Skip to main content

OPERESHENI YA KWANZA YA KUPANDIKIZA KICHWA CHA BINADAMU.

DR.SERGIO CANAVERO.
     
 Dr.Sergio Canavero ,Daktari bingwa wa upasuaji (Neurosurgeon) kutoka Italia, ametangaza kufanya operesheni ya kwanza ya kupandikiza kichwa cha binadamu kutoka mwili mmoja kwenda mwingine.
        Akizungumza na gazeti la OOOM la Ujerumani, Dr.Canavero amesema operesheni hiyo itafanyika mwezi Desemba mwaka huu nchini China na jopo la madaktari 80 kwa masaa 36 na itagharimu dola milioni 10 (takribani shilingi bilioni 21 za kitanzania).
        Tayari mtu wa kujitolea kufanyiwa operesheni hiyo amepatikana.Mtu huyo anaitwa Valery Spiridonov.Spiridonov ni mzaliwa wa Urusi anaesumbuliwa na ugonjwa unaoitwa Werning-Hoffman,ugonjwa uliosababisha misuli na mishipa yake ya kuanzia shingoni mpaka miguuni kushindwa kufanya kazi kiusahihi.Spiridonov anaishi kwenye kiti cha wagonjwa(wheelchair) ,hawezi hata kula mwenyewe.
VALERY SPIRIDONOV.

Dr Canavero ameelezea jinsi watakavyo hamisha kichwa cha Spirinov na kukipandikiza kwenye mwili wa mtu mwingine ambae ubongo wake umekufa.

         Akifafanua jinsi watakavyo tekeleza operesheni hiyo, Dr.Canavero amesema kwanza watapooza joto la mwili wa Spiridonov mpaka kufikia Fahrenheit 50 ( nyuzi joto 10) ili na kutumia saa moja kukikata kichwa kwa nyembe maalum (Transparent Diamond Blades) na kukihamisha kabla ubongo haujafa.Pia amefafanua kwamba kichwa hicho kitaunganishwa na uti wa mgongo wa mwili mpya kwa kutumia kemikali iitwayo Polyethylene Glycol (PEG).

        Dr.Canavero anaamini operesheni hiyo itafanikiwa kwa asilimia 90 baada kufanikisha kupandikiza kichwa cha panya mdogo kwenye mwili wa panya mkubwa miezi michache iliyopita.
         Pia, anaami hivyo kutokana na kufanikiwa kwa operesheni ya kupandikiza kichwa kwa nyani iliyofanywa na Dr.Xiaoping Ren wa Harpin Medical University.
DR.CANAVERO AKIWA NA DR.XIAOPING REN ,ALIYEFANIKISHA KUPANDIKIZA KICHWA KWA NYANI.


         Hata hivyo jaribio hilo la Dr.Canavero limepokewa kwa maoni tofauti na watu mbalimbali akiwemo akiwemo mtaalamu Arthur Caplan wa New York University ambae taadharisha kwamba ni kitendo cha hatari na cha kipumbavu sababu kinahatarisha maisha ya mgonjwa.

CHANZO:Christian Gollayan,New York Post.
                 William McKinney, Edgylabs.com
       

Comments

Habari Nyingine Kutoka Kioo17 Swahili;

MCHEZAJI WA ZAMANI WA UINGEREZA AMESEMA ALICHEZA NA WACHEZAJI WATATU MASHOGA KWENYE TIMU.

Carl Hoefkens (jezi no.2) alichezea West Bromwich Albion na Stoke City wakati wa enzi zake ligi kuu ya England. Beki wa zamani wa Ligi Kuu ya Uingereza amesema alicheza pamoja na wachezaji wenzake wawili wa mashoga ndani ya timu, na mmoja alikua na jina kubwa. Carl Hoefkens, West Bromwich Albion na Stoke City siku za nyuma, anasema wachezaji hao walikua wazi na hawakujificha kwenye vyumba vya kubadilishia nguo ingawa bado hawajulikani kwasababu ya maombi yao wenyewe ya kuomba kutotangazwa. Justin Fashanu, ambaye alijiua mwaka 1998, alikuwa mchezaji wa mwisho wa kazi nchini England kuja nje kama mashoga - mwaka 1990. Hoefkens alipokua (kushoto), alipokua anachezea Stock  City. Hoefkens aliyecheza Uingereza kwa miaka minne, akiondoka mwaka 2009, alidai kuwa mchezaji mwenzake mmoja wa timu alikua anaweza kuja kwenye uwanja wa mafunzo ya klabu na mpenzi wake wa kiume  lakini aliwaomba wenzake kutokuwaambia watu wangine wa nje ya timu. 'Nilicheza pamoja n...

