Skip to main content

MUATHIRIKA ASIMULIA JINSI "ALIVYONYONYWA DAMU" NCHINI MALAWI.




Hadithi za mashambulizi ya usiku wa manane na 'Wanyonya damu' (Vampires) za kunyonya damu zinaendelea kusababisha matatizo nchini Malawi, kusini mashariki mwa Afrika.

Madai 'ya waathirika' wanashambuliwa usiku na 'wanyonya damu' yamesababisha vurugu za wananchi kuchukua sheria mkononi na vifo katika sehemu za kusini za nchi hiyo.

Watu takribani saba wameuawa katika wilaya moja, na mapema mwaka huu, wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa na wafanyakazi wa kujitolea kutoka Marekani waliondolewa katika eneo hilo.

Wakati wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa waliporudi sasa, hadithi za mashambulizi ya kunyonya damu zinaendelea.



Jamiya Bauleni, mama mwenye umri wa miaka 40, alisema kuwa mshambulizi aliingia nyumbani kwake na kunyonya damu yake nyumbani kwake katika wilaya ya Thyolo.

'Hii sio kusikia,' aliuambia umati wa watu  katika kijiji cha Ngolongoliwa kusini mwa nchi hiyo ambayo imekuwa katika hali ya hofu hivi karibuni juu ya uvumi wa shughuli za 'wanyonya damu'.

"Najua damu yangu ilinyonywa. Niliona mwanga kwenye kona ya paa langu. Nilishindwa kusimama kutoka kitandani kwangu na nikasikia kitu cha kimetoboa mkono wangu wa kushoto, "alisema, akionesha karibu na kifua chake.


Hadithi yake ni sehemu ya mlolongo mrefu wa ushuhuda sawa nchini Malawi, ambapo imani katika uchawi na shughuli za vampire zinaenea na kusababisha watu kulipa kisasi kwa kujichukulia sheria mkononi na kuwaua watuhumiwa wa uchawi.


Bauleni, ambaye hufanya uuzaji wa chakula cha mchana, alisema kuwa kabla ya kuanguka na kupoteza fahamu alisikia mtu anayekimbia eneo hilo.

Alipelekwa kwenye kliniki na baadaye aliachiliwa baada ya kupewa virutubisho vya vitamini, lakini aliamua kutokuripoti shambulio hilo.

Uvumi wa kuwepo kwa 'wanyonya damu' unasemekana kutokea nchi jirani ya Msumbiji na kuvuka mpaka kuenea mpaka kwenye wilaya za Malawi za Mulanje na Phalombe, kwa mujibu wa ripoti ya Umoja wa Mataifa.

Watu takribani saba wameuawa katika wilaya ya Mulanje baada ya kuwindwa, polisi wanasema.




Muathirika mmoja, Florence Kalunga, mwenye umri wa miaka 27, anasema alikuwa amelala pamoja na mumewe nyumbani kwake alipoona mwanga kama moto.


"Nilisikia mlango unafunguliwa... Nilihisi kitu kama sindano katika kidole changu, "alisema.

Watu wanaolengwa katika vurugu kulipa kisasi mara nyingi ni watu wenye utajiri katika sehemu za vijijini za nchi hiyo ya kusini mwa Afrika ambapo umasikini umezoeleka na kiwango cha elimu ni duni sana.

Mjasiriamali Orlendo Chaponda alifanikiwa  kukimbia mashambulizi wakati wanakijiji 2,000, baadhi yao waliokuwa wamebeba mapanga na mawe walipovamia nyumba yake huko Thyolo mnamo Septemba 30.

"Wao walisema nilikuwa nikiwahifadhi wanyonya damu,",
alisema Chaponda, ambaye alikuwa nje wakati huo.
"Wangeweza kuniua ikiwa wangenipata."

Aliwaita polisi ambao walitumia mabomu ya machozi ili kutawanya umati uliokua umezunguka nyumba yake kwa masaa matano.

