Skip to main content

IGP MANGU KUONDOLEWA? ,ILISHATABILIWA KITAAMBO !!!

IGP ERNEST MANGU.


Ikiwa ni siku moja tu tangu Kurugenzi ya Habari Ikulu ilipotoa taarifa ya kumpandisha cheo mkuu wa polisi wa kanda maalumu ya Dar es Salaam, kamanda Simon Sirro kuwa mkuu wa polisi Tanzania na kutoa tamko kwamba mkuu wa jeshi hilo wa sasa Inspekta Jenerali Ernest Mangu atapangiwa kazi nyingine, Taarifa hiyo imepokelewa kwa mawazo tofauti tofauti na wananchi hasa ikiwa wengi wanajiuliza ni kwanini IGP Mangu ametolewa katika nyadhifa hiyo ya juu kabisa kwenye jeshi la polisi kabla ya muda wake wa kustaafu kufika !!!.
       
BARUA  KUTOKA IKULU KWA WAANDISHI WA HABARI.


    Chanzo cha blog yetu (Kioo17) siku ile ile ya jana 28 Mei 2017 ,kilibahatika kupata maoni ya mchambuzi nguli wa mambo ya siasa Bwana Malisa GJ alitukumbusha kwamba kuna mwanahabari wa gazeti la "MwanaHalisi" bwana Charles William           Alibashili haya ya jana takribani miaka miwili iliyopita !!!.

SOMA HII;

MALISA GJ: 
Mdogo wangu Charles William aliandika miaka miwili iliyopita kuwa Ernest Mangu atang'olewa ktk nafasi yake ya IGP na kupewa Simon Siro. Soma makala hii iliyoandikwa na Charless William na kuchapwa na gazeti la Mwanahalisi la December 21, mwaka 2015.
_____________________________________________

JGP MANGU KUNG'OKA

Na Charles William,
MwanaHALISI - Desemba 21, 2015.
__________________________________

Rais na Amiri Jeshi Mkuu, Dk. John Magufuli anajiandaa kufanya mabadiliko makubwa ndani ya Jeshi la Polisi kwa kumuondoa Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP) Ernest Mangu.

Taarifa zilizopatikana kutoka kwa mmoja wa maofisa wa Ikulu zinaeleza kuwa Dk. Magufuli sasa anahitaji kuwa na mkuu mpya wa Jeshi hilo huku IGP Mangu akitarajiwa kupewa ubalozi katika mojawapo ya nchi za Afrika, kusini mwa jangwa la Sahara na Naibu wake Abdurahmani Kaniki akitarajiwa kushushwa ngazi na kuwa mkuu wa polisi katika mkoa mojawapo kanda ya ziwa.

Iwapo Rais Magufuli atabadilisha mkuu wa jeshi hilo, IGP Mangu atakuwa amelitumikia jeshi hilo kwa muda wa miaka miwili tu baada ya kuteuliwa na Rais Kikwete kushika wadhifa huo Desemba 30, 2013 akitokea ofisi ya Polisi wa kimataifa (Interpol) jijini Nairobi, Kenya.

Wanaotajwa kuwa kwenye nafasi ya kumrithi IGP Mangu ni pamoja na mkuu wa Operesheni wa polisi, Simon Siro na mkuu wa Interpol Gustav Babile.

Kwasasa waliopo katika nafasi za juu za jeshi hilo ni kamishna Glodwig Mtweve (fedha na utawala), Mussa Ally Mussa (Polisi Jamii makao makuu), Thobias Andengenye (utawala na utumishi) na Diwani Athumani (Mkuu wa intelijensia ya jinai DCI).

Haya yanakuja ikiwa ni wiki mbili tu tangu Rais Magufuli afanye mabadiliko ya kushitua  akimuhamisha Kamishina wa Operesheni na Mafunzo Paul Chagonja na kumpeleka kuwa mkuu wa jeshi la zimamoto na uokoaji huku mkuu wa idara ya intelijensia Valentino Mlowola akiteuliwa kuwa kaimu mkurugenzi wa TAKUKURU.........
______________
©Charles William.



Comments

Habari Nyingine Kutoka Kioo17 Swahili;

MOURINHO KUMUONDOA MKHITARYAN ILI AWEZE KUMSAJILI OZIL.

