Skip to main content

OPERESHENI YA KWANZA YA KUPANDIKIZA KICHWA CHA BINADAMU.

DR.SERGIO CANAVERO.
     
 Dr.Sergio Canavero ,Daktari bingwa wa upasuaji (Neurosurgeon) kutoka Italia, ametangaza kufanya operesheni ya kwanza ya kupandikiza kichwa cha binadamu kutoka mwili mmoja kwenda mwingine.
        Akizungumza na gazeti la OOOM la Ujerumani, Dr.Canavero amesema operesheni hiyo itafanyika mwezi Desemba mwaka huu nchini China na jopo la madaktari 80 kwa masaa 36 na itagharimu dola milioni 10 (takribani shilingi bilioni 21 za kitanzania).
        Tayari mtu wa kujitolea kufanyiwa operesheni hiyo amepatikana.Mtu huyo anaitwa Valery Spiridonov.Spiridonov ni mzaliwa wa Urusi anaesumbuliwa na ugonjwa unaoitwa Werning-Hoffman,ugonjwa uliosababisha misuli na mishipa yake ya kuanzia shingoni mpaka miguuni kushindwa kufanya kazi kiusahihi.Spiridonov anaishi kwenye kiti cha wagonjwa(wheelchair) ,hawezi hata kula mwenyewe.
VALERY SPIRIDONOV.

Dr Canavero ameelezea jinsi watakavyo hamisha kichwa cha Spirinov na kukipandikiza kwenye mwili wa mtu mwingine ambae ubongo wake umekufa.

         Akifafanua jinsi watakavyo tekeleza operesheni hiyo, Dr.Canavero amesema kwanza watapooza joto la mwili wa Spiridonov mpaka kufikia Fahrenheit 50 ( nyuzi joto 10) ili na kutumia saa moja kukikata kichwa kwa nyembe maalum (Transparent Diamond Blades) na kukihamisha kabla ubongo haujafa.Pia amefafanua kwamba kichwa hicho kitaunganishwa na uti wa mgongo wa mwili mpya kwa kutumia kemikali iitwayo Polyethylene Glycol (PEG).

        Dr.Canavero anaamini operesheni hiyo itafanikiwa kwa asilimia 90 baada kufanikisha kupandikiza kichwa cha panya mdogo kwenye mwili wa panya mkubwa miezi michache iliyopita.
         Pia, anaami hivyo kutokana na kufanikiwa kwa operesheni ya kupandikiza kichwa kwa nyani iliyofanywa na Dr.Xiaoping Ren wa Harpin Medical University.
DR.CANAVERO AKIWA NA DR.XIAOPING REN ,ALIYEFANIKISHA KUPANDIKIZA KICHWA KWA NYANI.


         Hata hivyo jaribio hilo la Dr.Canavero limepokewa kwa maoni tofauti na watu mbalimbali akiwemo akiwemo mtaalamu Arthur Caplan wa New York University ambae taadharisha kwamba ni kitendo cha hatari na cha kipumbavu sababu kinahatarisha maisha ya mgonjwa.

CHANZO:Christian Gollayan,New York Post.
                 William McKinney, Edgylabs.com
       

Comments

Habari Nyingine Kutoka Kioo17 Swahili;

MOURINHO KUMUONDOA MKHITARYAN ILI AWEZE KUMSAJILI OZIL.

Henrikh Mkhitaryan atatupwa kando na meneja wa Manchester United Jose Mourinho ili apate nafasi ya kumsajili jiungo wa Arsenal, Mesut Ozil, kulingana na taarifa.  Bosi huyo wa Manchester United anajua lazima apunguze kikosi chake kama atataka kumsajili Ozil kutokana na madai ya mshahara mkubwa ya bingwa huyo wa Kombe la Dunia. Kiungo huyo mchezeshaji huyo ambaye mkataba wake Arsenal umalizika mwishoni mwa msimu huu, amekuwa akiomba mshahala wa Pauni Laki Tatu (£ 300,000) kwa wiki ili kukubali mkataba mpya wa kuendelea kuchezea Arsenal. Gazeti la 'The Mirror' la Uingereza limeripoti kwamba Mourinho ameamua Mkhitaryan, ambaye alijiunga na klabu kutoka Borussia Dortmund mwaka 2016, anaweza kuwa mchezaji kuondoka Ni uchaguzi wa mantiki kulingana na hali ya sasa ya mchezaji huyo katika kikosi cha Manchester United. Mchezaji huyo kutoka Armenia ameachwa mechi nane za mwisho na Mourinho huku akisema kuwa haamini kama kiungo huyo anastahilo kukukaa katika...

