Skip to main content

MAAJABU YA "MTUME" ELVIS MBONYE.





Picha za zinazo onesha kasisi wa Uganda akipigwa mabusu na wafuasi wake miguuni tayari zimekwisha zua gumzo miongoni mwa vyombo vya habari na mitandao ya kijamii kwa siku za karibuni.


Mtume Elvis Mbonye, ​​mwenye umri wa miaka 40, wa Zoe Fellowship, Jumapili iliyopita aliandaa tafrija ya chakula cha jioni kwa kiingilio cha takribani dola 185 (185$) kwa tiketi za platinum, dola 210 (210$) kwa tiketi za Gold, dola 135 (135$) kwa tiketi za Silver, na dola 75 (75$) kwa tiketi za kawaida.





Ibada za Mbonye hufanyika siku za Jumanne kinyume na za makanisa mangine za Jumapili au Jumamosi, akisema Mungu alimwambia afanye ibada siku za Jumanne. 

Wakati alipoanza kanisa mwaka 2014, Mbonye alikuwa na waumini 100, lakini sasa amefikisha waumini 5,000,
vyombo vya habari vya Uganda vinasema.

Mbonye, ​​kabla ya kuhamishia ibada zake kwenye uwanja wa Rugby wa Kyadondo, alikua anakodisha hoteli ya kifahari ya Kampala kwa gharama sawa na dola 13,500 za kimarekani kila wiki.




Mbonye amekua akituhumiwa na watu mbali mbali kwamba anaabudu mashetani ,kitu ambacho amekua anakataa kabisa.

Watu wengi wamekua wakiona aina ya mavazi ya gharama ambayo anayovaa hayafanani na mtu wa Mungu, lakini Mbonye hafikiri hivyo.

"Ndiyo nilivyo, ukiachana na yote mimi ni mtu nisiependa makuu",
aliliambia gazeti la Observer la Uganda katika mahojiano ya Septemba, 2016.



Mbonye anasema Zoe ni neno la Kiyunani kwa 'maisha ya kimungu' na ushirika huu huwavutia watu kutoka kila aina ya maisha, ikiwa ni pamoja na wachungaji kutoka makanisa mbalimbali.

Yote hii ilianza mwaka 2014 wakati Mbonye alifungua milango kwa watu katika Hotel Triangle huko Kampala ambapo alipanga mikutano ya kila mwaka.

"[Lakini] tulipoanza ibada za Jumanne, mahali ambapo tulianza na watu wapatao 100 kulipata mafuriko kwa haraka tulitafuta sehemu nyingine,"
alisema katika mahojiano na Observer.


Ibada zake za Jumanne zinaanza saa 11 jioni lakini waumini wanawasili kanisai saa 9 alasiri na Mbonye hufika saa 1 usiku kuongoza huduma.

Katika ibada ya Agosti 23, 2016, Mbonye alimaliza kuhubiri saa mbili na nusu usiku kwa kuwaita watu wote wanaoitwa Bruno. Watu watatu walijitokeza na aliwaambia kwa usahihi miezi halisi na tarehe walizozaliwa, kabla ya kuongoza umati huo katika nyimbo za sifa na ibada.




Mbonye ni mshabiki mkubwa wa Arsenal mwenye na anasema anapenda kutazama sinema, hasa za kuchekesha, za kipelelezi na za kutisha.

Mke wake anaitwa Harriet Mbonye, ​​mwanamke wa mfanyabiashara ambaye, kwa kushangaza, hajawahi kuhudhuria ibada yake yoyote.
"Lakini yeye (Harriet) anafuatilia ibada hizo kwenye televisheni nyumbani. Anaweza kuanza kutokea kwenye hadhara lakini nadhani huu si wakati sahihi.
 Bwana hakuonesha hiyo, "alisema.

Wao wawili wameoana kwa miaka sita sasa.
Siku za mapumziko utampata Mbonye kwenye Kahawa nzuri ya Afrika huko Lugogo lakini pamoja na walinzi wake ambapo anasema kuwa ni hatua za tahadhari.
Mbonye ana mpango wa kujenga jengo la kudumu kwa huduma zake - si kanisa, anasisitiza.



Mtume Mbonye alizaliwa katika familia ya watoto saba ya Leo na Teddy Ntiru wa Bugolobi, ambayo walifariki mwaka 1990 na 1996, kwa mtiririko huo. Alihudhuria shule ya awalu ya Mbuya, shule ya msingi ya Kiswa, Kigezi College Butobere kwa O-level na Standard High School huko Zana kwa ngazi zake za A-level.
Baadaye alijiunga na Chuo Kikuu cha Makerere ambapo alihitimu shahada ya Development Studies mwaka 2004.




