Skip to main content

MAAJABU YA "MTUME" ELVIS MBONYE.





Picha za zinazo onesha kasisi wa Uganda akipigwa mabusu na wafuasi wake miguuni tayari zimekwisha zua gumzo miongoni mwa vyombo vya habari na mitandao ya kijamii kwa siku za karibuni.


Mtume Elvis Mbonye, ​​mwenye umri wa miaka 40, wa Zoe Fellowship, Jumapili iliyopita aliandaa tafrija ya chakula cha jioni kwa kiingilio cha takribani dola 185 (185$) kwa tiketi za platinum, dola 210 (210$) kwa tiketi za Gold, dola 135 (135$) kwa tiketi za Silver, na dola 75 (75$) kwa tiketi za kawaida.





Ibada za Mbonye hufanyika siku za Jumanne kinyume na za makanisa mangine za Jumapili au Jumamosi, akisema Mungu alimwambia afanye ibada siku za Jumanne. 

Wakati alipoanza kanisa mwaka 2014, Mbonye alikuwa na waumini 100, lakini sasa amefikisha waumini 5,000,
vyombo vya habari vya Uganda vinasema.

Mbonye, ​​kabla ya kuhamishia ibada zake kwenye uwanja wa Rugby wa Kyadondo, alikua anakodisha hoteli ya kifahari ya Kampala kwa gharama sawa na dola 13,500 za kimarekani kila wiki.




Mbonye amekua akituhumiwa na watu mbali mbali kwamba anaabudu mashetani ,kitu ambacho amekua anakataa kabisa.

Watu wengi wamekua wakiona aina ya mavazi ya gharama ambayo anayovaa hayafanani na mtu wa Mungu, lakini Mbonye hafikiri hivyo.

"Ndiyo nilivyo, ukiachana na yote mimi ni mtu nisiependa makuu",
aliliambia gazeti la Observer la Uganda katika mahojiano ya Septemba, 2016.



Mbonye anasema Zoe ni neno la Kiyunani kwa 'maisha ya kimungu' na ushirika huu huwavutia watu kutoka kila aina ya maisha, ikiwa ni pamoja na wachungaji kutoka makanisa mbalimbali.

Yote hii ilianza mwaka 2014 wakati Mbonye alifungua milango kwa watu katika Hotel Triangle huko Kampala ambapo alipanga mikutano ya kila mwaka.

"[Lakini] tulipoanza ibada za Jumanne, mahali ambapo tulianza na watu wapatao 100 kulipata mafuriko kwa haraka tulitafuta sehemu nyingine,"
alisema katika mahojiano na Observer.


Ibada zake za Jumanne zinaanza saa 11 jioni lakini waumini wanawasili kanisai saa 9 alasiri na Mbonye hufika saa 1 usiku kuongoza huduma.

Katika ibada ya Agosti 23, 2016, Mbonye alimaliza kuhubiri saa mbili na nusu usiku kwa kuwaita watu wote wanaoitwa Bruno. Watu watatu walijitokeza na aliwaambia kwa usahihi miezi halisi na tarehe walizozaliwa, kabla ya kuongoza umati huo katika nyimbo za sifa na ibada.




Mbonye ni mshabiki mkubwa wa Arsenal mwenye na anasema anapenda kutazama sinema, hasa za kuchekesha, za kipelelezi na za kutisha.

Mke wake anaitwa Harriet Mbonye, ​​mwanamke wa mfanyabiashara ambaye, kwa kushangaza, hajawahi kuhudhuria ibada yake yoyote.
"Lakini yeye (Harriet) anafuatilia ibada hizo kwenye televisheni nyumbani. Anaweza kuanza kutokea kwenye hadhara lakini nadhani huu si wakati sahihi.
 Bwana hakuonesha hiyo, "alisema.

Wao wawili wameoana kwa miaka sita sasa.
Siku za mapumziko utampata Mbonye kwenye Kahawa nzuri ya Afrika huko Lugogo lakini pamoja na walinzi wake ambapo anasema kuwa ni hatua za tahadhari.
Mbonye ana mpango wa kujenga jengo la kudumu kwa huduma zake - si kanisa, anasisitiza.



Mtume Mbonye alizaliwa katika familia ya watoto saba ya Leo na Teddy Ntiru wa Bugolobi, ambayo walifariki mwaka 1990 na 1996, kwa mtiririko huo. Alihudhuria shule ya awalu ya Mbuya, shule ya msingi ya Kiswa, Kigezi College Butobere kwa O-level na Standard High School huko Zana kwa ngazi zake za A-level.
Baadaye alijiunga na Chuo Kikuu cha Makerere ambapo alihitimu shahada ya Development Studies mwaka 2004.




