Skip to main content

MWANAMKE WA MIAKA 64 ALIYETAPELIWA $100,000 NA MPENZI ALIYEKUTANA NAE FACEBOOK.

PATRICIA MEISTER (64).

Mwanamke mwenye umri wa miaka 64 amesimulia juu ya jinsi alivyotapeliwa dola 100,000 baada ya kupendana na mtu ambaye ambaye hawakuwahi  kukutana.


Patricia Meister, kutoka Queensland, Australia alianza uhusiano wa mtandaoni na mtu ambaye alidhani alikuwa mfanyabiashara mwenye umri wa miaka katikati baada ya mtu huyo kumtumiaa ombi la rafiki kwenye Facebook mwaka 2015.


Akizungumza na Daily Mail Australia, mwanamke huyo alifafanua wakati alipopiga kichwa juu ya visigino kwa upendo, kabla ya kugundua mpenzi wake wa Italia aitwaye 'Carlos' alikuwa tapeli wa Nigeria.



Bi Meister alisema mwanamume huyo alionekana kujali na kufuatilia kila kitu cha maisha yake alipokua anapiga simu kila siku.

'Sijawahi kuwa kwenye tovuti za marafiki(dating websites), na nilokua natumia Facebook kwasababu za kibiashara. Kwa hiyo nilipopata ombi la urafiki, nilidhani haiwezi kuwa na madhara yoyote ", Alisema.

'Nadhani wakati ule, nilikua napitia katika kipindi cha maisha yangu ambapo nilihisi nikiwa mpweke. Nilikua sina mume muda mrefu na sijawahi kuwa kwenye mitandao ya urafiki '






'Tulianza kuzungumza. Alikuwa mcheshi, mwenye akili na alionekana kuwa na elimu. Alikuwa mzuri sana kwenye lugha ya Kiingereza na alikuwa yuko kimapenzi sana.

Nilimpenda sana katika hatua hiyo '


Alisema huyo mtu ambaye alidai kuwa alikuwa mjini Brisbane,Australia, alimwambia alikuwa akifanya kazi za ubunifu wa ndani(interior design) na asili yake ilikua ni ya Kiitaliano na Scotland.


Wawili hao walibadilishana ujumbe kila siku kabla ya kuanza mazungumzo katika simu.


'Nilipoisikia sauti yake mara ya kwanza ilikua tofauti na ile niliyoitarajia. Nakumbuka nilipokua najiuliza kuwa ile ni rafudhi gani "...sikuweza kuitambua ilikua ni rafudhi gani'

'Sikuweza kuitambua ile rafudhi kwa wakati huo, lakini nikifikiria kwa sasa, ilikua ni dhahiri kutoka Afrika ... Alikua Mnigeria.'


Licha ya kumtilia baadhi ya mashaka, Bibi Meister aliendelea kuzungumza naye na wiki zilipita.


Ndani ya wiki nane katika uhusiano wao, 'Carlos' alimwomba kama angeweza kumkopesha $ 600 kwa sababu kadi yake ya benki ilikataa kufanya kazi wakati akiwa Malaysia kibiashara.

'Sikuona ni sawa lakini nilifikiri na kuona kuwa sio kiasi kikubwa cha pesa kupoteza". Halikuwa ombi kubwa kwa hiyo nilimtumia, "

'Kiasi fulani nilifikiri ilikuwa ni kosa hivyo nikamwuliza, nikisema "wewe ni mfanyabiashara, kadi yako ya benki lazima ifanye kazi ...!" Hadithi yake bado sikuielewa!'



Lakini kuomba kwake fedha hakukuishia hapo, aliweza kutengeneza sababu kila wakati alipotaka kuomba fedha.


'Carlos' alikuwa akipanga safari ya kurudi nyumbani kwa Brisbane wakati bidhaa zake zikishikiliwa na forodha(customs) ya Malaysia. Na hivyo alikuwa na haja ya kulipia.


'Kiasi cha kwanza nilichomtuma kilikuwa $ 7,000. Alipokwenda kuchukua fedha, aliniambia alikuwa anahitaji $ 7,000 $ nyingine ", Alisema Bibi Meister.

'Kila kitu alichosema kilikua na "nyaraka" - na daima kulikuwa na mwanasheria nyuma wakati tunazungumza kwenye simu.

