Skip to main content

MWANAMKE WA MIAKA 64 ALIYETAPELIWA $100,000 NA MPENZI ALIYEKUTANA NAE FACEBOOK.

PATRICIA MEISTER (64).

Mwanamke mwenye umri wa miaka 64 amesimulia juu ya jinsi alivyotapeliwa dola 100,000 baada ya kupendana na mtu ambaye ambaye hawakuwahi  kukutana.


Patricia Meister, kutoka Queensland, Australia alianza uhusiano wa mtandaoni na mtu ambaye alidhani alikuwa mfanyabiashara mwenye umri wa miaka katikati baada ya mtu huyo kumtumiaa ombi la rafiki kwenye Facebook mwaka 2015.


Akizungumza na Daily Mail Australia, mwanamke huyo alifafanua wakati alipopiga kichwa juu ya visigino kwa upendo, kabla ya kugundua mpenzi wake wa Italia aitwaye 'Carlos' alikuwa tapeli wa Nigeria.



Bi Meister alisema mwanamume huyo alionekana kujali na kufuatilia kila kitu cha maisha yake alipokua anapiga simu kila siku.

'Sijawahi kuwa kwenye tovuti za marafiki(dating websites), na nilokua natumia Facebook kwasababu za kibiashara. Kwa hiyo nilipopata ombi la urafiki, nilidhani haiwezi kuwa na madhara yoyote ", Alisema.

'Nadhani wakati ule, nilikua napitia katika kipindi cha maisha yangu ambapo nilihisi nikiwa mpweke. Nilikua sina mume muda mrefu na sijawahi kuwa kwenye mitandao ya urafiki '






'Tulianza kuzungumza. Alikuwa mcheshi, mwenye akili na alionekana kuwa na elimu. Alikuwa mzuri sana kwenye lugha ya Kiingereza na alikuwa yuko kimapenzi sana.

Nilimpenda sana katika hatua hiyo '


Alisema huyo mtu ambaye alidai kuwa alikuwa mjini Brisbane,Australia, alimwambia alikuwa akifanya kazi za ubunifu wa ndani(interior design) na asili yake ilikua ni ya Kiitaliano na Scotland.


Wawili hao walibadilishana ujumbe kila siku kabla ya kuanza mazungumzo katika simu.


'Nilipoisikia sauti yake mara ya kwanza ilikua tofauti na ile niliyoitarajia. Nakumbuka nilipokua najiuliza kuwa ile ni rafudhi gani "...sikuweza kuitambua ilikua ni rafudhi gani'

'Sikuweza kuitambua ile rafudhi kwa wakati huo, lakini nikifikiria kwa sasa, ilikua ni dhahiri kutoka Afrika ... Alikua Mnigeria.'


Licha ya kumtilia baadhi ya mashaka, Bibi Meister aliendelea kuzungumza naye na wiki zilipita.


Ndani ya wiki nane katika uhusiano wao, 'Carlos' alimwomba kama angeweza kumkopesha $ 600 kwa sababu kadi yake ya benki ilikataa kufanya kazi wakati akiwa Malaysia kibiashara.

'Sikuona ni sawa lakini nilifikiri na kuona kuwa sio kiasi kikubwa cha pesa kupoteza". Halikuwa ombi kubwa kwa hiyo nilimtumia, "

'Kiasi fulani nilifikiri ilikuwa ni kosa hivyo nikamwuliza, nikisema "wewe ni mfanyabiashara, kadi yako ya benki lazima ifanye kazi ...!" Hadithi yake bado sikuielewa!'



Lakini kuomba kwake fedha hakukuishia hapo, aliweza kutengeneza sababu kila wakati alipotaka kuomba fedha.


'Carlos' alikuwa akipanga safari ya kurudi nyumbani kwa Brisbane wakati bidhaa zake zikishikiliwa na forodha(customs) ya Malaysia. Na hivyo alikuwa na haja ya kulipia.


'Kiasi cha kwanza nilichomtuma kilikuwa $ 7,000. Alipokwenda kuchukua fedha, aliniambia alikuwa anahitaji $ 7,000 $ nyingine ", Alisema Bibi Meister.

'Kila kitu alichosema kilikua na "nyaraka" - na daima kulikuwa na mwanasheria nyuma wakati tunazungumza kwenye simu.

