Skip to main content

MUATHIRIKA ASIMULIA JINSI "ALIVYONYONYWA DAMU" NCHINI MALAWI.




Hadithi za mashambulizi ya usiku wa manane na 'Wanyonya damu' (Vampires) za kunyonya damu zinaendelea kusababisha matatizo nchini Malawi, kusini mashariki mwa Afrika.

Madai 'ya waathirika' wanashambuliwa usiku na 'wanyonya damu' yamesababisha vurugu za wananchi kuchukua sheria mkononi na vifo katika sehemu za kusini za nchi hiyo.

Watu takribani saba wameuawa katika wilaya moja, na mapema mwaka huu, wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa na wafanyakazi wa kujitolea kutoka Marekani waliondolewa katika eneo hilo.

Wakati wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa waliporudi sasa, hadithi za mashambulizi ya kunyonya damu zinaendelea.



Jamiya Bauleni, mama mwenye umri wa miaka 40, alisema kuwa mshambulizi aliingia nyumbani kwake na kunyonya damu yake nyumbani kwake katika wilaya ya Thyolo.

'Hii sio kusikia,' aliuambia umati wa watu  katika kijiji cha Ngolongoliwa kusini mwa nchi hiyo ambayo imekuwa katika hali ya hofu hivi karibuni juu ya uvumi wa shughuli za 'wanyonya damu'.

"Najua damu yangu ilinyonywa. Niliona mwanga kwenye kona ya paa langu. Nilishindwa kusimama kutoka kitandani kwangu na nikasikia kitu cha kimetoboa mkono wangu wa kushoto, "alisema, akionesha karibu na kifua chake.


Hadithi yake ni sehemu ya mlolongo mrefu wa ushuhuda sawa nchini Malawi, ambapo imani katika uchawi na shughuli za vampire zinaenea na kusababisha watu kulipa kisasi kwa kujichukulia sheria mkononi na kuwaua watuhumiwa wa uchawi.


Bauleni, ambaye hufanya uuzaji wa chakula cha mchana, alisema kuwa kabla ya kuanguka na kupoteza fahamu alisikia mtu anayekimbia eneo hilo.

Alipelekwa kwenye kliniki na baadaye aliachiliwa baada ya kupewa virutubisho vya vitamini, lakini aliamua kutokuripoti shambulio hilo.

Uvumi wa kuwepo kwa 'wanyonya damu' unasemekana kutokea nchi jirani ya Msumbiji na kuvuka mpaka kuenea mpaka kwenye wilaya za Malawi za Mulanje na Phalombe, kwa mujibu wa ripoti ya Umoja wa Mataifa.

Watu takribani saba wameuawa katika wilaya ya Mulanje baada ya kuwindwa, polisi wanasema.




Muathirika mmoja, Florence Kalunga, mwenye umri wa miaka 27, anasema alikuwa amelala pamoja na mumewe nyumbani kwake alipoona mwanga kama moto.


"Nilisikia mlango unafunguliwa... Nilihisi kitu kama sindano katika kidole changu, "alisema.

Watu wanaolengwa katika vurugu kulipa kisasi mara nyingi ni watu wenye utajiri katika sehemu za vijijini za nchi hiyo ya kusini mwa Afrika ambapo umasikini umezoeleka na kiwango cha elimu ni duni sana.

Mjasiriamali Orlendo Chaponda alifanikiwa  kukimbia mashambulizi wakati wanakijiji 2,000, baadhi yao waliokuwa wamebeba mapanga na mawe walipovamia nyumba yake huko Thyolo mnamo Septemba 30.

"Wao walisema nilikuwa nikiwahifadhi wanyonya damu,",
alisema Chaponda, ambaye alikuwa nje wakati huo.
"Wangeweza kuniua ikiwa wangenipata."

Aliwaita polisi ambao walitumia mabomu ya machozi ili kutawanya umati uliokua umezunguka nyumba yake kwa masaa matano.

"Hakuna ukweli juu ya wanyonya damu, ila watu wenye wivu na majambazi wanataka kuchukua nafasi hiyo kushambulia matajiri,"
Chaponda alisema.

"Ikiwa una gari nzuri, wewe ni mnyonya damu."

