Skip to main content

NDEGE YA TANZANIA KUPIGWA MNADA CANADA.




IMEANDIKWA NA MALISA GJ :

Tundu Lissu ameeleza kuwa ni kweli ndege aina ya 'Bombadier Dash Q400' mali ya shirika la ndege la ATCL imeshikiliwa huko nchini Canada na kampuni moja ya Ujenzi ijulikanayo kama Stirling Civil Engineering Ltd kutokana na kuidai serikali ya tanzania kiasi cha USD 38M (Takribani TZS 87BL). Kampuni hiyo imetishia kuipiga "mnada" ndege hiyo kufidia deni lao, ikiwa serikali ya Tanzania haitawalipa.

KWANINI NDEGE YETU IMEKAMATWA?

Mwaka 2009 kampuni Stirling Civil Engineering Ltd, ilikupewa kandarasi ya kutengeneza Barabara ya Wazo Hill – Bagamoyo. Kabla ya kukamilisha kandarasi hiyo, aliyekuwa Waziri wa ujenzi wakati huo alivunja mikataba bila kuzingatia sheria, na kuinyang'anya kampuni hiyo kandarasi hiyo na kuagiza kampuni hiyo kutimuliwa nchini.

Kampuni ya Stirling Civil Engineering Ltd, ilifungua kesi katika mahakama ya kimataifa ya usuluhishi mjini Paris. Tarehe 10 Desemba, 2009 mahakama hiyo iliipa ushindi kampuni hiyo na kuagiza serikali ya Tanzania kuilipa takriban dola za Marekani milioni 25 (Takribani TZS 40BL kwa wakati huo).

Serikali ya Tanzania ilikata rufaa, lakini ikaangukia pua kwenye hukumu ya tarehe 10 Juni, 2010 ambapo mahakama hiyo iliagiza Tanzania ilipe fedha hiyo pamoja na riba ya 8% kila mwaka hadi malipo kamili yatakapofanyika. Tuzo hiyo imesajiliwa na kutambuliwa kama deni halali la Serikali ya Tanzania kwa Stirling Civil Engineering Ltd.

Lakini serikali ilikataa kulipa deni hilo, licha ya jitihada mbalimbali zilizofanywa na kampuni hiyo. Kutokana na ucheleweshaji wa malipo, deni hilo limeongezeka hadi dola za Marekani 38.7M kufikia tarehe 30 Juni, 2017.

Hapo ndipo Stirling Civil Engineering Ltd. ilipoamua kuomba amri ya Mahakama Kuu ya Montreal ya kukamata mali zote za serikali ya Tanzania zilizopo nchini Canada zikijumuisha ndege ya Bombardier Q400. Mahakama ilitoa kibali na ndege hiyo kukamatwa.

SERIKALI IMECHUKUA HATUA GANI?

Kwa mujibu wa Mhe.Tundu Lissu serikali iliomba mazungumzo na kampuni ya Stirling Civil Engineering Ltd ili kutatua tatizo hilo. Katika mazungumzo hayo ambapo serikali ya Tanzania iliwakilishwa na Waziri wa mambo ya nje Balozi Augustine Mahiga, aliomba kampuni hiyo kuepuka suala hilo kujulikana hadharani.

Kwa upande wake, kampuni ya Stirling Civil Engineering Ltd. imekubali kuiachia ndege ya Bombardier Q400 kwa malipo ya mwanzo ya dola za Marekani milioni 12.5 (Takribani TZS 30B) na baadae itatuma ujumbe wake Tanzania kwa ajili ya kuja kufanya makubaliano ya mwisho juu ya kulipa deni hilo. Endapo malipo hayo yatafanywa na Serikali, Stirling Civil Engineering Ltd, itasitisha mpango wake wa kuipiga mnada ndege yetu ya Bombardier Q400. Ikiwa serikali itashindwa kutimiza makubaliano hayo basi ndege hiyo itapigwa mnada.

Wakati huohuo kampuni ya uchimbaji madini ya ACACIA Mining imetoa notisi ya kuishitaki Serikali ili kudai fidia ya Dola za Marekani bilioni 2 (Takribani TZS Trilioni 5) kwa kukamata mchanga wake wa dhahabu, kinyume na sheria na mkataba wa uchimbaji madini waliosani na serikali.

Kampuni hiyo imetoa tishio hilo wakati mazungumzo yakiendelea kati yake na serikali juu ya hatma ya mchanga huo wa dhahabu maarufu kama makinikia. Ikiwa Accacia watafanyia kazi notisi hiyo, Tanzania itaburuzwa tena kwenye mahakama ya usuluhishi ya kimataifa, na kutakiwa kulipa Trilioni 5 kwa Accacia.

Nini maoni yako?

CHANZO:
https://m.facebook.com/story.php?story_fbid=1478370308921323&id=100002451047207

Comments

Habari Nyingine Kutoka Kioo17 Swahili;

WASTANI WA ADA ZA VYUO VIKUU BORA ZAIDI DUNIANI.

