Skip to main content

MAGAVANA WAENDELEA KUFUTA KAZI WAFANYAKAZI.




 Friday, August 25   2017 at  14:56 (Gazeti Taifa Leo /KENYA)
Kwa Mukhtasari
MAGAVANA wameendelea kuwafuta kazi mawaziri na wafanyakazi wa kaunti zao. Gavana wa Meru Kiraitu Murungi alibandua bodi kadha Alhamisi jioni katika kile alichosema ni hatua ya kufichua makundi ya ufisadi ambayo yameteka kaunti hiyo. 


Alichukua hatua hiyo siku moja baada ya Bw Murungi kuwasimamisha kazi mawaziri wake ili kutoa fursa ya kufanyika kwa ukaguzi wa fedha na wafanyakazi wa kaunti.
Hata hivyo, Bw Murungi aliwahakikishia wafanyakazi hao kwamba lengo la zoezi hilo si kuwaandama kwa sababu linatekelezwa kwa mujibu wa sheria.“Tuliahidi kuendelea na zoezi hili la kusafisha. Ndiposa tumebandua bodi na kubatilisha uteuzi wa wanachama wote wa bodi za mashirika mbalimbali ya kaunti,” akasema Bw Murungi.
Mashirika yaliyoathiriwa ni pamoja na lile la uwekezaji na ustawi, fedha, mapato na kudhibiti vileo.
Gavana pia alibandua kamati za usimamizi za hospitali, vituo vya afya na zahanati akisema hatua hiyo inaambatana na ahadi yake ya kufanyia mageuzi huduma za matibabu. Aliagiza maafisa wasimamizi wa vituo hivyo kuchukua usukani.
Bw Murungi alisema zoezi la ukaguzi litasaidia kuwang’oa wafanyakazi hewa.
“Tunajua kuna wafanyakazi hewa katika kaunti hii. Serikali iliyopita imekuwa ikilipa Sh15 milioni kwa vibarua kila mwezi, jambo ambalo linaibua shaka. Kuna vibarua 5,000 ilhali serikali ikon a wafanyakazi wa kutosha,” alieleza na kuongeza kuwa wafanyakazi ambao watakaopita ukaguzi watarejeshwa kazini.
Gavana wa Kisumu Prof Anyang’ Nyong’o aliwasimamisha kazi maafisa wakuu 14 na kuwaagiza wakurugenzi kuchukua usukani hadi wakuu wengine watakapoajiriwa.
Prof Nyong’o pia aliwafuta kazi mawaziri tisa wa kaunti.
Katika kaunti ya Nandi, Gavana Stephen Sang alibandua bodi ya usimamizi wa afya na kamati ya hospitali ya rufaa na zile za kaunti ndogo. Maafisa zaidi ya 40 waliathirika.
Vile vile alimsimamisha kazi waziri wa afya na maafisa wengine wakuu katika idara ya afya ili kutoa fursa ya uchunguzi wa kile alichodai ni kutoweka kwa fedha za idara hiyo.
Katika taarifa, Bw Sang alisema kuwa aliagiza idara ya ndani ya ukaguzi kufanya uchunguzi wa kina kuhusu mapato ambayo idara ya afya imekusanya katika miaka minne iliyopita.
Gavana wa Pokot Magharibi Prof. John Lonyangapuo amewapa likizo ya lazima wafanyikazi wakuu wa kaunti ili kutoa fursa ya uchunguzi kufanyika .
Katika kikao na wanahabari mjini Kapenguria, Prof Lonyangapuo alisema kuwa ameagiza mara moja ukaguzi wa idara za fedha na uajiri.
“Wafanyakazi wa ziada wamepunguzwa isipokuwa katika idara za afya na ukusanyaji ushuru. Lengo ni kuondoa wafanyakazi ghushi; baadhi waliajiriwa miezi michache kabla kampeni za uchaguzi kuanza,” alisema na kuongeza kuwa ukaguzi huo pia utahusu wanakandarasi.
Gavana wa Marsabit Mohamud Ali alisitisha shughuli katika wizara nane na kuagiza magari yote ya kaunti yapelekwe katika makao makuu ya kaunti.
“Nimesitisha shughuli katika wizara zote za kaunti isipokuwa zile za afya na maji,” alisema Bw Ali katika taarifa.
Gavana pia aliunda jopo kazi la wanachama tisa kuchunguza operesheni za Bodi ya Kuajiri Watumishi wa Umma (CPSB) katika miaka mitano iliyopita.

CHANZO:

Comments

Habari Nyingine Kutoka Kioo17 Swahili;

ORODHA YA NCHI ZA KWANZA NA ZA MWISHO KWA AMANI DUNIANI.