CHANZO:
edaily.co.ke

Comments

Habari Nyingine Kutoka Kioo17 Swahili;

ORODHA YA NCHI 80 AMBAZO MTANZANIA ANARUHUSIWA KUINGIA BILA VIZA.

         Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni amesema kuna zaidi ya nchi 80 ambazo watanzania wanaweza kusafiri bila ya kuwa na viza . Mhandisi Hamad Masauni amesema kuna zaidi ya nchi 80 ambazo watanzania wanaweza kusafiri bila ya kuwa na viza za kusafiria kama ilivyokuwa nchi za afrika Mashariki. Mhandisi Massauni amebainisha hayo leo bungeni wakati akijibu swali la Mbunge wa Mlalo kupitia tiketi ya CCM Rashid Shangazi aliyetaka kujua ni nchi ngapi ambazo watanzania wanaweza kusafiri bila ya kuwa na viza (viza on arrival). "Zipo nchi 16 kwa Afrika ambazo watanzania wanaweza kuzitembelea bila ya kuwa na viza na duniani zipo 67" alisema Masauni. Aidha Massauni amezitaja nchi hizo kuwa ni Benin, Burkina Faso, Cape Verde, Ivory Coast, Djibouti, Gabon, Gambia, Guinea, Guinea­Bissau, Liberia, Mali, Mauritania, Niger, Sierra Leone pamoja na Togo. Pamoja na hayo Masauni amesema...

MCHEZAJI WA ZAMANI WA UINGEREZA AMESEMA ALICHEZA NA WACHEZAJI WATATU MASHOGA KWENYE TIMU.

Carl Hoefkens (jezi no.2) alichezea West Bromwich Albion na Stoke City wakati wa enzi zake ligi kuu ya England. Beki wa zamani wa Ligi Kuu ya Uingereza amesema alicheza pamoja na wachezaji wenzake wawili wa mashoga ndani ya timu, na mmoja alikua na jina kubwa. Carl Hoefkens, West Bromwich Albion na Stoke City siku za nyuma, anasema wachezaji hao walikua wazi na hawakujificha kwenye vyumba vya kubadilishia nguo ingawa bado hawajulikani kwasababu ya maombi yao wenyewe ya kuomba kutotangazwa. Justin Fashanu, ambaye alijiua mwaka 1998, alikuwa mchezaji wa mwisho wa kazi nchini England kuja nje kama mashoga - mwaka 1990. Hoefkens alipokua (kushoto), alipokua anachezea Stock  City. Hoefkens aliyecheza Uingereza kwa miaka minne, akiondoka mwaka 2009, alidai kuwa mchezaji mwenzake mmoja wa timu alikua anaweza kuja kwenye uwanja wa mafunzo ya klabu na mpenzi wake wa kiume  lakini aliwaomba wenzake kutokuwaambia watu wangine wa nje ya timu. 'Nilicheza pamoja n...

ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2017, TANZANIA

MH.GEORGE SIMBACHAWENE .               Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Tamisemi) George Simbachawene ametoa idadi ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na masomo ya kidato cha tano na vyuo vya ufundi kwa mwaka 2017 huku jumla ya wanafunzi 2,999 wakiachwa.             Simbachawene ametoa kauli hiyo leo mjini Dodoma wakati akizungumza na waandishi ws habari na kusema kuwa ufaulu kwa mwaka huu umeongezeka kwa asilimia 3.75 ukilinganisha na matokeo ya mwaka 2015. Waziri amedai kati ya wanafunzi 96,018 waliofaulu kwa daraja la kwanza hadi la tatu ni wanafunzi 93,019 tu ndiyo waliochaguliwa kujiunga na kidato cha tano na vyuo vya ufundi.              Waziri Simbachawene amesema kuwa jumla ya watahiniwa wote waliofanya mtihani wa kidato cha nne kwa shule kwa mwaka 2016 ni 349,524 huku waliofanya mtihani wa kujitegemea ni 47,751 ambapo watahiniwa waliofanya mtihani wa shule...

TUPAC SHAKUR ALIBAKWA JELA !!!

             Ulimwengu wa filamu za Hollywood na muziki wa Hip Hop juzi ulipatwa na mshangao baada ya mtayarishaji wa filamu inayohusu maisha ya hayati Tupac Shakur ,L.T Hutton kuelezea sababu zilizomfanya kumbadilisha muongozaji wa filamu hiyo kutoka John Singleton na kumuweka muongozaji Benny "Boom" Douglas.  Filamu hiyo inayoitwa "all eyez on me" tayari imekwisha andaliwa na inatarajiwa kuzinduliwa leo tarehe 16 Juni 2017.       Akizungumza kwenye mahojiano redioni L.T Hutton amewashtusha watu wengi baada ya kudai kwamba walishindwana na muongozaji wa mwanzo bwana John Singleton sababu muongozaji huyo aling'ang'ania kuwepo kwa matukio (scene) ambazo kwa maoni yake zisingependeza.        Matukio ambayo John Singleton alipenda yawepo katika filamu hiyo ni pamoja na kutaka filamu hiyo ianze na scene ya Tupac akilazimisha kumlawiti msichana wa kizungu.!!!          Singleton pia ali...

