Skip to main content

MWANAMKE WA MIAKA 64 ALIYETAPELIWA $100,000 NA MPENZI ALIYEKUTANA NAE FACEBOOK.

PATRICIA MEISTER (64).

Mwanamke mwenye umri wa miaka 64 amesimulia juu ya jinsi alivyotapeliwa dola 100,000 baada ya kupendana na mtu ambaye ambaye hawakuwahi  kukutana.


Patricia Meister, kutoka Queensland, Australia alianza uhusiano wa mtandaoni na mtu ambaye alidhani alikuwa mfanyabiashara mwenye umri wa miaka katikati baada ya mtu huyo kumtumiaa ombi la rafiki kwenye Facebook mwaka 2015.


Akizungumza na Daily Mail Australia, mwanamke huyo alifafanua wakati alipopiga kichwa juu ya visigino kwa upendo, kabla ya kugundua mpenzi wake wa Italia aitwaye 'Carlos' alikuwa tapeli wa Nigeria.



Bi Meister alisema mwanamume huyo alionekana kujali na kufuatilia kila kitu cha maisha yake alipokua anapiga simu kila siku.

'Sijawahi kuwa kwenye tovuti za marafiki(dating websites), na nilokua natumia Facebook kwasababu za kibiashara. Kwa hiyo nilipopata ombi la urafiki, nilidhani haiwezi kuwa na madhara yoyote ", Alisema.

'Nadhani wakati ule, nilikua napitia katika kipindi cha maisha yangu ambapo nilihisi nikiwa mpweke. Nilikua sina mume muda mrefu na sijawahi kuwa kwenye mitandao ya urafiki '






'Tulianza kuzungumza. Alikuwa mcheshi, mwenye akili na alionekana kuwa na elimu. Alikuwa mzuri sana kwenye lugha ya Kiingereza na alikuwa yuko kimapenzi sana.

Nilimpenda sana katika hatua hiyo '


Alisema huyo mtu ambaye alidai kuwa alikuwa mjini Brisbane,Australia, alimwambia alikuwa akifanya kazi za ubunifu wa ndani(interior design) na asili yake ilikua ni ya Kiitaliano na Scotland.


Wawili hao walibadilishana ujumbe kila siku kabla ya kuanza mazungumzo katika simu.


'Nilipoisikia sauti yake mara ya kwanza ilikua tofauti na ile niliyoitarajia. Nakumbuka nilipokua najiuliza kuwa ile ni rafudhi gani "...sikuweza kuitambua ilikua ni rafudhi gani'

'Sikuweza kuitambua ile rafudhi kwa wakati huo, lakini nikifikiria kwa sasa, ilikua ni dhahiri kutoka Afrika ... Alikua Mnigeria.'


Licha ya kumtilia baadhi ya mashaka, Bibi Meister aliendelea kuzungumza naye na wiki zilipita.


Ndani ya wiki nane katika uhusiano wao, 'Carlos' alimwomba kama angeweza kumkopesha $ 600 kwa sababu kadi yake ya benki ilikataa kufanya kazi wakati akiwa Malaysia kibiashara.

'Sikuona ni sawa lakini nilifikiri na kuona kuwa sio kiasi kikubwa cha pesa kupoteza". Halikuwa ombi kubwa kwa hiyo nilimtumia, "

'Kiasi fulani nilifikiri ilikuwa ni kosa hivyo nikamwuliza, nikisema "wewe ni mfanyabiashara, kadi yako ya benki lazima ifanye kazi ...!" Hadithi yake bado sikuielewa!'



Lakini kuomba kwake fedha hakukuishia hapo, aliweza kutengeneza sababu kila wakati alipotaka kuomba fedha.


'Carlos' alikuwa akipanga safari ya kurudi nyumbani kwa Brisbane wakati bidhaa zake zikishikiliwa na forodha(customs) ya Malaysia. Na hivyo alikuwa na haja ya kulipia.


'Kiasi cha kwanza nilichomtuma kilikuwa $ 7,000. Alipokwenda kuchukua fedha, aliniambia alikuwa anahitaji $ 7,000 $ nyingine ", Alisema Bibi Meister.

'Kila kitu alichosema kilikua na "nyaraka" - na daima kulikuwa na mwanasheria nyuma wakati tunazungumza kwenye simu.

