Skip to main content

MADAI YA MKUU WA WILAYA YA HAI KUWAWEKA WALIMU RUMANDE KIHOLELA.



Kwa siku za hivi karibuni wakuu wa mikoa na wilaya wamekuwa wakikemewa na wasomi, wanasheria na watetezi wa haki za binadamu kwa namna wanavyokiuka sheria kwa kuagiza watu wakamatwe na kuwekwa rumande kwa kutumia mamlaka waliyonayo.

Kwa mujibu wa sheria, viongozi hao wanauwezo wakumuweka rumande hadi saa 48 mtu au kikundi cha watu wanaotishia usalama wa eneo husika, kama hakuna njia nyingine wanayoweza kutumia kuhakikisha usalama wa raia na mali zao unakuwepo.

Katika hali ya kushangaza Mkuu wa Wilaya ya Hai, Gelasius Byakanwa amemuweka mahabusu mwalimu mmoja baada ya kushindwa kujibu swali alilomuuliza.

Tukio hilo lilitokea Agosti 11 mwaka huu wakati kiongozi huyo wa wilaya akiwa katika ziara ya kutembelea shule za sekondari alipofika Shule Sekondari Lerai akiwa ameambatana na Afisa Elimu Msaidizi ambapo walifanya kikao na walimu wa shule hiyo.

Wakiwa katika kikao hicho, Byakanwa aliwauliza walimu hao kama kuna yeyote anayefahamu kwa usahihi jina lake, hakuna aliyejibu na alipowapa karatasi waandike jina lake, wote walikosea.

Baada ya muda aliwataka waalimu waandike nafasi ya shule mwaka 2015 katika mtihani wa taifa ambapo mwalimu mmoja alishindwa kuandika na alipomfuata akimwamuru aandike, mwalimu alimjibu hawezi kuandika uongo kwani hakumbuki.

Punde kidogo, DC alimfuata Mwalimu Erasto Mhanga aliyesweka mahabusu na kumtaka aeleze Halmashauri ya Wilaya ya Hai ina shule ngapi, na alijibiwa na mwalimu huyo kuwa hawezi kutaja kwa sababu hana takwimu sahihi.

Majibu hayo yalimfanya DC awapigie simu polisi wafike shuleni hapo.

Kabla gari la Polisi halijafika eneo la tukio alimwita mwalimu huyo pembeni na kumwambia achague kati ya kwenda rumande au kupiga push-up 20, lakini mwalimu alimjibu hawezi kupiga push-up kwani anamatatizo ya kiafya. Polisi walipofika shuleni hapo aliwaamuru wampeleke mwalimu huyo katika Kituo cha Polisi Bomang’ombe.

Mwalimu Mhagama aliwekwa rumande kuanzia saa 8:30 mchana hadi saa 2:00 usiku alipoachiwa huru.

Kwa upande wa Chama cha Walimu (CWT) Mkoa wa Kilimanjaro kimesema kuwa kitendo hicho cha Mkuu wa Wilaya ya Hai hakikubaliki na ni kinyume na maadili ya utumishi wa umma.

CWT imemtaka kiongozi huyo kuomba msamaha ndani ya siku 30 kuanzia Agosti 21 vinginevyo atafikishwa katika vyombo vya sheria kwa hatua zaidi.

Walimu wa shule ambazo DC alipita, walilalamika kwa viongozi wa CWT kuwa waliulizwa maswali ambayo si ya kitaaluma.

Wakitaja baadhi ya maswali waliyoulizwa ni pamoja na majina ya DC, nafasi ya shule mwaka 2015, idadi ya shule Hai, magazeti ya serikali ambayo mtu kutokuyafahamu sio kosa la kupelekea kuwekwa mahabusu.

CWT imesema katu hawatalifumbia macho suala hilo na mengine kama hayo kwani ushahidi tayari wa nao na watafikisha malalamiko yao kwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Mama Anna Mghwira.


=====
Hili suala limekaaje kisheria wakuu.

Je kutomjua kwa jina kiongozi wako ni kosa kisheria?


CHANZO:

https://m.facebook.com/story.php?story_fbid=1585952301468758&id=255954351135233

Comments

Habari Nyingine Kutoka Kioo17 Swahili;

ORODHA YA NCHI ZA KWANZA NA ZA MWISHO KWA AMANI DUNIANI.