Henrikh Mkhitaryan atatupwa kando na meneja wa Manchester United Jose Mourinho ili apate nafasi ya kumsajili jiungo wa Arsenal, Mesut Ozil, kulingana na taarifa.  Bosi huyo wa Manchester United anajua lazima apunguze kikosi chake kama atataka kumsajili Ozil kutokana na madai ya mshahara mkubwa ya bingwa huyo wa Kombe la Dunia. Kiungo huyo mchezeshaji huyo ambaye mkataba wake Arsenal umalizika mwishoni mwa msimu huu, amekuwa akiomba mshahala wa Pauni Laki Tatu (£ 300,000) kwa wiki ili kukubali mkataba mpya wa kuendelea kuchezea Arsenal. Gazeti la 'The Mirror' la Uingereza limeripoti kwamba Mourinho ameamua Mkhitaryan, ambaye alijiunga na klabu kutoka Borussia Dortmund mwaka 2016, anaweza kuwa mchezaji kuondoka Ni uchaguzi wa mantiki kulingana na hali ya sasa ya mchezaji huyo katika kikosi cha Manchester United. Mchezaji huyo kutoka Armenia ameachwa mechi nane za mwisho na Mourinho huku akisema kuwa haamini kama kiungo huyo anastahilo kukukaa katika...

MCHEZAJI WA ZAMANI WA UINGEREZA AMESEMA ALICHEZA NA WACHEZAJI WATATU MASHOGA KWENYE TIMU.

Carl Hoefkens (jezi no.2) alichezea West Bromwich Albion na Stoke City wakati wa enzi zake ligi kuu ya England. Beki wa zamani wa Ligi Kuu ya Uingereza amesema alicheza pamoja na wachezaji wenzake wawili wa mashoga ndani ya timu, na mmoja alikua na jina kubwa. Carl Hoefkens, West Bromwich Albion na Stoke City siku za nyuma, anasema wachezaji hao walikua wazi na hawakujificha kwenye vyumba vya kubadilishia nguo ingawa bado hawajulikani kwasababu ya maombi yao wenyewe ya kuomba kutotangazwa. Justin Fashanu, ambaye alijiua mwaka 1998, alikuwa mchezaji wa mwisho wa kazi nchini England kuja nje kama mashoga - mwaka 1990. Hoefkens alipokua (kushoto), alipokua anachezea Stock  City. Hoefkens aliyecheza Uingereza kwa miaka minne, akiondoka mwaka 2009, alidai kuwa mchezaji mwenzake mmoja wa timu alikua anaweza kuja kwenye uwanja wa mafunzo ya klabu na mpenzi wake wa kiume  lakini aliwaomba wenzake kutokuwaambia watu wangine wa nje ya timu. 'Nilicheza pamoja n...

ORODHA YA NCHI 80 AMBAZO MTANZANIA ANARUHUSIWA KUINGIA BILA VIZA.

         Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni amesema kuna zaidi ya nchi 80 ambazo watanzania wanaweza kusafiri bila ya kuwa na viza . Mhandisi Hamad Masauni amesema kuna zaidi ya nchi 80 ambazo watanzania wanaweza kusafiri bila ya kuwa na viza za kusafiria kama ilivyokuwa nchi za afrika Mashariki. Mhandisi Massauni amebainisha hayo leo bungeni wakati akijibu swali la Mbunge wa Mlalo kupitia tiketi ya CCM Rashid Shangazi aliyetaka kujua ni nchi ngapi ambazo watanzania wanaweza kusafiri bila ya kuwa na viza (viza on arrival). "Zipo nchi 16 kwa Afrika ambazo watanzania wanaweza kuzitembelea bila ya kuwa na viza na duniani zipo 67" alisema Masauni. Aidha Massauni amezitaja nchi hizo kuwa ni Benin, Burkina Faso, Cape Verde, Ivory Coast, Djibouti, Gabon, Gambia, Guinea, Guinea­Bissau, Liberia, Mali, Mauritania, Niger, Sierra Leone pamoja na Togo. Pamoja na hayo Masauni amesema...

JINSI YA KUOMBA PASSPORT YA TANZANIA KWA NJIA YA INTERNET.

Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kupitia i dara ya Uhamiaji  imezindua huduma ya ujazaji fomu za maombi ya hati ya kusafiria (Passport) kwa njia ya mtandao, ambapo mwombaji atalazimika kujaza fomu hizo na kuzichapisha kabla ya kuziwasilisha kwenye ofisi za uhamiaji. Idara hiyo pia imeeleza kuwa matumizi ya huduma hiyo yataenda sambamba na huduma inayotumiwa sasa ya fomu za maombi ya pasipoti mpaka pale itakapotangazwa vinginevyo. Huduma hiyo itaanza kufanya kazi kuanzia Jumatatu tarehe  7/8/2017    na unaweza  kujaza fomu hizo  kwa kufungua tovuti hiyo ambayo ni  https://www.immigration.go.tz/ppt_application/ Utaratibu wa namna ya kujaza fomu hizo umeelekezwa katika fomu husika mtandaoni, na pia wateja wanaweza kupata ufafanuzi au maelezo zaidi kuhusu huduma hiyo kupitia anuani ya Idara ya Uhamiaji ambayo ni   info@immigration.go.tz   au katika Ofisi yoyote ya Uhamiaji iliyo karibu yako. CHANZO: http://dibute.com/muhimu-...