CHANZO:
edaily.co.ke

Comments

Habari Nyingine Kutoka Kioo17 Swahili;

MCHEZAJI WA ZAMANI WA UINGEREZA AMESEMA ALICHEZA NA WACHEZAJI WATATU MASHOGA KWENYE TIMU.

Carl Hoefkens (jezi no.2) alichezea West Bromwich Albion na Stoke City wakati wa enzi zake ligi kuu ya England. Beki wa zamani wa Ligi Kuu ya Uingereza amesema alicheza pamoja na wachezaji wenzake wawili wa mashoga ndani ya timu, na mmoja alikua na jina kubwa. Carl Hoefkens, West Bromwich Albion na Stoke City siku za nyuma, anasema wachezaji hao walikua wazi na hawakujificha kwenye vyumba vya kubadilishia nguo ingawa bado hawajulikani kwasababu ya maombi yao wenyewe ya kuomba kutotangazwa. Justin Fashanu, ambaye alijiua mwaka 1998, alikuwa mchezaji wa mwisho wa kazi nchini England kuja nje kama mashoga - mwaka 1990. Hoefkens alipokua (kushoto), alipokua anachezea Stock  City. Hoefkens aliyecheza Uingereza kwa miaka minne, akiondoka mwaka 2009, alidai kuwa mchezaji mwenzake mmoja wa timu alikua anaweza kuja kwenye uwanja wa mafunzo ya klabu na mpenzi wake wa kiume  lakini aliwaomba wenzake kutokuwaambia watu wangine wa nje ya timu. 'Nilicheza pamoja n...

STAR TV YAFUNGIWA NA TRA KWA KUKWEPA KODI.

Mamlaka ya mapato Tanzania inadaiwa kuifungia Radio Free Africa ya Mwanza inayomilikiwa na Antony Dialo kutokana na kudaiwa kodi kubwa. TRA wamewaondoa studio wafanyakazi wote na kuifunga radio hiyo. Kwa sasa ukiwasha radio utasikia matangazo ya kiingereza ya BBC. Diallo ni mwenyekiti wa CCM Mwanza na anadaiwa mamilioni ya kodi na TRA miaka mingi. Star Tv pia imekumbwa na sekeseke hilo. Ikumbukwe hii ndio TV pekee binafsi iliyokuwa ikipingana na MOAT na TEF katika sakata la RC Paul Makonda na walirusha kipindi maalum cha Makonda huku Jumuiya ya Wanahabari wakitangaza rasmi kujitenga na maswahibu yoyote yatakayokuja kuikuta RFA na Star TV. VYANZO : https://www.jamiiforums.com/threads/tra-waifungia-rfa-kwa-kudaiwa-kodi-ya-sh-bilioni-4-5.1283386/

JINSI YA KUOMBA PASSPORT YA TANZANIA KWA NJIA YA INTERNET.

Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kupitia i dara ya Uhamiaji  imezindua huduma ya ujazaji fomu za maombi ya hati ya kusafiria (Passport) kwa njia ya mtandao, ambapo mwombaji atalazimika kujaza fomu hizo na kuzichapisha kabla ya kuziwasilisha kwenye ofisi za uhamiaji. Idara hiyo pia imeeleza kuwa matumizi ya huduma hiyo yataenda sambamba na huduma inayotumiwa sasa ya fomu za maombi ya pasipoti mpaka pale itakapotangazwa vinginevyo. Huduma hiyo itaanza kufanya kazi kuanzia Jumatatu tarehe  7/8/2017    na unaweza  kujaza fomu hizo  kwa kufungua tovuti hiyo ambayo ni  https://www.immigration.go.tz/ppt_application/ Utaratibu wa namna ya kujaza fomu hizo umeelekezwa katika fomu husika mtandaoni, na pia wateja wanaweza kupata ufafanuzi au maelezo zaidi kuhusu huduma hiyo kupitia anuani ya Idara ya Uhamiaji ambayo ni   info@immigration.go.tz   au katika Ofisi yoyote ya Uhamiaji iliyo karibu yako. CHANZO: http://dibute.com/muhimu-...

MOURINHO KUMUONDOA MKHITARYAN ILI AWEZE KUMSAJILI OZIL.

