Skip to main content

RAIS MNANGAGWA KUTUMIA INTERPOL KUWAKAMATA WASHIRIKA WA MUGABE WALIOKIMBIA ZIMBABWE.



Serikali ya Emmerson Mnangagwa inataka kutumia huduma za Interpol(Polisi wa kimataifa) kuwasaka washirika wa karibu wa rais Robert Mugabe ambao walikimbia nchi wakati jeshi lilipositisha utawala wa zamani mwezi uliopita.

Mawaziri wa zamani Jonathan Moyo, Saviour Kasukuwere na Paddy Zhanda wanaaminika kuwa ndio walengwa wakuu wa msako huo kwa sababu za tuhuma za uhalifu unaohusishwa na rushwa.

Tume ya kupambana na rushwa ya Zimbabwe, Zimbabwe Anti-Corruption Commission (ZACC) inachunguza tuhuma za Moyo za wizi katika Shirika la Maendeleo ya Wanawake wa Zimbabwe wakati wa utawala wa Mugabe. Moyo alidai kuwa Mnangagwa alikuwa akitumia ZACC kutekeleza visasi binafsi vinavyohusishwa na mapambano ya kutaka kumrithi Mugabe.

ZACC tayari imekamata washirika wa karibu wa Mugabe yaani Joseph Made, Walter Chidakwa, Ignatius Chombo na Jason Machaya. Viongozi wa zamani wa vijana wa chama tawala cha Zanu PF, Kudzanai Chipanga na Innocent Hamandishe pia walikamatwa kwa mashtaka ya jinai  wakati jeshi lilipokua linachukua utawala.

Waziri wa Mambo ya Ndani Obert Mpofu alithibitisha katika mahojiano na gazeti la  'The Standard' la Zimbabwe, kwamba serikali itatumia Interpol kuwasaka wale walio nje ya nchi.

"Tunafanya kila linalowezekana ili kuhakikisha kuwa wale waliofanya uhalifu ndani ya Zimbabwe ambao wako nje ya Zimbabwe wanaletwa. Ikiwa inamaanisha kushirikisha Interpol, "
alisema.

"Mchakato huu ni wa pili, tunaangalia uchunguzi wa ndani na uchunguzi wa nje na uchunguzi wa nje, unahusisha Interpol."

Hata hivyo, Mpofu alikataa kusema kuwa Kasukuwere, Zhanda na Moyo ndio walengwa wakuu ya uchunguzi huo.

"Tunasema juu ya wote waliofanya uhalifu nchini Zimbabwe na ikiwa wamefanya uhalifu, watashiriki katika zoezi hili," 
alisema.

"Kama wale watatu wanahusika katika uhalifu uliofanywa nchini Zimbabwe watakuwa sehemu ya uchunguzi wetu."


Siku ya Ijumaa, Mnangagwa alisema kuwa amewasamehe wafusai wa G40, ikiwa ni pamoja na wale waliokimbia kwenda nchi nyingine, lakini walisema watatu kati yao bado wanatuhuma za kujibu. Lakini hakutaja mtu yeyote kwa jina.

Serikali mapema mwezi huu walifungia akaunti za benki za Kasukuwere na Moyo. Wakati huo huo, pamoja na matangazo ya umma ya Mnangagwa kwamba wa Zimbabwe wanapaswa kuruhusu "maadili kuwa sawa", dalili ni kwamba taasisi za serikali zinatafuta wafuasi wa G40.

Kulingana na ripoti, Chipanga amepoteza shamba lake huko Rusape kama adhabu ya kumsaidia mke wa rais wa zamani ,Grace Mugabe dhidi ya Mnangagwa.



Mkurugenzi wa shirika la haki za binadamu la nchi za kusini mwa Afrika Dewa Mavhinga alisema serikali ya Zimbabwe inapaswa kuthibitisha kuwa kamata kamata hiyo haina nia ya kulipiza kisasi kundi la Zanu PF Lacoste, lililoshinda vita ya kurithi urais wa nchi hiyo kutoka kwa Robert Mugabe.