Marekani:  Ripoti ya Taasisi ya Uchumi na Amani imepata mataifa kumi tu ulimwenguni ambayo hayapo katika vita na migogoro kabisa. Kwa mujibu wa Ripoti ya Kimataifa ya Amani 2016, Botswana, Chile, Costa Rica, Japan, Mauritius, Panama, Qatar, Uswisi, Uruguay na Vietnam ndio nchi pekee ambazo hazipo kwenye vita wala migogoro yeyote ile ya kuhatarisha amani.. Iceland inaongoza orodha ya nchi zinazoongoza kwa amani ulimwenguni, ikifuatiwa na Denmark, Austria, New Zealand, Ureno, Jamhuri ya Czech, Uswisi, Canada, Japan na Slovenia - wakati Marekani ikiwa kwenye nafasi ya 103. Palestina imepanda kutoka nafasi ya 163 mpaka nafasi ya 148. Syria iliyoharibiwa na vita imewekwa chini ya orodha, chini kuliko Sudan Kusini, Iraq, Afghanistan, Somalia, Yemen, Jamhuri ya Afrika ya Kati, Ukraine, Sudan na Libya. "Ripoti inalinganisha amani duniani kwa kutumia mandhari tatu pana: hali ya utulivu na usalama katika jamii; kiwango cha mgogoro wa ndani au wa kimataifa; na kiwango cha kije...

JAGUAR KUACHIA WIMBO BAADA YA KUAPISHWA MBUNGE.

Mbunge wa Starehe, Kenya, "Jaguar" anajipanga kutoa wimbo mpya mara tu baada ya kuapishwa kua mbunge. Katika chapisho lake la kwenye akaunti yake ya mtandao wa kijamii, Jaguar aliupendekeza wimbo wake wa "Ndoto" kama salamu kwa Wakenya na watu walio nje ya Kenya. Charles Njagua, ambae ni maarufu kwa jina la Jaguar, ana Aliahidi mashabiki wimbo mpya baada ya kuapa rasmi kama mbunge.  Mimbaji huyo ambaye ametoa hits kadhaa lakini sasa anazingatia siasa baada ya kushinda kiti, aliwaambia mashabiki kwenye vyombo vya habari vya kijamii kwamba wimbo mpya, unaitwa "Ndoto", uko tayari na utaachiliwa haraka baada ya kuapa. "Sasa ni karibu miongo miwili tangu mimi kuweka mguu katika studio ya kurekodi,   alisema Jaguar katika chapisho lake. CHANZO: www.tuko.news

KASHFA YA MAPENZI KATI MH.MBOWE NA WEMA SEPETU.

MH.FREEMAN MBOWE AKIWA NA WEMA SEPETU. Siku chache baada ya ile skendo ya ngono iliyosababisha wakili na mshauri wa Chama cha ACT -Wazalendo , Bwana Albert Msando kujiuzulu kwenye nyadhifa yake ya chama ,yameibuka mangine kwenye chama kikuu cha upinzani Tanzania ,CHADEMA ,baada ya kusambaa kwa kipande cha sauti kinachodaiwa kua ni mazungumzo kati ya mwenyekiti wa chama hicho na mbunge wa Hai Mh.Freeman Mbowe na Miss Tanzania 2006 ,mrembo Wema Isack Sepetu. SIKILIZA HIVI VIPANDE VYA SAUTI: Bonyeza hapa chini kusikiliza maongezi hayo yanayodaiwa kuwa ni kati ya Wema Sepetu na Mh.Freeman Mbowe; Bonyeza hapa chini kusikiliza majibu ya Wema Sepetu; Bonyeza hapa chini kusikiliza majibu ya Mh.Freeman Mbowe; VYANZO: Jamii Forums,                   YouTube.com,                   Perfect255.com.                   

"GIGGS HAFAI KUWA KOCHA WA TIMU YA TAIFA", BABA YAKE ANASEMA...!!!

Ryan Giggs. Chama cha Soka cha Wales (FAW) siku ya jumatatu kilitangaza kumchagua winga wa zamani wa Manchester United Ryan Giggs kama kocha wa timu yao ya taifa kwa mkataba wa miaka minne. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 44 anachukua kazi iyoachwa na Chris Coleman, ambaye aliiongoza Wales kwenye nusu fainali za Euro 2016 lakini aliacha kazi mwezi Novemba ili kuchukua nafasi ya kuifundisha timu ya Sunderland ya ligi kuu ya Uingereza. Giggs alisema kuwa anajivunia kwa kupewa kazi hiyo na pamoja na changamoto iliyo mbele yake baada ya Wales kushindwa kufuzu kucheza fainali za Kombe la Dunia mwaka huu nchini Urusi na sasa wanazingatia michuano ya Ulaya ya 2020. "Siwezi kusubiri kuanza kufanya kazi na wachezaji tunapojiandaa kwa ajili ya michezo muhimu baadaye mwaka huu," alisema. Lakini baba mzazi wa Giggs, Danny Wilson ana maoni  tofauti sana...!!! Anakiri kwamba mwanae anamtia aibu na anasema hastahili kuchukua kazi hiyo ya ukocha wa timu ya t...

