Skip to main content

MAGUFULI ALIVYOMLIPUA ABOOD.




PENGINE ilikuwa si rahisi kufikiri hapo kabla kuwa ipo siku mwenyekiti wa chama tawala anaweza kusema ukweli wenye kugusa maslahi ya mbunge wa chama chake kunako mkutano wa hadhara.
Hata hivyo, jambo hilo si la kushangaza tena katika serikali ya awamu ya tano iliyopania kusimamia misingi ya ukweli kwa maslahi mapana ya taifa.
Hali hiyo ilijidhihirisha jana mjini Morogoro wakati Rais John Magufuli alipomlipua mbele ya mkutano wa hadhara Mbunge wa Morogoro Mjini (CCM), Aziz Abood, kwa kumtaja kuwa miongoni mwa watu waliotwaa viwanda mkoani humo na baadhi yake kuvigeuza kuwa machungio ya mbuzi badala ya kuviendeleza kama ilivyotarajiwa.
Jana, akizungumzia agizo hilo la Rais Magufuli, Abood ambaye pia ni mmiliki wa kampuni ya mabasi ya Abood iliyopo mkoani humo, alisema anatekeleza agizo la Rais na tayari kiwanda chake cha Moproco kimefunga mashine mpya kwa ajili ya uzalishaji.
Akizungumza katika mkutano wake huo kwenye eneo la Msamvu mjini Morogoro jana, Rais Magufuli (JPM), ambaye pia mwenyekiti wa taifa wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), alisema Abood na watu wengine waliomilikishwa viwanda na serikali wanapaswa kuviendeleza au kuvirejesha serikalini ili wapewe wawekezaji wengine waviendeleze.
Rais Magufuli aliyasema hayo wakati akizungumza baada ya kusimama Msamvu kwa muda akitokea Dodoma kwenda jijini Dar es Salaam.
“Ninarudia wito wangu niliokwisha kuutoa huko nyuma, kwamba wenye viwanda hapa Morogoro ambao wameshindwa kuviendesha wavirejeshe serikalini. Na leo nataja, akiwemo Mbunge wa hapa wa Chama Cha Mapinduzi (CCM)… narudia, akiwamo Mbunge wa hapa wa CCM ambaye alibinafsishiwa viwanda vingi.
“Alipewa viwanda vingi na sasa nasikia anafugia mbuzi… sasa kama ameshindwa kuviendesha avirudishe ili tuwape watu wengine kwa sababu vijana hawa wanakosa ajira,” alisema Rais Magufuli na kuongeza:
“Nazungumza kwa uwazi kwa sababu msemakweli ni mpenzi wa Mungu.”
Rais Magufuli alisisitiza kuwa suala la kusimamia ukweli kwa manufaa ya taifa halichagui itikadi ya chama na ndiyo maana analisema hilo bila kificho.
“Uwe CCM, uwe CUF uwe Chadema, ukifanya ya ovyo mimi nakutandika tu, tena hadharani. Kwa hiyo mheshimiwa Mbunge wa hapa nampenda… na ni mbunge wa chama changu, lakini nataka viwanda alivyopewa vifanye kazi,” alisema Rais Magufuli na kuibua shangwe kubwa kutoka kwa mamia ya wananchi waliokuwa wakimsikiliza.
Kwenye mkutano huo, Rais Magufuli aliwapongeza pia wakulima wa mazao katika mkoa wa Morogoro kwa kuongeza uzalishaji.
Aidha, alimwagiza Kamanda wa Polisi wa Morogoro, SACP Ulrich Matei, kuhakikisha askari mgambo hawawasumbui wafanyabiashara wa Msamvu.
ABOOD AFUNGUKA
Akizungumza na Nipashe jana kuhusiana na maelekezo ya Rais juu ya viwanda alivyobinafsisha, Abood alisema anatekeleza na kiwanda anachomiliki cha Moproco kimeshaanza kufanya kazi.
Alisema mashine za kiwanda hicho zimeshafungwa na kwamba, kwa sasa kinachosubiriwa ni leseni tu.
“Rais Magufuli anahimiza, na sisi tunajitahidi kufuata kauli zake. Jitihada zinafanyika ili kila kitu kiende sawa na vijana wetu wapate ajira.
Morogoro kuna viwanda vingi ambavyo vitafunguliwa… siyo vya kwangu tu, Rais Magufuli anatumihimiza wote wenye viwanda,” alisema Abood.
Kwa mujibu wa ripoti ya mwaka 2012 ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma (POAC) , takribani viwanda na mashirika 17 ya umma nchini yaliyobinafsishwa mwaka 1993 yamefungwa baada ya kushindwa kuzalisha.

