Skip to main content

NDEGE YA TANZANIA KUPIGWA MNADA CANADA.




IMEANDIKWA NA MALISA GJ :

Tundu Lissu ameeleza kuwa ni kweli ndege aina ya 'Bombadier Dash Q400' mali ya shirika la ndege la ATCL imeshikiliwa huko nchini Canada na kampuni moja ya Ujenzi ijulikanayo kama Stirling Civil Engineering Ltd kutokana na kuidai serikali ya tanzania kiasi cha USD 38M (Takribani TZS 87BL). Kampuni hiyo imetishia kuipiga "mnada" ndege hiyo kufidia deni lao, ikiwa serikali ya Tanzania haitawalipa.

KWANINI NDEGE YETU IMEKAMATWA?

Mwaka 2009 kampuni Stirling Civil Engineering Ltd, ilikupewa kandarasi ya kutengeneza Barabara ya Wazo Hill – Bagamoyo. Kabla ya kukamilisha kandarasi hiyo, aliyekuwa Waziri wa ujenzi wakati huo alivunja mikataba bila kuzingatia sheria, na kuinyang'anya kampuni hiyo kandarasi hiyo na kuagiza kampuni hiyo kutimuliwa nchini.

Kampuni ya Stirling Civil Engineering Ltd, ilifungua kesi katika mahakama ya kimataifa ya usuluhishi mjini Paris. Tarehe 10 Desemba, 2009 mahakama hiyo iliipa ushindi kampuni hiyo na kuagiza serikali ya Tanzania kuilipa takriban dola za Marekani milioni 25 (Takribani TZS 40BL kwa wakati huo).

Serikali ya Tanzania ilikata rufaa, lakini ikaangukia pua kwenye hukumu ya tarehe 10 Juni, 2010 ambapo mahakama hiyo iliagiza Tanzania ilipe fedha hiyo pamoja na riba ya 8% kila mwaka hadi malipo kamili yatakapofanyika. Tuzo hiyo imesajiliwa na kutambuliwa kama deni halali la Serikali ya Tanzania kwa Stirling Civil Engineering Ltd.

Lakini serikali ilikataa kulipa deni hilo, licha ya jitihada mbalimbali zilizofanywa na kampuni hiyo. Kutokana na ucheleweshaji wa malipo, deni hilo limeongezeka hadi dola za Marekani 38.7M kufikia tarehe 30 Juni, 2017.

Hapo ndipo Stirling Civil Engineering Ltd. ilipoamua kuomba amri ya Mahakama Kuu ya Montreal ya kukamata mali zote za serikali ya Tanzania zilizopo nchini Canada zikijumuisha ndege ya Bombardier Q400. Mahakama ilitoa kibali na ndege hiyo kukamatwa.

SERIKALI IMECHUKUA HATUA GANI?

Kwa mujibu wa Mhe.Tundu Lissu serikali iliomba mazungumzo na kampuni ya Stirling Civil Engineering Ltd ili kutatua tatizo hilo. Katika mazungumzo hayo ambapo serikali ya Tanzania iliwakilishwa na Waziri wa mambo ya nje Balozi Augustine Mahiga, aliomba kampuni hiyo kuepuka suala hilo kujulikana hadharani.

Kwa upande wake, kampuni ya Stirling Civil Engineering Ltd. imekubali kuiachia ndege ya Bombardier Q400 kwa malipo ya mwanzo ya dola za Marekani milioni 12.5 (Takribani TZS 30B) na baadae itatuma ujumbe wake Tanzania kwa ajili ya kuja kufanya makubaliano ya mwisho juu ya kulipa deni hilo. Endapo malipo hayo yatafanywa na Serikali, Stirling Civil Engineering Ltd, itasitisha mpango wake wa kuipiga mnada ndege yetu ya Bombardier Q400. Ikiwa serikali itashindwa kutimiza makubaliano hayo basi ndege hiyo itapigwa mnada.

Wakati huohuo kampuni ya uchimbaji madini ya ACACIA Mining imetoa notisi ya kuishitaki Serikali ili kudai fidia ya Dola za Marekani bilioni 2 (Takribani TZS Trilioni 5) kwa kukamata mchanga wake wa dhahabu, kinyume na sheria na mkataba wa uchimbaji madini waliosani na serikali.

Kampuni hiyo imetoa tishio hilo wakati mazungumzo yakiendelea kati yake na serikali juu ya hatma ya mchanga huo wa dhahabu maarufu kama makinikia. Ikiwa Accacia watafanyia kazi notisi hiyo, Tanzania itaburuzwa tena kwenye mahakama ya usuluhishi ya kimataifa, na kutakiwa kulipa Trilioni 5 kwa Accacia.

