Skip to main content

MAJIBU YA FREDRICK WEREMA KUHUSU KUMUITA KAFULILA "TUMBILI".


FREDRICK WEREMA.



               Dar es Salaam. Mjadala mkali wa sakata la uchotwaji fedha kutoka Akaunti ya Tegeta Escrow ulisababisha aliyekuwa Mwanasheria Mkuu, Jaji Fredrick Werema kutumia msemo unaomtaja tumbili wakati akimjibu mbunge wa zamani wa Kigoma Kusini, David Kafulila.
Werema alijitokeza jana kufafanua kuhusu kauli yake, lakini mjadala huo wakati huo ulikuwa na matamko tofauti wakati joto bungeni lilipozidi, likigawa wabunge na hata viongozi wa Serikali.
Katika hotuba yake akiwa jimbo la Kigoma Kusini juzi, Rais John Magufuli alifufua tena mjadala huo wakati alipompongeza “kwa dhati” Kafulila kwa uzalendo wake wa kuibua kashfa hiyo iliyohusu Sh306 bilioni na kusimamia kutetea hoja yake hadi mwisho.
Rais alisema Kafulila alipata shida hadi baadhi walimuita tumbili, neno lililotamkwa na Werema wakati akijibu mwongozo wa mbunge huyo wa Kigoma Kusini, na kwamba waliomuita hivyo sasa wamegeuka tumbili.
“Lazima niwe mkweli na nisiposema hapa nitakuwa sijaitendea haki nafsi yangu, siku zote ukweli utabaki kuwa ukweli tu na ndiyo maana nampongeza Kafulila kwa sababu alisimama imara kupigania maslahi ya umma. Alionyesha uzalendo wa hali ya juu unaopaswa kuigwa na kila mmoja wetu,” alisema Rais.
Jana, Werema alimwambia mwandishi wetu kuwa alisema neno hilo kama msemo wa Kiswahili. Mwandishi wetu alipomuuliza kuhusu kauli ya Rais juzi, Jaji Werema alijibu:
Jaji Werema: Sasa unataka nifanyeje?
Mwandishi: Tunahitaji maoni yako kuhusu kauli hii.
Jaji Werema: Hilo jambo si liko mahakamani? Tunaweza kushtakiwa, wako mahakamani?
Mwandishi: Sawa. Lakini kwa kipindi kile kati ya watu ambao walimuita Kafulila tumbili, wewe ni mmoja wao.
Jaji Werema: Unajua wengi walishindwa kuelewa nilisema nini, mimi nilichokizungumza ni kwamba tumbili haamui mambo ya msituni, na huo ni msemo wa kawaida tu.
Kafulila, ambaye alikuwa mbunge wa Kigoma Kusini kuanzia 2010 hadi 2015 kwa tiketi ya NCCR-Mageuzi, aliibua kashfa hiyo bungeni baada ya kuisoma katika gazeti la The Citizen mwaka 2014.
Kwenye sakata hilo jumla ya Sh306 bilioni zilichotwa kutoka akaunti hiyo iliyofunguliwa kwa pamoja na Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) na kampuni ya kufua umeme ya IPTL baada ya kutokukubaliana katika tozo ya uwekezaji.
Baada ya Kafulila kuanzisha mjadala huo, Bunge liliagiza Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kufanya ukaguzi na taarifa yake ilitumiwa na chombo hicho cha kuisimamia Serikali kujadili kwa kina uchotwaji wa fedha hizo.
Licha ya kwamba wabunge wa CCM waliungana na upinzani katika sakata hilo, mjadala ulitawaliwa na mihemko na ushabiki na haikuwa ajabu kwa Werema kujikuta akitoa kauli hiyo.
Kila mbunge aliyesimama kutaka hatua zichukuliwe dhidi ya wote waliohusika, ukumbi ulikaa kimya kusikiliza lakini aliposimama mbunge aliyetetea kuwa fedha za escrow hazikuwa za umma kulikuwa na kelele za kumpinga na za kumshangilia, kiasi cha kulazimisha kiti cha spika kutuliza hali kila wakati.
Wakati Bunge lilipofikia kuweka maazimio, kikao kilifanyika hadi saa 5:00 usiku bila ya kufikia muafaka na kulazimika kuahirisha hadi siku iliyofuata kutoa nafasi kwa wabunge kujadiliana maazimio.
Miongoni mwa hoja zilizotolewa kukuza tatizo hilo ni zile zilizotolewa na mbunge wa zamani wa Nkenge (CCM), Assumpter Mshama, ambaye alidai kuna watu wengine waliopewa fedha wakiwa Mombasa nchini Kenya, na kumtaja mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe kuwa mmojawao.
“Hata mheshimiwa Mbowe amediriki kutajwa kwamba alipokea pesa kule Mombasa, lakini humu hakuna taarifa zake. Taarifa za benki ya Stanbic hatujasikia taarifa zake, lakini wanaojulikana wamepata pesa ni wa CCM. Ndio maana tunasema hata kama hiyo kamati ya PAC,” alisema huku sauti ikitaka kutoa taarifa.
Mshama alitakiwa atoe ushahidi kuwa Mbowe alitoa fedha lakini alishindwa na baadaye kufuta kauli yake.
Mwingine aliyetetea kuwa fedha hizo hazikuwa za Serikali ni mbunge wa Magomeni (CCM), Mohamed Chombo aliyewatuhumu walioshupalia suala hilo kuwa walikuwa na uchu wa madaraka.
“Sasa hivi, VIP imenunuliwa na PAP. Inabidi yeye-- kwa maana ya PAP-- alipe fedha zake za hisa parcent (asilimia) 30. Fedha hizi baada ya kutoka, PAP inabidi amlipe VIP. Sasa ndugu yangu nataka niwaambie--sasa nataka kuja kwenye ile ashki majinuni ni nani,” alisema.
“Kuna watu ambao maisha yao yote, wao ni watu wenye ashki. Ashki ni hamu ya kutaka na wao wapate kila wanachokipata wengine. Kuna watu wana ashki ya kupata madaraka haya.”