Shirika la huduma ya damu ya kitaifa ya Malawi - taasisi pekee iliyoruhusiwa na serikali kukusanya damu kwa ajiri ya hospitali kutoka kwa watu wanaojitolea - limesema kwamba uvumi wa matukio ya 'wanyonya damu' pia umeanza kurudisha nyuma shughuli za taasisi hiyo.

"Suala hili limeleta athari sana...limtuzuia kwenda kukusanya damu katika maeneo yaliyoathirika, "alisema Bridon M'baya, mkurugenzi wa huduma za matibabu.

Watu takribani 250 wamekamatwa nchini Malawi juu ya unyanyasaji wa watu, na wengine 40 walikamatwa juu ya makosa sawa na hayo katika nchi jirani ya Msumbiji.

Rais wa Malawi Peter Mutharika alilazimika kukubali kuwa kumekuwepo na tatizo hilo na kusisitiza kwamba serikali tayari imelidhibiti.

"Hakuna ushahidi wa wanyonya damu. Ni uwongo wenye nia ya kudhoofisha kanda, "alisema hivi karibuni.

"Wale wanaoeneza uvumi huu watapambana na sheria."




Anthony Mtuta, mwalimu msaidizi wa anthropolojia katika Chuo Kikuu cha Katoliki cha Malawi, alisema mizizi ya vitisho vya 'Wanyonya damu' imeanzia katika shida za uchumi na madara katika jamii'

"Ni matajiri dhidi ya masikini. Maskini wanaamini kuwa tajiri ni wenye tamaa na wananyonya damu za watu masikini,", alisema.

Malawi kwa kiasi kikubwa inategemea misaada ya kigeni, lakini baadhi ya wenyeji wanapokea misaada kwa mashaka.

"Kwa wanakijiji, hufikiri kwamba hakuna zawadi utaipata bure ... utailipa kupitia damu," alisema Mtuta.




McDonald Kolokombe, karani katika hifadhi ya misitu ya Likhubula ya serikali, alibainisha kuwa idadi ya watalii waliotembelea eneo la Mulanje imeshuka tangu katikati ya Septemba.

"Jamii hutegemea wageni kulisha familia zao kwa kufanya kazi kama kuongoza watalii na kuwauzia bidhaa", alisema.



"Tuna njaa kwa sababu ya uvumi mbaya juu ya 'wanyonya damu,' ", aliongeza muongoza watalii(tour guide), Eric John.
"Ni uongo mkubwa."




CHANZO:
hinnews.com

Comments

Habari Nyingine Kutoka Kioo17 Swahili;

MCHEZAJI WA ZAMANI WA UINGEREZA AMESEMA ALICHEZA NA WACHEZAJI WATATU MASHOGA KWENYE TIMU.

Carl Hoefkens (jezi no.2) alichezea West Bromwich Albion na Stoke City wakati wa enzi zake ligi kuu ya England. Beki wa zamani wa Ligi Kuu ya Uingereza amesema alicheza pamoja na wachezaji wenzake wawili wa mashoga ndani ya timu, na mmoja alikua na jina kubwa. Carl Hoefkens, West Bromwich Albion na Stoke City siku za nyuma, anasema wachezaji hao walikua wazi na hawakujificha kwenye vyumba vya kubadilishia nguo ingawa bado hawajulikani kwasababu ya maombi yao wenyewe ya kuomba kutotangazwa. Justin Fashanu, ambaye alijiua mwaka 1998, alikuwa mchezaji wa mwisho wa kazi nchini England kuja nje kama mashoga - mwaka 1990. Hoefkens alipokua (kushoto), alipokua anachezea Stock  City. Hoefkens aliyecheza Uingereza kwa miaka minne, akiondoka mwaka 2009, alidai kuwa mchezaji mwenzake mmoja wa timu alikua anaweza kuja kwenye uwanja wa mafunzo ya klabu na mpenzi wake wa kiume  lakini aliwaomba wenzake kutokuwaambia watu wangine wa nje ya timu. 'Nilicheza pamoja n...

ORODHA YA NCHI 80 AMBAZO MTANZANIA ANARUHUSIWA KUINGIA BILA VIZA.

         Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni amesema kuna zaidi ya nchi 80 ambazo watanzania wanaweza kusafiri bila ya kuwa na viza . Mhandisi Hamad Masauni amesema kuna zaidi ya nchi 80 ambazo watanzania wanaweza kusafiri bila ya kuwa na viza za kusafiria kama ilivyokuwa nchi za afrika Mashariki. Mhandisi Massauni amebainisha hayo leo bungeni wakati akijibu swali la Mbunge wa Mlalo kupitia tiketi ya CCM Rashid Shangazi aliyetaka kujua ni nchi ngapi ambazo watanzania wanaweza kusafiri bila ya kuwa na viza (viza on arrival). "Zipo nchi 16 kwa Afrika ambazo watanzania wanaweza kuzitembelea bila ya kuwa na viza na duniani zipo 67" alisema Masauni. Aidha Massauni amezitaja nchi hizo kuwa ni Benin, Burkina Faso, Cape Verde, Ivory Coast, Djibouti, Gabon, Gambia, Guinea, Guinea­Bissau, Liberia, Mali, Mauritania, Niger, Sierra Leone pamoja na Togo. Pamoja na hayo Masauni amesema...

WALICHOJIBU CHENGE ,NGELEJA NA DK.KAFUMU BAADA YA RIPOTI YA PILI YA RAISI.

              VIGOGO waliotajwa katika ripoti ya pili ya kuchunguza makontena yenye mchanga wa madini (makinikia)  kuisababishia Serikali hasara ya matrilioni ya fedha kupitia sekta ya madini, walipokuwa wakihudumu katika nyadhifa zao serikalini wamevunja ukimya. Vigogo hao wamezungumzia ripoti hiyo ya pili iliyowasilishwa kwa Rais Dk. John Magufuli Ikulu Dar es Salaam jana, ambapo kamati husika ilichunguza hasara ambayo nchi imepata tangu 1998 usafirishaji wa mchanga wa dhahabu nje ya nchi ulipoanza. Mbunge wa Bariadi, Andrew Chenge (CCM), alipoulizwa maoni yake juu ya kutajwa na kamati hiyo, alisema hataki kuzungumza chochote juu ya ripoti hiyo, huku Mbunge wa Sengerema, William Ngeleja (CCM), akisema sheria ya madini ya 2010 ingefuatwa, nchi isingekuwa hapa ilipo. Kwa upande wake Kamishna wa Madini wa zamani, Dk. Dalaly Kafumu, alisema kwa sasa  hawezi kuzungumza jambo lolote kwa kuwa ni yeye ni mmoja wa watuhumiwa waliotaj...

KIONGOZI MKUU WA UPINZANI NCHINI ZIMBABWE, MORGAN TSVANGIRAI AMEFARIKI DUNIA.

Kiongozi wa upinzani wa Zimbabwe Morgan Tsvangirai amefariki dunia nchini Afrika Kusini, afisa mkuu wa chama chake cha MDC amesema. Bw Tsvangirai, mwenye umri wa miaka 65, aliyekuwa waziri mkuu, alilipotiwa kuwa alikuwa akisumbuliwa na saratani ya koloni. "Amefariki jioni hii, familia yake imenitaarifu"  Makamu wa Rais wa MDC, Elias Mudzuri aliliambia shirika la habari la Uingereza, Reuters. Morgan Tsvangirai alizaliwa mnamo Machi 10, 1952 huko Gutu, Zimbabwe. Baba yake alikuwa mfanyakazi wa mgodi, fundi, na mkulima. Alihudhuria Shule ya Msingi ya Guco ya St. Marks. Kisha alihamishiwa Shule ya Msingi ya Chikara Gutu. Kwa elimu yake ya sekondari, alihudhuria Shule ya High Gokomere. Alikuwa waziri mkuu katika serikali ya mseto ya Zimbabwe tangu 2009 hadi 2013. Katika kazi yake ya awali alionekana kuwa mfanyakazi mwenye bidii sana na alifanya kazi katika mgodi wa madini ya nickel( kwa zaidi ya muongo mmoja. Alipanda cheo haraka kutambuliwa na akain...

