Skip to main content

IGP MANGU KUONDOLEWA? ,ILISHATABILIWA KITAAMBO !!!

IGP ERNEST MANGU.


Ikiwa ni siku moja tu tangu Kurugenzi ya Habari Ikulu ilipotoa taarifa ya kumpandisha cheo mkuu wa polisi wa kanda maalumu ya Dar es Salaam, kamanda Simon Sirro kuwa mkuu wa polisi Tanzania na kutoa tamko kwamba mkuu wa jeshi hilo wa sasa Inspekta Jenerali Ernest Mangu atapangiwa kazi nyingine, Taarifa hiyo imepokelewa kwa mawazo tofauti tofauti na wananchi hasa ikiwa wengi wanajiuliza ni kwanini IGP Mangu ametolewa katika nyadhifa hiyo ya juu kabisa kwenye jeshi la polisi kabla ya muda wake wa kustaafu kufika !!!.
       
BARUA  KUTOKA IKULU KWA WAANDISHI WA HABARI.


    Chanzo cha blog yetu (Kioo17) siku ile ile ya jana 28 Mei 2017 ,kilibahatika kupata maoni ya mchambuzi nguli wa mambo ya siasa Bwana Malisa GJ alitukumbusha kwamba kuna mwanahabari wa gazeti la "MwanaHalisi" bwana Charles William           Alibashili haya ya jana takribani miaka miwili iliyopita !!!.

SOMA HII;

MALISA GJ: 
Mdogo wangu Charles William aliandika miaka miwili iliyopita kuwa Ernest Mangu atang'olewa ktk nafasi yake ya IGP na kupewa Simon Siro. Soma makala hii iliyoandikwa na Charless William na kuchapwa na gazeti la Mwanahalisi la December 21, mwaka 2015.
_____________________________________________

JGP MANGU KUNG'OKA

Na Charles William,
MwanaHALISI - Desemba 21, 2015.
__________________________________

Rais na Amiri Jeshi Mkuu, Dk. John Magufuli anajiandaa kufanya mabadiliko makubwa ndani ya Jeshi la Polisi kwa kumuondoa Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP) Ernest Mangu.

Taarifa zilizopatikana kutoka kwa mmoja wa maofisa wa Ikulu zinaeleza kuwa Dk. Magufuli sasa anahitaji kuwa na mkuu mpya wa Jeshi hilo huku IGP Mangu akitarajiwa kupewa ubalozi katika mojawapo ya nchi za Afrika, kusini mwa jangwa la Sahara na Naibu wake Abdurahmani Kaniki akitarajiwa kushushwa ngazi na kuwa mkuu wa polisi katika mkoa mojawapo kanda ya ziwa.

Iwapo Rais Magufuli atabadilisha mkuu wa jeshi hilo, IGP Mangu atakuwa amelitumikia jeshi hilo kwa muda wa miaka miwili tu baada ya kuteuliwa na Rais Kikwete kushika wadhifa huo Desemba 30, 2013 akitokea ofisi ya Polisi wa kimataifa (Interpol) jijini Nairobi, Kenya.

Wanaotajwa kuwa kwenye nafasi ya kumrithi IGP Mangu ni pamoja na mkuu wa Operesheni wa polisi, Simon Siro na mkuu wa Interpol Gustav Babile.

Kwasasa waliopo katika nafasi za juu za jeshi hilo ni kamishna Glodwig Mtweve (fedha na utawala), Mussa Ally Mussa (Polisi Jamii makao makuu), Thobias Andengenye (utawala na utumishi) na Diwani Athumani (Mkuu wa intelijensia ya jinai DCI).

Haya yanakuja ikiwa ni wiki mbili tu tangu Rais Magufuli afanye mabadiliko ya kushitua  akimuhamisha Kamishina wa Operesheni na Mafunzo Paul Chagonja na kumpeleka kuwa mkuu wa jeshi la zimamoto na uokoaji huku mkuu wa idara ya intelijensia Valentino Mlowola akiteuliwa kuwa kaimu mkurugenzi wa TAKUKURU.........
______________
©Charles William.



Comments

Habari Nyingine Kutoka Kioo17 Swahili;

TRUMP NA KIM JONG-UN FEKI WAHUBIRI AMANI KATIKA SHEREHE ZA UZINDUZI WA OLIMPIKI.

