Skip to main content

Posts

MAAJABU YA KIJANA JOHN PAUL MWIRIGI, 23.

  JOHN PAUL MWIRIGI .    Kijana mwenye umri wa miaka 23, John Paul Mwirigi, ana nafasi kubwa ya kuwa kijana mdogo kabisa kua Mbunge katika Bunge la Jamhuri ya Kenya iwapo atatangazwa kushinda kiti cha ubunge wa Igembe Kusini katika Uchaguzi Mkuu wa Agosti 8. Mwirigi, amabae ni mgombea wa kujitegemea, anaongoza kwa kura zaidi ya 3,000 dhidi ya mpinzani wake wa karibu, Joseph Miriti Rufus Mwereria, ambaye ni mgombea kwa tiketi ya Chama cha Jubelee. Mpaka kufikia saa 7:50 jioni Jumatano, Mwirigi alikuwa na kura 19,366, ikilinganishwa na mpinzani wake wa kisiasa, Mwereria, ambaye - wakati huo huo - alikuwa na kura 15,977, ambayo ni asilimia 95.14 ya matokeo kutoka vituo vya kupigia kura. Mkutano wa kampeni ya Mwirigi ulikuwa na hisia ya unyenyekevu, aliweza kuzunguka kwa miguu mlango kwa mlango, kuwakumbusha wapiga kura kuwatambulisha wapiga kura kumtambua kwa sweta lake la kijivu lenye mstari mweusi kifuani katika karatasi za kura. Mwirigi kamwe hakuchapis...

SABABU ZA KANISA KATOLIKI KUKATAA KUMZIKA BILIONEA MREMA.

KANISA Katoliki Jimbo Kuu la Arusha, limekataa kuendesha misa ya maziko ya mfanyabiashara bilionea Faustine Mrema kwa madai hakuwa na Sakramenti ya ndoa na mke wake wala kipaimara. Paroko Msaidizi wa Parokia ya Mtakatifu Theresia, Mtoto Yesu, Jimbo Kuu la Arusha Padri Festus Mangwangi amekiri suala hilo na kuongeza kuwa marehemu enzi za uhai wake hakuweka heshima na kanisa. “Marehemu ni mkatoliki wa kuzaliwa, lakini hakuwahi kuwa na sakramenti ya ndoa na mke aliyezaa naye watoto wala kupata Kipaimara. Kanisa haliwezi kumzika kabisa, kawaida mazishi ya Kanisa Katoliki ni heshima inayotolewa kwa mhusika kama anastahili. “Huyu hakuwahi kufunga ndoa kanisani, alijitenga na kanisa kwa hiyo kusema tumemtenga si kweli, yeye ndiyo alijikataa hakutaka kutafuta heshima yake na kanisa akiwa hai,” alisema Padri Mangwangi. Kuhusu kutokwenda kwenye Misa za Jumuiya ambayo nayo ni moja ya taratibu muhimu inayowataka waumini wa kikatoliki kushiriki ibada za nyumba kwa nyumba Padri Mangwangi ame...

SABABU YA MANJI KUMKATAA WAKILI PETER KIBATALA.

Mpaka sasa unatakiwa kufahamu kwamba Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Dar es Salaam imetupilia mbali maombi ya dhamana yaliyowasilishwa na Mfanyabiashara Yusuf Manji ambae anakabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi. Hata hivyo kabla ya kutupiliwa maombi hayo, Manji alisimama na kuieleza Mahakama kwamba ameamua kukataa kuendelea kuwakilishwa na Wakili Peter Kibatala kwa sababu za kisiasa. Manji amedai alipopeleka maombi ya dhamana Mahakamani hapo alimpa maelekezo wakili Joseph Tedayo lakini alishangaa kesi ilipofika Mahakamani kwa ajili ya kisikilizwa maombi yake, akawakilishwa na wakili Peter Kibatala. TAZAMA VIDEO HAPA : CHANZO : http://millardayo.com/mnj2017a/

SIRI YA CHAMA CHA JUBILEE KUTUMIA MACHIFU KUPELEKA WATU VITUONI.

