Skip to main content

IGP MANGU KUONDOLEWA? ,ILISHATABILIWA KITAAMBO !!!

IGP ERNEST MANGU.


Ikiwa ni siku moja tu tangu Kurugenzi ya Habari Ikulu ilipotoa taarifa ya kumpandisha cheo mkuu wa polisi wa kanda maalumu ya Dar es Salaam, kamanda Simon Sirro kuwa mkuu wa polisi Tanzania na kutoa tamko kwamba mkuu wa jeshi hilo wa sasa Inspekta Jenerali Ernest Mangu atapangiwa kazi nyingine, Taarifa hiyo imepokelewa kwa mawazo tofauti tofauti na wananchi hasa ikiwa wengi wanajiuliza ni kwanini IGP Mangu ametolewa katika nyadhifa hiyo ya juu kabisa kwenye jeshi la polisi kabla ya muda wake wa kustaafu kufika !!!.
       
BARUA  KUTOKA IKULU KWA WAANDISHI WA HABARI.


    Chanzo cha blog yetu (Kioo17) siku ile ile ya jana 28 Mei 2017 ,kilibahatika kupata maoni ya mchambuzi nguli wa mambo ya siasa Bwana Malisa GJ alitukumbusha kwamba kuna mwanahabari wa gazeti la "MwanaHalisi" bwana Charles William           Alibashili haya ya jana takribani miaka miwili iliyopita !!!.

SOMA HII;

MALISA GJ: 
Mdogo wangu Charles William aliandika miaka miwili iliyopita kuwa Ernest Mangu atang'olewa ktk nafasi yake ya IGP na kupewa Simon Siro. Soma makala hii iliyoandikwa na Charless William na kuchapwa na gazeti la Mwanahalisi la December 21, mwaka 2015.
_____________________________________________

JGP MANGU KUNG'OKA

Na Charles William,
MwanaHALISI - Desemba 21, 2015.
__________________________________

Rais na Amiri Jeshi Mkuu, Dk. John Magufuli anajiandaa kufanya mabadiliko makubwa ndani ya Jeshi la Polisi kwa kumuondoa Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP) Ernest Mangu.

Taarifa zilizopatikana kutoka kwa mmoja wa maofisa wa Ikulu zinaeleza kuwa Dk. Magufuli sasa anahitaji kuwa na mkuu mpya wa Jeshi hilo huku IGP Mangu akitarajiwa kupewa ubalozi katika mojawapo ya nchi za Afrika, kusini mwa jangwa la Sahara na Naibu wake Abdurahmani Kaniki akitarajiwa kushushwa ngazi na kuwa mkuu wa polisi katika mkoa mojawapo kanda ya ziwa.

Iwapo Rais Magufuli atabadilisha mkuu wa jeshi hilo, IGP Mangu atakuwa amelitumikia jeshi hilo kwa muda wa miaka miwili tu baada ya kuteuliwa na Rais Kikwete kushika wadhifa huo Desemba 30, 2013 akitokea ofisi ya Polisi wa kimataifa (Interpol) jijini Nairobi, Kenya.

Wanaotajwa kuwa kwenye nafasi ya kumrithi IGP Mangu ni pamoja na mkuu wa Operesheni wa polisi, Simon Siro na mkuu wa Interpol Gustav Babile.

Kwasasa waliopo katika nafasi za juu za jeshi hilo ni kamishna Glodwig Mtweve (fedha na utawala), Mussa Ally Mussa (Polisi Jamii makao makuu), Thobias Andengenye (utawala na utumishi) na Diwani Athumani (Mkuu wa intelijensia ya jinai DCI).

Haya yanakuja ikiwa ni wiki mbili tu tangu Rais Magufuli afanye mabadiliko ya kushitua  akimuhamisha Kamishina wa Operesheni na Mafunzo Paul Chagonja na kumpeleka kuwa mkuu wa jeshi la zimamoto na uokoaji huku mkuu wa idara ya intelijensia Valentino Mlowola akiteuliwa kuwa kaimu mkurugenzi wa TAKUKURU.........
______________
©Charles William.



Comments

Habari Nyingine Kutoka Kioo17 Swahili;

MCHEZAJI WA ZAMANI WA UINGEREZA AMESEMA ALICHEZA NA WACHEZAJI WATATU MASHOGA KWENYE TIMU.

