Skip to main content

NDEGE YA TANZANIA KUPIGWA MNADA CANADA.




IMEANDIKWA NA MALISA GJ :

Tundu Lissu ameeleza kuwa ni kweli ndege aina ya 'Bombadier Dash Q400' mali ya shirika la ndege la ATCL imeshikiliwa huko nchini Canada na kampuni moja ya Ujenzi ijulikanayo kama Stirling Civil Engineering Ltd kutokana na kuidai serikali ya tanzania kiasi cha USD 38M (Takribani TZS 87BL). Kampuni hiyo imetishia kuipiga "mnada" ndege hiyo kufidia deni lao, ikiwa serikali ya Tanzania haitawalipa.

KWANINI NDEGE YETU IMEKAMATWA?

Mwaka 2009 kampuni Stirling Civil Engineering Ltd, ilikupewa kandarasi ya kutengeneza Barabara ya Wazo Hill – Bagamoyo. Kabla ya kukamilisha kandarasi hiyo, aliyekuwa Waziri wa ujenzi wakati huo alivunja mikataba bila kuzingatia sheria, na kuinyang'anya kampuni hiyo kandarasi hiyo na kuagiza kampuni hiyo kutimuliwa nchini.

Kampuni ya Stirling Civil Engineering Ltd, ilifungua kesi katika mahakama ya kimataifa ya usuluhishi mjini Paris. Tarehe 10 Desemba, 2009 mahakama hiyo iliipa ushindi kampuni hiyo na kuagiza serikali ya Tanzania kuilipa takriban dola za Marekani milioni 25 (Takribani TZS 40BL kwa wakati huo).

Serikali ya Tanzania ilikata rufaa, lakini ikaangukia pua kwenye hukumu ya tarehe 10 Juni, 2010 ambapo mahakama hiyo iliagiza Tanzania ilipe fedha hiyo pamoja na riba ya 8% kila mwaka hadi malipo kamili yatakapofanyika. Tuzo hiyo imesajiliwa na kutambuliwa kama deni halali la Serikali ya Tanzania kwa Stirling Civil Engineering Ltd.

Lakini serikali ilikataa kulipa deni hilo, licha ya jitihada mbalimbali zilizofanywa na kampuni hiyo. Kutokana na ucheleweshaji wa malipo, deni hilo limeongezeka hadi dola za Marekani 38.7M kufikia tarehe 30 Juni, 2017.

Hapo ndipo Stirling Civil Engineering Ltd. ilipoamua kuomba amri ya Mahakama Kuu ya Montreal ya kukamata mali zote za serikali ya Tanzania zilizopo nchini Canada zikijumuisha ndege ya Bombardier Q400. Mahakama ilitoa kibali na ndege hiyo kukamatwa.

SERIKALI IMECHUKUA HATUA GANI?

Kwa mujibu wa Mhe.Tundu Lissu serikali iliomba mazungumzo na kampuni ya Stirling Civil Engineering Ltd ili kutatua tatizo hilo. Katika mazungumzo hayo ambapo serikali ya Tanzania iliwakilishwa na Waziri wa mambo ya nje Balozi Augustine Mahiga, aliomba kampuni hiyo kuepuka suala hilo kujulikana hadharani.

Kwa upande wake, kampuni ya Stirling Civil Engineering Ltd. imekubali kuiachia ndege ya Bombardier Q400 kwa malipo ya mwanzo ya dola za Marekani milioni 12.5 (Takribani TZS 30B) na baadae itatuma ujumbe wake Tanzania kwa ajili ya kuja kufanya makubaliano ya mwisho juu ya kulipa deni hilo. Endapo malipo hayo yatafanywa na Serikali, Stirling Civil Engineering Ltd, itasitisha mpango wake wa kuipiga mnada ndege yetu ya Bombardier Q400. Ikiwa serikali itashindwa kutimiza makubaliano hayo basi ndege hiyo itapigwa mnada.

Wakati huohuo kampuni ya uchimbaji madini ya ACACIA Mining imetoa notisi ya kuishitaki Serikali ili kudai fidia ya Dola za Marekani bilioni 2 (Takribani TZS Trilioni 5) kwa kukamata mchanga wake wa dhahabu, kinyume na sheria na mkataba wa uchimbaji madini waliosani na serikali.

Kampuni hiyo imetoa tishio hilo wakati mazungumzo yakiendelea kati yake na serikali juu ya hatma ya mchanga huo wa dhahabu maarufu kama makinikia. Ikiwa Accacia watafanyia kazi notisi hiyo, Tanzania itaburuzwa tena kwenye mahakama ya usuluhishi ya kimataifa, na kutakiwa kulipa Trilioni 5 kwa Accacia.

Nini maoni yako?

