Skip to main content

MAGUFULI ALIVYOMLIPUA ABOOD.




PENGINE ilikuwa si rahisi kufikiri hapo kabla kuwa ipo siku mwenyekiti wa chama tawala anaweza kusema ukweli wenye kugusa maslahi ya mbunge wa chama chake kunako mkutano wa hadhara.
Hata hivyo, jambo hilo si la kushangaza tena katika serikali ya awamu ya tano iliyopania kusimamia misingi ya ukweli kwa maslahi mapana ya taifa.
Hali hiyo ilijidhihirisha jana mjini Morogoro wakati Rais John Magufuli alipomlipua mbele ya mkutano wa hadhara Mbunge wa Morogoro Mjini (CCM), Aziz Abood, kwa kumtaja kuwa miongoni mwa watu waliotwaa viwanda mkoani humo na baadhi yake kuvigeuza kuwa machungio ya mbuzi badala ya kuviendeleza kama ilivyotarajiwa.
Jana, akizungumzia agizo hilo la Rais Magufuli, Abood ambaye pia ni mmiliki wa kampuni ya mabasi ya Abood iliyopo mkoani humo, alisema anatekeleza agizo la Rais na tayari kiwanda chake cha Moproco kimefunga mashine mpya kwa ajili ya uzalishaji.
Akizungumza katika mkutano wake huo kwenye eneo la Msamvu mjini Morogoro jana, Rais Magufuli (JPM), ambaye pia mwenyekiti wa taifa wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), alisema Abood na watu wengine waliomilikishwa viwanda na serikali wanapaswa kuviendeleza au kuvirejesha serikalini ili wapewe wawekezaji wengine waviendeleze.
Rais Magufuli aliyasema hayo wakati akizungumza baada ya kusimama Msamvu kwa muda akitokea Dodoma kwenda jijini Dar es Salaam.
“Ninarudia wito wangu niliokwisha kuutoa huko nyuma, kwamba wenye viwanda hapa Morogoro ambao wameshindwa kuviendesha wavirejeshe serikalini. Na leo nataja, akiwemo Mbunge wa hapa wa Chama Cha Mapinduzi (CCM)… narudia, akiwamo Mbunge wa hapa wa CCM ambaye alibinafsishiwa viwanda vingi.
“Alipewa viwanda vingi na sasa nasikia anafugia mbuzi… sasa kama ameshindwa kuviendesha avirudishe ili tuwape watu wengine kwa sababu vijana hawa wanakosa ajira,” alisema Rais Magufuli na kuongeza:
“Nazungumza kwa uwazi kwa sababu msemakweli ni mpenzi wa Mungu.”
Rais Magufuli alisisitiza kuwa suala la kusimamia ukweli kwa manufaa ya taifa halichagui itikadi ya chama na ndiyo maana analisema hilo bila kificho.
“Uwe CCM, uwe CUF uwe Chadema, ukifanya ya ovyo mimi nakutandika tu, tena hadharani. Kwa hiyo mheshimiwa Mbunge wa hapa nampenda… na ni mbunge wa chama changu, lakini nataka viwanda alivyopewa vifanye kazi,” alisema Rais Magufuli na kuibua shangwe kubwa kutoka kwa mamia ya wananchi waliokuwa wakimsikiliza.
Kwenye mkutano huo, Rais Magufuli aliwapongeza pia wakulima wa mazao katika mkoa wa Morogoro kwa kuongeza uzalishaji.
Aidha, alimwagiza Kamanda wa Polisi wa Morogoro, SACP Ulrich Matei, kuhakikisha askari mgambo hawawasumbui wafanyabiashara wa Msamvu.
ABOOD AFUNGUKA
Akizungumza na Nipashe jana kuhusiana na maelekezo ya Rais juu ya viwanda alivyobinafsisha, Abood alisema anatekeleza na kiwanda anachomiliki cha Moproco kimeshaanza kufanya kazi.
Alisema mashine za kiwanda hicho zimeshafungwa na kwamba, kwa sasa kinachosubiriwa ni leseni tu.
“Rais Magufuli anahimiza, na sisi tunajitahidi kufuata kauli zake. Jitihada zinafanyika ili kila kitu kiende sawa na vijana wetu wapate ajira.
Morogoro kuna viwanda vingi ambavyo vitafunguliwa… siyo vya kwangu tu, Rais Magufuli anatumihimiza wote wenye viwanda,” alisema Abood.
Kwa mujibu wa ripoti ya mwaka 2012 ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma (POAC) , takribani viwanda na mashirika 17 ya umma nchini yaliyobinafsishwa mwaka 1993 yamefungwa baada ya kushindwa kuzalisha.