Carl Hoefkens (jezi no.2) alichezea West Bromwich Albion na Stoke City wakati wa enzi zake ligi kuu ya England. Beki wa zamani wa Ligi Kuu ya Uingereza amesema alicheza pamoja na wachezaji wenzake wawili wa mashoga ndani ya timu, na mmoja alikua na jina kubwa. Carl Hoefkens, West Bromwich Albion na Stoke City siku za nyuma, anasema wachezaji hao walikua wazi na hawakujificha kwenye vyumba vya kubadilishia nguo ingawa bado hawajulikani kwasababu ya maombi yao wenyewe ya kuomba kutotangazwa. Justin Fashanu, ambaye alijiua mwaka 1998, alikuwa mchezaji wa mwisho wa kazi nchini England kuja nje kama mashoga - mwaka 1990. Hoefkens alipokua (kushoto), alipokua anachezea Stock  City. Hoefkens aliyecheza Uingereza kwa miaka minne, akiondoka mwaka 2009, alidai kuwa mchezaji mwenzake mmoja wa timu alikua anaweza kuja kwenye uwanja wa mafunzo ya klabu na mpenzi wake wa kiume  lakini aliwaomba wenzake kutokuwaambia watu wangine wa nje ya timu. 'Nilicheza pamoja n...

KIONGOZI MKUU WA UPINZANI NCHINI ZIMBABWE, MORGAN TSVANGIRAI AMEFARIKI DUNIA.

Kiongozi wa upinzani wa Zimbabwe Morgan Tsvangirai amefariki dunia nchini Afrika Kusini, afisa mkuu wa chama chake cha MDC amesema. Bw Tsvangirai, mwenye umri wa miaka 65, aliyekuwa waziri mkuu, alilipotiwa kuwa alikuwa akisumbuliwa na saratani ya koloni. "Amefariki jioni hii, familia yake imenitaarifu"  Makamu wa Rais wa MDC, Elias Mudzuri aliliambia shirika la habari la Uingereza, Reuters. Morgan Tsvangirai alizaliwa mnamo Machi 10, 1952 huko Gutu, Zimbabwe. Baba yake alikuwa mfanyakazi wa mgodi, fundi, na mkulima. Alihudhuria Shule ya Msingi ya Guco ya St. Marks. Kisha alihamishiwa Shule ya Msingi ya Chikara Gutu. Kwa elimu yake ya sekondari, alihudhuria Shule ya High Gokomere. Alikuwa waziri mkuu katika serikali ya mseto ya Zimbabwe tangu 2009 hadi 2013. Katika kazi yake ya awali alionekana kuwa mfanyakazi mwenye bidii sana na alifanya kazi katika mgodi wa madini ya nickel( kwa zaidi ya muongo mmoja. Alipanda cheo haraka kutambuliwa na akain...

MADAI YA CUBA KWAMBA WAZIRI MKUU WA CANADA NI MTOTO WA FIDEL CASTRO.

Pichani ni waziri mkuu wa Canada, Justin Trudeau (kushoto), na Rais wa zamani wa Cuba, Hayati Fidel Castro (kulia). Maelezo yaliyoandikwa na mtoto wa kwanza wa rais wa zamani wa Cuba , Fidel Castro, kabla ya kujiua yamelishtua taifa la Cuba wiki hii. Maelezo hayo yaliyoandikwa na mtoto huyo mkubwa wa mwanamapinduzi na rais wa zamani wa nchi hiyo yalikuwa ya kushangaza baada ya  kuwa na madai ya kuwa Waziri Mkuu wa Canada Justin Trudeau ni mtoto wa nje wa baba yake marehemu Fidel Castro. Maelezo hayo yaliyoandikwa kwa mkono na mtoto huyo wa Fidel Castro aliyejiua siku chache zilizopita kwa msongo wa mawazo, Fidel Castro Diaz-Balart, aliyekuwa na umri wa miaka 68, yalionekana kuthibitisha uvumi wa muda mrefu nchini Cuba kwamba Fidel Castro ni baba wa damu wa waziri mkuu wa sasa wa Canada, Justin Trudeau ikiwa ni matokeo ya uhusiano wa siri wa kimapenzi na mke wa mwanasiasa maarufu wa Canada, Pierre Trudeau, Margaret Trudeau mwaka 1970. Kifo cha mwanasayansi wa ...

MAAJABU YA "MTUME" ELVIS MBONYE.

Picha za zinazo onesha kasisi wa Uganda akipigwa mabusu na wafuasi wake miguuni tayari zimekwisha zua gumzo miongoni mwa vyombo vya habari na mitandao ya kijamii kwa siku za karibuni. Mtume Elvis Mbonye, ​​mwenye umri wa miaka 40, wa Zoe Fellowship, Jumapili iliyopita aliandaa tafrija ya chakula cha jioni kwa kiingilio cha takribani dola 185 (185$) kwa tiketi za platinum, dola 210 (210$) kwa tiketi za Gold, dola 135 (135$) kwa tiketi za Silver, na dola 75 (75$) kwa tiketi za kawaida. Ibada za Mbonye hufanyika siku za Jumanne kinyume na za makanisa mangine za Jumapili au Jumamosi, akisema Mungu alimwambia afanye ibada siku za Jumanne.  Wakati alipoanza kanisa mwaka 2014, Mbonye alikuwa na waumini 100, lakini sasa amefikisha waumini 5,000 , vyombo vya habari vya Uganda vinasema. Mbonye, ​​kabla ya kuhamishia ibada zake kwenye uwanja wa Rugby wa Kyadondo, alikua anakodisha hoteli ya kifahari ya Kampala kwa gharama sawa na dola 13,500 za kimarekani kila wiki. ...