MFALME WA GHANA ASABABISHA AFISA MKUU WA BENKI KUFUKUZWA KAZI.

Afisa mtendaji mkuu wa benki alifukuzwa kazi na kuchunguzwa na Shirika la Uhalifu wa Taifa baada ya kuweka pauni za Uingereza 350,000 ( £ 350,000 ) pesa taslimu aliyopewa na Mfalme wa Ghana. Mark Arthur wa benki ya Kimataifa ya Ghana Bigwig aliitwa kwenye nyumba ya Osei Tutu II huko Henley-on-Thames na kupewa £ 200,000 pamoja na $ 200,000 na kuagizwa aiweke kwenye akaunti ya benki ya Mfalme huyo. Licha ya noti hizo kuwa na namba za mfululizo zinazofuatana (consecutive serial numbers) Bwana Arthur alisema aliona kuwa haifai kumhoji mfalme na kwenda kuiweka benki kwa kutumia usafiri wa teksi ya uber. Punde baada ya Bwana Arthur kuweka pesa hiyo benki, taarifa ya utakatishaji wa fedha ilifika katika jiji la London, Uingereza na kugharimu ajira yake. Bwana Arthur alielezea kwenye taarifa yake ya ushahidi kuwa Mfalme alimwambia kwamba pesa hizo zimekusanywa kutoka kwenye akaunti za benki za nchini Ghana na kupelekwa Uingereza. Pia alidai kwamba Mfale alimpa $ 200,000 ili ...

SABABU ZA KUVUNJIKA KWA KUNDI LA P-SQUARE.

WANAMUZIKI MAPACHA WA KUNDI LA PSQUARE, PETER (KUSHOTO) NA PAUL (KULIA) WAKIWA NA KAKA YAO AMBAE PIA NI MENEJA WAO, JUDES OKOYE. Mwanamuziki wa kundi la PSquare kutoka Nigeria, Peter Okoye ametangaza kujitoa kwenye kundi hilo la muziki wa Pop maarufu zaidi Afrika. Msanii huyo alidai kwamba amewasilisha maombi ya kuvunja kundi hilo katika barua aliyoandika kwa wakili wao Festus Keyamo. Kulingana na nakala ya barua iliyotolewa kwenye vyombo vya habari Jumatatu,Tarehe 25 Septemba, Peter alisema kuwa pacha wake na, Paul, na kaka yao, Judes waliahirisha ziara yao ya muziki ya Marekani bila kushauriana naye.Na hiyo ni moja kati ya sababu za msingi. Peter pia aliwalaumu Paul na kaka yao mkubwa mkubwa ambae ni meneja wao pia kwa udanganyifu walioufanya ili kutatua shida waliyokuwa nayo juu ya biashara ya muziki. Wasanii hao ndugu wamekua kwenye vita vya maneno kwenye mitandao ya kijamii tangu mwisho wa mwaka jana pamoja na juhudi za watu wao wa karibu kujaribu kuwapatanisha kifami...

ORODHA YA NCHI ZA KWANZA NA ZA MWISHO KWA AMANI DUNIANI.

Marekani:  Ripoti ya Taasisi ya Uchumi na Amani imepata mataifa kumi tu ulimwenguni ambayo hayapo katika vita na migogoro kabisa. Kwa mujibu wa Ripoti ya Kimataifa ya Amani 2016, Botswana, Chile, Costa Rica, Japan, Mauritius, Panama, Qatar, Uswisi, Uruguay na Vietnam ndio nchi pekee ambazo hazipo kwenye vita wala migogoro yeyote ile ya kuhatarisha amani.. Iceland inaongoza orodha ya nchi zinazoongoza kwa amani ulimwenguni, ikifuatiwa na Denmark, Austria, New Zealand, Ureno, Jamhuri ya Czech, Uswisi, Canada, Japan na Slovenia - wakati Marekani ikiwa kwenye nafasi ya 103. Palestina imepanda kutoka nafasi ya 163 mpaka nafasi ya 148. Syria iliyoharibiwa na vita imewekwa chini ya orodha, chini kuliko Sudan Kusini, Iraq, Afghanistan, Somalia, Yemen, Jamhuri ya Afrika ya Kati, Ukraine, Sudan na Libya. "Ripoti inalinganisha amani duniani kwa kutumia mandhari tatu pana: hali ya utulivu na usalama katika jamii; kiwango cha mgogoro wa ndani au wa kimataifa; na kiwango cha kije...