Nini maoni yako?

CHANZO:
https://m.facebook.com/story.php?story_fbid=1478370308921323&id=100002451047207

Comments

Habari Nyingine Kutoka Kioo17 Swahili;

ORODHA YA NCHI 80 AMBAZO MTANZANIA ANARUHUSIWA KUINGIA BILA VIZA.

         Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni amesema kuna zaidi ya nchi 80 ambazo watanzania wanaweza kusafiri bila ya kuwa na viza . Mhandisi Hamad Masauni amesema kuna zaidi ya nchi 80 ambazo watanzania wanaweza kusafiri bila ya kuwa na viza za kusafiria kama ilivyokuwa nchi za afrika Mashariki. Mhandisi Massauni amebainisha hayo leo bungeni wakati akijibu swali la Mbunge wa Mlalo kupitia tiketi ya CCM Rashid Shangazi aliyetaka kujua ni nchi ngapi ambazo watanzania wanaweza kusafiri bila ya kuwa na viza (viza on arrival). "Zipo nchi 16 kwa Afrika ambazo watanzania wanaweza kuzitembelea bila ya kuwa na viza na duniani zipo 67" alisema Masauni. Aidha Massauni amezitaja nchi hizo kuwa ni Benin, Burkina Faso, Cape Verde, Ivory Coast, Djibouti, Gabon, Gambia, Guinea, Guinea­Bissau, Liberia, Mali, Mauritania, Niger, Sierra Leone pamoja na Togo. Pamoja na hayo Masauni amesema...

USWISI KURUDISHA DOLA MILIONI 321($321M) ZA WIZI KWA NIGERIA.

Serikali ya Nigeria imechukua zaidi ya dola bilioni 1 zilizoaminiwa kuibwa na Rais wa zamani Sani Abacha. CNN: Serikali ya Uswisi kurudisha dola za kimarekani milioni 321 nchini Nigeria ambazo zilikuwa zimechukuliwa kutoka kwenye familia ya Rais wa zamani wa nchi hiyo, Sani Abacha. Mali hizo zilifanywa kama sehemu ya kesi za jinai dhidi ya Abba Abacha, mwana wa Sani, ambaye alitawala Nigeria kwa miaka mitano mpaka kufa kwake mwaka 1998. Wachunguzi wa Nigeria wanaamini rais huyo wa zamani aliiba zaidi ya dola bilioni 4 ($4 Billion) muda wake katika ofisi. Serikali ya Uswisi ilitoa tamko Jumatatu kutangaza makubaliano hayo yaliyofikiwa na viongozi kutoka serikali ya Nigeria na Benki ya Dunia kwa marekebisho. "Marejesho ya fedha yatatokea katika mfumo wa mradi unaoungwa mkono na kusimamiwa na Benki ya Dunia," ,  ilisema taarifa hiyo. "Mradi utaimarisha usalama wa kijamii kwa sehemu maskini zaidi ya idadi ya watu wa Nigeria." Serikali ya Nigeria ilit...

SABABU ZA KUVUNJIKA KWA KUNDI LA P-SQUARE.

WANAMUZIKI MAPACHA WA KUNDI LA PSQUARE, PETER (KUSHOTO) NA PAUL (KULIA) WAKIWA NA KAKA YAO AMBAE PIA NI MENEJA WAO, JUDES OKOYE. Mwanamuziki wa kundi la PSquare kutoka Nigeria, Peter Okoye ametangaza kujitoa kwenye kundi hilo la muziki wa Pop maarufu zaidi Afrika. Msanii huyo alidai kwamba amewasilisha maombi ya kuvunja kundi hilo katika barua aliyoandika kwa wakili wao Festus Keyamo. Kulingana na nakala ya barua iliyotolewa kwenye vyombo vya habari Jumatatu,Tarehe 25 Septemba, Peter alisema kuwa pacha wake na, Paul, na kaka yao, Judes waliahirisha ziara yao ya muziki ya Marekani bila kushauriana naye.Na hiyo ni moja kati ya sababu za msingi. Peter pia aliwalaumu Paul na kaka yao mkubwa mkubwa ambae ni meneja wao pia kwa udanganyifu walioufanya ili kutatua shida waliyokuwa nayo juu ya biashara ya muziki. Wasanii hao ndugu wamekua kwenye vita vya maneno kwenye mitandao ya kijamii tangu mwisho wa mwaka jana pamoja na juhudi za watu wao wa karibu kujaribu kuwapatanisha kifami...

TUPAC SHAKUR ALIBAKWA JELA !!!