BAYERN MUNICH WANAJENGA VYUMBA VYA HOTELI NDANI YA UWANJA.

Huu ndio utakaokuwa muonekano wa vyumba hivyo kwa ndani. Picha: Mariot International. Kama sehemu ya mpango wa miaka mingi ya Bayern na  kampuni kubwa ya hoteli za Mariot na Courtyard, mashabiki hivi karibuni wataweza kupata fursa ya kukaa katika vyumba ambavyo vina dirisha linaloangalia uwanja wa Alianz Arena moja kwa moja. Vyumba hivyo vya kifahari vya kulala vitakuwa na kitanda cha kikubwa na seti ya televisheni - tu ikiwa umechoka na hat-trick za Robert Lewandowski. Pia kutakuwa na mahali pa moto ambayo ni maalumu kwa siku za mechi kwenye majira ya baridi. Mkurugenzi Mtendaji wa Bayern Karl-Heinz Rummenigge alisema: "Tunafurahia bidhaa mbili zinazoongoza kama hoteli Courtyard zinazomilikiwa na kampuni ya Marriott na FC Bayern kuingia katika ushirikiano huu wa muda mrefu kibiashara. "Tunapendezwa na bidhaa mbili zinazoongoza kama Courtyard na Marriott na FC Bayern kuingia katika ushirikiano wa muda mrefu," "Kutokana na kwamba Marri...

ORODHA YA NCHI ZA KWANZA NA ZA MWISHO KWA AMANI DUNIANI.

Marekani:  Ripoti ya Taasisi ya Uchumi na Amani imepata mataifa kumi tu ulimwenguni ambayo hayapo katika vita na migogoro kabisa. Kwa mujibu wa Ripoti ya Kimataifa ya Amani 2016, Botswana, Chile, Costa Rica, Japan, Mauritius, Panama, Qatar, Uswisi, Uruguay na Vietnam ndio nchi pekee ambazo hazipo kwenye vita wala migogoro yeyote ile ya kuhatarisha amani.. Iceland inaongoza orodha ya nchi zinazoongoza kwa amani ulimwenguni, ikifuatiwa na Denmark, Austria, New Zealand, Ureno, Jamhuri ya Czech, Uswisi, Canada, Japan na Slovenia - wakati Marekani ikiwa kwenye nafasi ya 103. Palestina imepanda kutoka nafasi ya 163 mpaka nafasi ya 148. Syria iliyoharibiwa na vita imewekwa chini ya orodha, chini kuliko Sudan Kusini, Iraq, Afghanistan, Somalia, Yemen, Jamhuri ya Afrika ya Kati, Ukraine, Sudan na Libya. "Ripoti inalinganisha amani duniani kwa kutumia mandhari tatu pana: hali ya utulivu na usalama katika jamii; kiwango cha mgogoro wa ndani au wa kimataifa; na kiwango cha kije...

VIDEO YA NDEGE KUBWA ZAIDI DUNIANI.

Ndege kubwa kuliko zote duniani inasemekana kuwa katika hatua za mwisho za maandalizi ya kuanza safari zake. Ndege hiyo inayoitwa Stratolaunch yenye injini sita aina turbofan zenye uzito wa kilo 40000 (tani 4) kila moja. Utengenezaji wa ndege hiyo ni maono ya mwanzilishi mwenza wa kampuni ya Microsoft, ambaye anataka ndege hiyo ndio iwe chombo cha usafiri kikubwa zaidi angani ,chenye kasi zaidi na gharama nafuu kukiendesha kulinganisha na za teknolojia zilizopo sasa. Mabawa ya ndege hiyo ni marefu kuliko uwanja wa mpira wa miguu ambapo kama ukiiweka katikati ya uwanja wa mpira, mabawa yake yatazidi kwa kwa futi 12.5 (mita 3.8) nyuma ya kila goli. Tazama kipande hiki cha Video: CHANZO: dailymail.co.uk