'Alipojaribu kunilipa, alisema benki yake haiwezi kufanya uhamisho mkubwa wa kimataifa kwa hiyo alipanga kutumia kampuni ya kusafirisha vifurushi ili kunitumia fedha badala yake.'


Bi Meister alisema alipewa kiungo(link) kwenye tovuti na 'karatasi ya kufuatilia', ambako aliweka jicho la karibu juu ya usafirishaji wa kifurushi hicho.

Lakini wakati kifurushi hicho kilopofika uwanja wa ndege wa Kuala Lumpur, kulikuwa na ada ya $ 25,000 ya kuruhusu fedha ziondoke nchini.


'Carlos alikuwa ameorodhesha anwani yangu ya biashara kwenye nyaraka, hivyo nilikuwa na wasiwasi kwa kuwa kuna mkoba uliojaa fedha wenye jina langu.

'Kwa wakati huo, nilidhani ninaweza kuonekana muarifu ikiwa nitaruhusu fedha zangu kwa jina langu kukaa pale, nikaona ni vizuri kulipia pesa hiyo ili nipate fedha yangu'.


Bibi Meister alifanya malipo hayo makubwa lakini kifurushi hicho kilipofika uwanja wa ndege wa Melbourne, kilikumbana na ada nyingine.


'Nilikua tayari nimelipa sana.Fedha ilianza kuwa ngumu kupatikana. Alikua amesha chukua kiasi cha mwisho cha pesa zangu,'
,alisema.



Siku iliyopangwa kuwa ndiyo atakayopokea kifurushi cha fedha zake, alipokea simu.

'Nilipokea simu kutoka kwa mtu akisema Carlos na mwanasheria wake wamepata ajali kubwa ya gari hivyo walihitaji fedha kwa gharama za matibabu,'

'Tumbo langu lilishuka mpaka kwenye viatu vyangu... Nilitambua wakati huo kuwa nimesha tapeliwa. '


Bibi Meister hakulipia pesa hizo za matibabu na wawili hao hawakuzungumza kwa karibu wiki.


'Kisha akajaribu kuomba fedha zaidi ili kulipia ada zake za matibabu lakini wakati huo, nilikuwa nimeshatumumia dola yangu ya mwisho,'
,alisema.

'Sikuweza kumlipia tena na hata nikamwambia sitaki kumtumia pesa tena. Muda mfupi baada ya hayo, alipata "ahueni ya ajabu" lakini niliacha kuzungumza naye wakati huo.




Bi Meister alijaribu kutoa ripoti hiyo kwa polisi lakini hawakuwa na kitu ambacho wangeweza kufanya baada ya $100,000 kwa jumla.

Na miezi miwili baadaye, alipokea ujumbe wa maandishi kutoka kwa Carlos, akisema: 'Hii yote ni kutokuelewana.'

Bila kuwaza mara mbili, Bibi Meister alimjibu 'wewe ni tapeli'

Baada ya kumuita tapeli, alimaliza mazungumzo yetu kwakusema: "Nipate kama unaweza, mpendwa wangu",



Bibi Meister alisema hatimaye alipata kikundi cha msaada kinachoitwa Romance Scams ambapo wanawake wanasimulina hadithi zinazofanana na yake.



CHANZO:
dailymail.co.uk

Comments

Habari Nyingine Kutoka Kioo17 Swahili;

ORODHA YA NCHI ZA KWANZA NA ZA MWISHO KWA AMANI DUNIANI.

Marekani:  Ripoti ya Taasisi ya Uchumi na Amani imepata mataifa kumi tu ulimwenguni ambayo hayapo katika vita na migogoro kabisa. Kwa mujibu wa Ripoti ya Kimataifa ya Amani 2016, Botswana, Chile, Costa Rica, Japan, Mauritius, Panama, Qatar, Uswisi, Uruguay na Vietnam ndio nchi pekee ambazo hazipo kwenye vita wala migogoro yeyote ile ya kuhatarisha amani.. Iceland inaongoza orodha ya nchi zinazoongoza kwa amani ulimwenguni, ikifuatiwa na Denmark, Austria, New Zealand, Ureno, Jamhuri ya Czech, Uswisi, Canada, Japan na Slovenia - wakati Marekani ikiwa kwenye nafasi ya 103. Palestina imepanda kutoka nafasi ya 163 mpaka nafasi ya 148. Syria iliyoharibiwa na vita imewekwa chini ya orodha, chini kuliko Sudan Kusini, Iraq, Afghanistan, Somalia, Yemen, Jamhuri ya Afrika ya Kati, Ukraine, Sudan na Libya. "Ripoti inalinganisha amani duniani kwa kutumia mandhari tatu pana: hali ya utulivu na usalama katika jamii; kiwango cha mgogoro wa ndani au wa kimataifa; na kiwango cha kije...