"Hakuna ukweli juu ya wanyonya damu, ila watu wenye wivu na majambazi wanataka kuchukua nafasi hiyo kushambulia matajiri,"
Chaponda alisema.

"Ikiwa una gari nzuri, wewe ni mnyonya damu."

Shirika la huduma ya damu ya kitaifa ya Malawi - taasisi pekee iliyoruhusiwa na serikali kukusanya damu kwa ajiri ya hospitali kutoka kwa watu wanaojitolea - limesema kwamba uvumi wa matukio ya 'wanyonya damu' pia umeanza kurudisha nyuma shughuli za taasisi hiyo.

"Suala hili limeleta athari sana...limtuzuia kwenda kukusanya damu katika maeneo yaliyoathirika, "alisema Bridon M'baya, mkurugenzi wa huduma za matibabu.

Watu takribani 250 wamekamatwa nchini Malawi juu ya unyanyasaji wa watu, na wengine 40 walikamatwa juu ya makosa sawa na hayo katika nchi jirani ya Msumbiji.

Rais wa Malawi Peter Mutharika alilazimika kukubali kuwa kumekuwepo na tatizo hilo na kusisitiza kwamba serikali tayari imelidhibiti.

"Hakuna ushahidi wa wanyonya damu. Ni uwongo wenye nia ya kudhoofisha kanda, "alisema hivi karibuni.

"Wale wanaoeneza uvumi huu watapambana na sheria."




Anthony Mtuta, mwalimu msaidizi wa anthropolojia katika Chuo Kikuu cha Katoliki cha Malawi, alisema mizizi ya vitisho vya 'Wanyonya damu' imeanzia katika shida za uchumi na madara katika jamii'

"Ni matajiri dhidi ya masikini. Maskini wanaamini kuwa tajiri ni wenye tamaa na wananyonya damu za watu masikini,", alisema.

Malawi kwa kiasi kikubwa inategemea misaada ya kigeni, lakini baadhi ya wenyeji wanapokea misaada kwa mashaka.

"Kwa wanakijiji, hufikiri kwamba hakuna zawadi utaipata bure ... utailipa kupitia damu," alisema Mtuta.




McDonald Kolokombe, karani katika hifadhi ya misitu ya Likhubula ya serikali, alibainisha kuwa idadi ya watalii waliotembelea eneo la Mulanje imeshuka tangu katikati ya Septemba.

"Jamii hutegemea wageni kulisha familia zao kwa kufanya kazi kama kuongoza watalii na kuwauzia bidhaa", alisema.



"Tuna njaa kwa sababu ya uvumi mbaya juu ya 'wanyonya damu,' ", aliongeza muongoza watalii(tour guide), Eric John.
"Ni uongo mkubwa."




CHANZO:
hinnews.com

Comments

Habari Nyingine Kutoka Kioo17 Swahili;

ORODHA YA NCHI 80 AMBAZO MTANZANIA ANARUHUSIWA KUINGIA BILA VIZA.

         Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni amesema kuna zaidi ya nchi 80 ambazo watanzania wanaweza kusafiri bila ya kuwa na viza . Mhandisi Hamad Masauni amesema kuna zaidi ya nchi 80 ambazo watanzania wanaweza kusafiri bila ya kuwa na viza za kusafiria kama ilivyokuwa nchi za afrika Mashariki. Mhandisi Massauni amebainisha hayo leo bungeni wakati akijibu swali la Mbunge wa Mlalo kupitia tiketi ya CCM Rashid Shangazi aliyetaka kujua ni nchi ngapi ambazo watanzania wanaweza kusafiri bila ya kuwa na viza (viza on arrival). "Zipo nchi 16 kwa Afrika ambazo watanzania wanaweza kuzitembelea bila ya kuwa na viza na duniani zipo 67" alisema Masauni. Aidha Massauni amezitaja nchi hizo kuwa ni Benin, Burkina Faso, Cape Verde, Ivory Coast, Djibouti, Gabon, Gambia, Guinea, Guinea­Bissau, Liberia, Mali, Mauritania, Niger, Sierra Leone pamoja na Togo. Pamoja na hayo Masauni amesema...

