Skip to main content

MAJIBU YA FREDRICK WEREMA KUHUSU KUMUITA KAFULILA "TUMBILI".


FREDRICK WEREMA.



               Dar es Salaam. Mjadala mkali wa sakata la uchotwaji fedha kutoka Akaunti ya Tegeta Escrow ulisababisha aliyekuwa Mwanasheria Mkuu, Jaji Fredrick Werema kutumia msemo unaomtaja tumbili wakati akimjibu mbunge wa zamani wa Kigoma Kusini, David Kafulila.
Werema alijitokeza jana kufafanua kuhusu kauli yake, lakini mjadala huo wakati huo ulikuwa na matamko tofauti wakati joto bungeni lilipozidi, likigawa wabunge na hata viongozi wa Serikali.
Katika hotuba yake akiwa jimbo la Kigoma Kusini juzi, Rais John Magufuli alifufua tena mjadala huo wakati alipompongeza “kwa dhati” Kafulila kwa uzalendo wake wa kuibua kashfa hiyo iliyohusu Sh306 bilioni na kusimamia kutetea hoja yake hadi mwisho.
Rais alisema Kafulila alipata shida hadi baadhi walimuita tumbili, neno lililotamkwa na Werema wakati akijibu mwongozo wa mbunge huyo wa Kigoma Kusini, na kwamba waliomuita hivyo sasa wamegeuka tumbili.
“Lazima niwe mkweli na nisiposema hapa nitakuwa sijaitendea haki nafsi yangu, siku zote ukweli utabaki kuwa ukweli tu na ndiyo maana nampongeza Kafulila kwa sababu alisimama imara kupigania maslahi ya umma. Alionyesha uzalendo wa hali ya juu unaopaswa kuigwa na kila mmoja wetu,” alisema Rais.
Jana, Werema alimwambia mwandishi wetu kuwa alisema neno hilo kama msemo wa Kiswahili. Mwandishi wetu alipomuuliza kuhusu kauli ya Rais juzi, Jaji Werema alijibu:
Jaji Werema: Sasa unataka nifanyeje?
Mwandishi: Tunahitaji maoni yako kuhusu kauli hii.
Jaji Werema: Hilo jambo si liko mahakamani? Tunaweza kushtakiwa, wako mahakamani?
Mwandishi: Sawa. Lakini kwa kipindi kile kati ya watu ambao walimuita Kafulila tumbili, wewe ni mmoja wao.
Jaji Werema: Unajua wengi walishindwa kuelewa nilisema nini, mimi nilichokizungumza ni kwamba tumbili haamui mambo ya msituni, na huo ni msemo wa kawaida tu.
Kafulila, ambaye alikuwa mbunge wa Kigoma Kusini kuanzia 2010 hadi 2015 kwa tiketi ya NCCR-Mageuzi, aliibua kashfa hiyo bungeni baada ya kuisoma katika gazeti la The Citizen mwaka 2014.
Kwenye sakata hilo jumla ya Sh306 bilioni zilichotwa kutoka akaunti hiyo iliyofunguliwa kwa pamoja na Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) na kampuni ya kufua umeme ya IPTL baada ya kutokukubaliana katika tozo ya uwekezaji.
Baada ya Kafulila kuanzisha mjadala huo, Bunge liliagiza Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kufanya ukaguzi na taarifa yake ilitumiwa na chombo hicho cha kuisimamia Serikali kujadili kwa kina uchotwaji wa fedha hizo.
Licha ya kwamba wabunge wa CCM waliungana na upinzani katika sakata hilo, mjadala ulitawaliwa na mihemko na ushabiki na haikuwa ajabu kwa Werema kujikuta akitoa kauli hiyo.
Kila mbunge aliyesimama kutaka hatua zichukuliwe dhidi ya wote waliohusika, ukumbi ulikaa kimya kusikiliza lakini aliposimama mbunge aliyetetea kuwa fedha za escrow hazikuwa za umma kulikuwa na kelele za kumpinga na za kumshangilia, kiasi cha kulazimisha kiti cha spika kutuliza hali kila wakati.
Wakati Bunge lilipofikia kuweka maazimio, kikao kilifanyika hadi saa 5:00 usiku bila ya kufikia muafaka na kulazimika kuahirisha hadi siku iliyofuata kutoa nafasi kwa wabunge kujadiliana maazimio.
Miongoni mwa hoja zilizotolewa kukuza tatizo hilo ni zile zilizotolewa na mbunge wa zamani wa Nkenge (CCM), Assumpter Mshama, ambaye alidai kuna watu wengine waliopewa fedha wakiwa Mombasa nchini Kenya, na kumtaja mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe kuwa mmojawao.
“Hata mheshimiwa Mbowe amediriki kutajwa kwamba alipokea pesa kule Mombasa, lakini humu hakuna taarifa zake. Taarifa za benki ya Stanbic hatujasikia taarifa zake, lakini wanaojulikana wamepata pesa ni wa CCM. Ndio maana tunasema hata kama hiyo kamati ya PAC,” alisema huku sauti ikitaka kutoa taarifa.
Mshama alitakiwa atoe ushahidi kuwa Mbowe alitoa fedha lakini alishindwa na baadaye kufuta kauli yake.
Mwingine aliyetetea kuwa fedha hizo hazikuwa za Serikali ni mbunge wa Magomeni (CCM), Mohamed Chombo aliyewatuhumu walioshupalia suala hilo kuwa walikuwa na uchu wa madaraka.
“Sasa hivi, VIP imenunuliwa na PAP. Inabidi yeye-- kwa maana ya PAP-- alipe fedha zake za hisa parcent (asilimia) 30. Fedha hizi baada ya kutoka, PAP inabidi amlipe VIP. Sasa ndugu yangu nataka niwaambie--sasa nataka kuja kwenye ile ashki majinuni ni nani,” alisema.
“Kuna watu ambao maisha yao yote, wao ni watu wenye ashki. Ashki ni hamu ya kutaka na wao wapate kila wanachokipata wengine. Kuna watu wana ashki ya kupata madaraka haya.”

