Skip to main content

MAGUFULI ALIVYOMLIPUA ABOOD.




PENGINE ilikuwa si rahisi kufikiri hapo kabla kuwa ipo siku mwenyekiti wa chama tawala anaweza kusema ukweli wenye kugusa maslahi ya mbunge wa chama chake kunako mkutano wa hadhara.
Hata hivyo, jambo hilo si la kushangaza tena katika serikali ya awamu ya tano iliyopania kusimamia misingi ya ukweli kwa maslahi mapana ya taifa.
Hali hiyo ilijidhihirisha jana mjini Morogoro wakati Rais John Magufuli alipomlipua mbele ya mkutano wa hadhara Mbunge wa Morogoro Mjini (CCM), Aziz Abood, kwa kumtaja kuwa miongoni mwa watu waliotwaa viwanda mkoani humo na baadhi yake kuvigeuza kuwa machungio ya mbuzi badala ya kuviendeleza kama ilivyotarajiwa.
Jana, akizungumzia agizo hilo la Rais Magufuli, Abood ambaye pia ni mmiliki wa kampuni ya mabasi ya Abood iliyopo mkoani humo, alisema anatekeleza agizo la Rais na tayari kiwanda chake cha Moproco kimefunga mashine mpya kwa ajili ya uzalishaji.
Akizungumza katika mkutano wake huo kwenye eneo la Msamvu mjini Morogoro jana, Rais Magufuli (JPM), ambaye pia mwenyekiti wa taifa wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), alisema Abood na watu wengine waliomilikishwa viwanda na serikali wanapaswa kuviendeleza au kuvirejesha serikalini ili wapewe wawekezaji wengine waviendeleze.
Rais Magufuli aliyasema hayo wakati akizungumza baada ya kusimama Msamvu kwa muda akitokea Dodoma kwenda jijini Dar es Salaam.
“Ninarudia wito wangu niliokwisha kuutoa huko nyuma, kwamba wenye viwanda hapa Morogoro ambao wameshindwa kuviendesha wavirejeshe serikalini. Na leo nataja, akiwemo Mbunge wa hapa wa Chama Cha Mapinduzi (CCM)… narudia, akiwamo Mbunge wa hapa wa CCM ambaye alibinafsishiwa viwanda vingi.
“Alipewa viwanda vingi na sasa nasikia anafugia mbuzi… sasa kama ameshindwa kuviendesha avirudishe ili tuwape watu wengine kwa sababu vijana hawa wanakosa ajira,” alisema Rais Magufuli na kuongeza:
“Nazungumza kwa uwazi kwa sababu msemakweli ni mpenzi wa Mungu.”
Rais Magufuli alisisitiza kuwa suala la kusimamia ukweli kwa manufaa ya taifa halichagui itikadi ya chama na ndiyo maana analisema hilo bila kificho.
“Uwe CCM, uwe CUF uwe Chadema, ukifanya ya ovyo mimi nakutandika tu, tena hadharani. Kwa hiyo mheshimiwa Mbunge wa hapa nampenda… na ni mbunge wa chama changu, lakini nataka viwanda alivyopewa vifanye kazi,” alisema Rais Magufuli na kuibua shangwe kubwa kutoka kwa mamia ya wananchi waliokuwa wakimsikiliza.
Kwenye mkutano huo, Rais Magufuli aliwapongeza pia wakulima wa mazao katika mkoa wa Morogoro kwa kuongeza uzalishaji.
Aidha, alimwagiza Kamanda wa Polisi wa Morogoro, SACP Ulrich Matei, kuhakikisha askari mgambo hawawasumbui wafanyabiashara wa Msamvu.
ABOOD AFUNGUKA
Akizungumza na Nipashe jana kuhusiana na maelekezo ya Rais juu ya viwanda alivyobinafsisha, Abood alisema anatekeleza na kiwanda anachomiliki cha Moproco kimeshaanza kufanya kazi.
Alisema mashine za kiwanda hicho zimeshafungwa na kwamba, kwa sasa kinachosubiriwa ni leseni tu.
“Rais Magufuli anahimiza, na sisi tunajitahidi kufuata kauli zake. Jitihada zinafanyika ili kila kitu kiende sawa na vijana wetu wapate ajira.
Morogoro kuna viwanda vingi ambavyo vitafunguliwa… siyo vya kwangu tu, Rais Magufuli anatumihimiza wote wenye viwanda,” alisema Abood.
Kwa mujibu wa ripoti ya mwaka 2012 ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma (POAC) , takribani viwanda na mashirika 17 ya umma nchini yaliyobinafsishwa mwaka 1993 yamefungwa baada ya kushindwa kuzalisha.