            Elimu ya juu ya kupokea nje ya nchi (Nchi zilzo endelea) daima imekuwa kiwango cha kutambuliwa sana, na wanafunzi kutoka duniani kote siku zote wana ndoto kuhusu hilo.             Tovuti ya Bright Side imeamua kujua gharama za sasa za kujifunza * kwa wanafunzi wa kimataifa katika vyuo vikuu vya juu vya dunia, na tungependa kushiriki habari hii na wewe. * Wastani wa kila mwaka ada ya mafunzo ya shahada ya kwanza ; MAREKANI; Kwa maelezo zaidi kuhusiana na chuo hiki bonyeza hapa: http://www.harvard.edu/ Kwa maelezo zaidi kuhusiana na chuo hiki bonyeza hapa:  http://web.mit.edu/ UINGEREZA;     Kwa maelezo zaidi kuhusiana na chuo hiki bonyeza hapa; http://www.cam.ac.uk/     Kwa maelezo zaidi kuhusiana na chuo hiki bonyeza hapa: http://www.ox.ac.uk/ USWISI (SWITZERLAND ):     Kwa maelezo zaidi kuhusiana na chuo hiki bonyeza hapa:...

ORODHA YA NCHI ZA KWANZA NA ZA MWISHO KWA AMANI DUNIANI.

Marekani:  Ripoti ya Taasisi ya Uchumi na Amani imepata mataifa kumi tu ulimwenguni ambayo hayapo katika vita na migogoro kabisa. Kwa mujibu wa Ripoti ya Kimataifa ya Amani 2016, Botswana, Chile, Costa Rica, Japan, Mauritius, Panama, Qatar, Uswisi, Uruguay na Vietnam ndio nchi pekee ambazo hazipo kwenye vita wala migogoro yeyote ile ya kuhatarisha amani.. Iceland inaongoza orodha ya nchi zinazoongoza kwa amani ulimwenguni, ikifuatiwa na Denmark, Austria, New Zealand, Ureno, Jamhuri ya Czech, Uswisi, Canada, Japan na Slovenia - wakati Marekani ikiwa kwenye nafasi ya 103. Palestina imepanda kutoka nafasi ya 163 mpaka nafasi ya 148. Syria iliyoharibiwa na vita imewekwa chini ya orodha, chini kuliko Sudan Kusini, Iraq, Afghanistan, Somalia, Yemen, Jamhuri ya Afrika ya Kati, Ukraine, Sudan na Libya. "Ripoti inalinganisha amani duniani kwa kutumia mandhari tatu pana: hali ya utulivu na usalama katika jamii; kiwango cha mgogoro wa ndani au wa kimataifa; na kiwango cha kije...

WAZIRI WA MAMBO YA NJE WA GAMBIA AMTAKA RAIS WA TOGO KUACHIA MADARAKA KWA HIARI.

RAIS WA TOGO, FAURE GNASSINGBE. BANJUL, Oktoba 23 (Reuters) "Rais wa Togo Faure Gnassingbe anapaswa kujiuzulu mara moja na Umoja wa Afrika na kanda ya kikanda ya Afrika Magharibi ECOWAS inapaswa kumshawishi kushuka ikiwa hawaja fanya hivyo",  Waziri wa Mambo ya Nje wa Gambia Ousainou Darboe amesema. Maoni ya Darboe ni ishara ya mwanzo kwamba yuko dhidi ya Gnassingbe ambaye alinyakua madaraka kwa nguvu mwaka 2005 baada ya kifo cha baba yake ambaye alikuwa ametawala tangu mwaka 1967. Togo ni inakabiliwa na mgogoro wa kisiasa ambao takribani watu 10 wameuawa katika maandamano tangu Agosti. "Nadhani Umoja wa Afrika na ECOWAS inapaswa kushiriki na kumshawishi rais wa Togo kung'ooka ," Darboe aliiambia Shirika la habari la Uingereza (Reuters) mwishoni mwa wiki hii, akiongezea kuwa nchi nyingine zinahitaji kushiriki. "Wakati serikali ya Togo inakiuka kanuni zinazokubalika sidhani kama suala hili linapaswa kuchukuliwa kama ni mambo ya ndani ya nd...

SABABU YA ZIPU NYINGI KUWA NA HERUFI "YKK".

Ikiwa umewahi kuchunguza kwa ukaribu zipu kwenye nguo zako nyingi, utakua tayari umeona herufi zinazosomeka "YKK," katika herufi kubwa, kwa mengi yao.Herufi hizi zipo kwenye kila kitu kutoka kwenye nguo za jeans, makoti hata kwenye mabegi. Herufi hizo zinasimama kwa niaba ya "Yoshida Kogyo Kabushikikaisha" ambayo, kutoka kwenye lugha ya Kijapani, inaelezea  "Yoshida Company Limited" yaani "Kampuni ya Yoshida"  Kampuni hii ni ya mtengenezaji wa zipu aitwaye Tadao Yoshida, ambaye aliianzisha mwaka wa 1934. Kwa wastani, kampuni hiyo inatengeneza nusu ya zipu duniani, ambayo ni zaidi ya zipu bilioni 7 kila mwaka. Kwa uhalisia Yoshida hakua mvumbuzi wa zipu duniani, zipu zilivumbuliwa na Mmarekani, Whitcomb L. Judson, miaka ya 1890.  Kampuni yake sasa ipo,  na inabuni na kutengeneza zipu za kisasa ikijulikana kama Talon, Inc. Bidhaa za kampuni hiyo hutumiwa makampuni kama Brooks Brothers na Uniqlo. Lakini YKK ina sifa isiyofananishik...