MCHEZAJI WA ZAMANI WA UINGEREZA AMESEMA ALICHEZA NA WACHEZAJI WATATU MASHOGA KWENYE TIMU.

Carl Hoefkens (jezi no.2) alichezea West Bromwich Albion na Stoke City wakati wa enzi zake ligi kuu ya England. Beki wa zamani wa Ligi Kuu ya Uingereza amesema alicheza pamoja na wachezaji wenzake wawili wa mashoga ndani ya timu, na mmoja alikua na jina kubwa. Carl Hoefkens, West Bromwich Albion na Stoke City siku za nyuma, anasema wachezaji hao walikua wazi na hawakujificha kwenye vyumba vya kubadilishia nguo ingawa bado hawajulikani kwasababu ya maombi yao wenyewe ya kuomba kutotangazwa. Justin Fashanu, ambaye alijiua mwaka 1998, alikuwa mchezaji wa mwisho wa kazi nchini England kuja nje kama mashoga - mwaka 1990. Hoefkens alipokua (kushoto), alipokua anachezea Stock  City. Hoefkens aliyecheza Uingereza kwa miaka minne, akiondoka mwaka 2009, alidai kuwa mchezaji mwenzake mmoja wa timu alikua anaweza kuja kwenye uwanja wa mafunzo ya klabu na mpenzi wake wa kiume  lakini aliwaomba wenzake kutokuwaambia watu wangine wa nje ya timu. 'Nilicheza pamoja n...

ORODHA YA NCHI 80 AMBAZO MTANZANIA ANARUHUSIWA KUINGIA BILA VIZA.

         Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni amesema kuna zaidi ya nchi 80 ambazo watanzania wanaweza kusafiri bila ya kuwa na viza . Mhandisi Hamad Masauni amesema kuna zaidi ya nchi 80 ambazo watanzania wanaweza kusafiri bila ya kuwa na viza za kusafiria kama ilivyokuwa nchi za afrika Mashariki. Mhandisi Massauni amebainisha hayo leo bungeni wakati akijibu swali la Mbunge wa Mlalo kupitia tiketi ya CCM Rashid Shangazi aliyetaka kujua ni nchi ngapi ambazo watanzania wanaweza kusafiri bila ya kuwa na viza (viza on arrival). "Zipo nchi 16 kwa Afrika ambazo watanzania wanaweza kuzitembelea bila ya kuwa na viza na duniani zipo 67" alisema Masauni. Aidha Massauni amezitaja nchi hizo kuwa ni Benin, Burkina Faso, Cape Verde, Ivory Coast, Djibouti, Gabon, Gambia, Guinea, Guinea­Bissau, Liberia, Mali, Mauritania, Niger, Sierra Leone pamoja na Togo. Pamoja na hayo Masauni amesema...

JINSI YA KUOMBA PASSPORT YA TANZANIA KWA NJIA YA INTERNET.

Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kupitia i dara ya Uhamiaji  imezindua huduma ya ujazaji fomu za maombi ya hati ya kusafiria (Passport) kwa njia ya mtandao, ambapo mwombaji atalazimika kujaza fomu hizo na kuzichapisha kabla ya kuziwasilisha kwenye ofisi za uhamiaji. Idara hiyo pia imeeleza kuwa matumizi ya huduma hiyo yataenda sambamba na huduma inayotumiwa sasa ya fomu za maombi ya pasipoti mpaka pale itakapotangazwa vinginevyo. Huduma hiyo itaanza kufanya kazi kuanzia Jumatatu tarehe  7/8/2017    na unaweza  kujaza fomu hizo  kwa kufungua tovuti hiyo ambayo ni  https://www.immigration.go.tz/ppt_application/ Utaratibu wa namna ya kujaza fomu hizo umeelekezwa katika fomu husika mtandaoni, na pia wateja wanaweza kupata ufafanuzi au maelezo zaidi kuhusu huduma hiyo kupitia anuani ya Idara ya Uhamiaji ambayo ni   info@immigration.go.tz   au katika Ofisi yoyote ya Uhamiaji iliyo karibu yako. CHANZO: http://dibute.com/muhimu-...