CHANZO:
http://m.ippmedia.com/sw/habari/jpm-alivyomlipua-abood-wa-mabasi

Comments

Habari Nyingine Kutoka Kioo17 Swahili;

ORODHA YA NCHI 80 AMBAZO MTANZANIA ANARUHUSIWA KUINGIA BILA VIZA.

         Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni amesema kuna zaidi ya nchi 80 ambazo watanzania wanaweza kusafiri bila ya kuwa na viza . Mhandisi Hamad Masauni amesema kuna zaidi ya nchi 80 ambazo watanzania wanaweza kusafiri bila ya kuwa na viza za kusafiria kama ilivyokuwa nchi za afrika Mashariki. Mhandisi Massauni amebainisha hayo leo bungeni wakati akijibu swali la Mbunge wa Mlalo kupitia tiketi ya CCM Rashid Shangazi aliyetaka kujua ni nchi ngapi ambazo watanzania wanaweza kusafiri bila ya kuwa na viza (viza on arrival). "Zipo nchi 16 kwa Afrika ambazo watanzania wanaweza kuzitembelea bila ya kuwa na viza na duniani zipo 67" alisema Masauni. Aidha Massauni amezitaja nchi hizo kuwa ni Benin, Burkina Faso, Cape Verde, Ivory Coast, Djibouti, Gabon, Gambia, Guinea, Guinea­Bissau, Liberia, Mali, Mauritania, Niger, Sierra Leone pamoja na Togo. Pamoja na hayo Masauni amesema...

USWISI KURUDISHA DOLA MILIONI 321($321M) ZA WIZI KWA NIGERIA.

Serikali ya Nigeria imechukua zaidi ya dola bilioni 1 zilizoaminiwa kuibwa na Rais wa zamani Sani Abacha. CNN: Serikali ya Uswisi kurudisha dola za kimarekani milioni 321 nchini Nigeria ambazo zilikuwa zimechukuliwa kutoka kwenye familia ya Rais wa zamani wa nchi hiyo, Sani Abacha. Mali hizo zilifanywa kama sehemu ya kesi za jinai dhidi ya Abba Abacha, mwana wa Sani, ambaye alitawala Nigeria kwa miaka mitano mpaka kufa kwake mwaka 1998. Wachunguzi wa Nigeria wanaamini rais huyo wa zamani aliiba zaidi ya dola bilioni 4 ($4 Billion) muda wake katika ofisi. Serikali ya Uswisi ilitoa tamko Jumatatu kutangaza makubaliano hayo yaliyofikiwa na viongozi kutoka serikali ya Nigeria na Benki ya Dunia kwa marekebisho. "Marejesho ya fedha yatatokea katika mfumo wa mradi unaoungwa mkono na kusimamiwa na Benki ya Dunia," ,  ilisema taarifa hiyo. "Mradi utaimarisha usalama wa kijamii kwa sehemu maskini zaidi ya idadi ya watu wa Nigeria." Serikali ya Nigeria ilit...

SABABU ZA KUVUNJIKA KWA KUNDI LA P-SQUARE.

WANAMUZIKI MAPACHA WA KUNDI LA PSQUARE, PETER (KUSHOTO) NA PAUL (KULIA) WAKIWA NA KAKA YAO AMBAE PIA NI MENEJA WAO, JUDES OKOYE. Mwanamuziki wa kundi la PSquare kutoka Nigeria, Peter Okoye ametangaza kujitoa kwenye kundi hilo la muziki wa Pop maarufu zaidi Afrika. Msanii huyo alidai kwamba amewasilisha maombi ya kuvunja kundi hilo katika barua aliyoandika kwa wakili wao Festus Keyamo. Kulingana na nakala ya barua iliyotolewa kwenye vyombo vya habari Jumatatu,Tarehe 25 Septemba, Peter alisema kuwa pacha wake na, Paul, na kaka yao, Judes waliahirisha ziara yao ya muziki ya Marekani bila kushauriana naye.Na hiyo ni moja kati ya sababu za msingi. Peter pia aliwalaumu Paul na kaka yao mkubwa mkubwa ambae ni meneja wao pia kwa udanganyifu walioufanya ili kutatua shida waliyokuwa nayo juu ya biashara ya muziki. Wasanii hao ndugu wamekua kwenye vita vya maneno kwenye mitandao ya kijamii tangu mwisho wa mwaka jana pamoja na juhudi za watu wao wa karibu kujaribu kuwapatanisha kifami...

TUPAC SHAKUR ALIBAKWA JELA !!!

