Skip to main content

PAPA FRANCIS ASHINDANISHWA NA PABLO ESCOBAR KWA KUHESHIMIWA NCHINI COLOMBIA.


Medellín (Colombia) (AFP):
 Katika saluni yake ya nywele, Yamile Zapata anatumia faida ya ziara ya Papa Francis ili kuuza pete za funguo zenye picha ya kiongozi huyo wa kanisa katoliki duniani. Lakini anadai sio ambapo pesa halisi iko kwenye mji wa Medellin nchini Colombia.

Zawadi nyingi anazouza katika mji huu wa Colombia hubeba uso wa "mtakatifu" na shujaa wake mwenyewe: Pablo Escobar.

Wakati Francis alikuwa akihudumia na kufundisha kama kuhani wa Yesuit katika miaka ya 1980, Escobar alikuwa akiua mamia ya watu na kufanya biashara ya madawa ya kulevya ya mabilioni ya dola za kimarekani.

"Kila mtu anataka picha za papa sasa, lakini picha za Pablo zinauzika vizuri zaidi," ,alisema Zapata, mwenye umri wa miaka 34, wakati ambao jiji hilo limeandaliwa kwa ajili ya mkutano wa Papa Francis wa wazi siku ya Jumamosi.

PETE ZA FUNGUO ZENYE PICHA ZA PAPA FRANCIS NA PABLO ESCOBAR ZIKIWA ZINAUZWA KWENYE MITAA YA JIJI LA MEDELIN, COLOMBIA.


Francis alitoa maneno ya huruma kwa waathirika wa vurugu zinazohusiana na madawa ya kulevya jijini Medellin, Lakini licha ya yote, watu wengine huko Medellin humkumbuka Escobar kwa upendo.

"Ninaamini tu kwa Mungu, lakini kile ninachofanya kinaonyesha mema ambayo Pablo alifanya," Zapata alisema.

"Watu katika mji huu hawazungumzi juu ya mambo mabaya, kwa sababu hapa kila mtu anampenda."


WILAYA YA PABLO ESCOBAR;

Mamlaka zilimsaka na kumuua Pablo Escobar mwaka 1993 na kukomesha kile kilichokuwa ni mamlaka kubwa ya madawa ya kulevya ulimwenguni.

Lakini kwa watu wanaoishi katika nyumba ambazo alijenga katika wilaya ya Katoliki ya Medellin katika miaka ya 1980, ilikuwa zaidi kama ufalme wa mbinguni.

Katika jirani ya Yamile, Escobar alijenga nyumba 260 kwa wakazi wa makaazi katika miaka ya 1980. Makazi hayo sasa yameongezeka na kufikia nyumba 6,000.

"Karibu kwenye wilaya ya Pablo Escobar, hapa tunaishi na kupumua amani" , 
ndio maneno yanayosomeka katika bango wakati unaingia katika eneo hilo yakiwa na sura yake.

Sasa ni zaidi ya miongo miwili imepita tangu polisi walipompiga risasi na kumuua Escobar kwenye dari ya jijini Medellin kwa msaada kutoka kwa mamlaka za Marekani.

Hata hivyo bado Pablo ameendelea kua kivutio kwa watu kiasi cha kuendelea kuzungumzwa na kuigizwa kwenye mfululizo wa televisheni, filamu na vitabu vingi.

Mbali na kutengeneza nywele, Zapata huuza vikombe na t-shirt za "Pablo."

Tangu alipobadilisha jina la saluni yake na kuiita jina mbadala la Pablo Escobar,"El Patron,", wateja wake umeongezeka kwa mara mbili.



MADAWA YA KULEVYA NA DINI:

Papa Francis alikuja Colombia kuunga mkono jitihada zake za kukomesha vita vya wenyewe kwa wenyewe ambavyo vilikuwa vinatokana na biashara ya madawa ya kulevya.

