Skip to main content

MAJIBU YA FREDRICK WEREMA KUHUSU KUMUITA KAFULILA "TUMBILI".


FREDRICK WEREMA.



               Dar es Salaam. Mjadala mkali wa sakata la uchotwaji fedha kutoka Akaunti ya Tegeta Escrow ulisababisha aliyekuwa Mwanasheria Mkuu, Jaji Fredrick Werema kutumia msemo unaomtaja tumbili wakati akimjibu mbunge wa zamani wa Kigoma Kusini, David Kafulila.
Werema alijitokeza jana kufafanua kuhusu kauli yake, lakini mjadala huo wakati huo ulikuwa na matamko tofauti wakati joto bungeni lilipozidi, likigawa wabunge na hata viongozi wa Serikali.
Katika hotuba yake akiwa jimbo la Kigoma Kusini juzi, Rais John Magufuli alifufua tena mjadala huo wakati alipompongeza “kwa dhati” Kafulila kwa uzalendo wake wa kuibua kashfa hiyo iliyohusu Sh306 bilioni na kusimamia kutetea hoja yake hadi mwisho.
Rais alisema Kafulila alipata shida hadi baadhi walimuita tumbili, neno lililotamkwa na Werema wakati akijibu mwongozo wa mbunge huyo wa Kigoma Kusini, na kwamba waliomuita hivyo sasa wamegeuka tumbili.
“Lazima niwe mkweli na nisiposema hapa nitakuwa sijaitendea haki nafsi yangu, siku zote ukweli utabaki kuwa ukweli tu na ndiyo maana nampongeza Kafulila kwa sababu alisimama imara kupigania maslahi ya umma. Alionyesha uzalendo wa hali ya juu unaopaswa kuigwa na kila mmoja wetu,” alisema Rais.
Jana, Werema alimwambia mwandishi wetu kuwa alisema neno hilo kama msemo wa Kiswahili. Mwandishi wetu alipomuuliza kuhusu kauli ya Rais juzi, Jaji Werema alijibu:
Jaji Werema: Sasa unataka nifanyeje?
Mwandishi: Tunahitaji maoni yako kuhusu kauli hii.
Jaji Werema: Hilo jambo si liko mahakamani? Tunaweza kushtakiwa, wako mahakamani?
Mwandishi: Sawa. Lakini kwa kipindi kile kati ya watu ambao walimuita Kafulila tumbili, wewe ni mmoja wao.
Jaji Werema: Unajua wengi walishindwa kuelewa nilisema nini, mimi nilichokizungumza ni kwamba tumbili haamui mambo ya msituni, na huo ni msemo wa kawaida tu.
Kafulila, ambaye alikuwa mbunge wa Kigoma Kusini kuanzia 2010 hadi 2015 kwa tiketi ya NCCR-Mageuzi, aliibua kashfa hiyo bungeni baada ya kuisoma katika gazeti la The Citizen mwaka 2014.
Kwenye sakata hilo jumla ya Sh306 bilioni zilichotwa kutoka akaunti hiyo iliyofunguliwa kwa pamoja na Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) na kampuni ya kufua umeme ya IPTL baada ya kutokukubaliana katika tozo ya uwekezaji.
Baada ya Kafulila kuanzisha mjadala huo, Bunge liliagiza Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kufanya ukaguzi na taarifa yake ilitumiwa na chombo hicho cha kuisimamia Serikali kujadili kwa kina uchotwaji wa fedha hizo.
Licha ya kwamba wabunge wa CCM waliungana na upinzani katika sakata hilo, mjadala ulitawaliwa na mihemko na ushabiki na haikuwa ajabu kwa Werema kujikuta akitoa kauli hiyo.
Kila mbunge aliyesimama kutaka hatua zichukuliwe dhidi ya wote waliohusika, ukumbi ulikaa kimya kusikiliza lakini aliposimama mbunge aliyetetea kuwa fedha za escrow hazikuwa za umma kulikuwa na kelele za kumpinga na za kumshangilia, kiasi cha kulazimisha kiti cha spika kutuliza hali kila wakati.
Wakati Bunge lilipofikia kuweka maazimio, kikao kilifanyika hadi saa 5:00 usiku bila ya kufikia muafaka na kulazimika kuahirisha hadi siku iliyofuata kutoa nafasi kwa wabunge kujadiliana maazimio.
Miongoni mwa hoja zilizotolewa kukuza tatizo hilo ni zile zilizotolewa na mbunge wa zamani wa Nkenge (CCM), Assumpter Mshama, ambaye alidai kuna watu wengine waliopewa fedha wakiwa Mombasa nchini Kenya, na kumtaja mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe kuwa mmojawao.
“Hata mheshimiwa Mbowe amediriki kutajwa kwamba alipokea pesa kule Mombasa, lakini humu hakuna taarifa zake. Taarifa za benki ya Stanbic hatujasikia taarifa zake, lakini wanaojulikana wamepata pesa ni wa CCM. Ndio maana tunasema hata kama hiyo kamati ya PAC,” alisema huku sauti ikitaka kutoa taarifa.
Mshama alitakiwa atoe ushahidi kuwa Mbowe alitoa fedha lakini alishindwa na baadaye kufuta kauli yake.
Mwingine aliyetetea kuwa fedha hizo hazikuwa za Serikali ni mbunge wa Magomeni (CCM), Mohamed Chombo aliyewatuhumu walioshupalia suala hilo kuwa walikuwa na uchu wa madaraka.
“Sasa hivi, VIP imenunuliwa na PAP. Inabidi yeye-- kwa maana ya PAP-- alipe fedha zake za hisa parcent (asilimia) 30. Fedha hizi baada ya kutoka, PAP inabidi amlipe VIP. Sasa ndugu yangu nataka niwaambie--sasa nataka kuja kwenye ile ashki majinuni ni nani,” alisema.
“Kuna watu ambao maisha yao yote, wao ni watu wenye ashki. Ashki ni hamu ya kutaka na wao wapate kila wanachokipata wengine. Kuna watu wana ashki ya kupata madaraka haya.”