'Alipojaribu kunilipa, alisema benki yake haiwezi kufanya uhamisho mkubwa wa kimataifa kwa hiyo alipanga kutumia kampuni ya kusafirisha vifurushi ili kunitumia fedha badala yake.'


Bi Meister alisema alipewa kiungo(link) kwenye tovuti na 'karatasi ya kufuatilia', ambako aliweka jicho la karibu juu ya usafirishaji wa kifurushi hicho.

Lakini wakati kifurushi hicho kilopofika uwanja wa ndege wa Kuala Lumpur, kulikuwa na ada ya $ 25,000 ya kuruhusu fedha ziondoke nchini.


'Carlos alikuwa ameorodhesha anwani yangu ya biashara kwenye nyaraka, hivyo nilikuwa na wasiwasi kwa kuwa kuna mkoba uliojaa fedha wenye jina langu.

'Kwa wakati huo, nilidhani ninaweza kuonekana muarifu ikiwa nitaruhusu fedha zangu kwa jina langu kukaa pale, nikaona ni vizuri kulipia pesa hiyo ili nipate fedha yangu'.


Bibi Meister alifanya malipo hayo makubwa lakini kifurushi hicho kilipofika uwanja wa ndege wa Melbourne, kilikumbana na ada nyingine.


'Nilikua tayari nimelipa sana.Fedha ilianza kuwa ngumu kupatikana. Alikua amesha chukua kiasi cha mwisho cha pesa zangu,'
,alisema.



Siku iliyopangwa kuwa ndiyo atakayopokea kifurushi cha fedha zake, alipokea simu.

'Nilipokea simu kutoka kwa mtu akisema Carlos na mwanasheria wake wamepata ajali kubwa ya gari hivyo walihitaji fedha kwa gharama za matibabu,'

'Tumbo langu lilishuka mpaka kwenye viatu vyangu... Nilitambua wakati huo kuwa nimesha tapeliwa. '


Bibi Meister hakulipia pesa hizo za matibabu na wawili hao hawakuzungumza kwa karibu wiki.


'Kisha akajaribu kuomba fedha zaidi ili kulipia ada zake za matibabu lakini wakati huo, nilikuwa nimeshatumumia dola yangu ya mwisho,'
,alisema.

'Sikuweza kumlipia tena na hata nikamwambia sitaki kumtumia pesa tena. Muda mfupi baada ya hayo, alipata "ahueni ya ajabu" lakini niliacha kuzungumza naye wakati huo.




Bi Meister alijaribu kutoa ripoti hiyo kwa polisi lakini hawakuwa na kitu ambacho wangeweza kufanya baada ya $100,000 kwa jumla.

Na miezi miwili baadaye, alipokea ujumbe wa maandishi kutoka kwa Carlos, akisema: 'Hii yote ni kutokuelewana.'

Bila kuwaza mara mbili, Bibi Meister alimjibu 'wewe ni tapeli'

Baada ya kumuita tapeli, alimaliza mazungumzo yetu kwakusema: "Nipate kama unaweza, mpendwa wangu",



Bibi Meister alisema hatimaye alipata kikundi cha msaada kinachoitwa Romance Scams ambapo wanawake wanasimulina hadithi zinazofanana na yake.



CHANZO:
dailymail.co.uk

Comments

Habari Nyingine Kutoka Kioo17 Swahili;

ORODHA YA NCHI 80 AMBAZO MTANZANIA ANARUHUSIWA KUINGIA BILA VIZA.

         Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni amesema kuna zaidi ya nchi 80 ambazo watanzania wanaweza kusafiri bila ya kuwa na viza . Mhandisi Hamad Masauni amesema kuna zaidi ya nchi 80 ambazo watanzania wanaweza kusafiri bila ya kuwa na viza za kusafiria kama ilivyokuwa nchi za afrika Mashariki. Mhandisi Massauni amebainisha hayo leo bungeni wakati akijibu swali la Mbunge wa Mlalo kupitia tiketi ya CCM Rashid Shangazi aliyetaka kujua ni nchi ngapi ambazo watanzania wanaweza kusafiri bila ya kuwa na viza (viza on arrival). "Zipo nchi 16 kwa Afrika ambazo watanzania wanaweza kuzitembelea bila ya kuwa na viza na duniani zipo 67" alisema Masauni. Aidha Massauni amezitaja nchi hizo kuwa ni Benin, Burkina Faso, Cape Verde, Ivory Coast, Djibouti, Gabon, Gambia, Guinea, Guinea­Bissau, Liberia, Mali, Mauritania, Niger, Sierra Leone pamoja na Togo. Pamoja na hayo Masauni amesema...

