Skip to main content

MAGUFULI ALIVYOMLIPUA ABOOD.




PENGINE ilikuwa si rahisi kufikiri hapo kabla kuwa ipo siku mwenyekiti wa chama tawala anaweza kusema ukweli wenye kugusa maslahi ya mbunge wa chama chake kunako mkutano wa hadhara.
Hata hivyo, jambo hilo si la kushangaza tena katika serikali ya awamu ya tano iliyopania kusimamia misingi ya ukweli kwa maslahi mapana ya taifa.
Hali hiyo ilijidhihirisha jana mjini Morogoro wakati Rais John Magufuli alipomlipua mbele ya mkutano wa hadhara Mbunge wa Morogoro Mjini (CCM), Aziz Abood, kwa kumtaja kuwa miongoni mwa watu waliotwaa viwanda mkoani humo na baadhi yake kuvigeuza kuwa machungio ya mbuzi badala ya kuviendeleza kama ilivyotarajiwa.
Jana, akizungumzia agizo hilo la Rais Magufuli, Abood ambaye pia ni mmiliki wa kampuni ya mabasi ya Abood iliyopo mkoani humo, alisema anatekeleza agizo la Rais na tayari kiwanda chake cha Moproco kimefunga mashine mpya kwa ajili ya uzalishaji.
Akizungumza katika mkutano wake huo kwenye eneo la Msamvu mjini Morogoro jana, Rais Magufuli (JPM), ambaye pia mwenyekiti wa taifa wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), alisema Abood na watu wengine waliomilikishwa viwanda na serikali wanapaswa kuviendeleza au kuvirejesha serikalini ili wapewe wawekezaji wengine waviendeleze.
Rais Magufuli aliyasema hayo wakati akizungumza baada ya kusimama Msamvu kwa muda akitokea Dodoma kwenda jijini Dar es Salaam.
“Ninarudia wito wangu niliokwisha kuutoa huko nyuma, kwamba wenye viwanda hapa Morogoro ambao wameshindwa kuviendesha wavirejeshe serikalini. Na leo nataja, akiwemo Mbunge wa hapa wa Chama Cha Mapinduzi (CCM)… narudia, akiwamo Mbunge wa hapa wa CCM ambaye alibinafsishiwa viwanda vingi.
“Alipewa viwanda vingi na sasa nasikia anafugia mbuzi… sasa kama ameshindwa kuviendesha avirudishe ili tuwape watu wengine kwa sababu vijana hawa wanakosa ajira,” alisema Rais Magufuli na kuongeza:
“Nazungumza kwa uwazi kwa sababu msemakweli ni mpenzi wa Mungu.”
Rais Magufuli alisisitiza kuwa suala la kusimamia ukweli kwa manufaa ya taifa halichagui itikadi ya chama na ndiyo maana analisema hilo bila kificho.
“Uwe CCM, uwe CUF uwe Chadema, ukifanya ya ovyo mimi nakutandika tu, tena hadharani. Kwa hiyo mheshimiwa Mbunge wa hapa nampenda… na ni mbunge wa chama changu, lakini nataka viwanda alivyopewa vifanye kazi,” alisema Rais Magufuli na kuibua shangwe kubwa kutoka kwa mamia ya wananchi waliokuwa wakimsikiliza.
Kwenye mkutano huo, Rais Magufuli aliwapongeza pia wakulima wa mazao katika mkoa wa Morogoro kwa kuongeza uzalishaji.
Aidha, alimwagiza Kamanda wa Polisi wa Morogoro, SACP Ulrich Matei, kuhakikisha askari mgambo hawawasumbui wafanyabiashara wa Msamvu.
ABOOD AFUNGUKA
Akizungumza na Nipashe jana kuhusiana na maelekezo ya Rais juu ya viwanda alivyobinafsisha, Abood alisema anatekeleza na kiwanda anachomiliki cha Moproco kimeshaanza kufanya kazi.
Alisema mashine za kiwanda hicho zimeshafungwa na kwamba, kwa sasa kinachosubiriwa ni leseni tu.
“Rais Magufuli anahimiza, na sisi tunajitahidi kufuata kauli zake. Jitihada zinafanyika ili kila kitu kiende sawa na vijana wetu wapate ajira.
Morogoro kuna viwanda vingi ambavyo vitafunguliwa… siyo vya kwangu tu, Rais Magufuli anatumihimiza wote wenye viwanda,” alisema Abood.
Kwa mujibu wa ripoti ya mwaka 2012 ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma (POAC) , takribani viwanda na mashirika 17 ya umma nchini yaliyobinafsishwa mwaka 1993 yamefungwa baada ya kushindwa kuzalisha.

CHANZO:
http://m.ippmedia.com/sw/habari/jpm-alivyomlipua-abood-wa-mabasi

Comments

Habari Nyingine Kutoka Kioo17 Swahili;

MCHEZAJI WA ZAMANI WA UINGEREZA AMESEMA ALICHEZA NA WACHEZAJI WATATU MASHOGA KWENYE TIMU.