Marekani:  Ripoti ya Taasisi ya Uchumi na Amani imepata mataifa kumi tu ulimwenguni ambayo hayapo katika vita na migogoro kabisa. Kwa mujibu wa Ripoti ya Kimataifa ya Amani 2016, Botswana, Chile, Costa Rica, Japan, Mauritius, Panama, Qatar, Uswisi, Uruguay na Vietnam ndio nchi pekee ambazo hazipo kwenye vita wala migogoro yeyote ile ya kuhatarisha amani.. Iceland inaongoza orodha ya nchi zinazoongoza kwa amani ulimwenguni, ikifuatiwa na Denmark, Austria, New Zealand, Ureno, Jamhuri ya Czech, Uswisi, Canada, Japan na Slovenia - wakati Marekani ikiwa kwenye nafasi ya 103. Palestina imepanda kutoka nafasi ya 163 mpaka nafasi ya 148. Syria iliyoharibiwa na vita imewekwa chini ya orodha, chini kuliko Sudan Kusini, Iraq, Afghanistan, Somalia, Yemen, Jamhuri ya Afrika ya Kati, Ukraine, Sudan na Libya. "Ripoti inalinganisha amani duniani kwa kutumia mandhari tatu pana: hali ya utulivu na usalama katika jamii; kiwango cha mgogoro wa ndani au wa kimataifa; na kiwango cha kije...

JAGUAR KUACHIA WIMBO BAADA YA KUAPISHWA MBUNGE.

Mbunge wa Starehe, Kenya, "Jaguar" anajipanga kutoa wimbo mpya mara tu baada ya kuapishwa kua mbunge. Katika chapisho lake la kwenye akaunti yake ya mtandao wa kijamii, Jaguar aliupendekeza wimbo wake wa "Ndoto" kama salamu kwa Wakenya na watu walio nje ya Kenya. Charles Njagua, ambae ni maarufu kwa jina la Jaguar, ana Aliahidi mashabiki wimbo mpya baada ya kuapa rasmi kama mbunge.  Mimbaji huyo ambaye ametoa hits kadhaa lakini sasa anazingatia siasa baada ya kushinda kiti, aliwaambia mashabiki kwenye vyombo vya habari vya kijamii kwamba wimbo mpya, unaitwa "Ndoto", uko tayari na utaachiliwa haraka baada ya kuapa. "Sasa ni karibu miongo miwili tangu mimi kuweka mguu katika studio ya kurekodi,   alisema Jaguar katika chapisho lake. CHANZO: www.tuko.news

KASHFA YA MAPENZI KATI MH.MBOWE NA WEMA SEPETU.

MH.FREEMAN MBOWE AKIWA NA WEMA SEPETU. Siku chache baada ya ile skendo ya ngono iliyosababisha wakili na mshauri wa Chama cha ACT -Wazalendo , Bwana Albert Msando kujiuzulu kwenye nyadhifa yake ya chama ,yameibuka mangine kwenye chama kikuu cha upinzani Tanzania ,CHADEMA ,baada ya kusambaa kwa kipande cha sauti kinachodaiwa kua ni mazungumzo kati ya mwenyekiti wa chama hicho na mbunge wa Hai Mh.Freeman Mbowe na Miss Tanzania 2006 ,mrembo Wema Isack Sepetu. SIKILIZA HIVI VIPANDE VYA SAUTI: Bonyeza hapa chini kusikiliza maongezi hayo yanayodaiwa kuwa ni kati ya Wema Sepetu na Mh.Freeman Mbowe; Bonyeza hapa chini kusikiliza majibu ya Wema Sepetu; Bonyeza hapa chini kusikiliza majibu ya Mh.Freeman Mbowe; VYANZO: Jamii Forums,                   YouTube.com,                   Perfect255.com.                   

"GIGGS HAFAI KUWA KOCHA WA TIMU YA TAIFA", BABA YAKE ANASEMA...!!!

Ryan Giggs. Chama cha Soka cha Wales (FAW) siku ya jumatatu kilitangaza kumchagua winga wa zamani wa Manchester United Ryan Giggs kama kocha wa timu yao ya taifa kwa mkataba wa miaka minne. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 44 anachukua kazi iyoachwa na Chris Coleman, ambaye aliiongoza Wales kwenye nusu fainali za Euro 2016 lakini aliacha kazi mwezi Novemba ili kuchukua nafasi ya kuifundisha timu ya Sunderland ya ligi kuu ya Uingereza. Giggs alisema kuwa anajivunia kwa kupewa kazi hiyo na pamoja na changamoto iliyo mbele yake baada ya Wales kushindwa kufuzu kucheza fainali za Kombe la Dunia mwaka huu nchini Urusi na sasa wanazingatia michuano ya Ulaya ya 2020. "Siwezi kusubiri kuanza kufanya kazi na wachezaji tunapojiandaa kwa ajili ya michezo muhimu baadaye mwaka huu," alisema. Lakini baba mzazi wa Giggs, Danny Wilson ana maoni  tofauti sana...!!! Anakiri kwamba mwanae anamtia aibu na anasema hastahili kuchukua kazi hiyo ya ukocha wa timu ya t...