MCHEZAJI WA ZAMANI WA UINGEREZA AMESEMA ALICHEZA NA WACHEZAJI WATATU MASHOGA KWENYE TIMU.

Carl Hoefkens (jezi no.2) alichezea West Bromwich Albion na Stoke City wakati wa enzi zake ligi kuu ya England. Beki wa zamani wa Ligi Kuu ya Uingereza amesema alicheza pamoja na wachezaji wenzake wawili wa mashoga ndani ya timu, na mmoja alikua na jina kubwa. Carl Hoefkens, West Bromwich Albion na Stoke City siku za nyuma, anasema wachezaji hao walikua wazi na hawakujificha kwenye vyumba vya kubadilishia nguo ingawa bado hawajulikani kwasababu ya maombi yao wenyewe ya kuomba kutotangazwa. Justin Fashanu, ambaye alijiua mwaka 1998, alikuwa mchezaji wa mwisho wa kazi nchini England kuja nje kama mashoga - mwaka 1990. Hoefkens alipokua (kushoto), alipokua anachezea Stock  City. Hoefkens aliyecheza Uingereza kwa miaka minne, akiondoka mwaka 2009, alidai kuwa mchezaji mwenzake mmoja wa timu alikua anaweza kuja kwenye uwanja wa mafunzo ya klabu na mpenzi wake wa kiume  lakini aliwaomba wenzake kutokuwaambia watu wangine wa nje ya timu. 'Nilicheza pamoja n...

ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2017, TANZANIA

MH.GEORGE SIMBACHAWENE .               Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Tamisemi) George Simbachawene ametoa idadi ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na masomo ya kidato cha tano na vyuo vya ufundi kwa mwaka 2017 huku jumla ya wanafunzi 2,999 wakiachwa.             Simbachawene ametoa kauli hiyo leo mjini Dodoma wakati akizungumza na waandishi ws habari na kusema kuwa ufaulu kwa mwaka huu umeongezeka kwa asilimia 3.75 ukilinganisha na matokeo ya mwaka 2015. Waziri amedai kati ya wanafunzi 96,018 waliofaulu kwa daraja la kwanza hadi la tatu ni wanafunzi 93,019 tu ndiyo waliochaguliwa kujiunga na kidato cha tano na vyuo vya ufundi.              Waziri Simbachawene amesema kuwa jumla ya watahiniwa wote waliofanya mtihani wa kidato cha nne kwa shule kwa mwaka 2016 ni 349,524 huku waliofanya mtihani wa kujitegemea ni 47,751 ambapo watahiniwa waliofanya mtihani wa shule...

TUPAC SHAKUR ALIBAKWA JELA !!!

             Ulimwengu wa filamu za Hollywood na muziki wa Hip Hop juzi ulipatwa na mshangao baada ya mtayarishaji wa filamu inayohusu maisha ya hayati Tupac Shakur ,L.T Hutton kuelezea sababu zilizomfanya kumbadilisha muongozaji wa filamu hiyo kutoka John Singleton na kumuweka muongozaji Benny "Boom" Douglas.  Filamu hiyo inayoitwa "all eyez on me" tayari imekwisha andaliwa na inatarajiwa kuzinduliwa leo tarehe 16 Juni 2017.       Akizungumza kwenye mahojiano redioni L.T Hutton amewashtusha watu wengi baada ya kudai kwamba walishindwana na muongozaji wa mwanzo bwana John Singleton sababu muongozaji huyo aling'ang'ania kuwepo kwa matukio (scene) ambazo kwa maoni yake zisingependeza.        Matukio ambayo John Singleton alipenda yawepo katika filamu hiyo ni pamoja na kutaka filamu hiyo ianze na scene ya Tupac akilazimisha kumlawiti msichana wa kizungu.!!!          Singleton pia ali...

MFALME WA GHANA ASABABISHA AFISA MKUU WA BENKI KUFUKUZWA KAZI.