UGANDA IMEWAFUKUZA WATAALAM WA KIJESHI KUTOKA KOREA YA KASKAZINI.

Uganda imefukuza wataalamu wa kijeshi wa Korea Kaskazini na wawakilishi wa makampuni ya Kaskazini ya Korea, ikiwa ni pamoja na mfanyabiashara wake mkubwa wa silaha za juu kutokana na mataifa ya Kiafrika kukabiliwa na shinikizo la kuzingatia vikwazo vya Umoja wa Mataifa(UN) juu ya mpango wa silaha za nyuklia wa Pyongyang. "Raia wa Korea ya Kaskazini waliobaki katika taifa hilo la Afrika Mashariki ni wanadiplomasia na watu binafsi tu ", Okello Oryem, naibu waziri wa mambo ya kigeni, aliiambia The Associated Press. "Tunafuatana kabisa," alisema Oryem, akiongezea kwamba Uganda ina uhusiano wa kawaida wa kidiplomasia na Korea Kaskazini. Uganda hasa ilidai kuondoka kwa watu wanaowakilisha Shirika la Biashara la Maendeleo ya Madini ya Korea. Ni mkataba wa msingi wa Korea Kaskazini na chini ya vikwazo vya U.N. na U.S. Uhamisho huo unaashiria mabadiliko ya sera kwa serikali ya Uganda, ambayo hapo awali ilikuwa na mahusiano ya mazuri na Pyongyang. Korea ya Kaska...

PAPA FRANCIS ASHINDANISHWA NA PABLO ESCOBAR KWA KUHESHIMIWA NCHINI COLOMBIA.

MedellĂ­n (Colombia) (AFP):  Katika saluni yake ya nywele, Yamile Zapata anatumia faida ya ziara ya Papa Francis ili kuuza pete za funguo zenye picha ya kiongozi huyo wa kanisa katoliki duniani. Lakini anadai sio ambapo pesa halisi iko kwenye mji wa Medellin nchini Colombia. Zawadi nyingi anazouza katika mji huu wa Colombia hubeba uso wa "mtakatifu" na shujaa wake mwenyewe: Pablo Escobar. Wakati Francis alikuwa akihudumia na kufundisha kama kuhani wa Yesuit katika miaka ya 1980, Escobar alikuwa akiua mamia ya watu na kufanya biashara ya madawa ya kulevya ya mabilioni ya dola za kimarekani. "Kila mtu anataka picha za papa sasa, lakini picha za Pablo zinauzika vizuri zaidi," , alisema Zapata, mwenye umri wa miaka 34, wakati ambao jiji hilo limeandaliwa kwa ajili ya mkutano wa Papa Francis wa wazi siku ya Jumamosi. PETE ZA FUNGUO ZENYE PICHA ZA PAPA FRANCIS NA PABLO ESCOBAR ZIKIWA ZINAUZWA KWENYE MITAA YA JIJI LA MEDELIN, COLOMBIA. Francis alitoa mane...

MCHEZAJI WA ZAMANI WA UINGEREZA AMESEMA ALICHEZA NA WACHEZAJI WATATU MASHOGA KWENYE TIMU.

Carl Hoefkens (jezi no.2) alichezea West Bromwich Albion na Stoke City wakati wa enzi zake ligi kuu ya England. Beki wa zamani wa Ligi Kuu ya Uingereza amesema alicheza pamoja na wachezaji wenzake wawili wa mashoga ndani ya timu, na mmoja alikua na jina kubwa. Carl Hoefkens, West Bromwich Albion na Stoke City siku za nyuma, anasema wachezaji hao walikua wazi na hawakujificha kwenye vyumba vya kubadilishia nguo ingawa bado hawajulikani kwasababu ya maombi yao wenyewe ya kuomba kutotangazwa. Justin Fashanu, ambaye alijiua mwaka 1998, alikuwa mchezaji wa mwisho wa kazi nchini England kuja nje kama mashoga - mwaka 1990. Hoefkens alipokua (kushoto), alipokua anachezea Stock  City. Hoefkens aliyecheza Uingereza kwa miaka minne, akiondoka mwaka 2009, alidai kuwa mchezaji mwenzake mmoja wa timu alikua anaweza kuja kwenye uwanja wa mafunzo ya klabu na mpenzi wake wa kiume  lakini aliwaomba wenzake kutokuwaambia watu wangine wa nje ya timu. 'Nilicheza pamoja n...