Skip to main content

MRISHO GAMBO AGOMEA AGIZO LA MAKAMU WA RAISI !.




MKUU wa Mkoa wa Arusha,Tanzania, Mrisho Gambo amekiuka maagizo yaliyotolewa na Makamu wa Rais Samia Suluhu ya kutoa Sh milioni 20 kwa ajili ya kutunisha mfuko maalumu wa elimu ulioAnzishwa na Taasisi ya Stemm.

Kwa mujibu wa hotuba ya Makamu wa Rais iliyosomwa na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Anna Mughwira wakati wa mapokezi ya watoto walionusurika kwenye ajali ya basi ya Shule ya Lucky Vincent, Doreen Mshana, Sadia Ismail na Wilson Tarimo waliorejea kutoka Marekani, serikali ilimwagiza Gambo kutoa kiasi hicho cha fedha ili kuunga mkono juhudi za taasisi hiyo iliyoahidi kusomesha watoto hao.

Hata hivyo, badala ya kuzielekeza katika taasisi hiyo, Gambo amezigawa fedha hizo kwa wazazi wa watoto hao walionusurika katika ajali hiyo bila masharti yoyote huku akiikana hotuba ya Mughwira kuwa hana fedha za ziada.
“Uongozi wa mkoa uliamua kuzigawa fedha hizo kiasi cha Sh milioni 23.2 ambapo familia za watoto watatu walionusurika ambao ni kila moja ilipata mgawo wa Sh milioni 7.7.
“Mkoa wa Arusha hauna hizo Sh milioni 20 mnachosema bali fedha zote zilizobaki ndiyo hizi ambazo tumewakabidhi wazazi wa watoto wetu hawa ambao Mwenyezi Mungu aliwanusuru kutokana na ajali iliyotokea bila masharti yoyote,” amesema Gambo.

Pamoja na mambo mengine, Gambo amesema fedha za michango ya rambirambi zilichangwa na wadau ikiwamo Serikali na watu binafsi ambapo amewalaumu baadhi ya wanasiasa akidai kuwa walipotosha kwa makusudi tukio la ajali hiyo kwa maslahi yao ya kisiasa.

CHANZO:
http://mtanzania.co.tz/gambo-agomea-agizo-la-makamu-wa-rais/

Comments

Habari Nyingine Kutoka Kioo17 Swahili;

UTATA WA FORM 34A FEKI KATIKA TOVUTI YA IEBC.

  Na BERNADINE MUTANU  Imepakiwa - Wednesday, August 16   2017 at  11:11 Kwa Mukhtasari VISA vya dosari kwenye uchaguzi uliokamilika vinazidi kuripotiwa nchini Kenya, wiki moja baada ya wananchi kupiga kura, na siku kadhaa baada ya Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) kutangaza mshindi wa urais. Huku IEBC ikikosolewa kwa kutangaza matokeo ya mwisho ya urais Ijumaa usiku kabla ya matokeo yote kuingia, imeibuka kuwa kituo kimoja Kaunti ya Mandera kilitumia karatasi ya kawaida kurekodi matokeo ya urais, badala ya kutumia Fomu 34 A. Matokeo hayo yaliwekwa katika tovuti ya IEBC, na kushangaza wananchi, huku madai ya wizi wa kura yakizidi kuchacha. 'Fomu’ hiyo isiyo ya kawaida iliwekwa katika mtandao wa IEBC kutoka Kituo cha Kuhesabia kura cha Bulla Dadacha 2, Wadi ya Elwak Kusini, Eneo Bunge la Mandera Kusini, Kaunti ya Mandera. Haina nambari ya mfuatano  (serial number)  kama fomu za kawaida za uchaguzi,...

KIONGOZI MKUU WA UPINZANI NCHINI ZIMBABWE, MORGAN TSVANGIRAI AMEFARIKI DUNIA.