Afisa mtendaji mkuu wa benki alifukuzwa kazi na kuchunguzwa na Shirika la Uhalifu wa Taifa baada ya kuweka pauni za Uingereza 350,000 ( £ 350,000 ) pesa taslimu aliyopewa na Mfalme wa Ghana. Mark Arthur wa benki ya Kimataifa ya Ghana Bigwig aliitwa kwenye nyumba ya Osei Tutu II huko Henley-on-Thames na kupewa £ 200,000 pamoja na $ 200,000 na kuagizwa aiweke kwenye akaunti ya benki ya Mfalme huyo. Licha ya noti hizo kuwa na namba za mfululizo zinazofuatana (consecutive serial numbers) Bwana Arthur alisema aliona kuwa haifai kumhoji mfalme na kwenda kuiweka benki kwa kutumia usafiri wa teksi ya uber. Punde baada ya Bwana Arthur kuweka pesa hiyo benki, taarifa ya utakatishaji wa fedha ilifika katika jiji la London, Uingereza na kugharimu ajira yake. Bwana Arthur alielezea kwenye taarifa yake ya ushahidi kuwa Mfalme alimwambia kwamba pesa hizo zimekusanywa kutoka kwenye akaunti za benki za nchini Ghana na kupelekwa Uingereza. Pia alidai kwamba Mfale alimpa $ 200,000 ili ...

SABABU ZA KUVUNJIKA KWA KUNDI LA P-SQUARE.

WANAMUZIKI MAPACHA WA KUNDI LA PSQUARE, PETER (KUSHOTO) NA PAUL (KULIA) WAKIWA NA KAKA YAO AMBAE PIA NI MENEJA WAO, JUDES OKOYE. Mwanamuziki wa kundi la PSquare kutoka Nigeria, Peter Okoye ametangaza kujitoa kwenye kundi hilo la muziki wa Pop maarufu zaidi Afrika. Msanii huyo alidai kwamba amewasilisha maombi ya kuvunja kundi hilo katika barua aliyoandika kwa wakili wao Festus Keyamo. Kulingana na nakala ya barua iliyotolewa kwenye vyombo vya habari Jumatatu,Tarehe 25 Septemba, Peter alisema kuwa pacha wake na, Paul, na kaka yao, Judes waliahirisha ziara yao ya muziki ya Marekani bila kushauriana naye.Na hiyo ni moja kati ya sababu za msingi. Peter pia aliwalaumu Paul na kaka yao mkubwa mkubwa ambae ni meneja wao pia kwa udanganyifu walioufanya ili kutatua shida waliyokuwa nayo juu ya biashara ya muziki. Wasanii hao ndugu wamekua kwenye vita vya maneno kwenye mitandao ya kijamii tangu mwisho wa mwaka jana pamoja na juhudi za watu wao wa karibu kujaribu kuwapatanisha kifami...

ORODHA YA NCHI ZA KWANZA NA ZA MWISHO KWA AMANI DUNIANI.

Marekani:  Ripoti ya Taasisi ya Uchumi na Amani imepata mataifa kumi tu ulimwenguni ambayo hayapo katika vita na migogoro kabisa. Kwa mujibu wa Ripoti ya Kimataifa ya Amani 2016, Botswana, Chile, Costa Rica, Japan, Mauritius, Panama, Qatar, Uswisi, Uruguay na Vietnam ndio nchi pekee ambazo hazipo kwenye vita wala migogoro yeyote ile ya kuhatarisha amani.. Iceland inaongoza orodha ya nchi zinazoongoza kwa amani ulimwenguni, ikifuatiwa na Denmark, Austria, New Zealand, Ureno, Jamhuri ya Czech, Uswisi, Canada, Japan na Slovenia - wakati Marekani ikiwa kwenye nafasi ya 103. Palestina imepanda kutoka nafasi ya 163 mpaka nafasi ya 148. Syria iliyoharibiwa na vita imewekwa chini ya orodha, chini kuliko Sudan Kusini, Iraq, Afghanistan, Somalia, Yemen, Jamhuri ya Afrika ya Kati, Ukraine, Sudan na Libya. "Ripoti inalinganisha amani duniani kwa kutumia mandhari tatu pana: hali ya utulivu na usalama katika jamii; kiwango cha mgogoro wa ndani au wa kimataifa; na kiwango cha kije...