ORODHA YA NCHI 80 AMBAZO MTANZANIA ANARUHUSIWA KUINGIA BILA VIZA.

         Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni amesema kuna zaidi ya nchi 80 ambazo watanzania wanaweza kusafiri bila ya kuwa na viza . Mhandisi Hamad Masauni amesema kuna zaidi ya nchi 80 ambazo watanzania wanaweza kusafiri bila ya kuwa na viza za kusafiria kama ilivyokuwa nchi za afrika Mashariki. Mhandisi Massauni amebainisha hayo leo bungeni wakati akijibu swali la Mbunge wa Mlalo kupitia tiketi ya CCM Rashid Shangazi aliyetaka kujua ni nchi ngapi ambazo watanzania wanaweza kusafiri bila ya kuwa na viza (viza on arrival). "Zipo nchi 16 kwa Afrika ambazo watanzania wanaweza kuzitembelea bila ya kuwa na viza na duniani zipo 67" alisema Masauni. Aidha Massauni amezitaja nchi hizo kuwa ni Benin, Burkina Faso, Cape Verde, Ivory Coast, Djibouti, Gabon, Gambia, Guinea, Guinea­Bissau, Liberia, Mali, Mauritania, Niger, Sierra Leone pamoja na Togo. Pamoja na hayo Masauni amesema...

CRISTIANO RONALDO MSHINDI WA TUZO YA BALLON d'OR 2017.

CRISTIANO RONALDO ametangazwa kuwa mshindi wa tuzo ya Ballon d'Or kwa mara ya tano na kufikia rekodi ya mshindani wake mkubw Lionel Messi. Mshambuliaji huyo wa Real Madrid, ambaye amekuwa mchezaji wa kwanza kufunga goli katika kila mchezo wa hatua ya makundi ya ligi ya Mabingwa wa Ulaya msimu huu, bado haoneshi dalili ya kushuka kiwango chake cha soka. Tazama kipande kifupi cha Video ya tukio hilo hapa: Hapa kuna orodha kamili inayohesabiwa kutoka kwenye 29 ya pamoja hadi CR7. 29th: Coutinho/Mertens 28th: Dzeko 27th: Hummels 26th: Oblak 25th: Benzema 24th: Falcão 23rd: Mané 21st: Bonucci/Aubameyang 20th: De Gea 19th: Hazard 18th: Griezmann 17th: Kroos 16th: Marcelo 15th: Dybala 14th: KDB 13rd: Suarez 12th: Isco 11th: Edinson Cavani 10th: Harry Kane 9th: Robert Lewandowski 8th: N’Golo Kante 7th: Kylian Mbappe 6th: Sergio Ramos 5th: Luka Modric 4th: Gianluigi Buffon 2nd: Neymar 2nd: Lionel Messi 1st: Cristiano Ronaldo CHANZO: thesun...

WASTANI WA ADA ZA VYUO VIKUU BORA ZAIDI DUNIANI.

            Elimu ya juu ya kupokea nje ya nchi (Nchi zilzo endelea) daima imekuwa kiwango cha kutambuliwa sana, na wanafunzi kutoka duniani kote siku zote wana ndoto kuhusu hilo.             Tovuti ya Bright Side imeamua kujua gharama za sasa za kujifunza * kwa wanafunzi wa kimataifa katika vyuo vikuu vya juu vya dunia, na tungependa kushiriki habari hii na wewe. * Wastani wa kila mwaka ada ya mafunzo ya shahada ya kwanza ; MAREKANI; Kwa maelezo zaidi kuhusiana na chuo hiki bonyeza hapa: http://www.harvard.edu/ Kwa maelezo zaidi kuhusiana na chuo hiki bonyeza hapa:  http://web.mit.edu/ UINGEREZA;     Kwa maelezo zaidi kuhusiana na chuo hiki bonyeza hapa; http://www.cam.ac.uk/     Kwa maelezo zaidi kuhusiana na chuo hiki bonyeza hapa: http://www.ox.ac.uk/ USWISI (SWITZERLAND ):     Kwa maelezo zaidi kuhusiana na chuo hiki bonyeza hapa:...