JAGUAR KUACHIA WIMBO BAADA YA KUAPISHWA MBUNGE.

Mbunge wa Starehe, Kenya, "Jaguar" anajipanga kutoa wimbo mpya mara tu baada ya kuapishwa kua mbunge. Katika chapisho lake la kwenye akaunti yake ya mtandao wa kijamii, Jaguar aliupendekeza wimbo wake wa "Ndoto" kama salamu kwa Wakenya na watu walio nje ya Kenya. Charles Njagua, ambae ni maarufu kwa jina la Jaguar, ana Aliahidi mashabiki wimbo mpya baada ya kuapa rasmi kama mbunge.  Mimbaji huyo ambaye ametoa hits kadhaa lakini sasa anazingatia siasa baada ya kushinda kiti, aliwaambia mashabiki kwenye vyombo vya habari vya kijamii kwamba wimbo mpya, unaitwa "Ndoto", uko tayari na utaachiliwa haraka baada ya kuapa. "Sasa ni karibu miongo miwili tangu mimi kuweka mguu katika studio ya kurekodi,   alisema Jaguar katika chapisho lake. CHANZO: www.tuko.news

KASHFA YA MAPENZI KATI MH.MBOWE NA WEMA SEPETU.

MH.FREEMAN MBOWE AKIWA NA WEMA SEPETU. Siku chache baada ya ile skendo ya ngono iliyosababisha wakili na mshauri wa Chama cha ACT -Wazalendo , Bwana Albert Msando kujiuzulu kwenye nyadhifa yake ya chama ,yameibuka mangine kwenye chama kikuu cha upinzani Tanzania ,CHADEMA ,baada ya kusambaa kwa kipande cha sauti kinachodaiwa kua ni mazungumzo kati ya mwenyekiti wa chama hicho na mbunge wa Hai Mh.Freeman Mbowe na Miss Tanzania 2006 ,mrembo Wema Isack Sepetu. SIKILIZA HIVI VIPANDE VYA SAUTI: Bonyeza hapa chini kusikiliza maongezi hayo yanayodaiwa kuwa ni kati ya Wema Sepetu na Mh.Freeman Mbowe; Bonyeza hapa chini kusikiliza majibu ya Wema Sepetu; Bonyeza hapa chini kusikiliza majibu ya Mh.Freeman Mbowe; VYANZO: Jamii Forums,                   YouTube.com,                   Perfect255.com.                   

"GIGGS HAFAI KUWA KOCHA WA TIMU YA TAIFA", BABA YAKE ANASEMA...!!!

Ryan Giggs. Chama cha Soka cha Wales (FAW) siku ya jumatatu kilitangaza kumchagua winga wa zamani wa Manchester United Ryan Giggs kama kocha wa timu yao ya taifa kwa mkataba wa miaka minne. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 44 anachukua kazi iyoachwa na Chris Coleman, ambaye aliiongoza Wales kwenye nusu fainali za Euro 2016 lakini aliacha kazi mwezi Novemba ili kuchukua nafasi ya kuifundisha timu ya Sunderland ya ligi kuu ya Uingereza. Giggs alisema kuwa anajivunia kwa kupewa kazi hiyo na pamoja na changamoto iliyo mbele yake baada ya Wales kushindwa kufuzu kucheza fainali za Kombe la Dunia mwaka huu nchini Urusi na sasa wanazingatia michuano ya Ulaya ya 2020. "Siwezi kusubiri kuanza kufanya kazi na wachezaji tunapojiandaa kwa ajili ya michezo muhimu baadaye mwaka huu," alisema. Lakini baba mzazi wa Giggs, Danny Wilson ana maoni  tofauti sana...!!! Anakiri kwamba mwanae anamtia aibu na anasema hastahili kuchukua kazi hiyo ya ukocha wa timu ya t...

