Skip to main content

MADAI YA MKUU WA WILAYA YA HAI KUWAWEKA WALIMU RUMANDE KIHOLELA.



Kwa siku za hivi karibuni wakuu wa mikoa na wilaya wamekuwa wakikemewa na wasomi, wanasheria na watetezi wa haki za binadamu kwa namna wanavyokiuka sheria kwa kuagiza watu wakamatwe na kuwekwa rumande kwa kutumia mamlaka waliyonayo.

Kwa mujibu wa sheria, viongozi hao wanauwezo wakumuweka rumande hadi saa 48 mtu au kikundi cha watu wanaotishia usalama wa eneo husika, kama hakuna njia nyingine wanayoweza kutumia kuhakikisha usalama wa raia na mali zao unakuwepo.

Katika hali ya kushangaza Mkuu wa Wilaya ya Hai, Gelasius Byakanwa amemuweka mahabusu mwalimu mmoja baada ya kushindwa kujibu swali alilomuuliza.

Tukio hilo lilitokea Agosti 11 mwaka huu wakati kiongozi huyo wa wilaya akiwa katika ziara ya kutembelea shule za sekondari alipofika Shule Sekondari Lerai akiwa ameambatana na Afisa Elimu Msaidizi ambapo walifanya kikao na walimu wa shule hiyo.

Wakiwa katika kikao hicho, Byakanwa aliwauliza walimu hao kama kuna yeyote anayefahamu kwa usahihi jina lake, hakuna aliyejibu na alipowapa karatasi waandike jina lake, wote walikosea.

Baada ya muda aliwataka waalimu waandike nafasi ya shule mwaka 2015 katika mtihani wa taifa ambapo mwalimu mmoja alishindwa kuandika na alipomfuata akimwamuru aandike, mwalimu alimjibu hawezi kuandika uongo kwani hakumbuki.

Punde kidogo, DC alimfuata Mwalimu Erasto Mhanga aliyesweka mahabusu na kumtaka aeleze Halmashauri ya Wilaya ya Hai ina shule ngapi, na alijibiwa na mwalimu huyo kuwa hawezi kutaja kwa sababu hana takwimu sahihi.

Majibu hayo yalimfanya DC awapigie simu polisi wafike shuleni hapo.

Kabla gari la Polisi halijafika eneo la tukio alimwita mwalimu huyo pembeni na kumwambia achague kati ya kwenda rumande au kupiga push-up 20, lakini mwalimu alimjibu hawezi kupiga push-up kwani anamatatizo ya kiafya. Polisi walipofika shuleni hapo aliwaamuru wampeleke mwalimu huyo katika Kituo cha Polisi Bomang’ombe.

Mwalimu Mhagama aliwekwa rumande kuanzia saa 8:30 mchana hadi saa 2:00 usiku alipoachiwa huru.

Kwa upande wa Chama cha Walimu (CWT) Mkoa wa Kilimanjaro kimesema kuwa kitendo hicho cha Mkuu wa Wilaya ya Hai hakikubaliki na ni kinyume na maadili ya utumishi wa umma.

CWT imemtaka kiongozi huyo kuomba msamaha ndani ya siku 30 kuanzia Agosti 21 vinginevyo atafikishwa katika vyombo vya sheria kwa hatua zaidi.

Walimu wa shule ambazo DC alipita, walilalamika kwa viongozi wa CWT kuwa waliulizwa maswali ambayo si ya kitaaluma.

Wakitaja baadhi ya maswali waliyoulizwa ni pamoja na majina ya DC, nafasi ya shule mwaka 2015, idadi ya shule Hai, magazeti ya serikali ambayo mtu kutokuyafahamu sio kosa la kupelekea kuwekwa mahabusu.

CWT imesema katu hawatalifumbia macho suala hilo na mengine kama hayo kwani ushahidi tayari wa nao na watafikisha malalamiko yao kwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Mama Anna Mghwira.


=====
Hili suala limekaaje kisheria wakuu.

Je kutomjua kwa jina kiongozi wako ni kosa kisheria?


CHANZO:

https://m.facebook.com/story.php?story_fbid=1585952301468758&id=255954351135233

Comments

Habari Nyingine Kutoka Kioo17 Swahili;

MCHEZAJI WA ZAMANI WA UINGEREZA AMESEMA ALICHEZA NA WACHEZAJI WATATU MASHOGA KWENYE TIMU.