Carl Hoefkens (jezi no.2) alichezea West Bromwich Albion na Stoke City wakati wa enzi zake ligi kuu ya England. Beki wa zamani wa Ligi Kuu ya Uingereza amesema alicheza pamoja na wachezaji wenzake wawili wa mashoga ndani ya timu, na mmoja alikua na jina kubwa. Carl Hoefkens, West Bromwich Albion na Stoke City siku za nyuma, anasema wachezaji hao walikua wazi na hawakujificha kwenye vyumba vya kubadilishia nguo ingawa bado hawajulikani kwasababu ya maombi yao wenyewe ya kuomba kutotangazwa. Justin Fashanu, ambaye alijiua mwaka 1998, alikuwa mchezaji wa mwisho wa kazi nchini England kuja nje kama mashoga - mwaka 1990. Hoefkens alipokua (kushoto), alipokua anachezea Stock  City. Hoefkens aliyecheza Uingereza kwa miaka minne, akiondoka mwaka 2009, alidai kuwa mchezaji mwenzake mmoja wa timu alikua anaweza kuja kwenye uwanja wa mafunzo ya klabu na mpenzi wake wa kiume  lakini aliwaomba wenzake kutokuwaambia watu wangine wa nje ya timu. 'Nilicheza pamoja n...

ORODHA YA NCHI 80 AMBAZO MTANZANIA ANARUHUSIWA KUINGIA BILA VIZA.

         Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni amesema kuna zaidi ya nchi 80 ambazo watanzania wanaweza kusafiri bila ya kuwa na viza . Mhandisi Hamad Masauni amesema kuna zaidi ya nchi 80 ambazo watanzania wanaweza kusafiri bila ya kuwa na viza za kusafiria kama ilivyokuwa nchi za afrika Mashariki. Mhandisi Massauni amebainisha hayo leo bungeni wakati akijibu swali la Mbunge wa Mlalo kupitia tiketi ya CCM Rashid Shangazi aliyetaka kujua ni nchi ngapi ambazo watanzania wanaweza kusafiri bila ya kuwa na viza (viza on arrival). "Zipo nchi 16 kwa Afrika ambazo watanzania wanaweza kuzitembelea bila ya kuwa na viza na duniani zipo 67" alisema Masauni. Aidha Massauni amezitaja nchi hizo kuwa ni Benin, Burkina Faso, Cape Verde, Ivory Coast, Djibouti, Gabon, Gambia, Guinea, Guinea­Bissau, Liberia, Mali, Mauritania, Niger, Sierra Leone pamoja na Togo. Pamoja na hayo Masauni amesema...

WALICHOJIBU CHENGE ,NGELEJA NA DK.KAFUMU BAADA YA RIPOTI YA PILI YA RAISI.

              VIGOGO waliotajwa katika ripoti ya pili ya kuchunguza makontena yenye mchanga wa madini (makinikia)  kuisababishia Serikali hasara ya matrilioni ya fedha kupitia sekta ya madini, walipokuwa wakihudumu katika nyadhifa zao serikalini wamevunja ukimya. Vigogo hao wamezungumzia ripoti hiyo ya pili iliyowasilishwa kwa Rais Dk. John Magufuli Ikulu Dar es Salaam jana, ambapo kamati husika ilichunguza hasara ambayo nchi imepata tangu 1998 usafirishaji wa mchanga wa dhahabu nje ya nchi ulipoanza. Mbunge wa Bariadi, Andrew Chenge (CCM), alipoulizwa maoni yake juu ya kutajwa na kamati hiyo, alisema hataki kuzungumza chochote juu ya ripoti hiyo, huku Mbunge wa Sengerema, William Ngeleja (CCM), akisema sheria ya madini ya 2010 ingefuatwa, nchi isingekuwa hapa ilipo. Kwa upande wake Kamishna wa Madini wa zamani, Dk. Dalaly Kafumu, alisema kwa sasa  hawezi kuzungumza jambo lolote kwa kuwa ni yeye ni mmoja wa watuhumiwa waliotaj...

KIONGOZI MKUU WA UPINZANI NCHINI ZIMBABWE, MORGAN TSVANGIRAI AMEFARIKI DUNIA.