CHANZO ;
http://www.mwananchi.co.tz/habari/Aliyemuita-Kafulila-tumbili-afafanua/1597578-4030898-g5oxnnz/index.html

Comments

Habari Nyingine Kutoka Kioo17 Swahili;

MCHEZAJI WA ZAMANI WA UINGEREZA AMESEMA ALICHEZA NA WACHEZAJI WATATU MASHOGA KWENYE TIMU.

Carl Hoefkens (jezi no.2) alichezea West Bromwich Albion na Stoke City wakati wa enzi zake ligi kuu ya England. Beki wa zamani wa Ligi Kuu ya Uingereza amesema alicheza pamoja na wachezaji wenzake wawili wa mashoga ndani ya timu, na mmoja alikua na jina kubwa. Carl Hoefkens, West Bromwich Albion na Stoke City siku za nyuma, anasema wachezaji hao walikua wazi na hawakujificha kwenye vyumba vya kubadilishia nguo ingawa bado hawajulikani kwasababu ya maombi yao wenyewe ya kuomba kutotangazwa. Justin Fashanu, ambaye alijiua mwaka 1998, alikuwa mchezaji wa mwisho wa kazi nchini England kuja nje kama mashoga - mwaka 1990. Hoefkens alipokua (kushoto), alipokua anachezea Stock  City. Hoefkens aliyecheza Uingereza kwa miaka minne, akiondoka mwaka 2009, alidai kuwa mchezaji mwenzake mmoja wa timu alikua anaweza kuja kwenye uwanja wa mafunzo ya klabu na mpenzi wake wa kiume  lakini aliwaomba wenzake kutokuwaambia watu wangine wa nje ya timu. 'Nilicheza pamoja n...

ORODHA YA NCHI ZA KWANZA NA ZA MWISHO KWA AMANI DUNIANI.