             Ulimwengu wa filamu za Hollywood na muziki wa Hip Hop juzi ulipatwa na mshangao baada ya mtayarishaji wa filamu inayohusu maisha ya hayati Tupac Shakur ,L.T Hutton kuelezea sababu zilizomfanya kumbadilisha muongozaji wa filamu hiyo kutoka John Singleton na kumuweka muongozaji Benny "Boom" Douglas.  Filamu hiyo inayoitwa "all eyez on me" tayari imekwisha andaliwa na inatarajiwa kuzinduliwa leo tarehe 16 Juni 2017.       Akizungumza kwenye mahojiano redioni L.T Hutton amewashtusha watu wengi baada ya kudai kwamba walishindwana na muongozaji wa mwanzo bwana John Singleton sababu muongozaji huyo aling'ang'ania kuwepo kwa matukio (scene) ambazo kwa maoni yake zisingependeza.        Matukio ambayo John Singleton alipenda yawepo katika filamu hiyo ni pamoja na kutaka filamu hiyo ianze na scene ya Tupac akilazimisha kumlawiti msichana wa kizungu.!!!          Singleton pia ali...

ALICHOANDIKA MH.NGELEJA BAADA YA KURUDISHA FEDHA ZA ESCROW.

MH.WILLIAM NGELEJA .            Waziri wa zamani wa Nishati na Madini na Mbunge wa Jimbo la Sengerema, William Ngeleja amerejesha rasmi Serikalini fedha alizozipata katika mgao wa Escrow ambazo ni kiasi cha Shilingi Milioni 40.4 ili kukwepa kuendelea kuandamwa na kashfa.        Ngeleja amesema ingawa alipewa fedha hizo kama sehemu ya msaada , ameamua kurudisha fedha hizo ili kukwepa kashfa hiyo ya ESCROW.     SOMA HAPA BARUA ALIYOITOA KWA WAANDISHI WA HABARI ;

MCHEZAJI WA ZAMANI WA UINGEREZA AMESEMA ALICHEZA NA WACHEZAJI WATATU MASHOGA KWENYE TIMU.

Carl Hoefkens (jezi no.2) alichezea West Bromwich Albion na Stoke City wakati wa enzi zake ligi kuu ya England. Beki wa zamani wa Ligi Kuu ya Uingereza amesema alicheza pamoja na wachezaji wenzake wawili wa mashoga ndani ya timu, na mmoja alikua na jina kubwa. Carl Hoefkens, West Bromwich Albion na Stoke City siku za nyuma, anasema wachezaji hao walikua wazi na hawakujificha kwenye vyumba vya kubadilishia nguo ingawa bado hawajulikani kwasababu ya maombi yao wenyewe ya kuomba kutotangazwa. Justin Fashanu, ambaye alijiua mwaka 1998, alikuwa mchezaji wa mwisho wa kazi nchini England kuja nje kama mashoga - mwaka 1990. Hoefkens alipokua (kushoto), alipokua anachezea Stock  City. Hoefkens aliyecheza Uingereza kwa miaka minne, akiondoka mwaka 2009, alidai kuwa mchezaji mwenzake mmoja wa timu alikua anaweza kuja kwenye uwanja wa mafunzo ya klabu na mpenzi wake wa kiume  lakini aliwaomba wenzake kutokuwaambia watu wangine wa nje ya timu. 'Nilicheza pamoja n...

ALICHOSEMA SHEIKH PONDA KUHUSU MIILI INAYOOKOTWA BAHARINI.

SHEIKH PONDA. KUTOKA GAZETI LA NIPASHE ,22 Agosti 2017; Akizungumza na Nipashe kwa simu jana, Sheikh Ponda ambaye pia ni Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Taasisi za Kiislamu Tanzania, alisema kwa muda mrefu wamekuwa wakipaza sauti kuhusu uwapo wa mauaji ya raia kwenye mikoa ya kusini mwa Tanzania, lakini haijasikilizwa. "Tunapongeza Nipashe kwa habari hii," alisema Sheikh Ponda kwa sababu "imefichua mambo mengi.", "Haya tumeshayasema lakini hakuna aliyetusikiliza. "Ni wakati mwafaka serikali ikatoa tamko kwa vile vyombo vya dola vimeonyesha kushindwa kueleza miili hiyo ni ya watu gani na inatoka wapi, (na kibaya) zaidi wanasema wanatambua miili mitatu iliyookotwa ambayo kwa sasa iko Muhimbili." Kaimu Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Lucas Mkondya, aliiambia Nipashe kwa njia ya simu juzi kuwa miili iliyookotwa ni mitatu na haikuwa kwenye viroba. Sheikh Ponda alisema mauaji hayo ni makubwa na hayajawahi kutokea kwa serikali z...