Kiongozi wa upinzani wa Zimbabwe Morgan Tsvangirai amefariki dunia nchini Afrika Kusini, afisa mkuu wa chama chake cha MDC amesema. Bw Tsvangirai, mwenye umri wa miaka 65, aliyekuwa waziri mkuu, alilipotiwa kuwa alikuwa akisumbuliwa na saratani ya koloni. "Amefariki jioni hii, familia yake imenitaarifu"  Makamu wa Rais wa MDC, Elias Mudzuri aliliambia shirika la habari la Uingereza, Reuters. Morgan Tsvangirai alizaliwa mnamo Machi 10, 1952 huko Gutu, Zimbabwe. Baba yake alikuwa mfanyakazi wa mgodi, fundi, na mkulima. Alihudhuria Shule ya Msingi ya Guco ya St. Marks. Kisha alihamishiwa Shule ya Msingi ya Chikara Gutu. Kwa elimu yake ya sekondari, alihudhuria Shule ya High Gokomere. Alikuwa waziri mkuu katika serikali ya mseto ya Zimbabwe tangu 2009 hadi 2013. Katika kazi yake ya awali alionekana kuwa mfanyakazi mwenye bidii sana na alifanya kazi katika mgodi wa madini ya nickel( kwa zaidi ya muongo mmoja. Alipanda cheo haraka kutambuliwa na akain...

MADAI YA CUBA KWAMBA WAZIRI MKUU WA CANADA NI MTOTO WA FIDEL CASTRO.

Pichani ni waziri mkuu wa Canada, Justin Trudeau (kushoto), na Rais wa zamani wa Cuba, Hayati Fidel Castro (kulia). Maelezo yaliyoandikwa na mtoto wa kwanza wa rais wa zamani wa Cuba , Fidel Castro, kabla ya kujiua yamelishtua taifa la Cuba wiki hii. Maelezo hayo yaliyoandikwa na mtoto huyo mkubwa wa mwanamapinduzi na rais wa zamani wa nchi hiyo yalikuwa ya kushangaza baada ya  kuwa na madai ya kuwa Waziri Mkuu wa Canada Justin Trudeau ni mtoto wa nje wa baba yake marehemu Fidel Castro. Maelezo hayo yaliyoandikwa kwa mkono na mtoto huyo wa Fidel Castro aliyejiua siku chache zilizopita kwa msongo wa mawazo, Fidel Castro Diaz-Balart, aliyekuwa na umri wa miaka 68, yalionekana kuthibitisha uvumi wa muda mrefu nchini Cuba kwamba Fidel Castro ni baba wa damu wa waziri mkuu wa sasa wa Canada, Justin Trudeau ikiwa ni matokeo ya uhusiano wa siri wa kimapenzi na mke wa mwanasiasa maarufu wa Canada, Pierre Trudeau, Margaret Trudeau mwaka 1970. Kifo cha mwanasayansi wa ...

KASHFA YA MAPENZI KATI MH.MBOWE NA WEMA SEPETU.

MH.FREEMAN MBOWE AKIWA NA WEMA SEPETU. Siku chache baada ya ile skendo ya ngono iliyosababisha wakili na mshauri wa Chama cha ACT -Wazalendo , Bwana Albert Msando kujiuzulu kwenye nyadhifa yake ya chama ,yameibuka mangine kwenye chama kikuu cha upinzani Tanzania ,CHADEMA ,baada ya kusambaa kwa kipande cha sauti kinachodaiwa kua ni mazungumzo kati ya mwenyekiti wa chama hicho na mbunge wa Hai Mh.Freeman Mbowe na Miss Tanzania 2006 ,mrembo Wema Isack Sepetu. SIKILIZA HIVI VIPANDE VYA SAUTI: Bonyeza hapa chini kusikiliza maongezi hayo yanayodaiwa kuwa ni kati ya Wema Sepetu na Mh.Freeman Mbowe; Bonyeza hapa chini kusikiliza majibu ya Wema Sepetu; Bonyeza hapa chini kusikiliza majibu ya Mh.Freeman Mbowe; VYANZO: Jamii Forums,                   YouTube.com,                   Perfect255.com.                   

RAPA SNOOP DOGG AMETHIBITISHA MIPANGO YA KUHAMIA UGANDA.

Msanii wa muziki wa Hip Hop wa Marekani, Calvin Cordozar Broadus.Jr. maarufu kama Snoop Dogg amethibitisha kuwa anataka kuhamia Uganda baada ya rais wa Marekani, Donald Trump kudaiwa kuziita nchi za Afrika 'Shimo la Choo' . Snoop Doggy Dogg pia ni mwimbaji, mwandishi wa nyimbo, mtayarishaji wa muziki, mtangazaji katika televisheni, na mwigizaji wa filamu ambaye alianza kupata umaarufu mkubwa katika muziki mwaka 1992 wakati alipogunduliwa na mtayarishaji Dr.Dre, na kushiriki katika nyimbo za Dr.Dre kama "Deep Cover", na kisha kwenye albamu ya kwanza ya Dr.Dre, ' The Chronic' . Kwa sasa tayari ameshauza albamu zaidi ya milioni 23 nchini Marekani na albamu milioni 35 duniani kote. Mmarekani huyo mweusi mwenye miaka 46 wa ambaye anajulikana kwa nyimbo zake za maarufu kama; The next episode, Drop it like it’s hot, beautiful, Lay low,  nk Juzi alirekodi kipande cha video na kukisambaza akisema kuwa anataka kuhamia chini Uganda. Tazama V...