Carl Hoefkens (jezi no.2) alichezea West Bromwich Albion na Stoke City wakati wa enzi zake ligi kuu ya England. Beki wa zamani wa Ligi Kuu ya Uingereza amesema alicheza pamoja na wachezaji wenzake wawili wa mashoga ndani ya timu, na mmoja alikua na jina kubwa. Carl Hoefkens, West Bromwich Albion na Stoke City siku za nyuma, anasema wachezaji hao walikua wazi na hawakujificha kwenye vyumba vya kubadilishia nguo ingawa bado hawajulikani kwasababu ya maombi yao wenyewe ya kuomba kutotangazwa. Justin Fashanu, ambaye alijiua mwaka 1998, alikuwa mchezaji wa mwisho wa kazi nchini England kuja nje kama mashoga - mwaka 1990. Hoefkens alipokua (kushoto), alipokua anachezea Stock  City. Hoefkens aliyecheza Uingereza kwa miaka minne, akiondoka mwaka 2009, alidai kuwa mchezaji mwenzake mmoja wa timu alikua anaweza kuja kwenye uwanja wa mafunzo ya klabu na mpenzi wake wa kiume  lakini aliwaomba wenzake kutokuwaambia watu wangine wa nje ya timu. 'Nilicheza pamoja n...

STAR TV YAFUNGIWA NA TRA KWA KUKWEPA KODI.

Mamlaka ya mapato Tanzania inadaiwa kuifungia Radio Free Africa ya Mwanza inayomilikiwa na Antony Dialo kutokana na kudaiwa kodi kubwa. TRA wamewaondoa studio wafanyakazi wote na kuifunga radio hiyo. Kwa sasa ukiwasha radio utasikia matangazo ya kiingereza ya BBC. Diallo ni mwenyekiti wa CCM Mwanza na anadaiwa mamilioni ya kodi na TRA miaka mingi. Star Tv pia imekumbwa na sekeseke hilo. Ikumbukwe hii ndio TV pekee binafsi iliyokuwa ikipingana na MOAT na TEF katika sakata la RC Paul Makonda na walirusha kipindi maalum cha Makonda huku Jumuiya ya Wanahabari wakitangaza rasmi kujitenga na maswahibu yoyote yatakayokuja kuikuta RFA na Star TV. VYANZO : https://www.jamiiforums.com/threads/tra-waifungia-rfa-kwa-kudaiwa-kodi-ya-sh-bilioni-4-5.1283386/

JINSI YA KUOMBA PASSPORT YA TANZANIA KWA NJIA YA INTERNET.

Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kupitia i dara ya Uhamiaji  imezindua huduma ya ujazaji fomu za maombi ya hati ya kusafiria (Passport) kwa njia ya mtandao, ambapo mwombaji atalazimika kujaza fomu hizo na kuzichapisha kabla ya kuziwasilisha kwenye ofisi za uhamiaji. Idara hiyo pia imeeleza kuwa matumizi ya huduma hiyo yataenda sambamba na huduma inayotumiwa sasa ya fomu za maombi ya pasipoti mpaka pale itakapotangazwa vinginevyo. Huduma hiyo itaanza kufanya kazi kuanzia Jumatatu tarehe  7/8/2017    na unaweza  kujaza fomu hizo  kwa kufungua tovuti hiyo ambayo ni  https://www.immigration.go.tz/ppt_application/ Utaratibu wa namna ya kujaza fomu hizo umeelekezwa katika fomu husika mtandaoni, na pia wateja wanaweza kupata ufafanuzi au maelezo zaidi kuhusu huduma hiyo kupitia anuani ya Idara ya Uhamiaji ambayo ni   info@immigration.go.tz   au katika Ofisi yoyote ya Uhamiaji iliyo karibu yako. CHANZO: http://dibute.com/muhimu-...

MOURINHO KUMUONDOA MKHITARYAN ILI AWEZE KUMSAJILI OZIL.

Henrikh Mkhitaryan atatupwa kando na meneja wa Manchester United Jose Mourinho ili apate nafasi ya kumsajili jiungo wa Arsenal, Mesut Ozil, kulingana na taarifa.  Bosi huyo wa Manchester United anajua lazima apunguze kikosi chake kama atataka kumsajili Ozil kutokana na madai ya mshahara mkubwa ya bingwa huyo wa Kombe la Dunia. Kiungo huyo mchezeshaji huyo ambaye mkataba wake Arsenal umalizika mwishoni mwa msimu huu, amekuwa akiomba mshahala wa Pauni Laki Tatu (£ 300,000) kwa wiki ili kukubali mkataba mpya wa kuendelea kuchezea Arsenal. Gazeti la 'The Mirror' la Uingereza limeripoti kwamba Mourinho ameamua Mkhitaryan, ambaye alijiunga na klabu kutoka Borussia Dortmund mwaka 2016, anaweza kuwa mchezaji kuondoka Ni uchaguzi wa mantiki kulingana na hali ya sasa ya mchezaji huyo katika kikosi cha Manchester United. Mchezaji huyo kutoka Armenia ameachwa mechi nane za mwisho na Mourinho huku akisema kuwa haamini kama kiungo huyo anastahilo kukukaa katika...