TUPAC SHAKUR ALIBAKWA JELA !!!

             Ulimwengu wa filamu za Hollywood na muziki wa Hip Hop juzi ulipatwa na mshangao baada ya mtayarishaji wa filamu inayohusu maisha ya hayati Tupac Shakur ,L.T Hutton kuelezea sababu zilizomfanya kumbadilisha muongozaji wa filamu hiyo kutoka John Singleton na kumuweka muongozaji Benny "Boom" Douglas.  Filamu hiyo inayoitwa "all eyez on me" tayari imekwisha andaliwa na inatarajiwa kuzinduliwa leo tarehe 16 Juni 2017.       Akizungumza kwenye mahojiano redioni L.T Hutton amewashtusha watu wengi baada ya kudai kwamba walishindwana na muongozaji wa mwanzo bwana John Singleton sababu muongozaji huyo aling'ang'ania kuwepo kwa matukio (scene) ambazo kwa maoni yake zisingependeza.        Matukio ambayo John Singleton alipenda yawepo katika filamu hiyo ni pamoja na kutaka filamu hiyo ianze na scene ya Tupac akilazimisha kumlawiti msichana wa kizungu.!!!          Singleton pia ali...

MTOTO WA GADDAFI AMETANGAZA KURUDI KWENYE SIASA ZA LIBYA.

Mwana wa rais wa zamani wa Libya, Muammar Gaddafi, Saif Al-Islam Gaddafi, anajitayarisha kurudi kwenye siasa katika nchi hiyo ya Afrika Kaskazini, ripoti zimesema. Saif al-Islam Gaddafi alitolewa jela mwezi Juni baada ya kushikiliwa kwa miaka sita na wanamgambo wa mji wa Zintan kufuatia uasi wa wanamgambo waliokuwa wakisaidiwa na majeshi ya Nato nchini Libya mwaka 2011. Mwanasheria wa Saif al-Islam Khaled al-Zaidi, akizungumza katika mji mkuu wa Tunisia, Tunis, aliwaambia waandishi wa habari Saif al-Islam anarudi kwenye medani za kisiasa kwenye nchini Libya, akiongeza kuwa alikuwa na afya njema. "Anafanya kazi za siasa kutoka kwenye ngome yake Libya, na makabila, pamoja na miji, na wabunge,"  Zaidi alisema. "Ana afya nzuri ... katika hali ya juu. Hali yake ya matibabu na kisaikolojia ni nzuri. "Lengo ni kufikia amani Libya," alisema Zaidi. "Anafuatilia mambo ya Libya karibu kila siku." Bwana Gaddafi, ambaye alisoma katika Shule ya Uch...

MOURINHO KUMUONDOA MKHITARYAN ILI AWEZE KUMSAJILI OZIL.

Henrikh Mkhitaryan atatupwa kando na meneja wa Manchester United Jose Mourinho ili apate nafasi ya kumsajili jiungo wa Arsenal, Mesut Ozil, kulingana na taarifa.  Bosi huyo wa Manchester United anajua lazima apunguze kikosi chake kama atataka kumsajili Ozil kutokana na madai ya mshahara mkubwa ya bingwa huyo wa Kombe la Dunia. Kiungo huyo mchezeshaji huyo ambaye mkataba wake Arsenal umalizika mwishoni mwa msimu huu, amekuwa akiomba mshahala wa Pauni Laki Tatu (£ 300,000) kwa wiki ili kukubali mkataba mpya wa kuendelea kuchezea Arsenal. Gazeti la 'The Mirror' la Uingereza limeripoti kwamba Mourinho ameamua Mkhitaryan, ambaye alijiunga na klabu kutoka Borussia Dortmund mwaka 2016, anaweza kuwa mchezaji kuondoka Ni uchaguzi wa mantiki kulingana na hali ya sasa ya mchezaji huyo katika kikosi cha Manchester United. Mchezaji huyo kutoka Armenia ameachwa mechi nane za mwisho na Mourinho huku akisema kuwa haamini kama kiungo huyo anastahilo kukukaa katika...