Kiongozi wa upinzani wa Zimbabwe Morgan Tsvangirai amefariki dunia nchini Afrika Kusini, afisa mkuu wa chama chake cha MDC amesema. Bw Tsvangirai, mwenye umri wa miaka 65, aliyekuwa waziri mkuu, alilipotiwa kuwa alikuwa akisumbuliwa na saratani ya koloni. "Amefariki jioni hii, familia yake imenitaarifu"  Makamu wa Rais wa MDC, Elias Mudzuri aliliambia shirika la habari la Uingereza, Reuters. Morgan Tsvangirai alizaliwa mnamo Machi 10, 1952 huko Gutu, Zimbabwe. Baba yake alikuwa mfanyakazi wa mgodi, fundi, na mkulima. Alihudhuria Shule ya Msingi ya Guco ya St. Marks. Kisha alihamishiwa Shule ya Msingi ya Chikara Gutu. Kwa elimu yake ya sekondari, alihudhuria Shule ya High Gokomere. Alikuwa waziri mkuu katika serikali ya mseto ya Zimbabwe tangu 2009 hadi 2013. Katika kazi yake ya awali alionekana kuwa mfanyakazi mwenye bidii sana na alifanya kazi katika mgodi wa madini ya nickel( kwa zaidi ya muongo mmoja. Alipanda cheo haraka kutambuliwa na akain...

MCHEZAJI WA ZAMANI WA UINGEREZA AMESEMA ALICHEZA NA WACHEZAJI WATATU MASHOGA KWENYE TIMU.

Carl Hoefkens (jezi no.2) alichezea West Bromwich Albion na Stoke City wakati wa enzi zake ligi kuu ya England. Beki wa zamani wa Ligi Kuu ya Uingereza amesema alicheza pamoja na wachezaji wenzake wawili wa mashoga ndani ya timu, na mmoja alikua na jina kubwa. Carl Hoefkens, West Bromwich Albion na Stoke City siku za nyuma, anasema wachezaji hao walikua wazi na hawakujificha kwenye vyumba vya kubadilishia nguo ingawa bado hawajulikani kwasababu ya maombi yao wenyewe ya kuomba kutotangazwa. Justin Fashanu, ambaye alijiua mwaka 1998, alikuwa mchezaji wa mwisho wa kazi nchini England kuja nje kama mashoga - mwaka 1990. Hoefkens alipokua (kushoto), alipokua anachezea Stock  City. Hoefkens aliyecheza Uingereza kwa miaka minne, akiondoka mwaka 2009, alidai kuwa mchezaji mwenzake mmoja wa timu alikua anaweza kuja kwenye uwanja wa mafunzo ya klabu na mpenzi wake wa kiume  lakini aliwaomba wenzake kutokuwaambia watu wangine wa nje ya timu. 'Nilicheza pamoja n...

NAPE ASEMA KWAMBA TUNDU LISSU ALIMWAMBIA WANATAFUTWA, AHAME CCM.

MBUNGE WA MTAMA (CCM) AKICHEKA NA TUNDU LISSU MUDA MFUPI KABLA YA KUPIGWA RISASI. Imeandikwa na Edwin Mjwahuzi , Mwananchi; emjwahuzi@mwananchi.co.tz Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu (kulia) akifurahia jambo na mbunge wa Mtama, Nape Nnauye walipokuwa wakitoka kuhudhuria kikao cha Bunge, mjini Dodoma jana mchana. By Edwin Mjwahuzi, Mwananchi; emjwahuzi@mwananchi.co.tz Dodoma. Mbunge wa Mtama (CCM), Nape Nnauye ameeleza alichoambiwa na Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu jana Alhamisi mchana wakati wakitoka bungeni huku wakicheka. Nape amesema Lissu alimwambia, “Wewe Nape ni mjomba wangu, kwa nini unabaki CCM? Mimi na wewe tunafuatiliwa na jamaa zako wakitumia gari moja. Mimi na wewe ni watuhumiwa, hama CCM mjomba.” Lissu alipigwa risasi jana Alhamisi mchana na kupelekwa chumba cha upasuaji katika Hospitali ya Rufaa ya Dodoma na baadaye usiku alihamishiwa Hospitali ya Aga Khan ya Nairobi nchini Kenya. Mbunge wa Rombo, Joseph Selasini jana wakati Lissu...

MADAI YA CUBA KWAMBA WAZIRI MKUU WA CANADA NI MTOTO WA FIDEL CASTRO.