Serikali imefanya amani na kundi kubwa la waasi la FARC, kundi ambalo limejijenga na kufadhiliwa na biashara ya madawa ya kulevya.

Umoja wa Mataifa unaitambua Colombia kama mzalishaji mkuu duniani wa koka ambayo ni malighafi ya madawa ya kulevya aina ya Cocaine.


Lakini mbali na kuwa mji unaohusishwa na makundi ya madawa ya kulevya nchini Colombia, Medellin pia ni wazi kuwa ni jiji la Wakatoliki wengi.

Mji huo wenye wakazi milioni mbili, inasemekana kuwa ndio wenye makanisa zaidi kuliko mji mwingine wowote katika nchi hiyo yenye watu takribani milioni 48.


Katika nyumba yake iliyopo katika Wilaya ya Pablo Escobar, Wberney Zabala ana shimoni ndogo (sehemu ya kufanya ibada)yenye picha ya bosi huyo wa zamani wa madawa ya kulevya iliyopambwa kwa picha zake na mishumaa.

"Hakuna kiongozi wa dini na hakuna mwanasiasa anayeweza kumzidi Pablo," alisema Zabala, mwenye umri wa miaka 45, askari aliyekuwa mlemavu na sasa ni kiongozi wa jamii.
"Kujenga makazi haya ilikuwa ni muujiza wake wa kwanza ... kadili makazi haya yanavyoendelea ndivyo hadithi yake itakavyokuwa."



CHANZO:
yahoo.com/news

Comments

Habari Nyingine Kutoka Kioo17 Swahili;

UTATA WA FORM 34A FEKI KATIKA TOVUTI YA IEBC.

  Na BERNADINE MUTANU  Imepakiwa - Wednesday, August 16   2017 at  11:11 Kwa Mukhtasari VISA vya dosari kwenye uchaguzi uliokamilika vinazidi kuripotiwa nchini Kenya, wiki moja baada ya wananchi kupiga kura, na siku kadhaa baada ya Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) kutangaza mshindi wa urais. Huku IEBC ikikosolewa kwa kutangaza matokeo ya mwisho ya urais Ijumaa usiku kabla ya matokeo yote kuingia, imeibuka kuwa kituo kimoja Kaunti ya Mandera kilitumia karatasi ya kawaida kurekodi matokeo ya urais, badala ya kutumia Fomu 34 A. Matokeo hayo yaliwekwa katika tovuti ya IEBC, na kushangaza wananchi, huku madai ya wizi wa kura yakizidi kuchacha. 'Fomu’ hiyo isiyo ya kawaida iliwekwa katika mtandao wa IEBC kutoka Kituo cha Kuhesabia kura cha Bulla Dadacha 2, Wadi ya Elwak Kusini, Eneo Bunge la Mandera Kusini, Kaunti ya Mandera. Haina nambari ya mfuatano  (serial number)  kama fomu za kawaida za uchaguzi,...

KIONGOZI MKUU WA UPINZANI NCHINI ZIMBABWE, MORGAN TSVANGIRAI AMEFARIKI DUNIA.

Kiongozi wa upinzani wa Zimbabwe Morgan Tsvangirai amefariki dunia nchini Afrika Kusini, afisa mkuu wa chama chake cha MDC amesema. Bw Tsvangirai, mwenye umri wa miaka 65, aliyekuwa waziri mkuu, alilipotiwa kuwa alikuwa akisumbuliwa na saratani ya koloni. "Amefariki jioni hii, familia yake imenitaarifu"  Makamu wa Rais wa MDC, Elias Mudzuri aliliambia shirika la habari la Uingereza, Reuters. Morgan Tsvangirai alizaliwa mnamo Machi 10, 1952 huko Gutu, Zimbabwe. Baba yake alikuwa mfanyakazi wa mgodi, fundi, na mkulima. Alihudhuria Shule ya Msingi ya Guco ya St. Marks. Kisha alihamishiwa Shule ya Msingi ya Chikara Gutu. Kwa elimu yake ya sekondari, alihudhuria Shule ya High Gokomere. Alikuwa waziri mkuu katika serikali ya mseto ya Zimbabwe tangu 2009 hadi 2013. Katika kazi yake ya awali alionekana kuwa mfanyakazi mwenye bidii sana na alifanya kazi katika mgodi wa madini ya nickel( kwa zaidi ya muongo mmoja. Alipanda cheo haraka kutambuliwa na akain...