"Serikali ya Mnangagwa ina changamoto ya kuonyesha kwamba kukamatwa kwa hivi karibuni kwa mawaziri wa zamani hayaendeshwi na kisasi na uwindaji wa mchawi wa kisiasa na kwamba kuna dhamira kamili ya kuondokana na rushwa," alisema.

"Je, serikali itawakamata mawaziri wa sasa ambao wamekuwa wakihukumiwa hadharani kwa vitendo vya rushwa kama Obert Mpofu, ambaye alidaiwa kudai rushwa ya dola milioni 10 za kimarekani kutoka kwa Lovemore Kurotwi?


"Kuna haja ya haraka ya kujenga uaminifu kwa umma kwamba serikal ina nia ya dhati ya kumaliza rushwa bila kujali mpasuko wa kiitikadi uliopo."


Mwanaharakati wa haki za binadamu Patson Dzamara alisema kuwa kukamatwa hakuwa na uhusiano na rushwa lakini ni muendelezo wa vita vya mpasuko ndani ya chama tawala cha Zanu PF.

"Hakuna namna yoyote kuwa hii kamata kamata inaweza kuwa juu ya rushwa," alisema.

"Hauhitaji akili nyingi kutambua kwamba Zanu PF ni pango la rushwa, lakini unapomwona mtu mmoja mharifu akimkamata mwingine basi lazima ujue sio kuhusu rushwa."

"...Kwao wanataka tuamini kwamba ni wale tu waliokuwa katika G40 ni wala rushwa ni utani usiochekesha wa kitoto. "


Mnangagwa ameahidi kuondokana na rushwa, akisema kuwa ni moja ya sababu za uchumi wa Zimbabwe kuwa 'bomu'



CHANZO:

Comments

Habari Nyingine Kutoka Kioo17 Swahili;

MCHEZAJI WA ZAMANI WA UINGEREZA AMESEMA ALICHEZA NA WACHEZAJI WATATU MASHOGA KWENYE TIMU.

Carl Hoefkens (jezi no.2) alichezea West Bromwich Albion na Stoke City wakati wa enzi zake ligi kuu ya England. Beki wa zamani wa Ligi Kuu ya Uingereza amesema alicheza pamoja na wachezaji wenzake wawili wa mashoga ndani ya timu, na mmoja alikua na jina kubwa. Carl Hoefkens, West Bromwich Albion na Stoke City siku za nyuma, anasema wachezaji hao walikua wazi na hawakujificha kwenye vyumba vya kubadilishia nguo ingawa bado hawajulikani kwasababu ya maombi yao wenyewe ya kuomba kutotangazwa. Justin Fashanu, ambaye alijiua mwaka 1998, alikuwa mchezaji wa mwisho wa kazi nchini England kuja nje kama mashoga - mwaka 1990. Hoefkens alipokua (kushoto), alipokua anachezea Stock  City. Hoefkens aliyecheza Uingereza kwa miaka minne, akiondoka mwaka 2009, alidai kuwa mchezaji mwenzake mmoja wa timu alikua anaweza kuja kwenye uwanja wa mafunzo ya klabu na mpenzi wake wa kiume  lakini aliwaomba wenzake kutokuwaambia watu wangine wa nje ya timu. 'Nilicheza pamoja n...

ORODHA YA NCHI 80 AMBAZO MTANZANIA ANARUHUSIWA KUINGIA BILA VIZA.

         Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni amesema kuna zaidi ya nchi 80 ambazo watanzania wanaweza kusafiri bila ya kuwa na viza . Mhandisi Hamad Masauni amesema kuna zaidi ya nchi 80 ambazo watanzania wanaweza kusafiri bila ya kuwa na viza za kusafiria kama ilivyokuwa nchi za afrika Mashariki. Mhandisi Massauni amebainisha hayo leo bungeni wakati akijibu swali la Mbunge wa Mlalo kupitia tiketi ya CCM Rashid Shangazi aliyetaka kujua ni nchi ngapi ambazo watanzania wanaweza kusafiri bila ya kuwa na viza (viza on arrival). "Zipo nchi 16 kwa Afrika ambazo watanzania wanaweza kuzitembelea bila ya kuwa na viza na duniani zipo 67" alisema Masauni. Aidha Massauni amezitaja nchi hizo kuwa ni Benin, Burkina Faso, Cape Verde, Ivory Coast, Djibouti, Gabon, Gambia, Guinea, Guinea­Bissau, Liberia, Mali, Mauritania, Niger, Sierra Leone pamoja na Togo. Pamoja na hayo Masauni amesema...

WALICHOJIBU CHENGE ,NGELEJA NA DK.KAFUMU BAADA YA RIPOTI YA PILI YA RAISI.

              VIGOGO waliotajwa katika ripoti ya pili ya kuchunguza makontena yenye mchanga wa madini (makinikia)  kuisababishia Serikali hasara ya matrilioni ya fedha kupitia sekta ya madini, walipokuwa wakihudumu katika nyadhifa zao serikalini wamevunja ukimya. Vigogo hao wamezungumzia ripoti hiyo ya pili iliyowasilishwa kwa Rais Dk. John Magufuli Ikulu Dar es Salaam jana, ambapo kamati husika ilichunguza hasara ambayo nchi imepata tangu 1998 usafirishaji wa mchanga wa dhahabu nje ya nchi ulipoanza. Mbunge wa Bariadi, Andrew Chenge (CCM), alipoulizwa maoni yake juu ya kutajwa na kamati hiyo, alisema hataki kuzungumza chochote juu ya ripoti hiyo, huku Mbunge wa Sengerema, William Ngeleja (CCM), akisema sheria ya madini ya 2010 ingefuatwa, nchi isingekuwa hapa ilipo. Kwa upande wake Kamishna wa Madini wa zamani, Dk. Dalaly Kafumu, alisema kwa sasa  hawezi kuzungumza jambo lolote kwa kuwa ni yeye ni mmoja wa watuhumiwa waliotaj...

KIONGOZI MKUU WA UPINZANI NCHINI ZIMBABWE, MORGAN TSVANGIRAI AMEFARIKI DUNIA.

Kiongozi wa upinzani wa Zimbabwe Morgan Tsvangirai amefariki dunia nchini Afrika Kusini, afisa mkuu wa chama chake cha MDC amesema. Bw Tsvangirai, mwenye umri wa miaka 65, aliyekuwa waziri mkuu, alilipotiwa kuwa alikuwa akisumbuliwa na saratani ya koloni. "Amefariki jioni hii, familia yake imenitaarifu"  Makamu wa Rais wa MDC, Elias Mudzuri aliliambia shirika la habari la Uingereza, Reuters. Morgan Tsvangirai alizaliwa mnamo Machi 10, 1952 huko Gutu, Zimbabwe. Baba yake alikuwa mfanyakazi wa mgodi, fundi, na mkulima. Alihudhuria Shule ya Msingi ya Guco ya St. Marks. Kisha alihamishiwa Shule ya Msingi ya Chikara Gutu. Kwa elimu yake ya sekondari, alihudhuria Shule ya High Gokomere. Alikuwa waziri mkuu katika serikali ya mseto ya Zimbabwe tangu 2009 hadi 2013. Katika kazi yake ya awali alionekana kuwa mfanyakazi mwenye bidii sana na alifanya kazi katika mgodi wa madini ya nickel( kwa zaidi ya muongo mmoja. Alipanda cheo haraka kutambuliwa na akain...

MADAI YA CUBA KWAMBA WAZIRI MKUU WA CANADA NI MTOTO WA FIDEL CASTRO.