BAYERN MUNICH WANAJENGA VYUMBA VYA HOTELI NDANI YA UWANJA.

Huu ndio utakaokuwa muonekano wa vyumba hivyo kwa ndani. Picha: Mariot International. Kama sehemu ya mpango wa miaka mingi ya Bayern na  kampuni kubwa ya hoteli za Mariot na Courtyard, mashabiki hivi karibuni wataweza kupata fursa ya kukaa katika vyumba ambavyo vina dirisha linaloangalia uwanja wa Alianz Arena moja kwa moja. Vyumba hivyo vya kifahari vya kulala vitakuwa na kitanda cha kikubwa na seti ya televisheni - tu ikiwa umechoka na hat-trick za Robert Lewandowski. Pia kutakuwa na mahali pa moto ambayo ni maalumu kwa siku za mechi kwenye majira ya baridi. Mkurugenzi Mtendaji wa Bayern Karl-Heinz Rummenigge alisema: "Tunafurahia bidhaa mbili zinazoongoza kama hoteli Courtyard zinazomilikiwa na kampuni ya Marriott na FC Bayern kuingia katika ushirikiano huu wa muda mrefu kibiashara. "Tunapendezwa na bidhaa mbili zinazoongoza kama Courtyard na Marriott na FC Bayern kuingia katika ushirikiano wa muda mrefu," "Kutokana na kwamba Marri...

ORODHA YA NCHI ZA KWANZA NA ZA MWISHO KWA AMANI DUNIANI.

Marekani:  Ripoti ya Taasisi ya Uchumi na Amani imepata mataifa kumi tu ulimwenguni ambayo hayapo katika vita na migogoro kabisa. Kwa mujibu wa Ripoti ya Kimataifa ya Amani 2016, Botswana, Chile, Costa Rica, Japan, Mauritius, Panama, Qatar, Uswisi, Uruguay na Vietnam ndio nchi pekee ambazo hazipo kwenye vita wala migogoro yeyote ile ya kuhatarisha amani.. Iceland inaongoza orodha ya nchi zinazoongoza kwa amani ulimwenguni, ikifuatiwa na Denmark, Austria, New Zealand, Ureno, Jamhuri ya Czech, Uswisi, Canada, Japan na Slovenia - wakati Marekani ikiwa kwenye nafasi ya 103. Palestina imepanda kutoka nafasi ya 163 mpaka nafasi ya 148. Syria iliyoharibiwa na vita imewekwa chini ya orodha, chini kuliko Sudan Kusini, Iraq, Afghanistan, Somalia, Yemen, Jamhuri ya Afrika ya Kati, Ukraine, Sudan na Libya. "Ripoti inalinganisha amani duniani kwa kutumia mandhari tatu pana: hali ya utulivu na usalama katika jamii; kiwango cha mgogoro wa ndani au wa kimataifa; na kiwango cha kije...

VIDEO YA NDEGE KUBWA ZAIDI DUNIANI.

Ndege kubwa kuliko zote duniani inasemekana kuwa katika hatua za mwisho za maandalizi ya kuanza safari zake. Ndege hiyo inayoitwa Stratolaunch yenye injini sita aina turbofan zenye uzito wa kilo 40000 (tani 4) kila moja. Utengenezaji wa ndege hiyo ni maono ya mwanzilishi mwenza wa kampuni ya Microsoft, ambaye anataka ndege hiyo ndio iwe chombo cha usafiri kikubwa zaidi angani ,chenye kasi zaidi na gharama nafuu kukiendesha kulinganisha na za teknolojia zilizopo sasa. Mabawa ya ndege hiyo ni marefu kuliko uwanja wa mpira wa miguu ambapo kama ukiiweka katikati ya uwanja wa mpira, mabawa yake yatazidi kwa kwa futi 12.5 (mita 3.8) nyuma ya kila goli. Tazama kipande hiki cha Video: CHANZO: dailymail.co.uk