MCHEZAJI WA ZAMANI WA UINGEREZA AMESEMA ALICHEZA NA WACHEZAJI WATATU MASHOGA KWENYE TIMU.

Carl Hoefkens (jezi no.2) alichezea West Bromwich Albion na Stoke City wakati wa enzi zake ligi kuu ya England. Beki wa zamani wa Ligi Kuu ya Uingereza amesema alicheza pamoja na wachezaji wenzake wawili wa mashoga ndani ya timu, na mmoja alikua na jina kubwa. Carl Hoefkens, West Bromwich Albion na Stoke City siku za nyuma, anasema wachezaji hao walikua wazi na hawakujificha kwenye vyumba vya kubadilishia nguo ingawa bado hawajulikani kwasababu ya maombi yao wenyewe ya kuomba kutotangazwa. Justin Fashanu, ambaye alijiua mwaka 1998, alikuwa mchezaji wa mwisho wa kazi nchini England kuja nje kama mashoga - mwaka 1990. Hoefkens alipokua (kushoto), alipokua anachezea Stock  City. Hoefkens aliyecheza Uingereza kwa miaka minne, akiondoka mwaka 2009, alidai kuwa mchezaji mwenzake mmoja wa timu alikua anaweza kuja kwenye uwanja wa mafunzo ya klabu na mpenzi wake wa kiume  lakini aliwaomba wenzake kutokuwaambia watu wangine wa nje ya timu. 'Nilicheza pamoja n...

NAPE ASEMA KWAMBA TUNDU LISSU ALIMWAMBIA WANATAFUTWA, AHAME CCM.

MBUNGE WA MTAMA (CCM) AKICHEKA NA TUNDU LISSU MUDA MFUPI KABLA YA KUPIGWA RISASI. Imeandikwa na Edwin Mjwahuzi , Mwananchi; emjwahuzi@mwananchi.co.tz Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu (kulia) akifurahia jambo na mbunge wa Mtama, Nape Nnauye walipokuwa wakitoka kuhudhuria kikao cha Bunge, mjini Dodoma jana mchana. By Edwin Mjwahuzi, Mwananchi; emjwahuzi@mwananchi.co.tz Dodoma. Mbunge wa Mtama (CCM), Nape Nnauye ameeleza alichoambiwa na Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu jana Alhamisi mchana wakati wakitoka bungeni huku wakicheka. Nape amesema Lissu alimwambia, “Wewe Nape ni mjomba wangu, kwa nini unabaki CCM? Mimi na wewe tunafuatiliwa na jamaa zako wakitumia gari moja. Mimi na wewe ni watuhumiwa, hama CCM mjomba.” Lissu alipigwa risasi jana Alhamisi mchana na kupelekwa chumba cha upasuaji katika Hospitali ya Rufaa ya Dodoma na baadaye usiku alihamishiwa Hospitali ya Aga Khan ya Nairobi nchini Kenya. Mbunge wa Rombo, Joseph Selasini jana wakati Lissu...

MADAI YA CUBA KWAMBA WAZIRI MKUU WA CANADA NI MTOTO WA FIDEL CASTRO.