             Ulimwengu wa filamu za Hollywood na muziki wa Hip Hop juzi ulipatwa na mshangao baada ya mtayarishaji wa filamu inayohusu maisha ya hayati Tupac Shakur ,L.T Hutton kuelezea sababu zilizomfanya kumbadilisha muongozaji wa filamu hiyo kutoka John Singleton na kumuweka muongozaji Benny "Boom" Douglas.  Filamu hiyo inayoitwa "all eyez on me" tayari imekwisha andaliwa na inatarajiwa kuzinduliwa leo tarehe 16 Juni 2017.       Akizungumza kwenye mahojiano redioni L.T Hutton amewashtusha watu wengi baada ya kudai kwamba walishindwana na muongozaji wa mwanzo bwana John Singleton sababu muongozaji huyo aling'ang'ania kuwepo kwa matukio (scene) ambazo kwa maoni yake zisingependeza.        Matukio ambayo John Singleton alipenda yawepo katika filamu hiyo ni pamoja na kutaka filamu hiyo ianze na scene ya Tupac akilazimisha kumlawiti msichana wa kizungu.!!!          Singleton pia ali...

ALICHOANDIKA MH.NGELEJA BAADA YA KURUDISHA FEDHA ZA ESCROW.

MH.WILLIAM NGELEJA .            Waziri wa zamani wa Nishati na Madini na Mbunge wa Jimbo la Sengerema, William Ngeleja amerejesha rasmi Serikalini fedha alizozipata katika mgao wa Escrow ambazo ni kiasi cha Shilingi Milioni 40.4 ili kukwepa kuendelea kuandamwa na kashfa.        Ngeleja amesema ingawa alipewa fedha hizo kama sehemu ya msaada , ameamua kurudisha fedha hizo ili kukwepa kashfa hiyo ya ESCROW.     SOMA HAPA BARUA ALIYOITOA KWA WAANDISHI WA HABARI ;

MCHEZAJI WA ZAMANI WA UINGEREZA AMESEMA ALICHEZA NA WACHEZAJI WATATU MASHOGA KWENYE TIMU.

Carl Hoefkens (jezi no.2) alichezea West Bromwich Albion na Stoke City wakati wa enzi zake ligi kuu ya England. Beki wa zamani wa Ligi Kuu ya Uingereza amesema alicheza pamoja na wachezaji wenzake wawili wa mashoga ndani ya timu, na mmoja alikua na jina kubwa. Carl Hoefkens, West Bromwich Albion na Stoke City siku za nyuma, anasema wachezaji hao walikua wazi na hawakujificha kwenye vyumba vya kubadilishia nguo ingawa bado hawajulikani kwasababu ya maombi yao wenyewe ya kuomba kutotangazwa. Justin Fashanu, ambaye alijiua mwaka 1998, alikuwa mchezaji wa mwisho wa kazi nchini England kuja nje kama mashoga - mwaka 1990. Hoefkens alipokua (kushoto), alipokua anachezea Stock  City. Hoefkens aliyecheza Uingereza kwa miaka minne, akiondoka mwaka 2009, alidai kuwa mchezaji mwenzake mmoja wa timu alikua anaweza kuja kwenye uwanja wa mafunzo ya klabu na mpenzi wake wa kiume  lakini aliwaomba wenzake kutokuwaambia watu wangine wa nje ya timu. 'Nilicheza pamoja n...

ALICHOSEMA SHEIKH PONDA KUHUSU MIILI INAYOOKOTWA BAHARINI.

SHEIKH PONDA. KUTOKA GAZETI LA NIPASHE ,22 Agosti 2017; Akizungumza na Nipashe kwa simu jana, Sheikh Ponda ambaye pia ni Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Taasisi za Kiislamu Tanzania, alisema kwa muda mrefu wamekuwa wakipaza sauti kuhusu uwapo wa mauaji ya raia kwenye mikoa ya kusini mwa Tanzania, lakini haijasikilizwa. "Tunapongeza Nipashe kwa habari hii," alisema Sheikh Ponda kwa sababu "imefichua mambo mengi.", "Haya tumeshayasema lakini hakuna aliyetusikiliza. "Ni wakati mwafaka serikali ikatoa tamko kwa vile vyombo vya dola vimeonyesha kushindwa kueleza miili hiyo ni ya watu gani na inatoka wapi, (na kibaya) zaidi wanasema wanatambua miili mitatu iliyookotwa ambayo kwa sasa iko Muhimbili." Kaimu Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Lucas Mkondya, aliiambia Nipashe kwa njia ya simu juzi kuwa miili iliyookotwa ni mitatu na haikuwa kwenye viroba. Sheikh Ponda alisema mauaji hayo ni makubwa na hayajawahi kutokea kwa serikali z...