'Alipojaribu kunilipa, alisema benki yake haiwezi kufanya uhamisho mkubwa wa kimataifa kwa hiyo alipanga kutumia kampuni ya kusafirisha vifurushi ili kunitumia fedha badala yake.'


Bi Meister alisema alipewa kiungo(link) kwenye tovuti na 'karatasi ya kufuatilia', ambako aliweka jicho la karibu juu ya usafirishaji wa kifurushi hicho.

Lakini wakati kifurushi hicho kilopofika uwanja wa ndege wa Kuala Lumpur, kulikuwa na ada ya $ 25,000 ya kuruhusu fedha ziondoke nchini.


'Carlos alikuwa ameorodhesha anwani yangu ya biashara kwenye nyaraka, hivyo nilikuwa na wasiwasi kwa kuwa kuna mkoba uliojaa fedha wenye jina langu.

'Kwa wakati huo, nilidhani ninaweza kuonekana muarifu ikiwa nitaruhusu fedha zangu kwa jina langu kukaa pale, nikaona ni vizuri kulipia pesa hiyo ili nipate fedha yangu'.


Bibi Meister alifanya malipo hayo makubwa lakini kifurushi hicho kilipofika uwanja wa ndege wa Melbourne, kilikumbana na ada nyingine.


'Nilikua tayari nimelipa sana.Fedha ilianza kuwa ngumu kupatikana. Alikua amesha chukua kiasi cha mwisho cha pesa zangu,'
,alisema.



Siku iliyopangwa kuwa ndiyo atakayopokea kifurushi cha fedha zake, alipokea simu.

'Nilipokea simu kutoka kwa mtu akisema Carlos na mwanasheria wake wamepata ajali kubwa ya gari hivyo walihitaji fedha kwa gharama za matibabu,'

'Tumbo langu lilishuka mpaka kwenye viatu vyangu... Nilitambua wakati huo kuwa nimesha tapeliwa. '


Bibi Meister hakulipia pesa hizo za matibabu na wawili hao hawakuzungumza kwa karibu wiki.


'Kisha akajaribu kuomba fedha zaidi ili kulipia ada zake za matibabu lakini wakati huo, nilikuwa nimeshatumumia dola yangu ya mwisho,'
,alisema.

'Sikuweza kumlipia tena na hata nikamwambia sitaki kumtumia pesa tena. Muda mfupi baada ya hayo, alipata "ahueni ya ajabu" lakini niliacha kuzungumza naye wakati huo.




Bi Meister alijaribu kutoa ripoti hiyo kwa polisi lakini hawakuwa na kitu ambacho wangeweza kufanya baada ya $100,000 kwa jumla.

Na miezi miwili baadaye, alipokea ujumbe wa maandishi kutoka kwa Carlos, akisema: 'Hii yote ni kutokuelewana.'

Bila kuwaza mara mbili, Bibi Meister alimjibu 'wewe ni tapeli'

Baada ya kumuita tapeli, alimaliza mazungumzo yetu kwakusema: "Nipate kama unaweza, mpendwa wangu",



Bibi Meister alisema hatimaye alipata kikundi cha msaada kinachoitwa Romance Scams ambapo wanawake wanasimulina hadithi zinazofanana na yake.



CHANZO:
dailymail.co.uk

Comments

Habari Nyingine Kutoka Kioo17 Swahili;

MCHEZAJI WA ZAMANI WA UINGEREZA AMESEMA ALICHEZA NA WACHEZAJI WATATU MASHOGA KWENYE TIMU.

Carl Hoefkens (jezi no.2) alichezea West Bromwich Albion na Stoke City wakati wa enzi zake ligi kuu ya England. Beki wa zamani wa Ligi Kuu ya Uingereza amesema alicheza pamoja na wachezaji wenzake wawili wa mashoga ndani ya timu, na mmoja alikua na jina kubwa. Carl Hoefkens, West Bromwich Albion na Stoke City siku za nyuma, anasema wachezaji hao walikua wazi na hawakujificha kwenye vyumba vya kubadilishia nguo ingawa bado hawajulikani kwasababu ya maombi yao wenyewe ya kuomba kutotangazwa. Justin Fashanu, ambaye alijiua mwaka 1998, alikuwa mchezaji wa mwisho wa kazi nchini England kuja nje kama mashoga - mwaka 1990. Hoefkens alipokua (kushoto), alipokua anachezea Stock  City. Hoefkens aliyecheza Uingereza kwa miaka minne, akiondoka mwaka 2009, alidai kuwa mchezaji mwenzake mmoja wa timu alikua anaweza kuja kwenye uwanja wa mafunzo ya klabu na mpenzi wake wa kiume  lakini aliwaomba wenzake kutokuwaambia watu wangine wa nje ya timu. 'Nilicheza pamoja n...