Pichani ni waziri mkuu wa Canada, Justin Trudeau (kushoto), na Rais wa zamani wa Cuba, Hayati Fidel Castro (kulia). Maelezo yaliyoandikwa na mtoto wa kwanza wa rais wa zamani wa Cuba , Fidel Castro, kabla ya kujiua yamelishtua taifa la Cuba wiki hii. Maelezo hayo yaliyoandikwa na mtoto huyo mkubwa wa mwanamapinduzi na rais wa zamani wa nchi hiyo yalikuwa ya kushangaza baada ya  kuwa na madai ya kuwa Waziri Mkuu wa Canada Justin Trudeau ni mtoto wa nje wa baba yake marehemu Fidel Castro. Maelezo hayo yaliyoandikwa kwa mkono na mtoto huyo wa Fidel Castro aliyejiua siku chache zilizopita kwa msongo wa mawazo, Fidel Castro Diaz-Balart, aliyekuwa na umri wa miaka 68, yalionekana kuthibitisha uvumi wa muda mrefu nchini Cuba kwamba Fidel Castro ni baba wa damu wa waziri mkuu wa sasa wa Canada, Justin Trudeau ikiwa ni matokeo ya uhusiano wa siri wa kimapenzi na mke wa mwanasiasa maarufu wa Canada, Pierre Trudeau, Margaret Trudeau mwaka 1970. Kifo cha mwanasayansi wa ...

ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2017, TANZANIA

MH.GEORGE SIMBACHAWENE .               Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Tamisemi) George Simbachawene ametoa idadi ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na masomo ya kidato cha tano na vyuo vya ufundi kwa mwaka 2017 huku jumla ya wanafunzi 2,999 wakiachwa.             Simbachawene ametoa kauli hiyo leo mjini Dodoma wakati akizungumza na waandishi ws habari na kusema kuwa ufaulu kwa mwaka huu umeongezeka kwa asilimia 3.75 ukilinganisha na matokeo ya mwaka 2015. Waziri amedai kati ya wanafunzi 96,018 waliofaulu kwa daraja la kwanza hadi la tatu ni wanafunzi 93,019 tu ndiyo waliochaguliwa kujiunga na kidato cha tano na vyuo vya ufundi.              Waziri Simbachawene amesema kuwa jumla ya watahiniwa wote waliofanya mtihani wa kidato cha nne kwa shule kwa mwaka 2016 ni 349,524 huku waliofanya mtihani wa kujitegemea ni 47,751 ambapo watahiniwa waliofanya mtihani wa shule...

NAKUMATT IMEPATA TUZO YA MLIPAKODI BORA NCHINI RWANDA.

MENEJA WA NAKUMATT NCHINI RWANDA, ADAN RAMATA, AKIPOKEA TUZO YA MLIPA KODI BORA KUTOKA KWA MWENYEKITI WA SHIRIKISHO LA SEKTA BINAFSI LA RWANDA, BENJAMIN GASAMERA. KIGALI, Rwanda, Oktoba 16 Kampuni ya maduka ya kuuza bidhaa za rejareja ya Nakumatt imetangazwa kuwa walipa kodi bora na Mamlaka ya Mapato ya Rwanda. Nakumatt Rwanda ambayo inafanya kazi maduka ya rejareja 3 jijini Kigali, Rwanda ilitangazwa mlipakodi bora Ijumaa jioni katika tukio ambalo liliandaliwa na RRA ili kusherehekea walipa kodi katika nchi. Nakumatt Rwanda ilichukua tuzo bora ya walipa kodi ya 2016. Kampuni hiyo pia ilipokea tuzo bora ya mtumiaji wa umeme wa EBM (EBM). Akizungumza katika tukio hilo, Kamishna Mkuu wa RRA Richard Tusabe alithibitisha kwamba kiwango vya kulipa kodi nchini kimekuwa kwa kasi na kutokana na ushirikiano mzuri kutoka katika sekta kadhaa za uchumi ikiwa ni pamoja na sekta binafsi. Mkurugenzi huyo wa RRA alifafanua kuwa bodi ya kodi imeweza kufika lengo lake la kukusanya katika...