Skip to main content

SABABU YA SOKO LA NYAMA YA MBWA KUONGEZEKA NCHINI CHINA.



Kila mwaka wakati wa msimu wa majira ya joto, tamasha la kula mbwa linafanyika Yulin, jiji lililo katika jimbo la kusini mwa China la Guangxi. 
Tukio la mwaka jana lilimalizika na utata usio wa kawaida. Picha za mbwa wakichinjwa kikatili na kukaangwa zilisababisha gumzo kubwa ulimwenguni kote.

Tamasha la Nyama ya Mbwa la Jinhua Hutou, kama linavyoitwa, lilifungwa ghafla wiki chache zilizopita.


Wanaharakati wa haki za wanyama na wabunge wa Marekani walitaka Uchina kupiga marufuku kula na mbwa na paka, kama vile Taiwan alivyofanya mwaka 2017. 

Serikali za mitaa za Yulin zilichukua hatua za kuzuia na kuficha baadhi ya shughuli za baadhi ya shughuli hizo kama vile kuuza mbwa katika masoko ya chakula. 
Hata hivyo, tamasha hilo lilifanyika na kufana zaidi ya miaka mingine. 

Kwa nini tabia hii isiyo ya kawaida kwa nchi nyingine imekuwa maarufu sana nchini China?




Nyama ya mbwa haijawahi kuwa kitu cha kawaida katika chakula cha Kichina.

Tofauti na sehemu nyingine ulimwenguni, kula nyama ya mbwa hakujawahi kuwa haramu, lakini tabia hiyo inaoneka kuwa sio maarufu katika siku za nyuma ukilinganisha na sasa.


Kwa mujibu wa Guo Peng kutoka Chuo Kikuu cha Shandong, mmoja kati ya watu wachache ambao walifanya utafiti kuhusu soko la nyama ya mbwa, ni Wachina wachache wenye asili ya Kikorea hula mbwa karibu kila siku kama chakula cha kawaida.
Anasema idadi kubwa ya watu wa kabila kubwa la Han, wanaiona kama chakula cha dawa, ambacho kinaaminika kuupa mwili joto kwa wakati wa majira ya baridi na kuupa mwili baridi wakati wa majira ya joto.

Bio Guo anasema, watu wengi wamekula mbwa agalau mara moja kwa mwaka, ikiwa ni sawa.

Kulingana na utafiti uliofanywa mwaka 2016 na Dataway Horizon, kampuni ya kupigia kura, na Shirika la Ustawi wa Wanyama wa Mifugo, Shirika lisilo la kiserikali la China, karibu asilimia 70 ya watu wa China wanasema hawajawahi kula mbwa. Kati yao, wengi wanasema walifanya hivyo kwa ajali wakati walipo alikwa kwenye chakula cha jioni au kwenye mikusanyiko mingine ya kijamii kama sherehe na kadharika.


Kwa nini tamasha la Yulin limejaa? Na kwa nini migahawa katika miji mingi hujaribu kuweka mbwa kwenye orodha? Jibu ni neno moja ni: uhalifu.
Nyama ya mbwa, kama vile madawa ya kulevya, imekuwa chanzo kikubwa cha mapato kwa wahalifu.
Kwa kipindi cha miaka kumi iliyopita Bio Guo amekuwa akienda kutoka kijiji hadi kijiji katika jimbo la Shandong, pwani ya mashariki, akiwauliza wenyeji kile kilichokuwa kinachotokea kwa wanyama wao. Katika kijiji kimoja wanakijiji walimwambia kuwa theluthi moja ya mbwa wao waliibiwa kati ya 2007 na 2011.

Pia aligundua kuwa wawindaji wamekuwa wakipita vijijini na magari wakiua mbwa na mishale yenye sumu na kuwauza kwa watu wa kati(madalali).
Wawindaji wanapata Yuan 10 ($ 1.30) kwa kilo ya nyama, hivyo mbwa wa ukubwa wa kati anaweza kuwa na thamani ya Yuan 70-80 sawa na takribani dola 7 mpaka 8 za kimarekani.
Kijana mmoja wa kiume ambaye alihojiwa naye alikuwa akiwinda ili aweze kupata mapato aweze kuoa.


CHANZO:
Economist Asia.

Comments

Habari Nyingine Kutoka Kioo17 Swahili;

JAGUAR KUACHIA WIMBO BAADA YA KUAPISHWA MBUNGE.