ORODHA YA NCHI 80 AMBAZO MTANZANIA ANARUHUSIWA KUINGIA BILA VIZA.

         Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni amesema kuna zaidi ya nchi 80 ambazo watanzania wanaweza kusafiri bila ya kuwa na viza . Mhandisi Hamad Masauni amesema kuna zaidi ya nchi 80 ambazo watanzania wanaweza kusafiri bila ya kuwa na viza za kusafiria kama ilivyokuwa nchi za afrika Mashariki. Mhandisi Massauni amebainisha hayo leo bungeni wakati akijibu swali la Mbunge wa Mlalo kupitia tiketi ya CCM Rashid Shangazi aliyetaka kujua ni nchi ngapi ambazo watanzania wanaweza kusafiri bila ya kuwa na viza (viza on arrival). "Zipo nchi 16 kwa Afrika ambazo watanzania wanaweza kuzitembelea bila ya kuwa na viza na duniani zipo 67" alisema Masauni. Aidha Massauni amezitaja nchi hizo kuwa ni Benin, Burkina Faso, Cape Verde, Ivory Coast, Djibouti, Gabon, Gambia, Guinea, Guinea­Bissau, Liberia, Mali, Mauritania, Niger, Sierra Leone pamoja na Togo. Pamoja na hayo Masauni amesema...

WALICHOJIBU CHENGE ,NGELEJA NA DK.KAFUMU BAADA YA RIPOTI YA PILI YA RAISI.

              VIGOGO waliotajwa katika ripoti ya pili ya kuchunguza makontena yenye mchanga wa madini (makinikia)  kuisababishia Serikali hasara ya matrilioni ya fedha kupitia sekta ya madini, walipokuwa wakihudumu katika nyadhifa zao serikalini wamevunja ukimya. Vigogo hao wamezungumzia ripoti hiyo ya pili iliyowasilishwa kwa Rais Dk. John Magufuli Ikulu Dar es Salaam jana, ambapo kamati husika ilichunguza hasara ambayo nchi imepata tangu 1998 usafirishaji wa mchanga wa dhahabu nje ya nchi ulipoanza. Mbunge wa Bariadi, Andrew Chenge (CCM), alipoulizwa maoni yake juu ya kutajwa na kamati hiyo, alisema hataki kuzungumza chochote juu ya ripoti hiyo, huku Mbunge wa Sengerema, William Ngeleja (CCM), akisema sheria ya madini ya 2010 ingefuatwa, nchi isingekuwa hapa ilipo. Kwa upande wake Kamishna wa Madini wa zamani, Dk. Dalaly Kafumu, alisema kwa sasa  hawezi kuzungumza jambo lolote kwa kuwa ni yeye ni mmoja wa watuhumiwa waliotaj...

KIONGOZI MKUU WA UPINZANI NCHINI ZIMBABWE, MORGAN TSVANGIRAI AMEFARIKI DUNIA.

Kiongozi wa upinzani wa Zimbabwe Morgan Tsvangirai amefariki dunia nchini Afrika Kusini, afisa mkuu wa chama chake cha MDC amesema. Bw Tsvangirai, mwenye umri wa miaka 65, aliyekuwa waziri mkuu, alilipotiwa kuwa alikuwa akisumbuliwa na saratani ya koloni. "Amefariki jioni hii, familia yake imenitaarifu"  Makamu wa Rais wa MDC, Elias Mudzuri aliliambia shirika la habari la Uingereza, Reuters. Morgan Tsvangirai alizaliwa mnamo Machi 10, 1952 huko Gutu, Zimbabwe. Baba yake alikuwa mfanyakazi wa mgodi, fundi, na mkulima. Alihudhuria Shule ya Msingi ya Guco ya St. Marks. Kisha alihamishiwa Shule ya Msingi ya Chikara Gutu. Kwa elimu yake ya sekondari, alihudhuria Shule ya High Gokomere. Alikuwa waziri mkuu katika serikali ya mseto ya Zimbabwe tangu 2009 hadi 2013. Katika kazi yake ya awali alionekana kuwa mfanyakazi mwenye bidii sana na alifanya kazi katika mgodi wa madini ya nickel( kwa zaidi ya muongo mmoja. Alipanda cheo haraka kutambuliwa na akain...