Pichani ni waziri mkuu wa Canada, Justin Trudeau (kushoto), na Rais wa zamani wa Cuba, Hayati Fidel Castro (kulia). Maelezo yaliyoandikwa na mtoto wa kwanza wa rais wa zamani wa Cuba , Fidel Castro, kabla ya kujiua yamelishtua taifa la Cuba wiki hii. Maelezo hayo yaliyoandikwa na mtoto huyo mkubwa wa mwanamapinduzi na rais wa zamani wa nchi hiyo yalikuwa ya kushangaza baada ya  kuwa na madai ya kuwa Waziri Mkuu wa Canada Justin Trudeau ni mtoto wa nje wa baba yake marehemu Fidel Castro. Maelezo hayo yaliyoandikwa kwa mkono na mtoto huyo wa Fidel Castro aliyejiua siku chache zilizopita kwa msongo wa mawazo, Fidel Castro Diaz-Balart, aliyekuwa na umri wa miaka 68, yalionekana kuthibitisha uvumi wa muda mrefu nchini Cuba kwamba Fidel Castro ni baba wa damu wa waziri mkuu wa sasa wa Canada, Justin Trudeau ikiwa ni matokeo ya uhusiano wa siri wa kimapenzi na mke wa mwanasiasa maarufu wa Canada, Pierre Trudeau, Margaret Trudeau mwaka 1970. Kifo cha mwanasayansi wa ...

KASHFA YA MAPENZI KATI MH.MBOWE NA WEMA SEPETU.

MH.FREEMAN MBOWE AKIWA NA WEMA SEPETU. Siku chache baada ya ile skendo ya ngono iliyosababisha wakili na mshauri wa Chama cha ACT -Wazalendo , Bwana Albert Msando kujiuzulu kwenye nyadhifa yake ya chama ,yameibuka mangine kwenye chama kikuu cha upinzani Tanzania ,CHADEMA ,baada ya kusambaa kwa kipande cha sauti kinachodaiwa kua ni mazungumzo kati ya mwenyekiti wa chama hicho na mbunge wa Hai Mh.Freeman Mbowe na Miss Tanzania 2006 ,mrembo Wema Isack Sepetu. SIKILIZA HIVI VIPANDE VYA SAUTI: Bonyeza hapa chini kusikiliza maongezi hayo yanayodaiwa kuwa ni kati ya Wema Sepetu na Mh.Freeman Mbowe; Bonyeza hapa chini kusikiliza majibu ya Wema Sepetu; Bonyeza hapa chini kusikiliza majibu ya Mh.Freeman Mbowe; VYANZO: Jamii Forums,                   YouTube.com,                   Perfect255.com.                   

RAPA SNOOP DOGG AMETHIBITISHA MIPANGO YA KUHAMIA UGANDA.

Msanii wa muziki wa Hip Hop wa Marekani, Calvin Cordozar Broadus.Jr. maarufu kama Snoop Dogg amethibitisha kuwa anataka kuhamia Uganda baada ya rais wa Marekani, Donald Trump kudaiwa kuziita nchi za Afrika 'Shimo la Choo' . Snoop Doggy Dogg pia ni mwimbaji, mwandishi wa nyimbo, mtayarishaji wa muziki, mtangazaji katika televisheni, na mwigizaji wa filamu ambaye alianza kupata umaarufu mkubwa katika muziki mwaka 1992 wakati alipogunduliwa na mtayarishaji Dr.Dre, na kushiriki katika nyimbo za Dr.Dre kama "Deep Cover", na kisha kwenye albamu ya kwanza ya Dr.Dre, ' The Chronic' . Kwa sasa tayari ameshauza albamu zaidi ya milioni 23 nchini Marekani na albamu milioni 35 duniani kote. Mmarekani huyo mweusi mwenye miaka 46 wa ambaye anajulikana kwa nyimbo zake za maarufu kama; The next episode, Drop it like it’s hot, beautiful, Lay low,  nk Juzi alirekodi kipande cha video na kukisambaza akisema kuwa anataka kuhamia chini Uganda. Tazama V...