Skip to main content

MTOTO WA MOHAMMED ALI HANA HATA ELA YA KULA.

MOHAMMED ALI JR UTOTONI AKIWA NA HAYATI BABA YAKE BONDIA MOHAMMED ALI.

         Muda mfupi baada ya Kufariki kwa bingwa wa zamani wa dunia wa ngumi za uzito wa juu Mohammed Ali, kulitokea habari za kushtusha za mtoto wake aliedaiwa kua ametelekezwa na na familia aitwae Mohammed Ali Jr.

MOHAMMED ALI JR.


       Mtoto huyo wa pekee wa kiume aliyechukua jina la hayati baba yake (Mohammed Ali) ,alikutwa akiishi maisha ya kifukara kupindukia huko kusini mwa jiji la Chicago, Illinois,Marekani.
      Mohammed Ali jr mwenye umri wa miaka 45 ,ni mtoto wa mke wa kwanza wa hayati Mohammed Ali ,Khalilah Ali ,ambae kuna wakati aliwahi kusikika akidai kwamba mtoto huyo alianza kuathirika kisaikolojia tangu utoto baada ya kuanza kuishi mbali na baba yake.
HAYATI MOHAMMED ALI AKIWA NA MKE WAKE WA KWANZA ,KHALILAH ALI NA WATOTO WAO MARYUM, JAMILLA, RASHEDA NA MOHAMMED ALI JR.

       Kwenye mahojiano yalifanyika miaka miwili iyopita,Mohammed Ali Jr alisema kwamba alikua hajali kinacho endelea kwa baba yake sababu akili yake yote ilikua ni kwenye kuhangaikia maisha yake pekee ambayo yalikua duni sana.
       Aliongeza kusema kwamba ufa katikati yake na baba yake ulianza wakati baba yake alipo achana na mama yake na kuoa mke wake wa pili aliejulikana kama Veronica Porche.
HAYATI MOHAMMED ALI AKIWA NA MKE WAKE WA PILI, VERONICA PORCHE.

       "...Hali ilikua mbaya zaidi pale baba alipo amua kuoa mke wa tatu ,Lonnie ,...Lonnie alikua na wivu na mahusiano yetu kwakua hakua na watoto..."
  - Mohammed Ali Jr .


HAYATI MOHAMMED ALI AKIWA NA MKE WAKE WA TATU ,YORANDA WILLIAMS "LONNIE".
         
            Pamoja na ripoti zilizopo kudai kwamba Hayati Mohammed Ali aliacha mali zenye thamani ya dola za kimarekani milioni themanini ($80 million) sawa na shilingi za kitanzania bilioni 170, Mtoto huyo amedai kwamba yeye mpaka sasa ameshapewa dola elfu saba miatano tena kwa mafungu ,yaani dola elfu mbili miatano kwa vipindi vitatu tofauti.
        
      Pia Mohammed Ali Jr ambae ana mke na watoto wawili anasema hana hata ela ya kula, hana akaunti ya benki na hana hata sehemu yake ya kulala ndio maana sasa analala sakafuni nyumbani kwa rafiki yake huko Fort Lauderdale,Frolida.
MOHAMMED ALI JR AKIWA NA MKE NA WATOTO WAKE.

     Pamoja na malalamiko hayo ya Ali Jr, Tarehe 23 Julai 2016, tovuti ya dailymail.com iliwahi kuripoti jinsi Mohammed Ali Jr alivyo telekeza familia yake ya mke (Shakira) na watoto wawili Ameera (mwenye miaka nane) na Shakera (miaka saba) na kwenda kuishi maisha ya kifahari kwenye maeneo ya kitajiri karibu na Midway Airport baada ya kupata gawio lake kutoka kwenye urithi wa dola milioni themanini walizoachiwa na hayati baba yake.

        Kwa upande mwingine, mwezi Januari mwaka huu (2017) ,Binti mkubwa wa Hayati Mohammed Ali, Maryum Ali, ambaye ni dada yake na Mohammed Ali Jr, alisema kwamba wao kama watoto wote wa marehemu pamoja na mama yao wa kufikia "Lonnie" ,wanaishi kwa upendo sana na hakuna mvutano wowote wa kugombea mali zilizo achwa na marehemu.

VYANZO; bet.com
                  Dailymail.com

Comments

Habari Nyingine Kutoka Kioo17 Swahili;

ORODHA YA NCHI 80 AMBAZO MTANZANIA ANARUHUSIWA KUINGIA BILA VIZA.

         Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni amesema kuna zaidi ya nchi 80 ambazo watanzania wanaweza kusafiri bila ya kuwa na viza . Mhandisi Hamad Masauni amesema kuna zaidi ya nchi 80 ambazo watanzania wanaweza kusafiri bila ya kuwa na viza za kusafiria kama ilivyokuwa nchi za afrika Mashariki. Mhandisi Massauni amebainisha hayo leo bungeni wakati akijibu swali la Mbunge wa Mlalo kupitia tiketi ya CCM Rashid Shangazi aliyetaka kujua ni nchi ngapi ambazo watanzania wanaweza kusafiri bila ya kuwa na viza (viza on arrival). "Zipo nchi 16 kwa Afrika ambazo watanzania wanaweza kuzitembelea bila ya kuwa na viza na duniani zipo 67" alisema Masauni. Aidha Massauni amezitaja nchi hizo kuwa ni Benin, Burkina Faso, Cape Verde, Ivory Coast, Djibouti, Gabon, Gambia, Guinea, Guinea­Bissau, Liberia, Mali, Mauritania, Niger, Sierra Leone pamoja na Togo. Pamoja na hayo Masauni amesema...

ODINGA NA HASSAN JOHO WALIMTUMIA ALI KIBA NDEGE BINAFSI..

Imebainika kwamba mgombea wa uraisi wa Kenya kupitia muungano wa NASA pamoja na gavana wa Mombasa Hassan Joho walituma ndege binafsi kumchukua muimbaji wa Tanzania Ali Kiba ili kusherekea kutenguliwa kwa matokeo ya uchaguzi wa uraisi nchini humo juma lililopita. Meneja wa Ali Kiba , Aidan Seif, alithibitisha kwamba Odinga alituma ndege hiyo siku ya ijumaa ili Ali Kiba ajumuike nao katika kusherekea. Chanzo kililiambia gazeti la Tanzania kwamba"upinzani wa Kenya unakubali msaada wa Kiba .Muungano wa NASA unaamini Kiba alisaidia sana katika kampeni zao kabla ya uchaguzi mkuu wa Agosti 8. Walituma ndege ya kibinafsi, ambayo ilimchukua mwishoni mwa Ijumaa. " Odinga, Joho na Kiba wanauhusiano wa karibu sana na mara kwa mara Ali Kiba alionekana akiwapigia kampeni wanasiasa hao wa Kenya majukwaani CHANZO: edaily.co.ke

TRUMP NA KIM JONG-UN FEKI WAHUBIRI AMANI KATIKA SHEREHE ZA UZINDUZI WA OLIMPIKI.

Waigaji wa Rais wa Marekani Donald Trump na kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong-un walikua wakihubiri amani katika sherehe za uzinduzi wa michezo ya Olympiki kwa majira ya baridi(Winter Olympic) jijini Pyeong Chang, Korea ya Kaskazini kabla ya kutolewa nje na wanausalama. Watu hao walionekana kwa muda mfupi katika jukwaa la uwanja huo mkuu wa Pyeongchang, Korea Kusini ili kuwasalimu watu. Waigaji hao ambao wote walikataa kutoa majina yao halisi - walikuja kwenye sherehe ya ufunguzi -   "kuonyesha dunia, hii ndio amani inaweza kuonekana kama viongozi hao wawili watakapokutana,"  alisema Kim bandia. Trump bandia alimwiga Rais Trump kwa kuvaa kofia nyekundu ya mpira wa magongo (baseball), lakini ikiwa imeandikwa "USA" sio "Make America Great again"(Unda Amerika Kuu tena) kauli mbiu ambayo mara nyingi huandikwa kwenye mavazi na matangazo ya Trump. Pia alivaa tai ndefu ya rangi nyekundu kama ambavyo rais Trump mwenyewe hupendele...

WAZIRI GEORGE SIMBACHAWENE AJIUZULU.

Waziri wa TAMISEMI George Simbachawene ametangaza kujiuzulu nafasi yake kutokana na kutajwa kwenye ripoti za uchunguzi wa tanzanite na almasi. Akiwasilisha ripoti yake kwa Waziri Mkuu Bungeni Dodoma, Mwenyekiti wa Kamati Maalumu ya Bunge iliyoundwa kuchunguza biashara ya madini ya tanzanite, Dotto Biteko, alisema Simbachawene aulizwe ni kwa nini alitoa uhamisho wa hisa za Sky Associate bila kuhusisha wataalamu kwa sababu kamati ilishindwa kuelewa ni kwa nini alifanya hivyo. “Kwa muktadha huo, ridhaa iliyotolewa Januari 30, mwaka 2015 na aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini wa wakati huo, George Simbachawene, ina dosari za kisheria na ukiukwaji wa kiutendaji na utoaji wa ridhaa hii, unainyima Stamico kipaumbele cha kununua Kampuni ya TML. “Kwa msingi huo, kamati imebaini dosari zilizofanywa za kubadilisha watoa maamuzi wa Kampuni ya TLM, zilifanyiwa kazi katika ngazi ya Wizara ya Nishati na Madini chini ya Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Kamishna wa Nishati na Madini na idara za sher...