MADAI YA CUBA KWAMBA WAZIRI MKUU WA CANADA NI MTOTO WA FIDEL CASTRO.

Pichani ni waziri mkuu wa Canada, Justin Trudeau (kushoto), na Rais wa zamani wa Cuba, Hayati Fidel Castro (kulia). Maelezo yaliyoandikwa na mtoto wa kwanza wa rais wa zamani wa Cuba , Fidel Castro, kabla ya kujiua yamelishtua taifa la Cuba wiki hii. Maelezo hayo yaliyoandikwa na mtoto huyo mkubwa wa mwanamapinduzi na rais wa zamani wa nchi hiyo yalikuwa ya kushangaza baada ya  kuwa na madai ya kuwa Waziri Mkuu wa Canada Justin Trudeau ni mtoto wa nje wa baba yake marehemu Fidel Castro. Maelezo hayo yaliyoandikwa kwa mkono na mtoto huyo wa Fidel Castro aliyejiua siku chache zilizopita kwa msongo wa mawazo, Fidel Castro Diaz-Balart, aliyekuwa na umri wa miaka 68, yalionekana kuthibitisha uvumi wa muda mrefu nchini Cuba kwamba Fidel Castro ni baba wa damu wa waziri mkuu wa sasa wa Canada, Justin Trudeau ikiwa ni matokeo ya uhusiano wa siri wa kimapenzi na mke wa mwanasiasa maarufu wa Canada, Pierre Trudeau, Margaret Trudeau mwaka 1970. Kifo cha mwanasayansi wa ...

KASHFA YA MAPENZI KATI MH.MBOWE NA WEMA SEPETU.

MH.FREEMAN MBOWE AKIWA NA WEMA SEPETU. Siku chache baada ya ile skendo ya ngono iliyosababisha wakili na mshauri wa Chama cha ACT -Wazalendo , Bwana Albert Msando kujiuzulu kwenye nyadhifa yake ya chama ,yameibuka mangine kwenye chama kikuu cha upinzani Tanzania ,CHADEMA ,baada ya kusambaa kwa kipande cha sauti kinachodaiwa kua ni mazungumzo kati ya mwenyekiti wa chama hicho na mbunge wa Hai Mh.Freeman Mbowe na Miss Tanzania 2006 ,mrembo Wema Isack Sepetu. SIKILIZA HIVI VIPANDE VYA SAUTI: Bonyeza hapa chini kusikiliza maongezi hayo yanayodaiwa kuwa ni kati ya Wema Sepetu na Mh.Freeman Mbowe; Bonyeza hapa chini kusikiliza majibu ya Wema Sepetu; Bonyeza hapa chini kusikiliza majibu ya Mh.Freeman Mbowe; VYANZO: Jamii Forums,                   YouTube.com,                   Perfect255.com.                   

RAPA SNOOP DOGG AMETHIBITISHA MIPANGO YA KUHAMIA UGANDA.

Msanii wa muziki wa Hip Hop wa Marekani, Calvin Cordozar Broadus.Jr. maarufu kama Snoop Dogg amethibitisha kuwa anataka kuhamia Uganda baada ya rais wa Marekani, Donald Trump kudaiwa kuziita nchi za Afrika 'Shimo la Choo' . Snoop Doggy Dogg pia ni mwimbaji, mwandishi wa nyimbo, mtayarishaji wa muziki, mtangazaji katika televisheni, na mwigizaji wa filamu ambaye alianza kupata umaarufu mkubwa katika muziki mwaka 1992 wakati alipogunduliwa na mtayarishaji Dr.Dre, na kushiriki katika nyimbo za Dr.Dre kama "Deep Cover", na kisha kwenye albamu ya kwanza ya Dr.Dre, ' The Chronic' . Kwa sasa tayari ameshauza albamu zaidi ya milioni 23 nchini Marekani na albamu milioni 35 duniani kote. Mmarekani huyo mweusi mwenye miaka 46 wa ambaye anajulikana kwa nyimbo zake za maarufu kama; The next episode, Drop it like it’s hot, beautiful, Lay low,  nk Juzi alirekodi kipande cha video na kukisambaza akisema kuwa anataka kuhamia chini Uganda. Tazama V...