KAMISHNA WA KAUNTI YA KIAMBU ALEX OLE NKOYO (kulia) AKIZINDUA PIKIPIKI 12 ZILIZOTOLEWA NA KWA MACHIFU NA MANAIBU WAO MAPEMA 2016. Japo umekuwa ukitekelezwa kwa siri, mpango huo unaojulikana kama Cell Thirty (C30), unalenga kuhakikisha watu wamejitokeza kwa wingi vituoni na maafisa wa utawala wa mikoa wameagizwa kuhakikisha umefaulu. Chifu mmoja aliyeomba tusitaje jina lake ili asidhulumiwe alisema mikutano 15 ya siri iliandaliwa tangu Julai katika kaunti zote. Alieleza kwamba machifu wamekabidhiwa nakala za sajili ya wapigakura katika maeneo yao ili waweze kuwafuatilia kesho. Katibu Mkuu wa wizara ya usalama wa ndani Dkt Karanja Kibicho aliongoza mkutano wa machifu wote 250 kutoka kaunti ya Nyeri. Mkutano huo ulifanyika Kiamuiru Gatitu Julai 23. atibu Mkuu wa wizara ya usalama wa ndani Dkt Karanja Kibicho aliongoza mkutano wa machifu wote 250 kutoka kaunti ya Nyeri. Mkutano huo ulifanyika Kiamuiru Gatitu Julai 23 “Tumeagizwa kuhakikisha kuwa kila mmoja amefikisha w...

JINSI YA KUOMBA PASSPORT YA TANZANIA KWA NJIA YA INTERNET.

Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kupitia i dara ya Uhamiaji  imezindua huduma ya ujazaji fomu za maombi ya hati ya kusafiria (Passport) kwa njia ya mtandao, ambapo mwombaji atalazimika kujaza fomu hizo na kuzichapisha kabla ya kuziwasilisha kwenye ofisi za uhamiaji. Idara hiyo pia imeeleza kuwa matumizi ya huduma hiyo yataenda sambamba na huduma inayotumiwa sasa ya fomu za maombi ya pasipoti mpaka pale itakapotangazwa vinginevyo. Huduma hiyo itaanza kufanya kazi kuanzia Jumatatu tarehe  7/8/2017    na unaweza  kujaza fomu hizo  kwa kufungua tovuti hiyo ambayo ni  https://www.immigration.go.tz/ppt_application/ Utaratibu wa namna ya kujaza fomu hizo umeelekezwa katika fomu husika mtandaoni, na pia wateja wanaweza kupata ufafanuzi au maelezo zaidi kuhusu huduma hiyo kupitia anuani ya Idara ya Uhamiaji ambayo ni   info@immigration.go.tz   au katika Ofisi yoyote ya Uhamiaji iliyo karibu yako. CHANZO: http://dibute.com/muhimu-...

SABABU ZA MAKONDA KUTENGUA TAMKO LA POLISI KUHUSU TINTED ZA MAGARI.

AGIZO LA RC MAKONDA  KUHUSIANA NA ISHU YA TINTED JIJINI DAR "Nasitisha zoezi lililotolewa na polisi Mkoa wa Dsm la kuondoa tinted lililopangwa kuanza kesho hadi nitakapopewa na polisi hoja za msingi" " Hii ni kwasababu kwanza, kuna magari yanakuja nchini yakiwa na tinted hivyo kumtaka mtu aondoe ni kumtaka atoe kioo. Pili, tinted ni ulinzi wa gari ili mtu asiweze kuona kilichomo ndani na kuvunja. Tatu, kuna watanzania wa mikoani wanakuja na magari tinted kwani hili ni katazo la Dsm tu hivyo hatuwatendei haki. Nne, wakina mama wanaweka tinted kwavile hawataki kuonekana wako peke yao kwani wanaweza kuvamiwa. Hivyo nimelisitisha zoezi hilo" MH. PAUL MAKONDA (RC) CHANZO; https://m.facebook.com/story.php?story_fbid=1533367536771363&id=508599559248171

FILAMU ZILIZOWAHI KUIGIZWA NA DONALD TRUMP.

Wakati filamu ya Hollywood iliyofahamika kama "Ghosts can't do it" ikiingia sokoni mwaka 1989 na kutokufanya vizuri  kimapato, kwa upande mwingine ilikua na faida kwa mfanyabiashara maarufu wa marekani na Raisi wa sasa wa nchi hiyo Donald Trump katika tasnia ya maigizo.     Filamu hiyo ndiyo ilitoa fulsa ya kwanza kwa Donald Trump kupata kipande kidogo cha kuigiza kwenye filamu (cameo), kipande ambacho mchambuzi mashuhuri wa filamu wa kipindi hicho Bwana Roger Ebert alikiita ni kapande kinachofurahisha moyo.         Tazama kipande cha Video cha filamu ya kwanza ya Donald Trump kuigiza, "Ghosts can't do it" ;        Mwaka 1992,ulikua mwaka mzuri zaidi kwa Donald Trump wakati alipopata tena nafasi ya kuigiza katika filamu maarufu na iliyopata mafanikio makubwa kipindi hicho  iliyojulikana kama "Home Alone 2". Katika filamu hiyo Donald Trump alionekana akimwelekeza mtoto Macaulay Culkin aliye igiza kama Kevin McAllis...