Skip to main content

MWANAMKE WA MIAKA 64 ALIYETAPELIWA $100,000 NA MPENZI ALIYEKUTANA NAE FACEBOOK.

PATRICIA MEISTER (64).

Mwanamke mwenye umri wa miaka 64 amesimulia juu ya jinsi alivyotapeliwa dola 100,000 baada ya kupendana na mtu ambaye ambaye hawakuwahi  kukutana.


Patricia Meister, kutoka Queensland, Australia alianza uhusiano wa mtandaoni na mtu ambaye alidhani alikuwa mfanyabiashara mwenye umri wa miaka katikati baada ya mtu huyo kumtumiaa ombi la rafiki kwenye Facebook mwaka 2015.


Akizungumza na Daily Mail Australia, mwanamke huyo alifafanua wakati alipopiga kichwa juu ya visigino kwa upendo, kabla ya kugundua mpenzi wake wa Italia aitwaye 'Carlos' alikuwa tapeli wa Nigeria.



Bi Meister alisema mwanamume huyo alionekana kujali na kufuatilia kila kitu cha maisha yake alipokua anapiga simu kila siku.

'Sijawahi kuwa kwenye tovuti za marafiki(dating websites), na nilokua natumia Facebook kwasababu za kibiashara. Kwa hiyo nilipopata ombi la urafiki, nilidhani haiwezi kuwa na madhara yoyote ", Alisema.

'Nadhani wakati ule, nilikua napitia katika kipindi cha maisha yangu ambapo nilihisi nikiwa mpweke. Nilikua sina mume muda mrefu na sijawahi kuwa kwenye mitandao ya urafiki '






'Tulianza kuzungumza. Alikuwa mcheshi, mwenye akili na alionekana kuwa na elimu. Alikuwa mzuri sana kwenye lugha ya Kiingereza na alikuwa yuko kimapenzi sana.

Nilimpenda sana katika hatua hiyo '


Alisema huyo mtu ambaye alidai kuwa alikuwa mjini Brisbane,Australia, alimwambia alikuwa akifanya kazi za ubunifu wa ndani(interior design) na asili yake ilikua ni ya Kiitaliano na Scotland.


Wawili hao walibadilishana ujumbe kila siku kabla ya kuanza mazungumzo katika simu.


'Nilipoisikia sauti yake mara ya kwanza ilikua tofauti na ile niliyoitarajia. Nakumbuka nilipokua najiuliza kuwa ile ni rafudhi gani "...sikuweza kuitambua ilikua ni rafudhi gani'

'Sikuweza kuitambua ile rafudhi kwa wakati huo, lakini nikifikiria kwa sasa, ilikua ni dhahiri kutoka Afrika ... Alikua Mnigeria.'


Licha ya kumtilia baadhi ya mashaka, Bibi Meister aliendelea kuzungumza naye na wiki zilipita.


Ndani ya wiki nane katika uhusiano wao, 'Carlos' alimwomba kama angeweza kumkopesha $ 600 kwa sababu kadi yake ya benki ilikataa kufanya kazi wakati akiwa Malaysia kibiashara.

'Sikuona ni sawa lakini nilifikiri na kuona kuwa sio kiasi kikubwa cha pesa kupoteza". Halikuwa ombi kubwa kwa hiyo nilimtumia, "

'Kiasi fulani nilifikiri ilikuwa ni kosa hivyo nikamwuliza, nikisema "wewe ni mfanyabiashara, kadi yako ya benki lazima ifanye kazi ...!" Hadithi yake bado sikuielewa!'



Lakini kuomba kwake fedha hakukuishia hapo, aliweza kutengeneza sababu kila wakati alipotaka kuomba fedha.


'Carlos' alikuwa akipanga safari ya kurudi nyumbani kwa Brisbane wakati bidhaa zake zikishikiliwa na forodha(customs) ya Malaysia. Na hivyo alikuwa na haja ya kulipia.


'Kiasi cha kwanza nilichomtuma kilikuwa $ 7,000. Alipokwenda kuchukua fedha, aliniambia alikuwa anahitaji $ 7,000 $ nyingine ", Alisema Bibi Meister.

'Kila kitu alichosema kilikua na "nyaraka" - na daima kulikuwa na mwanasheria nyuma wakati tunazungumza kwenye simu.