USWISI KURUDISHA DOLA MILIONI 321($321M) ZA WIZI KWA NIGERIA.

Serikali ya Nigeria imechukua zaidi ya dola bilioni 1 zilizoaminiwa kuibwa na Rais wa zamani Sani Abacha. CNN: Serikali ya Uswisi kurudisha dola za kimarekani milioni 321 nchini Nigeria ambazo zilikuwa zimechukuliwa kutoka kwenye familia ya Rais wa zamani wa nchi hiyo, Sani Abacha. Mali hizo zilifanywa kama sehemu ya kesi za jinai dhidi ya Abba Abacha, mwana wa Sani, ambaye alitawala Nigeria kwa miaka mitano mpaka kufa kwake mwaka 1998. Wachunguzi wa Nigeria wanaamini rais huyo wa zamani aliiba zaidi ya dola bilioni 4 ($4 Billion) muda wake katika ofisi. Serikali ya Uswisi ilitoa tamko Jumatatu kutangaza makubaliano hayo yaliyofikiwa na viongozi kutoka serikali ya Nigeria na Benki ya Dunia kwa marekebisho. "Marejesho ya fedha yatatokea katika mfumo wa mradi unaoungwa mkono na kusimamiwa na Benki ya Dunia," ,  ilisema taarifa hiyo. "Mradi utaimarisha usalama wa kijamii kwa sehemu maskini zaidi ya idadi ya watu wa Nigeria." Serikali ya Nigeria ilit...

SABABU ZA KUVUNJIKA KWA KUNDI LA P-SQUARE.

WANAMUZIKI MAPACHA WA KUNDI LA PSQUARE, PETER (KUSHOTO) NA PAUL (KULIA) WAKIWA NA KAKA YAO AMBAE PIA NI MENEJA WAO, JUDES OKOYE. Mwanamuziki wa kundi la PSquare kutoka Nigeria, Peter Okoye ametangaza kujitoa kwenye kundi hilo la muziki wa Pop maarufu zaidi Afrika. Msanii huyo alidai kwamba amewasilisha maombi ya kuvunja kundi hilo katika barua aliyoandika kwa wakili wao Festus Keyamo. Kulingana na nakala ya barua iliyotolewa kwenye vyombo vya habari Jumatatu,Tarehe 25 Septemba, Peter alisema kuwa pacha wake na, Paul, na kaka yao, Judes waliahirisha ziara yao ya muziki ya Marekani bila kushauriana naye.Na hiyo ni moja kati ya sababu za msingi. Peter pia aliwalaumu Paul na kaka yao mkubwa mkubwa ambae ni meneja wao pia kwa udanganyifu walioufanya ili kutatua shida waliyokuwa nayo juu ya biashara ya muziki. Wasanii hao ndugu wamekua kwenye vita vya maneno kwenye mitandao ya kijamii tangu mwisho wa mwaka jana pamoja na juhudi za watu wao wa karibu kujaribu kuwapatanisha kifami...

TUPAC SHAKUR ALIBAKWA JELA !!!

             Ulimwengu wa filamu za Hollywood na muziki wa Hip Hop juzi ulipatwa na mshangao baada ya mtayarishaji wa filamu inayohusu maisha ya hayati Tupac Shakur ,L.T Hutton kuelezea sababu zilizomfanya kumbadilisha muongozaji wa filamu hiyo kutoka John Singleton na kumuweka muongozaji Benny "Boom" Douglas.  Filamu hiyo inayoitwa "all eyez on me" tayari imekwisha andaliwa na inatarajiwa kuzinduliwa leo tarehe 16 Juni 2017.       Akizungumza kwenye mahojiano redioni L.T Hutton amewashtusha watu wengi baada ya kudai kwamba walishindwana na muongozaji wa mwanzo bwana John Singleton sababu muongozaji huyo aling'ang'ania kuwepo kwa matukio (scene) ambazo kwa maoni yake zisingependeza.        Matukio ambayo John Singleton alipenda yawepo katika filamu hiyo ni pamoja na kutaka filamu hiyo ianze na scene ya Tupac akilazimisha kumlawiti msichana wa kizungu.!!!          Singleton pia ali...