MCHEZAJI WA ZAMANI WA UINGEREZA AMESEMA ALICHEZA NA WACHEZAJI WATATU MASHOGA KWENYE TIMU.

Carl Hoefkens (jezi no.2) alichezea West Bromwich Albion na Stoke City wakati wa enzi zake ligi kuu ya England. Beki wa zamani wa Ligi Kuu ya Uingereza amesema alicheza pamoja na wachezaji wenzake wawili wa mashoga ndani ya timu, na mmoja alikua na jina kubwa. Carl Hoefkens, West Bromwich Albion na Stoke City siku za nyuma, anasema wachezaji hao walikua wazi na hawakujificha kwenye vyumba vya kubadilishia nguo ingawa bado hawajulikani kwasababu ya maombi yao wenyewe ya kuomba kutotangazwa. Justin Fashanu, ambaye alijiua mwaka 1998, alikuwa mchezaji wa mwisho wa kazi nchini England kuja nje kama mashoga - mwaka 1990. Hoefkens alipokua (kushoto), alipokua anachezea Stock  City. Hoefkens aliyecheza Uingereza kwa miaka minne, akiondoka mwaka 2009, alidai kuwa mchezaji mwenzake mmoja wa timu alikua anaweza kuja kwenye uwanja wa mafunzo ya klabu na mpenzi wake wa kiume  lakini aliwaomba wenzake kutokuwaambia watu wangine wa nje ya timu. 'Nilicheza pamoja n...

TUPAC SHAKUR ALIBAKWA JELA !!!

             Ulimwengu wa filamu za Hollywood na muziki wa Hip Hop juzi ulipatwa na mshangao baada ya mtayarishaji wa filamu inayohusu maisha ya hayati Tupac Shakur ,L.T Hutton kuelezea sababu zilizomfanya kumbadilisha muongozaji wa filamu hiyo kutoka John Singleton na kumuweka muongozaji Benny "Boom" Douglas.  Filamu hiyo inayoitwa "all eyez on me" tayari imekwisha andaliwa na inatarajiwa kuzinduliwa leo tarehe 16 Juni 2017.       Akizungumza kwenye mahojiano redioni L.T Hutton amewashtusha watu wengi baada ya kudai kwamba walishindwana na muongozaji wa mwanzo bwana John Singleton sababu muongozaji huyo aling'ang'ania kuwepo kwa matukio (scene) ambazo kwa maoni yake zisingependeza.        Matukio ambayo John Singleton alipenda yawepo katika filamu hiyo ni pamoja na kutaka filamu hiyo ianze na scene ya Tupac akilazimisha kumlawiti msichana wa kizungu.!!!          Singleton pia ali...

MOHAMMED DEWJI NA BILL GATES KUTOA NUSU YA UTAJIRI WAO...!!!

MOHAMMED DEWJI AKIWA NA BILL GATES. Mfanyabiashara tajiri namba moja Tanzania (kwa mujibu wa jarida la Forbes) na mmiliki wa makampuni ya METL , Mohammed "Mo" Dewji ,wiki chache zilizopita amekua mmoja wa mabilionea 14 wapya kujiunga katika mpango wa kuchangia misaada kwa jamii uitwao "Giving Pledge".                 Mpango huo ulioanzishwa na familia ya mfanyabiashara tajiri namba moja duniani (kwa mujibu wa jarida la Forbes) na mmiliki wa kampuni ya Microsoft Bill Gates pamoja na rafiki yake bilionea Warren Buffet mwaka 2010, ulikua na tayari umeshaungwa mkono na mabilionea 154 mpaka mwanzo wa mwaka huu (2017). WAASISI WA "GIVIN PLEDGE",WARREN BUFFET, MELINDA GATES NA BILL GATES.         Mohammed Dewji anakua mmoja kati ya matajiri wachache sana kutoka Afrika kama Patrice Motsepe (Afrika Kusini) na Mo Ibrahim (Sudan) kujiunga na kampeni hiyo ambayo nia yake kubwa ni kushawishi watu matajiri kutoa angalau nu...