CHANZO ;
http://www.mwananchi.co.tz/habari/Aliyemuita-Kafulila-tumbili-afafanua/1597578-4030898-g5oxnnz/index.html

Comments

Habari Nyingine Kutoka Kioo17 Swahili;

MCHEZAJI WA ZAMANI WA UINGEREZA AMESEMA ALICHEZA NA WACHEZAJI WATATU MASHOGA KWENYE TIMU.

Carl Hoefkens (jezi no.2) alichezea West Bromwich Albion na Stoke City wakati wa enzi zake ligi kuu ya England. Beki wa zamani wa Ligi Kuu ya Uingereza amesema alicheza pamoja na wachezaji wenzake wawili wa mashoga ndani ya timu, na mmoja alikua na jina kubwa. Carl Hoefkens, West Bromwich Albion na Stoke City siku za nyuma, anasema wachezaji hao walikua wazi na hawakujificha kwenye vyumba vya kubadilishia nguo ingawa bado hawajulikani kwasababu ya maombi yao wenyewe ya kuomba kutotangazwa. Justin Fashanu, ambaye alijiua mwaka 1998, alikuwa mchezaji wa mwisho wa kazi nchini England kuja nje kama mashoga - mwaka 1990. Hoefkens alipokua (kushoto), alipokua anachezea Stock  City. Hoefkens aliyecheza Uingereza kwa miaka minne, akiondoka mwaka 2009, alidai kuwa mchezaji mwenzake mmoja wa timu alikua anaweza kuja kwenye uwanja wa mafunzo ya klabu na mpenzi wake wa kiume  lakini aliwaomba wenzake kutokuwaambia watu wangine wa nje ya timu. 'Nilicheza pamoja n...

ORODHA YA NCHI 80 AMBAZO MTANZANIA ANARUHUSIWA KUINGIA BILA VIZA.

         Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni amesema kuna zaidi ya nchi 80 ambazo watanzania wanaweza kusafiri bila ya kuwa na viza . Mhandisi Hamad Masauni amesema kuna zaidi ya nchi 80 ambazo watanzania wanaweza kusafiri bila ya kuwa na viza za kusafiria kama ilivyokuwa nchi za afrika Mashariki. Mhandisi Massauni amebainisha hayo leo bungeni wakati akijibu swali la Mbunge wa Mlalo kupitia tiketi ya CCM Rashid Shangazi aliyetaka kujua ni nchi ngapi ambazo watanzania wanaweza kusafiri bila ya kuwa na viza (viza on arrival). "Zipo nchi 16 kwa Afrika ambazo watanzania wanaweza kuzitembelea bila ya kuwa na viza na duniani zipo 67" alisema Masauni. Aidha Massauni amezitaja nchi hizo kuwa ni Benin, Burkina Faso, Cape Verde, Ivory Coast, Djibouti, Gabon, Gambia, Guinea, Guinea­Bissau, Liberia, Mali, Mauritania, Niger, Sierra Leone pamoja na Togo. Pamoja na hayo Masauni amesema...

WALICHOJIBU CHENGE ,NGELEJA NA DK.KAFUMU BAADA YA RIPOTI YA PILI YA RAISI.

              VIGOGO waliotajwa katika ripoti ya pili ya kuchunguza makontena yenye mchanga wa madini (makinikia)  kuisababishia Serikali hasara ya matrilioni ya fedha kupitia sekta ya madini, walipokuwa wakihudumu katika nyadhifa zao serikalini wamevunja ukimya. Vigogo hao wamezungumzia ripoti hiyo ya pili iliyowasilishwa kwa Rais Dk. John Magufuli Ikulu Dar es Salaam jana, ambapo kamati husika ilichunguza hasara ambayo nchi imepata tangu 1998 usafirishaji wa mchanga wa dhahabu nje ya nchi ulipoanza. Mbunge wa Bariadi, Andrew Chenge (CCM), alipoulizwa maoni yake juu ya kutajwa na kamati hiyo, alisema hataki kuzungumza chochote juu ya ripoti hiyo, huku Mbunge wa Sengerema, William Ngeleja (CCM), akisema sheria ya madini ya 2010 ingefuatwa, nchi isingekuwa hapa ilipo. Kwa upande wake Kamishna wa Madini wa zamani, Dk. Dalaly Kafumu, alisema kwa sasa  hawezi kuzungumza jambo lolote kwa kuwa ni yeye ni mmoja wa watuhumiwa waliotaj...

KIONGOZI MKUU WA UPINZANI NCHINI ZIMBABWE, MORGAN TSVANGIRAI AMEFARIKI DUNIA.

Kiongozi wa upinzani wa Zimbabwe Morgan Tsvangirai amefariki dunia nchini Afrika Kusini, afisa mkuu wa chama chake cha MDC amesema. Bw Tsvangirai, mwenye umri wa miaka 65, aliyekuwa waziri mkuu, alilipotiwa kuwa alikuwa akisumbuliwa na saratani ya koloni. "Amefariki jioni hii, familia yake imenitaarifu"  Makamu wa Rais wa MDC, Elias Mudzuri aliliambia shirika la habari la Uingereza, Reuters. Morgan Tsvangirai alizaliwa mnamo Machi 10, 1952 huko Gutu, Zimbabwe. Baba yake alikuwa mfanyakazi wa mgodi, fundi, na mkulima. Alihudhuria Shule ya Msingi ya Guco ya St. Marks. Kisha alihamishiwa Shule ya Msingi ya Chikara Gutu. Kwa elimu yake ya sekondari, alihudhuria Shule ya High Gokomere. Alikuwa waziri mkuu katika serikali ya mseto ya Zimbabwe tangu 2009 hadi 2013. Katika kazi yake ya awali alionekana kuwa mfanyakazi mwenye bidii sana na alifanya kazi katika mgodi wa madini ya nickel( kwa zaidi ya muongo mmoja. Alipanda cheo haraka kutambuliwa na akain...

MADAI YA CUBA KWAMBA WAZIRI MKUU WA CANADA NI MTOTO WA FIDEL CASTRO.