ORODHA YA NCHI ZA KWANZA NA ZA MWISHO KWA AMANI DUNIANI.

Marekani:  Ripoti ya Taasisi ya Uchumi na Amani imepata mataifa kumi tu ulimwenguni ambayo hayapo katika vita na migogoro kabisa. Kwa mujibu wa Ripoti ya Kimataifa ya Amani 2016, Botswana, Chile, Costa Rica, Japan, Mauritius, Panama, Qatar, Uswisi, Uruguay na Vietnam ndio nchi pekee ambazo hazipo kwenye vita wala migogoro yeyote ile ya kuhatarisha amani.. Iceland inaongoza orodha ya nchi zinazoongoza kwa amani ulimwenguni, ikifuatiwa na Denmark, Austria, New Zealand, Ureno, Jamhuri ya Czech, Uswisi, Canada, Japan na Slovenia - wakati Marekani ikiwa kwenye nafasi ya 103. Palestina imepanda kutoka nafasi ya 163 mpaka nafasi ya 148. Syria iliyoharibiwa na vita imewekwa chini ya orodha, chini kuliko Sudan Kusini, Iraq, Afghanistan, Somalia, Yemen, Jamhuri ya Afrika ya Kati, Ukraine, Sudan na Libya. "Ripoti inalinganisha amani duniani kwa kutumia mandhari tatu pana: hali ya utulivu na usalama katika jamii; kiwango cha mgogoro wa ndani au wa kimataifa; na kiwango cha kije...

"GIGGS HAFAI KUWA KOCHA WA TIMU YA TAIFA", BABA YAKE ANASEMA...!!!

Ryan Giggs. Chama cha Soka cha Wales (FAW) siku ya jumatatu kilitangaza kumchagua winga wa zamani wa Manchester United Ryan Giggs kama kocha wa timu yao ya taifa kwa mkataba wa miaka minne. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 44 anachukua kazi iyoachwa na Chris Coleman, ambaye aliiongoza Wales kwenye nusu fainali za Euro 2016 lakini aliacha kazi mwezi Novemba ili kuchukua nafasi ya kuifundisha timu ya Sunderland ya ligi kuu ya Uingereza. Giggs alisema kuwa anajivunia kwa kupewa kazi hiyo na pamoja na changamoto iliyo mbele yake baada ya Wales kushindwa kufuzu kucheza fainali za Kombe la Dunia mwaka huu nchini Urusi na sasa wanazingatia michuano ya Ulaya ya 2020. "Siwezi kusubiri kuanza kufanya kazi na wachezaji tunapojiandaa kwa ajili ya michezo muhimu baadaye mwaka huu," alisema. Lakini baba mzazi wa Giggs, Danny Wilson ana maoni  tofauti sana...!!! Anakiri kwamba mwanae anamtia aibu na anasema hastahili kuchukua kazi hiyo ya ukocha wa timu ya t...

MCHEZAJI WA ZAMANI WA UINGEREZA AMESEMA ALICHEZA NA WACHEZAJI WATATU MASHOGA KWENYE TIMU.

Carl Hoefkens (jezi no.2) alichezea West Bromwich Albion na Stoke City wakati wa enzi zake ligi kuu ya England. Beki wa zamani wa Ligi Kuu ya Uingereza amesema alicheza pamoja na wachezaji wenzake wawili wa mashoga ndani ya timu, na mmoja alikua na jina kubwa. Carl Hoefkens, West Bromwich Albion na Stoke City siku za nyuma, anasema wachezaji hao walikua wazi na hawakujificha kwenye vyumba vya kubadilishia nguo ingawa bado hawajulikani kwasababu ya maombi yao wenyewe ya kuomba kutotangazwa. Justin Fashanu, ambaye alijiua mwaka 1998, alikuwa mchezaji wa mwisho wa kazi nchini England kuja nje kama mashoga - mwaka 1990. Hoefkens alipokua (kushoto), alipokua anachezea Stock  City. Hoefkens aliyecheza Uingereza kwa miaka minne, akiondoka mwaka 2009, alidai kuwa mchezaji mwenzake mmoja wa timu alikua anaweza kuja kwenye uwanja wa mafunzo ya klabu na mpenzi wake wa kiume  lakini aliwaomba wenzake kutokuwaambia watu wangine wa nje ya timu. 'Nilicheza pamoja n...