Mbunge wa Starehe, Kenya, "Jaguar" anajipanga kutoa wimbo mpya mara tu baada ya kuapishwa kua mbunge. Katika chapisho lake la kwenye akaunti yake ya mtandao wa kijamii, Jaguar aliupendekeza wimbo wake wa "Ndoto" kama salamu kwa Wakenya na watu walio nje ya Kenya. Charles Njagua, ambae ni maarufu kwa jina la Jaguar, ana Aliahidi mashabiki wimbo mpya baada ya kuapa rasmi kama mbunge.  Mimbaji huyo ambaye ametoa hits kadhaa lakini sasa anazingatia siasa baada ya kushinda kiti, aliwaambia mashabiki kwenye vyombo vya habari vya kijamii kwamba wimbo mpya, unaitwa "Ndoto", uko tayari na utaachiliwa haraka baada ya kuapa. "Sasa ni karibu miongo miwili tangu mimi kuweka mguu katika studio ya kurekodi,   alisema Jaguar katika chapisho lake. CHANZO: www.tuko.news

KASHFA YA MAPENZI KATI MH.MBOWE NA WEMA SEPETU.

MH.FREEMAN MBOWE AKIWA NA WEMA SEPETU. Siku chache baada ya ile skendo ya ngono iliyosababisha wakili na mshauri wa Chama cha ACT -Wazalendo , Bwana Albert Msando kujiuzulu kwenye nyadhifa yake ya chama ,yameibuka mangine kwenye chama kikuu cha upinzani Tanzania ,CHADEMA ,baada ya kusambaa kwa kipande cha sauti kinachodaiwa kua ni mazungumzo kati ya mwenyekiti wa chama hicho na mbunge wa Hai Mh.Freeman Mbowe na Miss Tanzania 2006 ,mrembo Wema Isack Sepetu. SIKILIZA HIVI VIPANDE VYA SAUTI: Bonyeza hapa chini kusikiliza maongezi hayo yanayodaiwa kuwa ni kati ya Wema Sepetu na Mh.Freeman Mbowe; Bonyeza hapa chini kusikiliza majibu ya Wema Sepetu; Bonyeza hapa chini kusikiliza majibu ya Mh.Freeman Mbowe; VYANZO: Jamii Forums,                   YouTube.com,                   Perfect255.com.                   

ORODHA YA NCHI ZA KWANZA NA ZA MWISHO KWA AMANI DUNIANI.

Marekani:  Ripoti ya Taasisi ya Uchumi na Amani imepata mataifa kumi tu ulimwenguni ambayo hayapo katika vita na migogoro kabisa. Kwa mujibu wa Ripoti ya Kimataifa ya Amani 2016, Botswana, Chile, Costa Rica, Japan, Mauritius, Panama, Qatar, Uswisi, Uruguay na Vietnam ndio nchi pekee ambazo hazipo kwenye vita wala migogoro yeyote ile ya kuhatarisha amani.. Iceland inaongoza orodha ya nchi zinazoongoza kwa amani ulimwenguni, ikifuatiwa na Denmark, Austria, New Zealand, Ureno, Jamhuri ya Czech, Uswisi, Canada, Japan na Slovenia - wakati Marekani ikiwa kwenye nafasi ya 103. Palestina imepanda kutoka nafasi ya 163 mpaka nafasi ya 148. Syria iliyoharibiwa na vita imewekwa chini ya orodha, chini kuliko Sudan Kusini, Iraq, Afghanistan, Somalia, Yemen, Jamhuri ya Afrika ya Kati, Ukraine, Sudan na Libya. "Ripoti inalinganisha amani duniani kwa kutumia mandhari tatu pana: hali ya utulivu na usalama katika jamii; kiwango cha mgogoro wa ndani au wa kimataifa; na kiwango cha kije...

"GIGGS HAFAI KUWA KOCHA WA TIMU YA TAIFA", BABA YAKE ANASEMA...!!!

Ryan Giggs. Chama cha Soka cha Wales (FAW) siku ya jumatatu kilitangaza kumchagua winga wa zamani wa Manchester United Ryan Giggs kama kocha wa timu yao ya taifa kwa mkataba wa miaka minne. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 44 anachukua kazi iyoachwa na Chris Coleman, ambaye aliiongoza Wales kwenye nusu fainali za Euro 2016 lakini aliacha kazi mwezi Novemba ili kuchukua nafasi ya kuifundisha timu ya Sunderland ya ligi kuu ya Uingereza. Giggs alisema kuwa anajivunia kwa kupewa kazi hiyo na pamoja na changamoto iliyo mbele yake baada ya Wales kushindwa kufuzu kucheza fainali za Kombe la Dunia mwaka huu nchini Urusi na sasa wanazingatia michuano ya Ulaya ya 2020. "Siwezi kusubiri kuanza kufanya kazi na wachezaji tunapojiandaa kwa ajili ya michezo muhimu baadaye mwaka huu," alisema. Lakini baba mzazi wa Giggs, Danny Wilson ana maoni  tofauti sana...!!! Anakiri kwamba mwanae anamtia aibu na anasema hastahili kuchukua kazi hiyo ya ukocha wa timu ya t...