ALICHOANDIKA MH.NGELEJA BAADA YA KURUDISHA FEDHA ZA ESCROW.

MH.WILLIAM NGELEJA .            Waziri wa zamani wa Nishati na Madini na Mbunge wa Jimbo la Sengerema, William Ngeleja amerejesha rasmi Serikalini fedha alizozipata katika mgao wa Escrow ambazo ni kiasi cha Shilingi Milioni 40.4 ili kukwepa kuendelea kuandamwa na kashfa.        Ngeleja amesema ingawa alipewa fedha hizo kama sehemu ya msaada , ameamua kurudisha fedha hizo ili kukwepa kashfa hiyo ya ESCROW.     SOMA HAPA BARUA ALIYOITOA KWA WAANDISHI WA HABARI ;

MCHEZAJI WA ZAMANI WA UINGEREZA AMESEMA ALICHEZA NA WACHEZAJI WATATU MASHOGA KWENYE TIMU.

Carl Hoefkens (jezi no.2) alichezea West Bromwich Albion na Stoke City wakati wa enzi zake ligi kuu ya England. Beki wa zamani wa Ligi Kuu ya Uingereza amesema alicheza pamoja na wachezaji wenzake wawili wa mashoga ndani ya timu, na mmoja alikua na jina kubwa. Carl Hoefkens, West Bromwich Albion na Stoke City siku za nyuma, anasema wachezaji hao walikua wazi na hawakujificha kwenye vyumba vya kubadilishia nguo ingawa bado hawajulikani kwasababu ya maombi yao wenyewe ya kuomba kutotangazwa. Justin Fashanu, ambaye alijiua mwaka 1998, alikuwa mchezaji wa mwisho wa kazi nchini England kuja nje kama mashoga - mwaka 1990. Hoefkens alipokua (kushoto), alipokua anachezea Stock  City. Hoefkens aliyecheza Uingereza kwa miaka minne, akiondoka mwaka 2009, alidai kuwa mchezaji mwenzake mmoja wa timu alikua anaweza kuja kwenye uwanja wa mafunzo ya klabu na mpenzi wake wa kiume  lakini aliwaomba wenzake kutokuwaambia watu wangine wa nje ya timu. 'Nilicheza pamoja n...

ALICHOSEMA SHEIKH PONDA KUHUSU MIILI INAYOOKOTWA BAHARINI.

SHEIKH PONDA. KUTOKA GAZETI LA NIPASHE ,22 Agosti 2017; Akizungumza na Nipashe kwa simu jana, Sheikh Ponda ambaye pia ni Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Taasisi za Kiislamu Tanzania, alisema kwa muda mrefu wamekuwa wakipaza sauti kuhusu uwapo wa mauaji ya raia kwenye mikoa ya kusini mwa Tanzania, lakini haijasikilizwa. "Tunapongeza Nipashe kwa habari hii," alisema Sheikh Ponda kwa sababu "imefichua mambo mengi.", "Haya tumeshayasema lakini hakuna aliyetusikiliza. "Ni wakati mwafaka serikali ikatoa tamko kwa vile vyombo vya dola vimeonyesha kushindwa kueleza miili hiyo ni ya watu gani na inatoka wapi, (na kibaya) zaidi wanasema wanatambua miili mitatu iliyookotwa ambayo kwa sasa iko Muhimbili." Kaimu Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Lucas Mkondya, aliiambia Nipashe kwa njia ya simu juzi kuwa miili iliyookotwa ni mitatu na haikuwa kwenye viroba. Sheikh Ponda alisema mauaji hayo ni makubwa na hayajawahi kutokea kwa serikali z...