Marekani:  Ripoti ya Taasisi ya Uchumi na Amani imepata mataifa kumi tu ulimwenguni ambayo hayapo katika vita na migogoro kabisa. Kwa mujibu wa Ripoti ya Kimataifa ya Amani 2016, Botswana, Chile, Costa Rica, Japan, Mauritius, Panama, Qatar, Uswisi, Uruguay na Vietnam ndio nchi pekee ambazo hazipo kwenye vita wala migogoro yeyote ile ya kuhatarisha amani.. Iceland inaongoza orodha ya nchi zinazoongoza kwa amani ulimwenguni, ikifuatiwa na Denmark, Austria, New Zealand, Ureno, Jamhuri ya Czech, Uswisi, Canada, Japan na Slovenia - wakati Marekani ikiwa kwenye nafasi ya 103. Palestina imepanda kutoka nafasi ya 163 mpaka nafasi ya 148. Syria iliyoharibiwa na vita imewekwa chini ya orodha, chini kuliko Sudan Kusini, Iraq, Afghanistan, Somalia, Yemen, Jamhuri ya Afrika ya Kati, Ukraine, Sudan na Libya. "Ripoti inalinganisha amani duniani kwa kutumia mandhari tatu pana: hali ya utulivu na usalama katika jamii; kiwango cha mgogoro wa ndani au wa kimataifa; na kiwango cha kije...

SUMU YA NYUKI INAWEZA KUUA SELI ZA VVU NA KUTIBU UKIMWI.

Wanasayansi kutoka shule ya chuo kikuu cha Washington ya St.Louis, wamegundua kuwa kwa kuvuta mashimo katika bahasha ya kinga inayozunguka VVU na virusi vingine, melittin - sumu inayopatikana katika sumu ya nyuki - huua virusi vya ukimwi (VVU) wakati ikiacha mwili bila madhara .  Mafanikio haya yanaweza kusababisha kupatikana kwa madawa ambayo yataweza kukabiliana na VVU kama kutengenezwa kwa gel ya uke ya kupambana na VVU ambayo inaweza kuzuia kuenea kwa VVU; pamoja na matibabu ya uwezekano wa maambukizo ya VVU  (Kwa mwaka 2015, watu milioni 40 walikuwa wanaishi na virusi hivyo hatari duniani kote). Dr Joshua L. Hood, mwalimu wa utafiti katika dawa katika Chuo Kikuu cha Washington, alisema: "Melittin juu ya nanoparticles ina fuses na bahasha ya virusi. Melittin huunda tata ndogo za kushambulia na huvunja bahasha; kuondosha virusi ... Tunashambulia mali ya kimwili ya VVU. Kinadharia, hakuna njia yoyote ya kuwa virusi vitaweza kuendana na mazingira hayo. Virusi lazi...

ORODHA YA NCHI 80 AMBAZO MTANZANIA ANARUHUSIWA KUINGIA BILA VIZA.

         Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni amesema kuna zaidi ya nchi 80 ambazo watanzania wanaweza kusafiri bila ya kuwa na viza . Mhandisi Hamad Masauni amesema kuna zaidi ya nchi 80 ambazo watanzania wanaweza kusafiri bila ya kuwa na viza za kusafiria kama ilivyokuwa nchi za afrika Mashariki. Mhandisi Massauni amebainisha hayo leo bungeni wakati akijibu swali la Mbunge wa Mlalo kupitia tiketi ya CCM Rashid Shangazi aliyetaka kujua ni nchi ngapi ambazo watanzania wanaweza kusafiri bila ya kuwa na viza (viza on arrival). "Zipo nchi 16 kwa Afrika ambazo watanzania wanaweza kuzitembelea bila ya kuwa na viza na duniani zipo 67" alisema Masauni. Aidha Massauni amezitaja nchi hizo kuwa ni Benin, Burkina Faso, Cape Verde, Ivory Coast, Djibouti, Gabon, Gambia, Guinea, Guinea­Bissau, Liberia, Mali, Mauritania, Niger, Sierra Leone pamoja na Togo. Pamoja na hayo Masauni amesema...

CRISTIANO RONALDO MSHINDI WA TUZO YA BALLON d'OR 2017.

