na Libya. "Ripoti inalinganisha amani duniani kwa kutumia mandhari tatu pana: hali ya utulivu na usalama katika jamii; kiwango cha mgogoro wa ndani au wa kimataifa; na kiwango cha kije...