CHANZO ;
http://www.mwananchi.co.tz/habari/Aliyemuita-Kafulila-tumbili-afafanua/1597578-4030898-g5oxnnz/index.html

Comments

Habari Nyingine Kutoka Kioo17 Swahili;

WASTANI WA ADA ZA VYUO VIKUU BORA ZAIDI DUNIANI.

            Elimu ya juu ya kupokea nje ya nchi (Nchi zilzo endelea) daima imekuwa kiwango cha kutambuliwa sana, na wanafunzi kutoka duniani kote siku zote wana ndoto kuhusu hilo.             Tovuti ya Bright Side imeamua kujua gharama za sasa za kujifunza * kwa wanafunzi wa kimataifa katika vyuo vikuu vya juu vya dunia, na tungependa kushiriki habari hii na wewe. * Wastani wa kila mwaka ada ya mafunzo ya shahada ya kwanza ; MAREKANI; Kwa maelezo zaidi kuhusiana na chuo hiki bonyeza hapa: http://www.harvard.edu/ Kwa maelezo zaidi kuhusiana na chuo hiki bonyeza hapa:  http://web.mit.edu/ UINGEREZA;     Kwa maelezo zaidi kuhusiana na chuo hiki bonyeza hapa; http://www.cam.ac.uk/     Kwa maelezo zaidi kuhusiana na chuo hiki bonyeza hapa: http://www.ox.ac.uk/ USWISI (SWITZERLAND ):     Kwa maelezo zaidi kuhusiana na chuo hiki bonyeza hapa:...

ORODHA YA NCHI ZA KWANZA NA ZA MWISHO KWA AMANI DUNIANI.