Henrikh Mkhitaryan atatupwa kando na meneja wa Manchester United Jose Mourinho ili apate nafasi ya kumsajili jiungo wa Arsenal, Mesut Ozil, kulingana na taarifa.  Bosi huyo wa Manchester United anajua lazima apunguze kikosi chake kama atataka kumsajili Ozil kutokana na madai ya mshahara mkubwa ya bingwa huyo wa Kombe la Dunia. Kiungo huyo mchezeshaji huyo ambaye mkataba wake Arsenal umalizika mwishoni mwa msimu huu, amekuwa akiomba mshahala wa Pauni Laki Tatu (£ 300,000) kwa wiki ili kukubali mkataba mpya wa kuendelea kuchezea Arsenal. Gazeti la 'The Mirror' la Uingereza limeripoti kwamba Mourinho ameamua Mkhitaryan, ambaye alijiunga na klabu kutoka Borussia Dortmund mwaka 2016, anaweza kuwa mchezaji kuondoka Ni uchaguzi wa mantiki kulingana na hali ya sasa ya mchezaji huyo katika kikosi cha Manchester United. Mchezaji huyo kutoka Armenia ameachwa mechi nane za mwisho na Mourinho huku akisema kuwa haamini kama kiungo huyo anastahilo kukukaa katika...

TUPAC SHAKUR ALIBAKWA JELA !!!

             Ulimwengu wa filamu za Hollywood na muziki wa Hip Hop juzi ulipatwa na mshangao baada ya mtayarishaji wa filamu inayohusu maisha ya hayati Tupac Shakur ,L.T Hutton kuelezea sababu zilizomfanya kumbadilisha muongozaji wa filamu hiyo kutoka John Singleton na kumuweka muongozaji Benny "Boom" Douglas.  Filamu hiyo inayoitwa "all eyez on me" tayari imekwisha andaliwa na inatarajiwa kuzinduliwa leo tarehe 16 Juni 2017.       Akizungumza kwenye mahojiano redioni L.T Hutton amewashtusha watu wengi baada ya kudai kwamba walishindwana na muongozaji wa mwanzo bwana John Singleton sababu muongozaji huyo aling'ang'ania kuwepo kwa matukio (scene) ambazo kwa maoni yake zisingependeza.        Matukio ambayo John Singleton alipenda yawepo katika filamu hiyo ni pamoja na kutaka filamu hiyo ianze na scene ya Tupac akilazimisha kumlawiti msichana wa kizungu.!!!          Singleton pia ali...

ORODHA YA NCHI 80 AMBAZO MTANZANIA ANARUHUSIWA KUINGIA BILA VIZA.

         Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni amesema kuna zaidi ya nchi 80 ambazo watanzania wanaweza kusafiri bila ya kuwa na viza . Mhandisi Hamad Masauni amesema kuna zaidi ya nchi 80 ambazo watanzania wanaweza kusafiri bila ya kuwa na viza za kusafiria kama ilivyokuwa nchi za afrika Mashariki. Mhandisi Massauni amebainisha hayo leo bungeni wakati akijibu swali la Mbunge wa Mlalo kupitia tiketi ya CCM Rashid Shangazi aliyetaka kujua ni nchi ngapi ambazo watanzania wanaweza kusafiri bila ya kuwa na viza (viza on arrival). "Zipo nchi 16 kwa Afrika ambazo watanzania wanaweza kuzitembelea bila ya kuwa na viza na duniani zipo 67" alisema Masauni. Aidha Massauni amezitaja nchi hizo kuwa ni Benin, Burkina Faso, Cape Verde, Ivory Coast, Djibouti, Gabon, Gambia, Guinea, Guinea­Bissau, Liberia, Mali, Mauritania, Niger, Sierra Leone pamoja na Togo. Pamoja na hayo Masauni amesema...

"BUREAU DE CHANGE" ZOTE TANZANIA KUFUTIWA LESENI.

BENKI Kuu ya Tanzania (BoT) imetoa waraka kwa wafanyabiashara wa maduka ya kuuza na kununua fedha za kigeni kuomba upya leseni kwa ajili ya kufanya biashara hiyo. Leseni zote za maduka ya kubadilisha fedha za kigeni zitafutwa ifikapo Septemba 2, mwaka huu ili wamiliki waombe upya. Hayo yalisemwa jana na Ofisa Msimamizi Maduka ya Kuuza na Kununua Fedha za Kigeni wa Benki Kuu ya Tanzania, Kanuti Mosha kwenye Maonesho ya 41 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (DITF) yanayoendelea kwenye Viwanja vya Mwalimu Nyerere, Barabara ya Kilwa, Temeke jijini Dar es Salaam. Mosha alisema kwa sheria ya sasa, mfanyabiashara atatakiwa kumiliki duka moja tu tofauti na ilivyokuwa awali mtu mmoja anaweza kumiliki maduka hata matano. Alisema sambamba na kutoa leseni upya, BoT imeweka viwango vipya vya mtaji ambavyo vinaanzia Sh milioni 100 hadi 300 kwa daraja A, na kuanzia Sh milioni 250 hadi Sh bilioni moja kwa daraja B na Amana ya Thamani kuanzia Dola za Marekani milioni 50 hadi milioni 100. A...