CHANZO:
http://m.ippmedia.com/sw/habari/jpm-alivyomlipua-abood-wa-mabasi

Comments

Habari Nyingine Kutoka Kioo17 Swahili;

ORODHA YA NCHI ZA KWANZA NA ZA MWISHO KWA AMANI DUNIANI.

Marekani:  Ripoti ya Taasisi ya Uchumi na Amani imepata mataifa kumi tu ulimwenguni ambayo hayapo katika vita na migogoro kabisa. Kwa mujibu wa Ripoti ya Kimataifa ya Amani 2016, Botswana, Chile, Costa Rica, Japan, Mauritius, Panama, Qatar, Uswisi, Uruguay na Vietnam ndio nchi pekee ambazo hazipo kwenye vita wala migogoro yeyote ile ya kuhatarisha amani.. Iceland inaongoza orodha ya nchi zinazoongoza kwa amani ulimwenguni, ikifuatiwa na Denmark, Austria, New Zealand, Ureno, Jamhuri ya Czech, Uswisi, Canada, Japan na Slovenia - wakati Marekani ikiwa kwenye nafasi ya 103. Palestina imepanda kutoka nafasi ya 163 mpaka nafasi ya 148. Syria iliyoharibiwa na vita imewekwa chini ya orodha, chini kuliko Sudan Kusini, Iraq, Afghanistan, Somalia, Yemen, Jamhuri ya Afrika ya Kati, Ukraine, Sudan na Libya. "Ripoti inalinganisha amani duniani kwa kutumia mandhari tatu pana: hali ya utulivu na usalama katika jamii; kiwango cha mgogoro wa ndani au wa kimataifa; na kiwango cha kije...

JAGUAR KUACHIA WIMBO BAADA YA KUAPISHWA MBUNGE.

Mbunge wa Starehe, Kenya, "Jaguar" anajipanga kutoa wimbo mpya mara tu baada ya kuapishwa kua mbunge. Katika chapisho lake la kwenye akaunti yake ya mtandao wa kijamii, Jaguar aliupendekeza wimbo wake wa "Ndoto" kama salamu kwa Wakenya na watu walio nje ya Kenya. Charles Njagua, ambae ni maarufu kwa jina la Jaguar, ana Aliahidi mashabiki wimbo mpya baada ya kuapa rasmi kama mbunge.  Mimbaji huyo ambaye ametoa hits kadhaa lakini sasa anazingatia siasa baada ya kushinda kiti, aliwaambia mashabiki kwenye vyombo vya habari vya kijamii kwamba wimbo mpya, unaitwa "Ndoto", uko tayari na utaachiliwa haraka baada ya kuapa. "Sasa ni karibu miongo miwili tangu mimi kuweka mguu katika studio ya kurekodi,   alisema Jaguar katika chapisho lake. CHANZO: www.tuko.news

KASHFA YA MAPENZI KATI MH.MBOWE NA WEMA SEPETU.

MH.FREEMAN MBOWE AKIWA NA WEMA SEPETU. Siku chache baada ya ile skendo ya ngono iliyosababisha wakili na mshauri wa Chama cha ACT -Wazalendo , Bwana Albert Msando kujiuzulu kwenye nyadhifa yake ya chama ,yameibuka mangine kwenye chama kikuu cha upinzani Tanzania ,CHADEMA ,baada ya kusambaa kwa kipande cha sauti kinachodaiwa kua ni mazungumzo kati ya mwenyekiti wa chama hicho na mbunge wa Hai Mh.Freeman Mbowe na Miss Tanzania 2006 ,mrembo Wema Isack Sepetu. SIKILIZA HIVI VIPANDE VYA SAUTI: Bonyeza hapa chini kusikiliza maongezi hayo yanayodaiwa kuwa ni kati ya Wema Sepetu na Mh.Freeman Mbowe; Bonyeza hapa chini kusikiliza majibu ya Wema Sepetu; Bonyeza hapa chini kusikiliza majibu ya Mh.Freeman Mbowe; VYANZO: Jamii Forums,                   YouTube.com,                   Perfect255.com.                   

"GIGGS HAFAI KUWA KOCHA WA TIMU YA TAIFA", BABA YAKE ANASEMA...!!!