MCHEZAJI WA ZAMANI WA UINGEREZA AMESEMA ALICHEZA NA WACHEZAJI WATATU MASHOGA KWENYE TIMU.

Carl Hoefkens (jezi no.2) alichezea West Bromwich Albion na Stoke City wakati wa enzi zake ligi kuu ya England. Beki wa zamani wa Ligi Kuu ya Uingereza amesema alicheza pamoja na wachezaji wenzake wawili wa mashoga ndani ya timu, na mmoja alikua na jina kubwa. Carl Hoefkens, West Bromwich Albion na Stoke City siku za nyuma, anasema wachezaji hao walikua wazi na hawakujificha kwenye vyumba vya kubadilishia nguo ingawa bado hawajulikani kwasababu ya maombi yao wenyewe ya kuomba kutotangazwa. Justin Fashanu, ambaye alijiua mwaka 1998, alikuwa mchezaji wa mwisho wa kazi nchini England kuja nje kama mashoga - mwaka 1990. Hoefkens alipokua (kushoto), alipokua anachezea Stock  City. Hoefkens aliyecheza Uingereza kwa miaka minne, akiondoka mwaka 2009, alidai kuwa mchezaji mwenzake mmoja wa timu alikua anaweza kuja kwenye uwanja wa mafunzo ya klabu na mpenzi wake wa kiume  lakini aliwaomba wenzake kutokuwaambia watu wangine wa nje ya timu. 'Nilicheza pamoja n...

TUPAC SHAKUR ALIBAKWA JELA !!!

             Ulimwengu wa filamu za Hollywood na muziki wa Hip Hop juzi ulipatwa na mshangao baada ya mtayarishaji wa filamu inayohusu maisha ya hayati Tupac Shakur ,L.T Hutton kuelezea sababu zilizomfanya kumbadilisha muongozaji wa filamu hiyo kutoka John Singleton na kumuweka muongozaji Benny "Boom" Douglas.  Filamu hiyo inayoitwa "all eyez on me" tayari imekwisha andaliwa na inatarajiwa kuzinduliwa leo tarehe 16 Juni 2017.       Akizungumza kwenye mahojiano redioni L.T Hutton amewashtusha watu wengi baada ya kudai kwamba walishindwana na muongozaji wa mwanzo bwana John Singleton sababu muongozaji huyo aling'ang'ania kuwepo kwa matukio (scene) ambazo kwa maoni yake zisingependeza.        Matukio ambayo John Singleton alipenda yawepo katika filamu hiyo ni pamoja na kutaka filamu hiyo ianze na scene ya Tupac akilazimisha kumlawiti msichana wa kizungu.!!!          Singleton pia ali...

MOHAMMED DEWJI NA BILL GATES KUTOA NUSU YA UTAJIRI WAO...!!!

MOHAMMED DEWJI AKIWA NA BILL GATES. Mfanyabiashara tajiri namba moja Tanzania (kwa mujibu wa jarida la Forbes) na mmiliki wa makampuni ya METL , Mohammed "Mo" Dewji ,wiki chache zilizopita amekua mmoja wa mabilionea 14 wapya kujiunga katika mpango wa kuchangia misaada kwa jamii uitwao "Giving Pledge".                 Mpango huo ulioanzishwa na familia ya mfanyabiashara tajiri namba moja duniani (kwa mujibu wa jarida la Forbes) na mmiliki wa kampuni ya Microsoft Bill Gates pamoja na rafiki yake bilionea Warren Buffet mwaka 2010, ulikua na tayari umeshaungwa mkono na mabilionea 154 mpaka mwanzo wa mwaka huu (2017). WAASISI WA "GIVIN PLEDGE",WARREN BUFFET, MELINDA GATES NA BILL GATES.         Mohammed Dewji anakua mmoja kati ya matajiri wachache sana kutoka Afrika kama Patrice Motsepe (Afrika Kusini) na Mo Ibrahim (Sudan) kujiunga na kampeni hiyo ambayo nia yake kubwa ni kushawishi watu matajiri kutoa angalau nu...