Marekani:  Ripoti ya Taasisi ya Uchumi na Amani imepata mataifa kumi tu ulimwenguni ambayo hayapo katika vita na migogoro kabisa. Kwa mujibu wa Ripoti ya Kimataifa ya Amani 2016, Botswana, Chile, Costa Rica, Japan, Mauritius, Panama, Qatar, Uswisi, Uruguay na Vietnam ndio nchi pekee ambazo hazipo kwenye vita wala migogoro yeyote ile ya kuhatarisha amani.. Iceland inaongoza orodha ya nchi zinazoongoza kwa amani ulimwenguni, ikifuatiwa na Denmark, Austria, New Zealand, Ureno, Jamhuri ya Czech, Uswisi, Canada, Japan na Slovenia - wakati Marekani ikiwa kwenye nafasi ya 103. Palestina imepanda kutoka nafasi ya 163 mpaka nafasi ya 148. Syria iliyoharibiwa na vita imewekwa chini ya orodha, chini kuliko Sudan Kusini, Iraq, Afghanistan, Somalia, Yemen, Jamhuri ya Afrika ya Kati, Ukraine, Sudan na Libya. "Ripoti inalinganisha amani duniani kwa kutumia mandhari tatu pana: hali ya utulivu na usalama katika jamii; kiwango cha mgogoro wa ndani au wa kimataifa; na kiwango cha kije...

WAZIRI WA MAMBO YA NJE WA GAMBIA AMTAKA RAIS WA TOGO KUACHIA MADARAKA KWA HIARI.

RAIS WA TOGO, FAURE GNASSINGBE. BANJUL, Oktoba 23 (Reuters) "Rais wa Togo Faure Gnassingbe anapaswa kujiuzulu mara moja na Umoja wa Afrika na kanda ya kikanda ya Afrika Magharibi ECOWAS inapaswa kumshawishi kushuka ikiwa hawaja fanya hivyo",  Waziri wa Mambo ya Nje wa Gambia Ousainou Darboe amesema. Maoni ya Darboe ni ishara ya mwanzo kwamba yuko dhidi ya Gnassingbe ambaye alinyakua madaraka kwa nguvu mwaka 2005 baada ya kifo cha baba yake ambaye alikuwa ametawala tangu mwaka 1967. Togo ni inakabiliwa na mgogoro wa kisiasa ambao takribani watu 10 wameuawa katika maandamano tangu Agosti. "Nadhani Umoja wa Afrika na ECOWAS inapaswa kushiriki na kumshawishi rais wa Togo kung'ooka ," Darboe aliiambia Shirika la habari la Uingereza (Reuters) mwishoni mwa wiki hii, akiongezea kuwa nchi nyingine zinahitaji kushiriki. "Wakati serikali ya Togo inakiuka kanuni zinazokubalika sidhani kama suala hili linapaswa kuchukuliwa kama ni mambo ya ndani ya nd...

SABABU YA ZIPU NYINGI KUWA NA HERUFI "YKK".

Ikiwa umewahi kuchunguza kwa ukaribu zipu kwenye nguo zako nyingi, utakua tayari umeona herufi zinazosomeka "YKK," katika herufi kubwa, kwa mengi yao.Herufi hizi zipo kwenye kila kitu kutoka kwenye nguo za jeans, makoti hata kwenye mabegi. Herufi hizo zinasimama kwa niaba ya "Yoshida Kogyo Kabushikikaisha" ambayo, kutoka kwenye lugha ya Kijapani, inaelezea  "Yoshida Company Limited" yaani "Kampuni ya Yoshida"  Kampuni hii ni ya mtengenezaji wa zipu aitwaye Tadao Yoshida, ambaye aliianzisha mwaka wa 1934. Kwa wastani, kampuni hiyo inatengeneza nusu ya zipu duniani, ambayo ni zaidi ya zipu bilioni 7 kila mwaka. Kwa uhalisia Yoshida hakua mvumbuzi wa zipu duniani, zipu zilivumbuliwa na Mmarekani, Whitcomb L. Judson, miaka ya 1890.  Kampuni yake sasa ipo,  na inabuni na kutengeneza zipu za kisasa ikijulikana kama Talon, Inc. Bidhaa za kampuni hiyo hutumiwa makampuni kama Brooks Brothers na Uniqlo. Lakini YKK ina sifa isiyofananishik...

UGANDA IMEWAFUKUZA WATAALAM WA KIJESHI KUTOKA KOREA YA KASKAZINI.