TUPAC SHAKUR ALIBAKWA JELA !!!

             Ulimwengu wa filamu za Hollywood na muziki wa Hip Hop juzi ulipatwa na mshangao baada ya mtayarishaji wa filamu inayohusu maisha ya hayati Tupac Shakur ,L.T Hutton kuelezea sababu zilizomfanya kumbadilisha muongozaji wa filamu hiyo kutoka John Singleton na kumuweka muongozaji Benny "Boom" Douglas.  Filamu hiyo inayoitwa "all eyez on me" tayari imekwisha andaliwa na inatarajiwa kuzinduliwa leo tarehe 16 Juni 2017.       Akizungumza kwenye mahojiano redioni L.T Hutton amewashtusha watu wengi baada ya kudai kwamba walishindwana na muongozaji wa mwanzo bwana John Singleton sababu muongozaji huyo aling'ang'ania kuwepo kwa matukio (scene) ambazo kwa maoni yake zisingependeza.        Matukio ambayo John Singleton alipenda yawepo katika filamu hiyo ni pamoja na kutaka filamu hiyo ianze na scene ya Tupac akilazimisha kumlawiti msichana wa kizungu.!!!          Singleton pia ali...

ORODHA YA NCHI 80 AMBAZO MTANZANIA ANARUHUSIWA KUINGIA BILA VIZA.

         Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni amesema kuna zaidi ya nchi 80 ambazo watanzania wanaweza kusafiri bila ya kuwa na viza . Mhandisi Hamad Masauni amesema kuna zaidi ya nchi 80 ambazo watanzania wanaweza kusafiri bila ya kuwa na viza za kusafiria kama ilivyokuwa nchi za afrika Mashariki. Mhandisi Massauni amebainisha hayo leo bungeni wakati akijibu swali la Mbunge wa Mlalo kupitia tiketi ya CCM Rashid Shangazi aliyetaka kujua ni nchi ngapi ambazo watanzania wanaweza kusafiri bila ya kuwa na viza (viza on arrival). "Zipo nchi 16 kwa Afrika ambazo watanzania wanaweza kuzitembelea bila ya kuwa na viza na duniani zipo 67" alisema Masauni. Aidha Massauni amezitaja nchi hizo kuwa ni Benin, Burkina Faso, Cape Verde, Ivory Coast, Djibouti, Gabon, Gambia, Guinea, Guinea­Bissau, Liberia, Mali, Mauritania, Niger, Sierra Leone pamoja na Togo. Pamoja na hayo Masauni amesema...

"BUREAU DE CHANGE" ZOTE TANZANIA KUFUTIWA LESENI.

BENKI Kuu ya Tanzania (BoT) imetoa waraka kwa wafanyabiashara wa maduka ya kuuza na kununua fedha za kigeni kuomba upya leseni kwa ajili ya kufanya biashara hiyo. Leseni zote za maduka ya kubadilisha fedha za kigeni zitafutwa ifikapo Septemba 2, mwaka huu ili wamiliki waombe upya. Hayo yalisemwa jana na Ofisa Msimamizi Maduka ya Kuuza na Kununua Fedha za Kigeni wa Benki Kuu ya Tanzania, Kanuti Mosha kwenye Maonesho ya 41 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (DITF) yanayoendelea kwenye Viwanja vya Mwalimu Nyerere, Barabara ya Kilwa, Temeke jijini Dar es Salaam. Mosha alisema kwa sheria ya sasa, mfanyabiashara atatakiwa kumiliki duka moja tu tofauti na ilivyokuwa awali mtu mmoja anaweza kumiliki maduka hata matano. Alisema sambamba na kutoa leseni upya, BoT imeweka viwango vipya vya mtaji ambavyo vinaanzia Sh milioni 100 hadi 300 kwa daraja A, na kuanzia Sh milioni 250 hadi Sh bilioni moja kwa daraja B na Amana ya Thamani kuanzia Dola za Marekani milioni 50 hadi milioni 100. A...