'Alipojaribu kunilipa, alisema benki yake haiwezi kufanya uhamisho mkubwa wa kimataifa kwa hiyo alipanga kutumia kampuni ya kusafirisha vifurushi ili kunitumia fedha badala yake.'


Bi Meister alisema alipewa kiungo(link) kwenye tovuti na 'karatasi ya kufuatilia', ambako aliweka jicho la karibu juu ya usafirishaji wa kifurushi hicho.

Lakini wakati kifurushi hicho kilopofika uwanja wa ndege wa Kuala Lumpur, kulikuwa na ada ya $ 25,000 ya kuruhusu fedha ziondoke nchini.


'Carlos alikuwa ameorodhesha anwani yangu ya biashara kwenye nyaraka, hivyo nilikuwa na wasiwasi kwa kuwa kuna mkoba uliojaa fedha wenye jina langu.

'Kwa wakati huo, nilidhani ninaweza kuonekana muarifu ikiwa nitaruhusu fedha zangu kwa jina langu kukaa pale, nikaona ni vizuri kulipia pesa hiyo ili nipate fedha yangu'.


Bibi Meister alifanya malipo hayo makubwa lakini kifurushi hicho kilipofika uwanja wa ndege wa Melbourne, kilikumbana na ada nyingine.


'Nilikua tayari nimelipa sana.Fedha ilianza kuwa ngumu kupatikana. Alikua amesha chukua kiasi cha mwisho cha pesa zangu,'
,alisema.



Siku iliyopangwa kuwa ndiyo atakayopokea kifurushi cha fedha zake, alipokea simu.

'Nilipokea simu kutoka kwa mtu akisema Carlos na mwanasheria wake wamepata ajali kubwa ya gari hivyo walihitaji fedha kwa gharama za matibabu,'

'Tumbo langu lilishuka mpaka kwenye viatu vyangu... Nilitambua wakati huo kuwa nimesha tapeliwa. '


Bibi Meister hakulipia pesa hizo za matibabu na wawili hao hawakuzungumza kwa karibu wiki.


'Kisha akajaribu kuomba fedha zaidi ili kulipia ada zake za matibabu lakini wakati huo, nilikuwa nimeshatumumia dola yangu ya mwisho,'
,alisema.

'Sikuweza kumlipia tena na hata nikamwambia sitaki kumtumia pesa tena. Muda mfupi baada ya hayo, alipata "ahueni ya ajabu" lakini niliacha kuzungumza naye wakati huo.




Bi Meister alijaribu kutoa ripoti hiyo kwa polisi lakini hawakuwa na kitu ambacho wangeweza kufanya baada ya $100,000 kwa jumla.

Na miezi miwili baadaye, alipokea ujumbe wa maandishi kutoka kwa Carlos, akisema: 'Hii yote ni kutokuelewana.'

Bila kuwaza mara mbili, Bibi Meister alimjibu 'wewe ni tapeli'

Baada ya kumuita tapeli, alimaliza mazungumzo yetu kwakusema: "Nipate kama unaweza, mpendwa wangu",



Bibi Meister alisema hatimaye alipata kikundi cha msaada kinachoitwa Romance Scams ambapo wanawake wanasimulina hadithi zinazofanana na yake.



CHANZO:
dailymail.co.uk

Comments

Habari Nyingine Kutoka Kioo17 Swahili;

MCHEZAJI WA ZAMANI WA UINGEREZA AMESEMA ALICHEZA NA WACHEZAJI WATATU MASHOGA KWENYE TIMU.

Carl Hoefkens (jezi no.2) alichezea West Bromwich Albion na Stoke City wakati wa enzi zake ligi kuu ya England. Beki wa zamani wa Ligi Kuu ya Uingereza amesema alicheza pamoja na wachezaji wenzake wawili wa mashoga ndani ya timu, na mmoja alikua na jina kubwa. Carl Hoefkens, West Bromwich Albion na Stoke City siku za nyuma, anasema wachezaji hao walikua wazi na hawakujificha kwenye vyumba vya kubadilishia nguo ingawa bado hawajulikani kwasababu ya maombi yao wenyewe ya kuomba kutotangazwa. Justin Fashanu, ambaye alijiua mwaka 1998, alikuwa mchezaji wa mwisho wa kazi nchini England kuja nje kama mashoga - mwaka 1990. Hoefkens alipokua (kushoto), alipokua anachezea Stock  City. Hoefkens aliyecheza Uingereza kwa miaka minne, akiondoka mwaka 2009, alidai kuwa mchezaji mwenzake mmoja wa timu alikua anaweza kuja kwenye uwanja wa mafunzo ya klabu na mpenzi wake wa kiume  lakini aliwaomba wenzake kutokuwaambia watu wangine wa nje ya timu. 'Nilicheza pamoja n...