MCHEZAJI WA ZAMANI WA UINGEREZA AMESEMA ALICHEZA NA WACHEZAJI WATATU MASHOGA KWENYE TIMU.

Carl Hoefkens (jezi no.2) alichezea West Bromwich Albion na Stoke City wakati wa enzi zake ligi kuu ya England. Beki wa zamani wa Ligi Kuu ya Uingereza amesema alicheza pamoja na wachezaji wenzake wawili wa mashoga ndani ya timu, na mmoja alikua na jina kubwa. Carl Hoefkens, West Bromwich Albion na Stoke City siku za nyuma, anasema wachezaji hao walikua wazi na hawakujificha kwenye vyumba vya kubadilishia nguo ingawa bado hawajulikani kwasababu ya maombi yao wenyewe ya kuomba kutotangazwa. Justin Fashanu, ambaye alijiua mwaka 1998, alikuwa mchezaji wa mwisho wa kazi nchini England kuja nje kama mashoga - mwaka 1990. Hoefkens alipokua (kushoto), alipokua anachezea Stock  City. Hoefkens aliyecheza Uingereza kwa miaka minne, akiondoka mwaka 2009, alidai kuwa mchezaji mwenzake mmoja wa timu alikua anaweza kuja kwenye uwanja wa mafunzo ya klabu na mpenzi wake wa kiume  lakini aliwaomba wenzake kutokuwaambia watu wangine wa nje ya timu. 'Nilicheza pamoja n...

TUPAC SHAKUR ALIBAKWA JELA !!!

             Ulimwengu wa filamu za Hollywood na muziki wa Hip Hop juzi ulipatwa na mshangao baada ya mtayarishaji wa filamu inayohusu maisha ya hayati Tupac Shakur ,L.T Hutton kuelezea sababu zilizomfanya kumbadilisha muongozaji wa filamu hiyo kutoka John Singleton na kumuweka muongozaji Benny "Boom" Douglas.  Filamu hiyo inayoitwa "all eyez on me" tayari imekwisha andaliwa na inatarajiwa kuzinduliwa leo tarehe 16 Juni 2017.       Akizungumza kwenye mahojiano redioni L.T Hutton amewashtusha watu wengi baada ya kudai kwamba walishindwana na muongozaji wa mwanzo bwana John Singleton sababu muongozaji huyo aling'ang'ania kuwepo kwa matukio (scene) ambazo kwa maoni yake zisingependeza.        Matukio ambayo John Singleton alipenda yawepo katika filamu hiyo ni pamoja na kutaka filamu hiyo ianze na scene ya Tupac akilazimisha kumlawiti msichana wa kizungu.!!!          Singleton pia ali...

MOHAMMED DEWJI NA BILL GATES KUTOA NUSU YA UTAJIRI WAO...!!!

MOHAMMED DEWJI AKIWA NA BILL GATES. Mfanyabiashara tajiri namba moja Tanzania (kwa mujibu wa jarida la Forbes) na mmiliki wa makampuni ya METL , Mohammed "Mo" Dewji ,wiki chache zilizopita amekua mmoja wa mabilionea 14 wapya kujiunga katika mpango wa kuchangia misaada kwa jamii uitwao "Giving Pledge".                 Mpango huo ulioanzishwa na familia ya mfanyabiashara tajiri namba moja duniani (kwa mujibu wa jarida la Forbes) na mmiliki wa kampuni ya Microsoft Bill Gates pamoja na rafiki yake bilionea Warren Buffet mwaka 2010, ulikua na tayari umeshaungwa mkono na mabilionea 154 mpaka mwanzo wa mwaka huu (2017). WAASISI WA "GIVIN PLEDGE",WARREN BUFFET, MELINDA GATES NA BILL GATES.         Mohammed Dewji anakua mmoja kati ya matajiri wachache sana kutoka Afrika kama Patrice Motsepe (Afrika Kusini) na Mo Ibrahim (Sudan) kujiunga na kampeni hiyo ambayo nia yake kubwa ni kushawishi watu matajiri kutoa angalau nu...