Uganda imefukuza wataalamu wa kijeshi wa Korea Kaskazini na wawakilishi wa makampuni ya Kaskazini ya Korea, ikiwa ni pamoja na mfanyabiashara wake mkubwa wa silaha za juu kutokana na mataifa ya Kiafrika kukabiliwa na shinikizo la kuzingatia vikwazo vya Umoja wa Mataifa(UN) juu ya mpango wa silaha za nyuklia wa Pyongyang. "Raia wa Korea ya Kaskazini waliobaki katika taifa hilo la Afrika Mashariki ni wanadiplomasia na watu binafsi tu ", Okello Oryem, naibu waziri wa mambo ya kigeni, aliiambia The Associated Press. "Tunafuatana kabisa," alisema Oryem, akiongezea kwamba Uganda ina uhusiano wa kawaida wa kidiplomasia na Korea Kaskazini. Uganda hasa ilidai kuondoka kwa watu wanaowakilisha Shirika la Biashara la Maendeleo ya Madini ya Korea. Ni mkataba wa msingi wa Korea Kaskazini na chini ya vikwazo vya U.N. na U.S. Uhamisho huo unaashiria mabadiliko ya sera kwa serikali ya Uganda, ambayo hapo awali ilikuwa na mahusiano ya mazuri na Pyongyang. Korea ya Kaska...

PAPA FRANCIS ASHINDANISHWA NA PABLO ESCOBAR KWA KUHESHIMIWA NCHINI COLOMBIA.

Medellín (Colombia) (AFP):  Katika saluni yake ya nywele, Yamile Zapata anatumia faida ya ziara ya Papa Francis ili kuuza pete za funguo zenye picha ya kiongozi huyo wa kanisa katoliki duniani. Lakini anadai sio ambapo pesa halisi iko kwenye mji wa Medellin nchini Colombia. Zawadi nyingi anazouza katika mji huu wa Colombia hubeba uso wa "mtakatifu" na shujaa wake mwenyewe: Pablo Escobar. Wakati Francis alikuwa akihudumia na kufundisha kama kuhani wa Yesuit katika miaka ya 1980, Escobar alikuwa akiua mamia ya watu na kufanya biashara ya madawa ya kulevya ya mabilioni ya dola za kimarekani. "Kila mtu anataka picha za papa sasa, lakini picha za Pablo zinauzika vizuri zaidi," , alisema Zapata, mwenye umri wa miaka 34, wakati ambao jiji hilo limeandaliwa kwa ajili ya mkutano wa Papa Francis wa wazi siku ya Jumamosi. PETE ZA FUNGUO ZENYE PICHA ZA PAPA FRANCIS NA PABLO ESCOBAR ZIKIWA ZINAUZWA KWENYE MITAA YA JIJI LA MEDELIN, COLOMBIA. Francis alitoa mane...

MCHEZAJI WA ZAMANI WA UINGEREZA AMESEMA ALICHEZA NA WACHEZAJI WATATU MASHOGA KWENYE TIMU.

Carl Hoefkens (jezi no.2) alichezea West Bromwich Albion na Stoke City wakati wa enzi zake ligi kuu ya England. Beki wa zamani wa Ligi Kuu ya Uingereza amesema alicheza pamoja na wachezaji wenzake wawili wa mashoga ndani ya timu, na mmoja alikua na jina kubwa. Carl Hoefkens, West Bromwich Albion na Stoke City siku za nyuma, anasema wachezaji hao walikua wazi na hawakujificha kwenye vyumba vya kubadilishia nguo ingawa bado hawajulikani kwasababu ya maombi yao wenyewe ya kuomba kutotangazwa. Justin Fashanu, ambaye alijiua mwaka 1998, alikuwa mchezaji wa mwisho wa kazi nchini England kuja nje kama mashoga - mwaka 1990. Hoefkens alipokua (kushoto), alipokua anachezea Stock  City. Hoefkens aliyecheza Uingereza kwa miaka minne, akiondoka mwaka 2009, alidai kuwa mchezaji mwenzake mmoja wa timu alikua anaweza kuja kwenye uwanja wa mafunzo ya klabu na mpenzi wake wa kiume  lakini aliwaomba wenzake kutokuwaambia watu wangine wa nje ya timu. 'Nilicheza pamoja n...