STAR TV YAFUNGIWA NA TRA KWA KUKWEPA KODI.

Mamlaka ya mapato Tanzania inadaiwa kuifungia Radio Free Africa ya Mwanza inayomilikiwa na Antony Dialo kutokana na kudaiwa kodi kubwa. TRA wamewaondoa studio wafanyakazi wote na kuifunga radio hiyo. Kwa sasa ukiwasha radio utasikia matangazo ya kiingereza ya BBC. Diallo ni mwenyekiti wa CCM Mwanza na anadaiwa mamilioni ya kodi na TRA miaka mingi. Star Tv pia imekumbwa na sekeseke hilo. Ikumbukwe hii ndio TV pekee binafsi iliyokuwa ikipingana na MOAT na TEF katika sakata la RC Paul Makonda na walirusha kipindi maalum cha Makonda huku Jumuiya ya Wanahabari wakitangaza rasmi kujitenga na maswahibu yoyote yatakayokuja kuikuta RFA na Star TV. VYANZO : https://www.jamiiforums.com/threads/tra-waifungia-rfa-kwa-kudaiwa-kodi-ya-sh-bilioni-4-5.1283386/

JINSI YA KUOMBA PASSPORT YA TANZANIA KWA NJIA YA INTERNET.

Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kupitia i dara ya Uhamiaji  imezindua huduma ya ujazaji fomu za maombi ya hati ya kusafiria (Passport) kwa njia ya mtandao, ambapo mwombaji atalazimika kujaza fomu hizo na kuzichapisha kabla ya kuziwasilisha kwenye ofisi za uhamiaji. Idara hiyo pia imeeleza kuwa matumizi ya huduma hiyo yataenda sambamba na huduma inayotumiwa sasa ya fomu za maombi ya pasipoti mpaka pale itakapotangazwa vinginevyo. Huduma hiyo itaanza kufanya kazi kuanzia Jumatatu tarehe  7/8/2017    na unaweza  kujaza fomu hizo  kwa kufungua tovuti hiyo ambayo ni  https://www.immigration.go.tz/ppt_application/ Utaratibu wa namna ya kujaza fomu hizo umeelekezwa katika fomu husika mtandaoni, na pia wateja wanaweza kupata ufafanuzi au maelezo zaidi kuhusu huduma hiyo kupitia anuani ya Idara ya Uhamiaji ambayo ni   info@immigration.go.tz   au katika Ofisi yoyote ya Uhamiaji iliyo karibu yako. CHANZO: http://dibute.com/muhimu-...

MOURINHO KUMUONDOA MKHITARYAN ILI AWEZE KUMSAJILI OZIL.

Henrikh Mkhitaryan atatupwa kando na meneja wa Manchester United Jose Mourinho ili apate nafasi ya kumsajili jiungo wa Arsenal, Mesut Ozil, kulingana na taarifa.  Bosi huyo wa Manchester United anajua lazima apunguze kikosi chake kama atataka kumsajili Ozil kutokana na madai ya mshahara mkubwa ya bingwa huyo wa Kombe la Dunia. Kiungo huyo mchezeshaji huyo ambaye mkataba wake Arsenal umalizika mwishoni mwa msimu huu, amekuwa akiomba mshahala wa Pauni Laki Tatu (£ 300,000) kwa wiki ili kukubali mkataba mpya wa kuendelea kuchezea Arsenal. Gazeti la 'The Mirror' la Uingereza limeripoti kwamba Mourinho ameamua Mkhitaryan, ambaye alijiunga na klabu kutoka Borussia Dortmund mwaka 2016, anaweza kuwa mchezaji kuondoka Ni uchaguzi wa mantiki kulingana na hali ya sasa ya mchezaji huyo katika kikosi cha Manchester United. Mchezaji huyo kutoka Armenia ameachwa mechi nane za mwisho na Mourinho huku akisema kuwa haamini kama kiungo huyo anastahilo kukukaa katika...