CHANZO:
http://m.ippmedia.com/sw/habari/jpm-alivyomlipua-abood-wa-mabasi

Comments

Habari Nyingine Kutoka Kioo17 Swahili;

ORODHA YA NCHI 80 AMBAZO MTANZANIA ANARUHUSIWA KUINGIA BILA VIZA.

         Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni amesema kuna zaidi ya nchi 80 ambazo watanzania wanaweza kusafiri bila ya kuwa na viza . Mhandisi Hamad Masauni amesema kuna zaidi ya nchi 80 ambazo watanzania wanaweza kusafiri bila ya kuwa na viza za kusafiria kama ilivyokuwa nchi za afrika Mashariki. Mhandisi Massauni amebainisha hayo leo bungeni wakati akijibu swali la Mbunge wa Mlalo kupitia tiketi ya CCM Rashid Shangazi aliyetaka kujua ni nchi ngapi ambazo watanzania wanaweza kusafiri bila ya kuwa na viza (viza on arrival). "Zipo nchi 16 kwa Afrika ambazo watanzania wanaweza kuzitembelea bila ya kuwa na viza na duniani zipo 67" alisema Masauni. Aidha Massauni amezitaja nchi hizo kuwa ni Benin, Burkina Faso, Cape Verde, Ivory Coast, Djibouti, Gabon, Gambia, Guinea, Guinea­Bissau, Liberia, Mali, Mauritania, Niger, Sierra Leone pamoja na Togo. Pamoja na hayo Masauni amesema...

MCHEZAJI WA ZAMANI WA UINGEREZA AMESEMA ALICHEZA NA WACHEZAJI WATATU MASHOGA KWENYE TIMU.

Carl Hoefkens (jezi no.2) alichezea West Bromwich Albion na Stoke City wakati wa enzi zake ligi kuu ya England. Beki wa zamani wa Ligi Kuu ya Uingereza amesema alicheza pamoja na wachezaji wenzake wawili wa mashoga ndani ya timu, na mmoja alikua na jina kubwa. Carl Hoefkens, West Bromwich Albion na Stoke City siku za nyuma, anasema wachezaji hao walikua wazi na hawakujificha kwenye vyumba vya kubadilishia nguo ingawa bado hawajulikani kwasababu ya maombi yao wenyewe ya kuomba kutotangazwa. Justin Fashanu, ambaye alijiua mwaka 1998, alikuwa mchezaji wa mwisho wa kazi nchini England kuja nje kama mashoga - mwaka 1990. Hoefkens alipokua (kushoto), alipokua anachezea Stock  City. Hoefkens aliyecheza Uingereza kwa miaka minne, akiondoka mwaka 2009, alidai kuwa mchezaji mwenzake mmoja wa timu alikua anaweza kuja kwenye uwanja wa mafunzo ya klabu na mpenzi wake wa kiume  lakini aliwaomba wenzake kutokuwaambia watu wangine wa nje ya timu. 'Nilicheza pamoja n...

ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 2017, TANZANIA

MH.GEORGE SIMBACHAWENE .               Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Tamisemi) George Simbachawene ametoa idadi ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na masomo ya kidato cha tano na vyuo vya ufundi kwa mwaka 2017 huku jumla ya wanafunzi 2,999 wakiachwa.             Simbachawene ametoa kauli hiyo leo mjini Dodoma wakati akizungumza na waandishi ws habari na kusema kuwa ufaulu kwa mwaka huu umeongezeka kwa asilimia 3.75 ukilinganisha na matokeo ya mwaka 2015. Waziri amedai kati ya wanafunzi 96,018 waliofaulu kwa daraja la kwanza hadi la tatu ni wanafunzi 93,019 tu ndiyo waliochaguliwa kujiunga na kidato cha tano na vyuo vya ufundi.              Waziri Simbachawene amesema kuwa jumla ya watahiniwa wote waliofanya mtihani wa kidato cha nne kwa shule kwa mwaka 2016 ni 349,524 huku waliofanya mtihani wa kujitegemea ni 47,751 ambapo watahiniwa waliofanya mtihani wa shule...

TUPAC SHAKUR ALIBAKWA JELA !!!

             Ulimwengu wa filamu za Hollywood na muziki wa Hip Hop juzi ulipatwa na mshangao baada ya mtayarishaji wa filamu inayohusu maisha ya hayati Tupac Shakur ,L.T Hutton kuelezea sababu zilizomfanya kumbadilisha muongozaji wa filamu hiyo kutoka John Singleton na kumuweka muongozaji Benny "Boom" Douglas.  Filamu hiyo inayoitwa "all eyez on me" tayari imekwisha andaliwa na inatarajiwa kuzinduliwa leo tarehe 16 Juni 2017.       Akizungumza kwenye mahojiano redioni L.T Hutton amewashtusha watu wengi baada ya kudai kwamba walishindwana na muongozaji wa mwanzo bwana John Singleton sababu muongozaji huyo aling'ang'ania kuwepo kwa matukio (scene) ambazo kwa maoni yake zisingependeza.        Matukio ambayo John Singleton alipenda yawepo katika filamu hiyo ni pamoja na kutaka filamu hiyo ianze na scene ya Tupac akilazimisha kumlawiti msichana wa kizungu.!!!          Singleton pia ali...