CAVANI AGEUKA KIKWAZO KWA NEYMAR.

Image: AFP. Inafahamika kwamba moja kati ya vitu vilivyomshawishi mshambuliaji wa Brazil na timu ya Paris Saint Germain (PSG) ya Ufaransa, Neymar Jr kuondoka klabu yake ya zamani, Fc Barcelona ilikua ni wachezaji wenzake, hasa Lionel Messi. Aina maana kwamba Neymar alikua na uadui na Messi lakini kwasababu Neymar aliona hataweza kuwika kama anavyotaka mbele ya Messi. Kwa hiyo alienda PSG kujenga himaya yake akiamini anakwenda kuwa mchezaji mkubwa kuliko wote kwenye klabu hiyo. Maisha ya Neymar klabuni hapo yalianza vizuri kwa Neymar, akifunga mabao matano lakini inaonekana kuwa tayari kuna kitu hakimpendezi. Kwa mujibu wa kituo cha michezo ya Kifaransa SFR Sport ,nyota huyo wa zamani wa Santos hapendezwi na Edinson Cavani kwa sababu Cavani ndio mwenye jukumu la kupiga penati za klabu hiyo, jukumu ambalo Neymar analitaka. Image: G.d.S.S Inasemekana kwamba mchezaji huyo aliyevunja rekodi ya dunia ya ada ya uhamisho wakati akijiunga klabuni hapo tayari amelalamikia swala...

NAPE ASEMA KWAMBA TUNDU LISSU ALIMWAMBIA WANATAFUTWA, AHAME CCM.

MBUNGE WA MTAMA (CCM) AKICHEKA NA TUNDU LISSU MUDA MFUPI KABLA YA KUPIGWA RISASI. Imeandikwa na Edwin Mjwahuzi , Mwananchi; emjwahuzi@mwananchi.co.tz Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu (kulia) akifurahia jambo na mbunge wa Mtama, Nape Nnauye walipokuwa wakitoka kuhudhuria kikao cha Bunge, mjini Dodoma jana mchana. By Edwin Mjwahuzi, Mwananchi; emjwahuzi@mwananchi.co.tz Dodoma. Mbunge wa Mtama (CCM), Nape Nnauye ameeleza alichoambiwa na Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu jana Alhamisi mchana wakati wakitoka bungeni huku wakicheka. Nape amesema Lissu alimwambia, “Wewe Nape ni mjomba wangu, kwa nini unabaki CCM? Mimi na wewe tunafuatiliwa na jamaa zako wakitumia gari moja. Mimi na wewe ni watuhumiwa, hama CCM mjomba.” Lissu alipigwa risasi jana Alhamisi mchana na kupelekwa chumba cha upasuaji katika Hospitali ya Rufaa ya Dodoma na baadaye usiku alihamishiwa Hospitali ya Aga Khan ya Nairobi nchini Kenya. Mbunge wa Rombo, Joseph Selasini jana wakati Lissu...

SABABU ZA KUVUNJIKA KWA KUNDI LA P-SQUARE.

WANAMUZIKI MAPACHA WA KUNDI LA PSQUARE, PETER (KUSHOTO) NA PAUL (KULIA) WAKIWA NA KAKA YAO AMBAE PIA NI MENEJA WAO, JUDES OKOYE. Mwanamuziki wa kundi la PSquare kutoka Nigeria, Peter Okoye ametangaza kujitoa kwenye kundi hilo la muziki wa Pop maarufu zaidi Afrika. Msanii huyo alidai kwamba amewasilisha maombi ya kuvunja kundi hilo katika barua aliyoandika kwa wakili wao Festus Keyamo. Kulingana na nakala ya barua iliyotolewa kwenye vyombo vya habari Jumatatu,Tarehe 25 Septemba, Peter alisema kuwa pacha wake na, Paul, na kaka yao, Judes waliahirisha ziara yao ya muziki ya Marekani bila kushauriana naye.Na hiyo ni moja kati ya sababu za msingi. Peter pia aliwalaumu Paul na kaka yao mkubwa mkubwa ambae ni meneja wao pia kwa udanganyifu walioufanya ili kutatua shida waliyokuwa nayo juu ya biashara ya muziki. Wasanii hao ndugu wamekua kwenye vita vya maneno kwenye mitandao ya kijamii tangu mwisho wa mwaka jana pamoja na juhudi za watu wao wa karibu kujaribu kuwapatanisha kifami...