TUPAC SHAKUR ALIBAKWA JELA !!!

             Ulimwengu wa filamu za Hollywood na muziki wa Hip Hop juzi ulipatwa na mshangao baada ya mtayarishaji wa filamu inayohusu maisha ya hayati Tupac Shakur ,L.T Hutton kuelezea sababu zilizomfanya kumbadilisha muongozaji wa filamu hiyo kutoka John Singleton na kumuweka muongozaji Benny "Boom" Douglas.  Filamu hiyo inayoitwa "all eyez on me" tayari imekwisha andaliwa na inatarajiwa kuzinduliwa leo tarehe 16 Juni 2017.       Akizungumza kwenye mahojiano redioni L.T Hutton amewashtusha watu wengi baada ya kudai kwamba walishindwana na muongozaji wa mwanzo bwana John Singleton sababu muongozaji huyo aling'ang'ania kuwepo kwa matukio (scene) ambazo kwa maoni yake zisingependeza.        Matukio ambayo John Singleton alipenda yawepo katika filamu hiyo ni pamoja na kutaka filamu hiyo ianze na scene ya Tupac akilazimisha kumlawiti msichana wa kizungu.!!!          Singleton pia ali...

ORODHA YA NCHI 80 AMBAZO MTANZANIA ANARUHUSIWA KUINGIA BILA VIZA.

         Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni amesema kuna zaidi ya nchi 80 ambazo watanzania wanaweza kusafiri bila ya kuwa na viza . Mhandisi Hamad Masauni amesema kuna zaidi ya nchi 80 ambazo watanzania wanaweza kusafiri bila ya kuwa na viza za kusafiria kama ilivyokuwa nchi za afrika Mashariki. Mhandisi Massauni amebainisha hayo leo bungeni wakati akijibu swali la Mbunge wa Mlalo kupitia tiketi ya CCM Rashid Shangazi aliyetaka kujua ni nchi ngapi ambazo watanzania wanaweza kusafiri bila ya kuwa na viza (viza on arrival). "Zipo nchi 16 kwa Afrika ambazo watanzania wanaweza kuzitembelea bila ya kuwa na viza na duniani zipo 67" alisema Masauni. Aidha Massauni amezitaja nchi hizo kuwa ni Benin, Burkina Faso, Cape Verde, Ivory Coast, Djibouti, Gabon, Gambia, Guinea, Guinea­Bissau, Liberia, Mali, Mauritania, Niger, Sierra Leone pamoja na Togo. Pamoja na hayo Masauni amesema...

"BUREAU DE CHANGE" ZOTE TANZANIA KUFUTIWA LESENI.

BENKI Kuu ya Tanzania (BoT) imetoa waraka kwa wafanyabiashara wa maduka ya kuuza na kununua fedha za kigeni kuomba upya leseni kwa ajili ya kufanya biashara hiyo. Leseni zote za maduka ya kubadilisha fedha za kigeni zitafutwa ifikapo Septemba 2, mwaka huu ili wamiliki waombe upya. Hayo yalisemwa jana na Ofisa Msimamizi Maduka ya Kuuza na Kununua Fedha za Kigeni wa Benki Kuu ya Tanzania, Kanuti Mosha kwenye Maonesho ya 41 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (DITF) yanayoendelea kwenye Viwanja vya Mwalimu Nyerere, Barabara ya Kilwa, Temeke jijini Dar es Salaam. Mosha alisema kwa sheria ya sasa, mfanyabiashara atatakiwa kumiliki duka moja tu tofauti na ilivyokuwa awali mtu mmoja anaweza kumiliki maduka hata matano. Alisema sambamba na kutoa leseni upya, BoT imeweka viwango vipya vya mtaji ambavyo vinaanzia Sh milioni 100 hadi 300 kwa daraja A, na kuanzia Sh milioni 250 hadi Sh bilioni moja kwa daraja B na Amana ya Thamani kuanzia Dola za Marekani milioni 50 hadi milioni 100. A...