MFALME WA GHANA ASABABISHA AFISA MKUU WA BENKI KUFUKUZWA KAZI.

Afisa mtendaji mkuu wa benki alifukuzwa kazi na kuchunguzwa na Shirika la Uhalifu wa Taifa baada ya kuweka pauni za Uingereza 350,000 ( £ 350,000 ) pesa taslimu aliyopewa na Mfalme wa Ghana. Mark Arthur wa benki ya Kimataifa ya Ghana Bigwig aliitwa kwenye nyumba ya Osei Tutu II huko Henley-on-Thames na kupewa £ 200,000 pamoja na $ 200,000 na kuagizwa aiweke kwenye akaunti ya benki ya Mfalme huyo. Licha ya noti hizo kuwa na namba za mfululizo zinazofuatana (consecutive serial numbers) Bwana Arthur alisema aliona kuwa haifai kumhoji mfalme na kwenda kuiweka benki kwa kutumia usafiri wa teksi ya uber. Punde baada ya Bwana Arthur kuweka pesa hiyo benki, taarifa ya utakatishaji wa fedha ilifika katika jiji la London, Uingereza na kugharimu ajira yake. Bwana Arthur alielezea kwenye taarifa yake ya ushahidi kuwa Mfalme alimwambia kwamba pesa hizo zimekusanywa kutoka kwenye akaunti za benki za nchini Ghana na kupelekwa Uingereza. Pia alidai kwamba Mfale alimpa $ 200,000 ili ...

SABABU ZA KUVUNJIKA KWA KUNDI LA P-SQUARE.

WANAMUZIKI MAPACHA WA KUNDI LA PSQUARE, PETER (KUSHOTO) NA PAUL (KULIA) WAKIWA NA KAKA YAO AMBAE PIA NI MENEJA WAO, JUDES OKOYE. Mwanamuziki wa kundi la PSquare kutoka Nigeria, Peter Okoye ametangaza kujitoa kwenye kundi hilo la muziki wa Pop maarufu zaidi Afrika. Msanii huyo alidai kwamba amewasilisha maombi ya kuvunja kundi hilo katika barua aliyoandika kwa wakili wao Festus Keyamo. Kulingana na nakala ya barua iliyotolewa kwenye vyombo vya habari Jumatatu,Tarehe 25 Septemba, Peter alisema kuwa pacha wake na, Paul, na kaka yao, Judes waliahirisha ziara yao ya muziki ya Marekani bila kushauriana naye.Na hiyo ni moja kati ya sababu za msingi. Peter pia aliwalaumu Paul na kaka yao mkubwa mkubwa ambae ni meneja wao pia kwa udanganyifu walioufanya ili kutatua shida waliyokuwa nayo juu ya biashara ya muziki. Wasanii hao ndugu wamekua kwenye vita vya maneno kwenye mitandao ya kijamii tangu mwisho wa mwaka jana pamoja na juhudi za watu wao wa karibu kujaribu kuwapatanisha kifami...

ORODHA YA NCHI ZA KWANZA NA ZA MWISHO KWA AMANI DUNIANI.

Marekani:  Ripoti ya Taasisi ya Uchumi na Amani imepata mataifa kumi tu ulimwenguni ambayo hayapo katika vita na migogoro kabisa. Kwa mujibu wa Ripoti ya Kimataifa ya Amani 2016, Botswana, Chile, Costa Rica, Japan, Mauritius, Panama, Qatar, Uswisi, Uruguay na Vietnam ndio nchi pekee ambazo hazipo kwenye vita wala migogoro yeyote ile ya kuhatarisha amani.. Iceland inaongoza orodha ya nchi zinazoongoza kwa amani ulimwenguni, ikifuatiwa na Denmark, Austria, New Zealand, Ureno, Jamhuri ya Czech, Uswisi, Canada, Japan na Slovenia - wakati Marekani ikiwa kwenye nafasi ya 103. Palestina imepanda kutoka nafasi ya 163 mpaka nafasi ya 148. Syria iliyoharibiwa na vita imewekwa chini ya orodha, chini kuliko Sudan Kusini, Iraq, Afghanistan, Somalia, Yemen, Jamhuri ya Afrika ya Kati, Ukraine, Sudan na Libya. "Ripoti inalinganisha amani duniani kwa kutumia mandhari tatu pana: hali ya utulivu na usalama katika jamii; kiwango cha mgogoro wa ndani au wa kimataifa; na kiwango cha kije...