Waigaji wa Rais wa Marekani Donald Trump na kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong-un walikua wakihubiri amani katika sherehe za uzinduzi wa michezo ya Olympiki kwa majira ya baridi(Winter Olympic) jijini Pyeong Chang, Korea ya Kaskazini kabla ya kutolewa nje na wanausalama. Watu hao walionekana kwa muda mfupi katika jukwaa la uwanja huo mkuu wa Pyeongchang, Korea Kusini ili kuwasalimu watu. Waigaji hao ambao wote walikataa kutoa majina yao halisi - walikuja kwenye sherehe ya ufunguzi -   "kuonyesha dunia, hii ndio amani inaweza kuonekana kama viongozi hao wawili watakapokutana,"  alisema Kim bandia. Trump bandia alimwiga Rais Trump kwa kuvaa kofia nyekundu ya mpira wa magongo (baseball), lakini ikiwa imeandikwa "USA" sio "Make America Great again"(Unda Amerika Kuu tena) kauli mbiu ambayo mara nyingi huandikwa kwenye mavazi na matangazo ya Trump. Pia alivaa tai ndefu ya rangi nyekundu kama ambavyo rais Trump mwenyewe hupendele...

MFALME WA GHANA ASABABISHA AFISA MKUU WA BENKI KUFUKUZWA KAZI.

Afisa mtendaji mkuu wa benki alifukuzwa kazi na kuchunguzwa na Shirika la Uhalifu wa Taifa baada ya kuweka pauni za Uingereza 350,000 ( £ 350,000 ) pesa taslimu aliyopewa na Mfalme wa Ghana. Mark Arthur wa benki ya Kimataifa ya Ghana Bigwig aliitwa kwenye nyumba ya Osei Tutu II huko Henley-on-Thames na kupewa £ 200,000 pamoja na $ 200,000 na kuagizwa aiweke kwenye akaunti ya benki ya Mfalme huyo. Licha ya noti hizo kuwa na namba za mfululizo zinazofuatana (consecutive serial numbers) Bwana Arthur alisema aliona kuwa haifai kumhoji mfalme na kwenda kuiweka benki kwa kutumia usafiri wa teksi ya uber. Punde baada ya Bwana Arthur kuweka pesa hiyo benki, taarifa ya utakatishaji wa fedha ilifika katika jiji la London, Uingereza na kugharimu ajira yake. Bwana Arthur alielezea kwenye taarifa yake ya ushahidi kuwa Mfalme alimwambia kwamba pesa hizo zimekusanywa kutoka kwenye akaunti za benki za nchini Ghana na kupelekwa Uingereza. Pia alidai kwamba Mfale alimpa $ 200,000 ili ...

CHANZO CHA MAPIGANO YA WACHEZAJI WA MANCHESTER UNITED NA MANCHESTER CITY BAADA YA MECHI.

Maafisa wa polisi na wahudumu wa uwanja walilazimika kuwatenganisha wachezaji wasiopungua 20 na wafanyakazi wa timu za Manchester United na Manchester City baada ya kupigana katika vurugu kubwa ilijitokeza kwenye njia za kuelekea kwenye vyumba vya kubadilishia nguo kwenye uwanja wa Old Trafford jana(jumapili, 20, Desemba, 2017). Kwa mujibu wa gazeti la Guardian la Uingereza chupa na ngumi zilirushwa baada ya mchezo huo ambao Manchester City ilishinda 2-1 dhidi ya mahasimu wao wa jiji, Manchester United na msaidizi wa kocha meneja wa Manchester city, Pep Guardioa, Mikel Arteta aliondoka akiwa ametapakaa damu chini ya uso wake. Machafuko hayo yalidaiwa kuanza baada ya meneja wa Manchester United, Jose Mourinho kugonga mlango wa chumba cha wapinzani wake kuwaambia wachezaji hao kupunguza sauti ya muziki wao. Punde baadae Mourinho alijikuta katika mzozo mwingine na kipa wa Manchester city, Mbrazili Ederson, ambapo Mourinho alidai mchezaji huyo alikua anapoteza muda kwa makus...

GIGGS ANALAUMIWA NA BABA YAKE KWA KUHARIBU MAISHA YA MDOGO WAKE.

Mdogo wa mchezaji wazamani wa Manchester United, RYAN Giggs amebaki bila makazi wala kazi baada ya maisha yake kuvurugwa na kaka yake huyo kwa kwa kujihuaisha na mkewe kimapenzi. Rhodri Giggs, mwenye umri wa miaka 40, amelazimika kukaa na familia baada ya "kutelekezwa" na ndugu yake millionea. Lakini mchezaji huyo wa zamani wa Manchester United, mwenye umri wa miaka 43, hajawahi kumwomba msamaha ndugu yake kwa kumsaliti, anadai baba yao mzazi. Mahusiano ya miaka nane ya Ryan na mke wa mdogo wake, Rhodri, Natasha, mwenye umri wa miaka 35, yalibainika mwaka 2011. RHODRI GIGGS. Picha:Planet Photos. Baba yao, Danny, mwenye umri wa miaka 61, alisema: "Ikiwa angeomba msamaha tu Rhodri anaweza tu kuendelea lakini hakuomba msamaha na amemtelekeza ndugu yake. " MKE WA RHODRI AMBAE ALIKUWA NA UHUSIANO WA KIMAPENZI NA RYAN. Picha:FLYNET.  Rhodri ambaye kwa sasa hana kipato chochote alihamia Wales kutoka Manchester mapema mwezi huu ili kupata msaada w...