CHANZO:
https://m.facebook.com/story.php?story_fbid=1478370308921323&id=100002451047207

Comments

Habari Nyingine Kutoka Kioo17 Swahili;

MCHEZAJI WA ZAMANI WA UINGEREZA AMESEMA ALICHEZA NA WACHEZAJI WATATU MASHOGA KWENYE TIMU.

Carl Hoefkens (jezi no.2) alichezea West Bromwich Albion na Stoke City wakati wa enzi zake ligi kuu ya England. Beki wa zamani wa Ligi Kuu ya Uingereza amesema alicheza pamoja na wachezaji wenzake wawili wa mashoga ndani ya timu, na mmoja alikua na jina kubwa. Carl Hoefkens, West Bromwich Albion na Stoke City siku za nyuma, anasema wachezaji hao walikua wazi na hawakujificha kwenye vyumba vya kubadilishia nguo ingawa bado hawajulikani kwasababu ya maombi yao wenyewe ya kuomba kutotangazwa. Justin Fashanu, ambaye alijiua mwaka 1998, alikuwa mchezaji wa mwisho wa kazi nchini England kuja nje kama mashoga - mwaka 1990. Hoefkens alipokua (kushoto), alipokua anachezea Stock  City. Hoefkens aliyecheza Uingereza kwa miaka minne, akiondoka mwaka 2009, alidai kuwa mchezaji mwenzake mmoja wa timu alikua anaweza kuja kwenye uwanja wa mafunzo ya klabu na mpenzi wake wa kiume  lakini aliwaomba wenzake kutokuwaambia watu wangine wa nje ya timu. 'Nilicheza pamoja n...

STAR TV YAFUNGIWA NA TRA KWA KUKWEPA KODI.

Mamlaka ya mapato Tanzania inadaiwa kuifungia Radio Free Africa ya Mwanza inayomilikiwa na Antony Dialo kutokana na kudaiwa kodi kubwa. TRA wamewaondoa studio wafanyakazi wote na kuifunga radio hiyo. Kwa sasa ukiwasha radio utasikia matangazo ya kiingereza ya BBC. Diallo ni mwenyekiti wa CCM Mwanza na anadaiwa mamilioni ya kodi na TRA miaka mingi. Star Tv pia imekumbwa na sekeseke hilo. Ikumbukwe hii ndio TV pekee binafsi iliyokuwa ikipingana na MOAT na TEF katika sakata la RC Paul Makonda na walirusha kipindi maalum cha Makonda huku Jumuiya ya Wanahabari wakitangaza rasmi kujitenga na maswahibu yoyote yatakayokuja kuikuta RFA na Star TV. VYANZO : https://www.jamiiforums.com/threads/tra-waifungia-rfa-kwa-kudaiwa-kodi-ya-sh-bilioni-4-5.1283386/

JINSI YA KUOMBA PASSPORT YA TANZANIA KWA NJIA YA INTERNET.

Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kupitia i dara ya Uhamiaji  imezindua huduma ya ujazaji fomu za maombi ya hati ya kusafiria (Passport) kwa njia ya mtandao, ambapo mwombaji atalazimika kujaza fomu hizo na kuzichapisha kabla ya kuziwasilisha kwenye ofisi za uhamiaji. Idara hiyo pia imeeleza kuwa matumizi ya huduma hiyo yataenda sambamba na huduma inayotumiwa sasa ya fomu za maombi ya pasipoti mpaka pale itakapotangazwa vinginevyo. Huduma hiyo itaanza kufanya kazi kuanzia Jumatatu tarehe  7/8/2017    na unaweza  kujaza fomu hizo  kwa kufungua tovuti hiyo ambayo ni  https://www.immigration.go.tz/ppt_application/ Utaratibu wa namna ya kujaza fomu hizo umeelekezwa katika fomu husika mtandaoni, na pia wateja wanaweza kupata ufafanuzi au maelezo zaidi kuhusu huduma hiyo kupitia anuani ya Idara ya Uhamiaji ambayo ni   info@immigration.go.tz   au katika Ofisi yoyote ya Uhamiaji iliyo karibu yako. CHANZO: http://dibute.com/muhimu-...

MOURINHO KUMUONDOA MKHITARYAN ILI AWEZE KUMSAJILI OZIL.