Pichani ni waziri mkuu wa Canada, Justin Trudeau (kushoto), na Rais wa zamani wa Cuba, Hayati Fidel Castro (kulia). Maelezo yaliyoandikwa na mtoto wa kwanza wa rais wa zamani wa Cuba , Fidel Castro, kabla ya kujiua yamelishtua taifa la Cuba wiki hii. Maelezo hayo yaliyoandikwa na mtoto huyo mkubwa wa mwanamapinduzi na rais wa zamani wa nchi hiyo yalikuwa ya kushangaza baada ya  kuwa na madai ya kuwa Waziri Mkuu wa Canada Justin Trudeau ni mtoto wa nje wa baba yake marehemu Fidel Castro. Maelezo hayo yaliyoandikwa kwa mkono na mtoto huyo wa Fidel Castro aliyejiua siku chache zilizopita kwa msongo wa mawazo, Fidel Castro Diaz-Balart, aliyekuwa na umri wa miaka 68, yalionekana kuthibitisha uvumi wa muda mrefu nchini Cuba kwamba Fidel Castro ni baba wa damu wa waziri mkuu wa sasa wa Canada, Justin Trudeau ikiwa ni matokeo ya uhusiano wa siri wa kimapenzi na mke wa mwanasiasa maarufu wa Canada, Pierre Trudeau, Margaret Trudeau mwaka 1970. Kifo cha mwanasayansi wa ...

ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2017, TANZANIA

MH.GEORGE SIMBACHAWENE .               Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Tamisemi) George Simbachawene ametoa idadi ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na masomo ya kidato cha tano na vyuo vya ufundi kwa mwaka 2017 huku jumla ya wanafunzi 2,999 wakiachwa.             Simbachawene ametoa kauli hiyo leo mjini Dodoma wakati akizungumza na waandishi ws habari na kusema kuwa ufaulu kwa mwaka huu umeongezeka kwa asilimia 3.75 ukilinganisha na matokeo ya mwaka 2015. Waziri amedai kati ya wanafunzi 96,018 waliofaulu kwa daraja la kwanza hadi la tatu ni wanafunzi 93,019 tu ndiyo waliochaguliwa kujiunga na kidato cha tano na vyuo vya ufundi.              Waziri Simbachawene amesema kuwa jumla ya watahiniwa wote waliofanya mtihani wa kidato cha nne kwa shule kwa mwaka 2016 ni 349,524 huku waliofanya mtihani wa kujitegemea ni 47,751 ambapo watahiniwa waliofanya mtihani wa shule...

NAKUMATT IMEPATA TUZO YA MLIPAKODI BORA NCHINI RWANDA.

MENEJA WA NAKUMATT NCHINI RWANDA, ADAN RAMATA, AKIPOKEA TUZO YA MLIPA KODI BORA KUTOKA KWA MWENYEKITI WA SHIRIKISHO LA SEKTA BINAFSI LA RWANDA, BENJAMIN GASAMERA. KIGALI, Rwanda, Oktoba 16 Kampuni ya maduka ya kuuza bidhaa za rejareja ya Nakumatt imetangazwa kuwa walipa kodi bora na Mamlaka ya Mapato ya Rwanda. Nakumatt Rwanda ambayo inafanya kazi maduka ya rejareja 3 jijini Kigali, Rwanda ilitangazwa mlipakodi bora Ijumaa jioni katika tukio ambalo liliandaliwa na RRA ili kusherehekea walipa kodi katika nchi. Nakumatt Rwanda ilichukua tuzo bora ya walipa kodi ya 2016. Kampuni hiyo pia ilipokea tuzo bora ya mtumiaji wa umeme wa EBM (EBM). Akizungumza katika tukio hilo, Kamishna Mkuu wa RRA Richard Tusabe alithibitisha kwamba kiwango vya kulipa kodi nchini kimekuwa kwa kasi na kutokana na ushirikiano mzuri kutoka katika sekta kadhaa za uchumi ikiwa ni pamoja na sekta binafsi. Mkurugenzi huyo wa RRA alifafanua kuwa bodi ya kodi imeweza kufika lengo lake la kukusanya katika...