MCHEZAJI WA ZAMANI WA UINGEREZA AMESEMA ALICHEZA NA WACHEZAJI WATATU MASHOGA KWENYE TIMU.

Carl Hoefkens (jezi no.2) alichezea West Bromwich Albion na Stoke City wakati wa enzi zake ligi kuu ya England. Beki wa zamani wa Ligi Kuu ya Uingereza amesema alicheza pamoja na wachezaji wenzake wawili wa mashoga ndani ya timu, na mmoja alikua na jina kubwa. Carl Hoefkens, West Bromwich Albion na Stoke City siku za nyuma, anasema wachezaji hao walikua wazi na hawakujificha kwenye vyumba vya kubadilishia nguo ingawa bado hawajulikani kwasababu ya maombi yao wenyewe ya kuomba kutotangazwa. Justin Fashanu, ambaye alijiua mwaka 1998, alikuwa mchezaji wa mwisho wa kazi nchini England kuja nje kama mashoga - mwaka 1990. Hoefkens alipokua (kushoto), alipokua anachezea Stock  City. Hoefkens aliyecheza Uingereza kwa miaka minne, akiondoka mwaka 2009, alidai kuwa mchezaji mwenzake mmoja wa timu alikua anaweza kuja kwenye uwanja wa mafunzo ya klabu na mpenzi wake wa kiume  lakini aliwaomba wenzake kutokuwaambia watu wangine wa nje ya timu. 'Nilicheza pamoja n...

TUPAC SHAKUR ALIBAKWA JELA !!!

             Ulimwengu wa filamu za Hollywood na muziki wa Hip Hop juzi ulipatwa na mshangao baada ya mtayarishaji wa filamu inayohusu maisha ya hayati Tupac Shakur ,L.T Hutton kuelezea sababu zilizomfanya kumbadilisha muongozaji wa filamu hiyo kutoka John Singleton na kumuweka muongozaji Benny "Boom" Douglas.  Filamu hiyo inayoitwa "all eyez on me" tayari imekwisha andaliwa na inatarajiwa kuzinduliwa leo tarehe 16 Juni 2017.       Akizungumza kwenye mahojiano redioni L.T Hutton amewashtusha watu wengi baada ya kudai kwamba walishindwana na muongozaji wa mwanzo bwana John Singleton sababu muongozaji huyo aling'ang'ania kuwepo kwa matukio (scene) ambazo kwa maoni yake zisingependeza.        Matukio ambayo John Singleton alipenda yawepo katika filamu hiyo ni pamoja na kutaka filamu hiyo ianze na scene ya Tupac akilazimisha kumlawiti msichana wa kizungu.!!!          Singleton pia ali...

MOHAMMED DEWJI NA BILL GATES KUTOA NUSU YA UTAJIRI WAO...!!!

MOHAMMED DEWJI AKIWA NA BILL GATES. Mfanyabiashara tajiri namba moja Tanzania (kwa mujibu wa jarida la Forbes) na mmiliki wa makampuni ya METL , Mohammed "Mo" Dewji ,wiki chache zilizopita amekua mmoja wa mabilionea 14 wapya kujiunga katika mpango wa kuchangia misaada kwa jamii uitwao "Giving Pledge".                 Mpango huo ulioanzishwa na familia ya mfanyabiashara tajiri namba moja duniani (kwa mujibu wa jarida la Forbes) na mmiliki wa kampuni ya Microsoft Bill Gates pamoja na rafiki yake bilionea Warren Buffet mwaka 2010, ulikua na tayari umeshaungwa mkono na mabilionea 154 mpaka mwanzo wa mwaka huu (2017). WAASISI WA "GIVIN PLEDGE",WARREN BUFFET, MELINDA GATES NA BILL GATES.         Mohammed Dewji anakua mmoja kati ya matajiri wachache sana kutoka Afrika kama Patrice Motsepe (Afrika Kusini) na Mo Ibrahim (Sudan) kujiunga na kampeni hiyo ambayo nia yake kubwa ni kushawishi watu matajiri kutoa angalau nu...