Henrikh Mkhitaryan atatupwa kando na meneja wa Manchester United Jose Mourinho ili apate nafasi ya kumsajili jiungo wa Arsenal, Mesut Ozil, kulingana na taarifa.  Bosi huyo wa Manchester United anajua lazima apunguze kikosi chake kama atataka kumsajili Ozil kutokana na madai ya mshahara mkubwa ya bingwa huyo wa Kombe la Dunia. Kiungo huyo mchezeshaji huyo ambaye mkataba wake Arsenal umalizika mwishoni mwa msimu huu, amekuwa akiomba mshahala wa Pauni Laki Tatu (£ 300,000) kwa wiki ili kukubali mkataba mpya wa kuendelea kuchezea Arsenal. Gazeti la 'The Mirror' la Uingereza limeripoti kwamba Mourinho ameamua Mkhitaryan, ambaye alijiunga na klabu kutoka Borussia Dortmund mwaka 2016, anaweza kuwa mchezaji kuondoka Ni uchaguzi wa mantiki kulingana na hali ya sasa ya mchezaji huyo katika kikosi cha Manchester United. Mchezaji huyo kutoka Armenia ameachwa mechi nane za mwisho na Mourinho huku akisema kuwa haamini kama kiungo huyo anastahilo kukukaa katika...

TUPAC SHAKUR ALIBAKWA JELA !!!

             Ulimwengu wa filamu za Hollywood na muziki wa Hip Hop juzi ulipatwa na mshangao baada ya mtayarishaji wa filamu inayohusu maisha ya hayati Tupac Shakur ,L.T Hutton kuelezea sababu zilizomfanya kumbadilisha muongozaji wa filamu hiyo kutoka John Singleton na kumuweka muongozaji Benny "Boom" Douglas.  Filamu hiyo inayoitwa "all eyez on me" tayari imekwisha andaliwa na inatarajiwa kuzinduliwa leo tarehe 16 Juni 2017.       Akizungumza kwenye mahojiano redioni L.T Hutton amewashtusha watu wengi baada ya kudai kwamba walishindwana na muongozaji wa mwanzo bwana John Singleton sababu muongozaji huyo aling'ang'ania kuwepo kwa matukio (scene) ambazo kwa maoni yake zisingependeza.        Matukio ambayo John Singleton alipenda yawepo katika filamu hiyo ni pamoja na kutaka filamu hiyo ianze na scene ya Tupac akilazimisha kumlawiti msichana wa kizungu.!!!          Singleton pia ali...

ORODHA YA NCHI 80 AMBAZO MTANZANIA ANARUHUSIWA KUINGIA BILA VIZA.

         Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni amesema kuna zaidi ya nchi 80 ambazo watanzania wanaweza kusafiri bila ya kuwa na viza . Mhandisi Hamad Masauni amesema kuna zaidi ya nchi 80 ambazo watanzania wanaweza kusafiri bila ya kuwa na viza za kusafiria kama ilivyokuwa nchi za afrika Mashariki. Mhandisi Massauni amebainisha hayo leo bungeni wakati akijibu swali la Mbunge wa Mlalo kupitia tiketi ya CCM Rashid Shangazi aliyetaka kujua ni nchi ngapi ambazo watanzania wanaweza kusafiri bila ya kuwa na viza (viza on arrival). "Zipo nchi 16 kwa Afrika ambazo watanzania wanaweza kuzitembelea bila ya kuwa na viza na duniani zipo 67" alisema Masauni. Aidha Massauni amezitaja nchi hizo kuwa ni Benin, Burkina Faso, Cape Verde, Ivory Coast, Djibouti, Gabon, Gambia, Guinea, Guinea­Bissau, Liberia, Mali, Mauritania, Niger, Sierra Leone pamoja na Togo. Pamoja na hayo Masauni amesema...

"BUREAU DE CHANGE" ZOTE TANZANIA KUFUTIWA LESENI.

BENKI Kuu ya Tanzania (BoT) imetoa waraka kwa wafanyabiashara wa maduka ya kuuza na kununua fedha za kigeni kuomba upya leseni kwa ajili ya kufanya biashara hiyo. Leseni zote za maduka ya kubadilisha fedha za kigeni zitafutwa ifikapo Septemba 2, mwaka huu ili wamiliki waombe upya. Hayo yalisemwa jana na Ofisa Msimamizi Maduka ya Kuuza na Kununua Fedha za Kigeni wa Benki Kuu ya Tanzania, Kanuti Mosha kwenye Maonesho ya 41 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (DITF) yanayoendelea kwenye Viwanja vya Mwalimu Nyerere, Barabara ya Kilwa, Temeke jijini Dar es Salaam. Mosha alisema kwa sheria ya sasa, mfanyabiashara atatakiwa kumiliki duka moja tu tofauti na ilivyokuwa awali mtu mmoja anaweza kumiliki maduka hata matano. Alisema sambamba na kutoa leseni upya, BoT imeweka viwango vipya vya mtaji ambavyo vinaanzia Sh milioni 100 hadi 300 kwa daraja A, na kuanzia Sh milioni 250 hadi Sh bilioni moja kwa daraja B na Amana ya Thamani kuanzia Dola za Marekani milioni 50 hadi milioni 100. A...