Pichani ni waziri mkuu wa Canada, Justin Trudeau (kushoto), na Rais wa zamani wa Cuba, Hayati Fidel Castro (kulia). Maelezo yaliyoandikwa na mtoto wa kwanza wa rais wa zamani wa Cuba , Fidel Castro, kabla ya kujiua yamelishtua taifa la Cuba wiki hii. Maelezo hayo yaliyoandikwa na mtoto huyo mkubwa wa mwanamapinduzi na rais wa zamani wa nchi hiyo yalikuwa ya kushangaza baada ya  kuwa na madai ya kuwa Waziri Mkuu wa Canada Justin Trudeau ni mtoto wa nje wa baba yake marehemu Fidel Castro. Maelezo hayo yaliyoandikwa kwa mkono na mtoto huyo wa Fidel Castro aliyejiua siku chache zilizopita kwa msongo wa mawazo, Fidel Castro Diaz-Balart, aliyekuwa na umri wa miaka 68, yalionekana kuthibitisha uvumi wa muda mrefu nchini Cuba kwamba Fidel Castro ni baba wa damu wa waziri mkuu wa sasa wa Canada, Justin Trudeau ikiwa ni matokeo ya uhusiano wa siri wa kimapenzi na mke wa mwanasiasa maarufu wa Canada, Pierre Trudeau, Margaret Trudeau mwaka 1970. Kifo cha mwanasayansi wa ...

KASHFA YA MAPENZI KATI MH.MBOWE NA WEMA SEPETU.

MH.FREEMAN MBOWE AKIWA NA WEMA SEPETU. Siku chache baada ya ile skendo ya ngono iliyosababisha wakili na mshauri wa Chama cha ACT -Wazalendo , Bwana Albert Msando kujiuzulu kwenye nyadhifa yake ya chama ,yameibuka mangine kwenye chama kikuu cha upinzani Tanzania ,CHADEMA ,baada ya kusambaa kwa kipande cha sauti kinachodaiwa kua ni mazungumzo kati ya mwenyekiti wa chama hicho na mbunge wa Hai Mh.Freeman Mbowe na Miss Tanzania 2006 ,mrembo Wema Isack Sepetu. SIKILIZA HIVI VIPANDE VYA SAUTI: Bonyeza hapa chini kusikiliza maongezi hayo yanayodaiwa kuwa ni kati ya Wema Sepetu na Mh.Freeman Mbowe; Bonyeza hapa chini kusikiliza majibu ya Wema Sepetu; Bonyeza hapa chini kusikiliza majibu ya Mh.Freeman Mbowe; VYANZO: Jamii Forums,                   YouTube.com,                   Perfect255.com.                   

RAPA SNOOP DOGG AMETHIBITISHA MIPANGO YA KUHAMIA UGANDA.

Msanii wa muziki wa Hip Hop wa Marekani, Calvin Cordozar Broadus.Jr. maarufu kama Snoop Dogg amethibitisha kuwa anataka kuhamia Uganda baada ya rais wa Marekani, Donald Trump kudaiwa kuziita nchi za Afrika 'Shimo la Choo' . Snoop Doggy Dogg pia ni mwimbaji, mwandishi wa nyimbo, mtayarishaji wa muziki, mtangazaji katika televisheni, na mwigizaji wa filamu ambaye alianza kupata umaarufu mkubwa katika muziki mwaka 1992 wakati alipogunduliwa na mtayarishaji Dr.Dre, na kushiriki katika nyimbo za Dr.Dre kama "Deep Cover", na kisha kwenye albamu ya kwanza ya Dr.Dre, ' The Chronic' . Kwa sasa tayari ameshauza albamu zaidi ya milioni 23 nchini Marekani na albamu milioni 35 duniani kote. Mmarekani huyo mweusi mwenye miaka 46 wa ambaye anajulikana kwa nyimbo zake za maarufu kama; The next episode, Drop it like it’s hot, beautiful, Lay low,  nk Juzi alirekodi kipande cha video na kukisambaza akisema kuwa anataka kuhamia chini Uganda. Tazama V...