Ryan Giggs. Chama cha Soka cha Wales (FAW) siku ya jumatatu kilitangaza kumchagua winga wa zamani wa Manchester United Ryan Giggs kama kocha wa timu yao ya taifa kwa mkataba wa miaka minne. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 44 anachukua kazi iyoachwa na Chris Coleman, ambaye aliiongoza Wales kwenye nusu fainali za Euro 2016 lakini aliacha kazi mwezi Novemba ili kuchukua nafasi ya kuifundisha timu ya Sunderland ya ligi kuu ya Uingereza. Giggs alisema kuwa anajivunia kwa kupewa kazi hiyo na pamoja na changamoto iliyo mbele yake baada ya Wales kushindwa kufuzu kucheza fainali za Kombe la Dunia mwaka huu nchini Urusi na sasa wanazingatia michuano ya Ulaya ya 2020. "Siwezi kusubiri kuanza kufanya kazi na wachezaji tunapojiandaa kwa ajili ya michezo muhimu baadaye mwaka huu," alisema. Lakini baba mzazi wa Giggs, Danny Wilson ana maoni  tofauti sana...!!! Anakiri kwamba mwanae anamtia aibu na anasema hastahili kuchukua kazi hiyo ya ukocha wa timu ya t...

MCHEZAJI WA ZAMANI WA UINGEREZA AMESEMA ALICHEZA NA WACHEZAJI WATATU MASHOGA KWENYE TIMU.

Carl Hoefkens (jezi no.2) alichezea West Bromwich Albion na Stoke City wakati wa enzi zake ligi kuu ya England. Beki wa zamani wa Ligi Kuu ya Uingereza amesema alicheza pamoja na wachezaji wenzake wawili wa mashoga ndani ya timu, na mmoja alikua na jina kubwa. Carl Hoefkens, West Bromwich Albion na Stoke City siku za nyuma, anasema wachezaji hao walikua wazi na hawakujificha kwenye vyumba vya kubadilishia nguo ingawa bado hawajulikani kwasababu ya maombi yao wenyewe ya kuomba kutotangazwa. Justin Fashanu, ambaye alijiua mwaka 1998, alikuwa mchezaji wa mwisho wa kazi nchini England kuja nje kama mashoga - mwaka 1990. Hoefkens alipokua (kushoto), alipokua anachezea Stock  City. Hoefkens aliyecheza Uingereza kwa miaka minne, akiondoka mwaka 2009, alidai kuwa mchezaji mwenzake mmoja wa timu alikua anaweza kuja kwenye uwanja wa mafunzo ya klabu na mpenzi wake wa kiume  lakini aliwaomba wenzake kutokuwaambia watu wangine wa nje ya timu. 'Nilicheza pamoja n...

TUPAC SHAKUR ALIBAKWA JELA !!!

             Ulimwengu wa filamu za Hollywood na muziki wa Hip Hop juzi ulipatwa na mshangao baada ya mtayarishaji wa filamu inayohusu maisha ya hayati Tupac Shakur ,L.T Hutton kuelezea sababu zilizomfanya kumbadilisha muongozaji wa filamu hiyo kutoka John Singleton na kumuweka muongozaji Benny "Boom" Douglas.  Filamu hiyo inayoitwa "all eyez on me" tayari imekwisha andaliwa na inatarajiwa kuzinduliwa leo tarehe 16 Juni 2017.       Akizungumza kwenye mahojiano redioni L.T Hutton amewashtusha watu wengi baada ya kudai kwamba walishindwana na muongozaji wa mwanzo bwana John Singleton sababu muongozaji huyo aling'ang'ania kuwepo kwa matukio (scene) ambazo kwa maoni yake zisingependeza.        Matukio ambayo John Singleton alipenda yawepo katika filamu hiyo ni pamoja na kutaka filamu hiyo ianze na scene ya Tupac akilazimisha kumlawiti msichana wa kizungu.!!!          Singleton pia ali...

MOHAMMED DEWJI NA BILL GATES KUTOA NUSU YA UTAJIRI WAO...!!!

MOHAMMED DEWJI AKIWA NA BILL GATES. Mfanyabiashara tajiri namba moja Tanzania (kwa mujibu wa jarida la Forbes) na mmiliki wa makampuni ya METL , Mohammed "Mo" Dewji ,wiki chache zilizopita amekua mmoja wa mabilionea 14 wapya kujiunga katika mpango wa kuchangia misaada kwa jamii uitwao "Giving Pledge".                 Mpango huo ulioanzishwa na familia ya mfanyabiashara tajiri namba moja duniani (kwa mujibu wa jarida la Forbes) na mmiliki wa kampuni ya Microsoft Bill Gates pamoja na rafiki yake bilionea Warren Buffet mwaka 2010, ulikua na tayari umeshaungwa mkono na mabilionea 154 mpaka mwanzo wa mwaka huu (2017). WAASISI WA "GIVIN PLEDGE",WARREN BUFFET, MELINDA GATES NA BILL GATES.         Mohammed Dewji anakua mmoja kati ya matajiri wachache sana kutoka Afrika kama Patrice Motsepe (Afrika Kusini) na Mo Ibrahim (Sudan) kujiunga na kampeni hiyo ambayo nia yake kubwa ni kushawishi watu matajiri kutoa angalau nu...