CRISTIANO RONALDO ametangazwa kuwa mshindi wa tuzo ya Ballon d'Or kwa mara ya tano na kufikia rekodi ya mshindani wake mkubw Lionel Messi. Mshambuliaji huyo wa Real Madrid, ambaye amekuwa mchezaji wa kwanza kufunga goli katika kila mchezo wa hatua ya makundi ya ligi ya Mabingwa wa Ulaya msimu huu, bado haoneshi dalili ya kushuka kiwango chake cha soka. Tazama kipande kifupi cha Video ya tukio hilo hapa: Hapa kuna orodha kamili inayohesabiwa kutoka kwenye 29 ya pamoja hadi CR7. 29th: Coutinho/Mertens 28th: Dzeko 27th: Hummels 26th: Oblak 25th: Benzema 24th: Falcão 23rd: Mané 21st: Bonucci/Aubameyang 20th: De Gea 19th: Hazard 18th: Griezmann 17th: Kroos 16th: Marcelo 15th: Dybala 14th: KDB 13rd: Suarez 12th: Isco 11th: Edinson Cavani 10th: Harry Kane 9th: Robert Lewandowski 8th: N’Golo Kante 7th: Kylian Mbappe 6th: Sergio Ramos 5th: Luka Modric 4th: Gianluigi Buffon 2nd: Neymar 2nd: Lionel Messi 1st: Cristiano Ronaldo CHANZO: thesun...

MOURINHO KUMUONDOA MKHITARYAN ILI AWEZE KUMSAJILI OZIL.

Henrikh Mkhitaryan atatupwa kando na meneja wa Manchester United Jose Mourinho ili apate nafasi ya kumsajili jiungo wa Arsenal, Mesut Ozil, kulingana na taarifa.  Bosi huyo wa Manchester United anajua lazima apunguze kikosi chake kama atataka kumsajili Ozil kutokana na madai ya mshahara mkubwa ya bingwa huyo wa Kombe la Dunia. Kiungo huyo mchezeshaji huyo ambaye mkataba wake Arsenal umalizika mwishoni mwa msimu huu, amekuwa akiomba mshahala wa Pauni Laki Tatu (£ 300,000) kwa wiki ili kukubali mkataba mpya wa kuendelea kuchezea Arsenal. Gazeti la 'The Mirror' la Uingereza limeripoti kwamba Mourinho ameamua Mkhitaryan, ambaye alijiunga na klabu kutoka Borussia Dortmund mwaka 2016, anaweza kuwa mchezaji kuondoka Ni uchaguzi wa mantiki kulingana na hali ya sasa ya mchezaji huyo katika kikosi cha Manchester United. Mchezaji huyo kutoka Armenia ameachwa mechi nane za mwisho na Mourinho huku akisema kuwa haamini kama kiungo huyo anastahilo kukukaa katika...

WADUKUZI WA KOREA YA KASKAZINI WAMEIBA NYARAKA ZA KIVITA ZA MAREKANI NA KOREA YA KUSINI.

Wadukuzi(hackers) kutoka Korea ya Kaskazini wameripotiwa kuiba sehemu kubwa ya nyaraka za kijeshi za siri kutoka Korea Kusini, ikiwa ni pamoja na mipango ya kina ya uendeshaji wa vita inayohusisha Marekani na mipango ya kumuua kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong-un. Rhee Cheol-hee, mwanasheria wa chama cha tawala la Korea Kusini, anasema wadukuzi(hackers) waliingia katika Kituo cha Takwimu cha Ulinzi kilichohifadhiwa huko Seoul mnamo Septemba 2016 na kupata upatikanaji wa data gigabytes 235. Wizara ya ulinzi wa Korea Kusini hadi sasa imekataa kutoa maoni juu ya madai hayo. Ingawa Rhee alisema asilimia 80 ya nyaraka zilizotajwa bado haijajulikana, alithibitisha mpango wa dharura kwa vikosi maalum vya Korea Kusini, maelezo kuhusu mizinga ya kijeshi ya pamoja ya kila mwaka na Marekani, na habari juu ya vituo muhimu vya kijeshi na vitalu vya nishati ziliibiwa. Miongoni mwa faili hizo ni Mpangilio wa Uendeshaji 5015, unaohusiana na "mpango wa hivi karibuni wa Seoul-Washing...