MADAI YA CUBA KWAMBA WAZIRI MKUU WA CANADA NI MTOTO WA FIDEL CASTRO.

Pichani ni waziri mkuu wa Canada, Justin Trudeau (kushoto), na Rais wa zamani wa Cuba, Hayati Fidel Castro (kulia). Maelezo yaliyoandikwa na mtoto wa kwanza wa rais wa zamani wa Cuba , Fidel Castro, kabla ya kujiua yamelishtua taifa la Cuba wiki hii. Maelezo hayo yaliyoandikwa na mtoto huyo mkubwa wa mwanamapinduzi na rais wa zamani wa nchi hiyo yalikuwa ya kushangaza baada ya  kuwa na madai ya kuwa Waziri Mkuu wa Canada Justin Trudeau ni mtoto wa nje wa baba yake marehemu Fidel Castro. Maelezo hayo yaliyoandikwa kwa mkono na mtoto huyo wa Fidel Castro aliyejiua siku chache zilizopita kwa msongo wa mawazo, Fidel Castro Diaz-Balart, aliyekuwa na umri wa miaka 68, yalionekana kuthibitisha uvumi wa muda mrefu nchini Cuba kwamba Fidel Castro ni baba wa damu wa waziri mkuu wa sasa wa Canada, Justin Trudeau ikiwa ni matokeo ya uhusiano wa siri wa kimapenzi na mke wa mwanasiasa maarufu wa Canada, Pierre Trudeau, Margaret Trudeau mwaka 1970. Kifo cha mwanasayansi wa ...

KASHFA YA MAPENZI KATI MH.MBOWE NA WEMA SEPETU.

MH.FREEMAN MBOWE AKIWA NA WEMA SEPETU. Siku chache baada ya ile skendo ya ngono iliyosababisha wakili na mshauri wa Chama cha ACT -Wazalendo , Bwana Albert Msando kujiuzulu kwenye nyadhifa yake ya chama ,yameibuka mangine kwenye chama kikuu cha upinzani Tanzania ,CHADEMA ,baada ya kusambaa kwa kipande cha sauti kinachodaiwa kua ni mazungumzo kati ya mwenyekiti wa chama hicho na mbunge wa Hai Mh.Freeman Mbowe na Miss Tanzania 2006 ,mrembo Wema Isack Sepetu. SIKILIZA HIVI VIPANDE VYA SAUTI: Bonyeza hapa chini kusikiliza maongezi hayo yanayodaiwa kuwa ni kati ya Wema Sepetu na Mh.Freeman Mbowe; Bonyeza hapa chini kusikiliza majibu ya Wema Sepetu; Bonyeza hapa chini kusikiliza majibu ya Mh.Freeman Mbowe; VYANZO: Jamii Forums,                   YouTube.com,                   Perfect255.com.                   

RAPA SNOOP DOGG AMETHIBITISHA MIPANGO YA KUHAMIA UGANDA.

Msanii wa muziki wa Hip Hop wa Marekani, Calvin Cordozar Broadus.Jr. maarufu kama Snoop Dogg amethibitisha kuwa anataka kuhamia Uganda baada ya rais wa Marekani, Donald Trump kudaiwa kuziita nchi za Afrika 'Shimo la Choo' . Snoop Doggy Dogg pia ni mwimbaji, mwandishi wa nyimbo, mtayarishaji wa muziki, mtangazaji katika televisheni, na mwigizaji wa filamu ambaye alianza kupata umaarufu mkubwa katika muziki mwaka 1992 wakati alipogunduliwa na mtayarishaji Dr.Dre, na kushiriki katika nyimbo za Dr.Dre kama "Deep Cover", na kisha kwenye albamu ya kwanza ya Dr.Dre, ' The Chronic' . Kwa sasa tayari ameshauza albamu zaidi ya milioni 23 nchini Marekani na albamu milioni 35 duniani kote. Mmarekani huyo mweusi mwenye miaka 46 wa ambaye anajulikana kwa nyimbo zake za maarufu kama; The next episode, Drop it like it’s hot, beautiful, Lay low,  nk Juzi alirekodi kipande cha video na kukisambaza akisema kuwa anataka kuhamia chini Uganda. Tazama V...