ORODHA YA NCHI 80 AMBAZO MTANZANIA ANARUHUSIWA KUINGIA BILA VIZA.

         Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni amesema kuna zaidi ya nchi 80 ambazo watanzania wanaweza kusafiri bila ya kuwa na viza . Mhandisi Hamad Masauni amesema kuna zaidi ya nchi 80 ambazo watanzania wanaweza kusafiri bila ya kuwa na viza za kusafiria kama ilivyokuwa nchi za afrika Mashariki. Mhandisi Massauni amebainisha hayo leo bungeni wakati akijibu swali la Mbunge wa Mlalo kupitia tiketi ya CCM Rashid Shangazi aliyetaka kujua ni nchi ngapi ambazo watanzania wanaweza kusafiri bila ya kuwa na viza (viza on arrival). "Zipo nchi 16 kwa Afrika ambazo watanzania wanaweza kuzitembelea bila ya kuwa na viza na duniani zipo 67" alisema Masauni. Aidha Massauni amezitaja nchi hizo kuwa ni Benin, Burkina Faso, Cape Verde, Ivory Coast, Djibouti, Gabon, Gambia, Guinea, Guinea­Bissau, Liberia, Mali, Mauritania, Niger, Sierra Leone pamoja na Togo. Pamoja na hayo Masauni amesema...

KASHFA YA MAPENZI KATI MH.MBOWE NA WEMA SEPETU.

MH.FREEMAN MBOWE AKIWA NA WEMA SEPETU. Siku chache baada ya ile skendo ya ngono iliyosababisha wakili na mshauri wa Chama cha ACT -Wazalendo , Bwana Albert Msando kujiuzulu kwenye nyadhifa yake ya chama ,yameibuka mangine kwenye chama kikuu cha upinzani Tanzania ,CHADEMA ,baada ya kusambaa kwa kipande cha sauti kinachodaiwa kua ni mazungumzo kati ya mwenyekiti wa chama hicho na mbunge wa Hai Mh.Freeman Mbowe na Miss Tanzania 2006 ,mrembo Wema Isack Sepetu. SIKILIZA HIVI VIPANDE VYA SAUTI: Bonyeza hapa chini kusikiliza maongezi hayo yanayodaiwa kuwa ni kati ya Wema Sepetu na Mh.Freeman Mbowe; Bonyeza hapa chini kusikiliza majibu ya Wema Sepetu; Bonyeza hapa chini kusikiliza majibu ya Mh.Freeman Mbowe; VYANZO: Jamii Forums,                   YouTube.com,                   Perfect255.com.                   

SABABU ZA KUVUNJIKA KWA KUNDI LA P-SQUARE.

WANAMUZIKI MAPACHA WA KUNDI LA PSQUARE, PETER (KUSHOTO) NA PAUL (KULIA) WAKIWA NA KAKA YAO AMBAE PIA NI MENEJA WAO, JUDES OKOYE. Mwanamuziki wa kundi la PSquare kutoka Nigeria, Peter Okoye ametangaza kujitoa kwenye kundi hilo la muziki wa Pop maarufu zaidi Afrika. Msanii huyo alidai kwamba amewasilisha maombi ya kuvunja kundi hilo katika barua aliyoandika kwa wakili wao Festus Keyamo. Kulingana na nakala ya barua iliyotolewa kwenye vyombo vya habari Jumatatu,Tarehe 25 Septemba, Peter alisema kuwa pacha wake na, Paul, na kaka yao, Judes waliahirisha ziara yao ya muziki ya Marekani bila kushauriana naye.Na hiyo ni moja kati ya sababu za msingi. Peter pia aliwalaumu Paul na kaka yao mkubwa mkubwa ambae ni meneja wao pia kwa udanganyifu walioufanya ili kutatua shida waliyokuwa nayo juu ya biashara ya muziki. Wasanii hao ndugu wamekua kwenye vita vya maneno kwenye mitandao ya kijamii tangu mwisho wa mwaka jana pamoja na juhudi za watu wao wa karibu kujaribu kuwapatanisha kifami...